BARD AI

JF-Expert Member
Jul 24, 2018
3,413
8,199
Leo Januari 31, 2023 Rais Samia amezungumzia suala la Plea Bargain, utaratibu wa Makubaliano ya Kumaliza Kesi kwa Kulipa Fedha kwa Serikali ambao ulitumika wakati wa Utawala wa Hayati Rais Magufuli chini ya DPP Biswalo Mganga aliyeondolewa na kuteuliwa kuwa Jaji wa Mahakama Kuu, huku akieleza kuwa Suala hilo limekuwa na utata ikiwemo baadhi ya pesa zilizolipwa kwenye akaunti zimeoneka kupelekwa Nchini China.

Ukiachana na hilo Jaji Biswalo amekuwa kwenye kashfa nyingi ikiwemo kuchukua mali za washtakiwa bila utaratibu wenye uwazi, bila uwepo wa sheria na akaunti maalumu ya Serikali inayokusanya fedha hizo.

Sasa kwa hili la leo, Jaji Biswalo anasubiri nini kuachia nafasi hiyo kuonesha Uwajibikaji? Lakini Pia, Rais Samia anasubiri nini kuunda Tume ya Majaji watatu wanaotakiwa kuchunguza suala hilo na kutoa uamuzi wa nini Rais afanye?

Anyway Taifa linasubiria ripoti ya matumizi ya fedha zaidi ya Tsh. Bilioni 50 zilizotokana na makubaliano ya washtakiwa na Ofisi ya Taifa ya Mashtaka (NPS), Rais Samia Suluhu Hassan amesema ofisi hiyo ilipitia kipindi ambacho kuna michezo ilikuwa inafanyika ambayo iliharibu taswira ya taasisi hiyo.
 
Mama huwezi jisafisha wakati naye alikuwa kwenye hilo hilo jahazi. Kiongozi makini alipaswa awe amesha jiuzulu zamani.

Yeye kuendelea kukaa hapo, na hao waliofanya haya madudu kuendelea kuwateua ni ishara kwamba yeye kiongozi anabariki hayo madudu.

Kulialia na kutafuta sympathy hakuta msaidia, ni heri akae kimya sio kusema halafu huwa uwezo wa kuchukua hatua. Watanzania sio wajinga.
 
Mzigo wote mtupie msukuma ndio inadhihirika lawama we rusha kwa mfu tu wote wataitikia anhaa ndio maana, anayeelekezewa tuhuma hawezi kujibu.
Ila kipo kiama
 
Mama huwezi jisafisha wakati naye alikuwa kwenye hilo hilo jahazi. Kiongozi makini alipaswa awe amesha jiuzulu zamani. Yeye kuendelea kukaa hapo, na hao waliofanya haya madudu kuendelea kuwateua ni ishara kwamba yeye kiongozi anabariki hayo madudu.Kulialia na kutafuta sympathy hakuta msaidia, ni heri akae kimya sio kusema halafu huwa uwezo wa kuchukua hatua. Watanzania sio wajinga.
Mkuu unazijua kazi ya makamu wa rais?
 
Nimemsikiliza sana mama na kwa maelekezo ya mama lile ni agizo inatakiwa TAKUKURU na Jeshi la Polisi wamkamate dpp aliyemaliza muda wake ndugu biswalo, awe chini ya ulinzi huyu mtu aliwaumiza watu wengi sana kupitia ofisi yake.

Huyu mtu DPP alijigeuza Mungu kwenye Ile ofisi hata hizo pesa walizokuwa wanatozwa akina Seth, ili waachiwe yeye ndiye alikuwa kinara, aliweka wafanyabiashara mahabusu kwa kuwasingizia kesi za uhujumu bila sababu ili ajipatie pesa, kama kweli mama umeamua kuisafisha nchi huyu hatakiwi kabisa kuwa uraiani!
 
Unajua kabisa mtu anaiba na una awezo wa kumzuia au kumfanya chochote halafu unakuja kutuambia sisi ili tufanyaje?

Huyu maza ngoja nimtetee Kwa hili , kipindi cha Marehemu gaidi huyu maza hakua na nguvu yeyote ndio maana kuna kipindi alitaka hata kujiuzulu ila alipigwa biti.

Wacha tu nae ateme nyongo.
Ila Kwa mitazamo wangu maza inabidi mambo mengine ya hovyo yaliyofanyika kipindi cha Mwenda zake awe anayafanyia kazi kimyakimya bila kutaarifu umma kwani ni kama analeta taharuki na kuongeza kinyongo Kwa wananchi.

Namshauri wote waliofanikisha madhambi hayo awawajibishe kimya kimya
 
Sioni chochote kikifanyika.

Kwa sisi watu wa Galilaya tunasema YATAPITA.

Wataibua lingine na hili tutalisahau
 
Hawa walikuwa ni wezi halafu wababe, yani wanakuibia na ukijua wamekuibia ukataka kuwauliza wanakutishia na wakati mwingine wanakupiga kabisa.

Huyo Jaji aliteuliwa kwenye hiyo nafasi ili tu atoke kwenye ile nafasi ya DPP aliyokuwa anaitumia kujineemesha, hakuwa na sifa ya kuwa Jaji. Ilimpasa yeye mwenyewe kujipima na kuikataa nafasi ya Ujaji na kujiuzulu nafasi aliyokuwa nayo ya DPP.
 
Leo Januari 31, 2023 Rais Samia amezungumzia suala la Plea Bargain, utaratibu wa Makubaliano ya Kumaliza Kesi kwa Kulipa Fedha kwa Serikali ambao ulitumika wakati wa Utawala wa Hayati Rais Magufuli chini ya DPP Biswalo Mganga .
Alikua sera ya serikali hakufanya peke yake, wengi wanahusika mnyororo ni mrefu, wengi watakamatwa akiwemo IGP, Jaji Mkuu, Raisi aliepita na wasaidizi wake, labda atolewe huyu kama kafara.....
 
Sasa kwa hili la leo, Jaji Biswalo anasubiri nini kuachia nafasi hiyo kuonesha Uwajibikaji? Lakini Pia, Rais Samia anasubiri nini kuunda Tume ya Majaji watatu wanaotakiwa kuchunguza suala hilo na kutoa uamuzi wa nini Rais afanye?
Aswekwe ndani asahaulikie huko
 
Back
Top Bottom