SoC03 Kuibuka kwa Taasisi/vikundi vingi vya kukopesha pesa mtandaoni: Je, wananchi wana uelewa? Usalama wa Taarifa Binafsi unazingatiwa?

Stories of Change - 2023 Competition

DON YRN

JF-Expert Member
Jan 14, 2019
474
999
Na DON YRN.
Habari za wakati huu wadau wa JamiiForums?, matumaini yangu tupo salama katika ujenzi wa Taifa letu. Lengo langu kutoa mada hii siyo kuleta uchonganishi au kuchafuliana biashara, hapana, lengo ni kufichua kile kinachoonekana kipo kinyume kwenye jamii.

Kumekuwa na ongezeko kubwa sana la taasisi/vikundi mbalimbali vinavyokopesha fedha kupitia mitandao mbalimbali ya simu hapa nchini Tanzania kama Airtel, Vodacom, Tigo, Halotel, Zantel, n.k. Vikundi/taasisi hivi vimekuwa vikijitangaza kutoa mikopo hii kupitia majukwaa mbalimbali ya kijamii kama facebook, twitter, Instagram, n.k. na muda mwingine vimekuwa vikitumia kujitangaza kupitia baadhi ya vyombo vikubwa vya habari vinavyoaminika kwa umma.

Swali la kujiuliza hapa ni Je, hivi vikundi/taasisi zinatambulika na serikali au hazitambuliki?.

Lengo la kutolewa kwa mikopo huwa ni jema kwa maana ya kumsaidia mhusika/mkopeshwaji palipo na uhitaji wa pesa na mkopeshaji apate faida. Pamoja na yote hayo, hakuna elimu ya kueleweka inayotolewa na hizi taasisi/vikundi kwa wakopaji vilivyoibuka ghafla kabla ya kuchukua mkopo bali elimu hutolewa baada ya mkopaji kuchukua mkopo.

Kwa mfano; katika uchunguzi wangu kwenye hili jambo, niliwahi kuomba mkopo kwenye mojawapo ya taasisi inayokopesha pesa mtandaoni. Niliwapigia kuuliza namna ya kupata mkopo nikajibiwa kuwa tuvuti yao ina maelezo zaidi yanayojitosheleza. Nilifungua wavuti yao nikaambiwa kujaza taarifa zangu muhimu binafsi km Majina yangu matatu(3), Namba ya simu, barua pepe, namba ya kitambulisho cha Taifa(NIDA), mahali ninapoishi pamoja na kupakia picha inayoonesha sura yangu(Passport size). Baada ya hapo nikaandikiwa "OMBA MKOPO", hapo kwenye OMBA MKOPO nilitegemea nitaletewa chaguo la kuomba kiasi ninachohitaji lakini haikuwa hivyo, nilitumiwa ujumbe kwamba nimekopeshwa TSH 4,850 na ninapaswa kulipa TSH 7,750 ndani ya siku saba(7).

Niliwapigia kuwauliza inakuwaje napewa mkopo ambao sijaomba?, nikajibiwa kuwa mpangilio wao wa uombaji mkopo ndo ulivyo na RIBA yao ni 35% (kiasi cha RIBA kilicho kikubwa sana)na zikizidi siku 7 deni litakuwa linaongezeka kwa RIBA ya 5% kila siku. Hii ina maana Elimu au taratibu zilizokamilika za mkopo nilipewa baada ya kupewa mkopo hali ambayo inazua utata na kuhusisha UTAPELI.
Screenshot_20230522_163312_PesaX.jpg
Picha mbalimbali zikionesha namna ya kujisajili kwenye mojawapo ya taasisi ya kukopesha pesa mtandaoni.
Screenshot_20230522_163651_PesaX.jpg

Hali nyingine ni kwamba; Hizi taasisi/vikundi vya kukopesha hela mtandaoni, vinatambulika na taasisi za kiserikali zinazosimamia masuala ya fedha kama wizara ya Fedha, Benki kuu, wizara ya viwanda na biashara, n.k?. Na sheria zinatafsiri vipi kuanzishwa kwa taasisi za kukopesha pesa sana sana kwenye RIBA na muda wa kurejesha?. Kama havitambuliki, ni hatua gani zimechukuliwa maana udhibiti wa mitandao inayotumika kutangazia hizi taasisi iko chini ya usimamizi wa mamlaka ya mawasiliano Tanzania(TCRA)?.
Screenshot_20230522_163521_Permission controller.jpg

