Awamu ya 5 Biswalo Mganga alikuwa Kinara wa Plea Bargain aliyetumia sheria za mfukoni mwake , Pesa alizokusanya hazijulikani ziliko

Erythrocyte

JF-Expert Member
Nov 6, 2012
117,788
218,415
Bado twaendelea na nyuzi za mwezi 3 ambao ni Mwezi wa Mungu

Kama tulivyoandika awali kuhusu lundo la watu kukamatwa na kupewa kesi nzito za Uhujumu uchumi , Baadaye watu hao wakapewa option ya kurudi uraiani ambayo ni kukiri makosa na kulipa kiasi kizito cha fedha ili kufidia uchumi waliouhujumu .

Wengi kutokana na uoga na kuchoshwa kukaa jela wakaamua kukubali jambo hilo bila kujali kama lipo kisheria au ni matakwa ya Wakamataji , wale ambao walikuwa na mzigo mkubwa kwenye akaunti zao ukapigwa chakachua juu kwa juu , wale wenzangu na miye , ikalazimika ndugu zao kujikamua na kuchangishana kwa kuuza hiki na kile , zikiwemo nyumba , mazao na mashamba ili kuwaokoa ndugu zao , wamo hata wauza bia waliokamatwa kwa makosa ya kodi tu lakini wakapewa Uhujumu uchumi (soma ripoti ya CAG hii hapa)

Screenshot_2024-03-20-18-03-06-1.png


Screenshot_2024-03-20-18-00-58-1.png


Pamoja na DPP kuwa Mwanasheria lakini bado alivunja Sheria na wala hakuguswa

Kwenye kampeni hii haramu Biswalo Mganga alishirikiana na wafuatao kwa karibu sana , japo kuna mnyororo mrefu

Screenshot_2024-03-20-17-59-21-1.png


Screenshot_2024-03-20-18-01-51-1.png


Hata hivyo lundo la hela walizokusanya hazikujulikana ziliwekwa kwenye akaunti gani , hii ni kwa mujibu wa serikali mpya iliyoingia madarakani baada ya Magufuli

Sasa ikiwa kama Nchi inaweza kuwa na kikundi cha watu wakaamua kupanga mambo yao kwa kutumia Mahakama zetu na wakavunja sheria , hata kama walikuwa wanazuia uhalifu jambo lao linakosa Uhalali .

Cha kushangaza ni hiki , Pamoja na makosa yote haya , ilikuwaje Rais wa sasa ameendelea kumteua Biswalo kwenye nafasi zingine ? siri hii anaijua mwenyewe .

Screenshot_2024-03-20-18-05-49-1.png




Swali letu ni hili PLEA BARGAIN ilianzishwa kwa faida ya nani na pesa zilizokabidhiwa ziko wapi ?

NITASEMA KWELI DAIMA FITINA KWANGU MWIKO
 
Bado twaendelea na nyuzi za mwezi 3 ambao ni Mwezi wa Mungu

Kama tulivyoandika awali kuhusu lundo la watu kukamatwa na kupewa kesi nzito za Uhujumu uchumi , Baadaye watu hao wakapewa option ya kurudi uraiani ambayo ni kukiri makosa na kulipa kiasi kizito cha fedha ili kufidia uchumi waliouhujumu .

Wengi kutokana na uoga na kuchoshwa kukaa jela wakaamua kukubali jambo hilo bila kujali kama lipo kisheria au ni matakwa ya Wakamataji , ndugu wa Washitakiwa hao wakachangishana kwa kuuza hiki na kile , zikiwemo nyumba , mazao na mashamba ili kuwaokoa ndugu zao , wamo hata wauza bia waliokamatwa kwa makosa ya kodi tu lakini wakapewa Uhujumu uchumi (soma ripoti ya CAG hii hapa)

View attachment 2940270

View attachment 2940315

Pamoja na DPP kuwa Mwanasheria lakini bado alivunja Sheria na wala hakuguswa

Kwenye kampeni hii haramu Biswalo Mganga alishirikiana na wafuatao kwa karibu sana , japo kuna mnyororo mrefu

View attachment 2940283

View attachment 2940280

Hata hivyo lundo la hela walizokusanya hazikujulikana ziliwekwa kwenye akaunti gani , hii ni kwa mujibu wa serikali mpya iliyoingia madarakani baada ya Magufuli

Sasa ikiwa kama Nchi inaweza kuwa na kikundi cha watu wakaamua kupanga mambo yao kwa kutumia Mahakama zetu na wakavunja sheria , hata kama walikuwa wanazuia uhalifu jambo lao linakosa Uhalali .

Cha kushangaza ni hiki , Pamoja na makosa yote haya , ilikuwaje Rais wa sasa ameendelea kumteua Biswalo kwenye nafasi zingine ? siri hii anaijua mwenyewe .

View attachment 2940288



Swali letu ni hili PLEA BARGAIN ilianzishwa kwa faida ya nani na pesa zilizokabidhiwa ziko wapi ?

NITASEMA KWELI DAIMA FITINA KWANGU MWIKO
Mama si karudisha hizi pesa kelele za nini tena
 
Sijaelewa hiyo picha ya CAG kusema masuala ya kikodi sio jinai.

Kutokulipa kodi sio jinai? Kukwepa kulipa kodi sio jinai?

Ni masuala gani yanayohusiana na kodi ambayo sio jinai?
Ngoja wanasheria watusaidie , lakini kuna kudaiwa kodi na kuna kukaidi kulipa kodi , karibu kila Mfanyabiashara anadaiwa kodi , na sidhani kama wamekaidi kulipa , je kudaiwa tu ni jinai ?
 
Back
Top Bottom