Kama vikundi/taasisi hizi za kifedha havitambuliki, taarifa za wananchi/mwananchi mmoja mmoja zinaweza kuwa hatarini kwa maana mwananchi anaweza asielewe taarifa zinazochukuliwa tena mtandaoni zinaenda kutumika kwenye malengo yapi. Hii inarejea mfano wa taarifa nilizozitoa wakati nafanya uchunguzi wangu binafsi kuhusu mikopo ya mtandaoni. Taarifa hizo ni kama Majina yangu Matatu(3), barua pepe, namba ya simu, namba ya kitambulisho cha Taifa(NIDA), Mahali ninapoishi na kupakia picha ya passport size. Hizi taarifa ni muhimu mno maana zinaweza kutumika hata kufanyia UTAPELI/UHALIFU wa kimtandao au kutumika na majasusi wa nje kudukua taarifa muhimu za NCHI maana wananchi wanakuwa hawana uelewa kama wakopeshaji ni watu wema au siyo wema kwa maana mikopo inatolewa bila kuonana bali njia ya mtandao. Mfano, hizi taasisi/vikundi zinatumia programu tumishi(Apps) ambazo ili mkopaji apate mkopo, inamlazimu apakue programu tumishi husika na ajisajili. Hii ni hatari sana sababu watu wengi siku hizi wanatumia simu hata kuhifadhi nyaraka za kiofisi.

Kwa upande wangu na mawazo yangu huenda hivi vikundi/taasisi vimebadili mfumo kutoka kushawishi wananchi kwamba wakiwekeza kiasi fulani cha fedha wanaweza kupata FAIDA baada ya muda fulani na sasa vimekuja na mtindo huu wa kukopesha. Muda mwingine vinatumia hata majina ya watu maarufu kama viongozi, wasanii, n.k.

Kwa ujumla, ni jukumu na wajibu serikali kutoa elimu kwa wananchi wake ili kuendana na mabadiliko ya ukuaji wa teknolojia hasa biashara za mtandaoni ili kuepusha mianya yote ya UTAPELI inayoweza jitokeza. Pia hatua kali za kisheria zinapaswa kuchukuliwa kwa wale wanaopatikana na hatia ya UTAPELI ili kufikia hatua halali ya ujenzi wa nchi yetu pendwa Tanzania.
Screenshot_20230519_175351_Facebook.jpg
Screenshot_20230521_072750_Facebook.jpg
Screenshot_20230521_072907_Facebook.jpg
Screenshot_20230521_084114_Facebook.jpg
Screenshot_20230522_043620_Facebook.jpg
Screenshot_20230522_043954_Facebook.jpg
Screenshot_20230522_044221_Facebook.jpg

Hizi ni baadhi ya picha zinazowakilisha baadhi ya taasisi zinazokopesha fedha kwenye mitandao hasa.
Chanzo: Facebook.
 
Watamzania msiogope Hawa majama matapeli Kama wale tuna kwenye namba hii huwezi mkopesha mtu elfu ishirini Kisha alipe na riba ellfu ishirini na tano ndani ya siku Saba

Kibaya zaidi kipindi Cha marejesho kikaribia unapigiwa sm mteja wetu tumeona tukuongeze kiwango Cha kukopa na siku za marejesho kwaiyo tuambie unaweza kukopa bei gani na mda upi unaweza rudisha ili tukupe mkopo wako ukowambia mda unaoweza kufanya rejesho na kiasi unachotaka wanakwambia sawa fanya rejesho la kwanza ili uweze kukopa hicho kiwango kipya maana mfumo wetu hauwezi kuhudumia Mara mbili ukiwa bado una deni la kwanza basi mteja akifanya rejesho la kwanza tu akitaka kufanya mhamala mpya hapo ndio kituko anakutana nacho akikopa elfu ishirini arudishe elfu 25, ndani ya siku nane kutokana na kupigiwa sm kushawishiwa akarudisha hiyo elfu 25 ndani ya siku sita kwa ahadi atapewa mkopo mpya kwa siku aaliyotaka mteja na kiwango alichotaka mteja sasa mteja akikopa tu akiingia kweye huduma anakuta wamemuongezea elfu kumi tu😂😂😂 Yani akope elfu 30 arudishe elfu 35 kwa siku zile zile nane mteja akipiga sm wamemblock haya ni PESAX wahuni sana dawa yao nini sasa

Mtanzania mwenzangu wewe chukua hiyo pesa arafu usiwallipe sm zaoo pokea jibu sina pesa hata wakutishe vipi usiogope maana ni wahuni so na wewe kuwa mhuni acha wajinga waliwe Ila wewe usikubali
 
Watamzania msiogope Hawa majama matapeli Kama wale tuna kwenye namba hii huwezi mkopesha mtu elfu ishirini Kisha alipe na riba ellfu ishirini na tano ndani ya siku Saba

Kibaya zaidi kipindi Cha marejesho kikaribia unapigiwa sm mteja wetu tumeona tukuongeze kiwango Cha kukopa na siku za marejesho kwaiyo tuambie unaweza kukopa bei gani na mda upi unaweza rudisha ili tukupe mkopo wako ukowambia mda unaoweza kufanya rejesho na kiasi unachotaka wanakwambia sawa fanya rejesho la kwanza ili uweze kukopa hicho kiwango kipya maana mfumo wetu hauwezi kuhudumia Mara mbili ukiwa bado una deni la kwanza basi mteja akifanya rejesho la kwanza tu akitaka kufanya mhamala mpya hapo ndio kituko anakutana nacho akikopa elfu ishirini arudishe elfu 25, ndani ya siku nane kutokana na kupigiwa sm kushawishiwa akarudisha hiyo elfu 25 ndani ya siku sita kwa ahadi atapewa mkopo mpya kwa siku aaliyotaka mteja na kiwango alichotaka mteja sasa mteja akikopa tu akiingia kweye huduma anakuta wamemuongezea elfu kumi tu😂😂😂 Yani akope elfu 30 arudishe elfu 35 kwa siku zile zile nane mteja akipiga sm wamemblock haya ni PESAX wahuni sana dawa yao nini sasa

Mtanzania mwenzangu wewe chukua hiyo pesa arafu usiwallipe sm zaoo pokea jibu sina pesa hata wakutishe vipi usiogope maana ni wahuni so na wewe kuwa mhuni acha wajinga waliwe Ila wewe usikubali na tutakiwasha hapa jamii forum waziri wa FEDHa siku anawasilisha bajeti yake atuambie huu utitiri umetokea wapi maana kmpuni moja in app Kama kumi majina tofauti tofauti Ila ni kampuni ile ile
 
Watamzania msiogope Hawa majama matapeli Kama wale tuna kwenye namba hii huwezi mkopesha mtu elfu ishirini Kisha alipe na riba ellfu ishirini na tano ndani ya siku Saba

Kibaya zaidi kipindi Cha marejesho kikaribia unapigiwa sm mteja wetu tumeona tukuongeze kiwango Cha kukopa na siku za marejesho kwaiyo tuambie unaweza kukopa bei gani na mda upi unaweza rudisha ili tukupe mkopo wako ukowambia mda unaoweza kufanya rejesho na kiasi unachotaka wanakwambia sawa fanya rejesho la kwanza ili uweze kukopa hicho kiwango kipya maana mfumo wetu hauwezi kuhudumia Mara mbili ukiwa bado una deni la kwanza basi mteja akifanya rejesho la kwanza tu akitaka kufanya mhamala mpya hapo ndio kituko anakutana nacho akikopa elfu ishirini arudishe elfu 25, ndani ya siku nane kutokana na kupigiwa sm kushawishiwa akarudisha hiyo elfu 25 ndani ya siku sita kwa ahadi atapewa mkopo mpya kwa siku aaliyotaka mteja na kiwango alichotaka mteja sasa mteja akikopa tu akiingia kweye huduma anakuta wamemuongezea elfu kumi tu😂😂😂 Yani akope elfu 30 arudishe elfu 35 kwa siku zile zile nane mteja akipiga sm wamemblock haya ni PESAX wahuni sana dawa yao nini sasa

Mtanzania mwenzangu wewe chukua hiyo pesa arafu usiwallipe sm zaoo pokea jibu sina pesa hata wakutishe vipi usiogope maana ni wahuni so na wewe kuwa mhuni acha wajinga waliwe Ila wewe usikubali

😮😮😮
 

Attachments

  • Screenshot_20230522_043954_Facebook.jpg
    Screenshot_20230522_043954_Facebook.jpg
    83.5 KB · Views: 64
  • Screenshot_20230522_043620_Facebook.jpg
    Screenshot_20230522_043620_Facebook.jpg
    79.5 KB · Views: 63
  • Screenshot_20230521_084114_Facebook.jpg
    Screenshot_20230521_084114_Facebook.jpg
    74.3 KB · Views: 83
  • Screenshot_20230521_072907_Facebook.jpg
    Screenshot_20230521_072907_Facebook.jpg
    65.6 KB · Views: 51
  • Screenshot_20230521_072750_Facebook.jpg
    Screenshot_20230521_072750_Facebook.jpg
    59.9 KB · Views: 63
  • Screenshot_20230522_044221_Facebook.jpg
    Screenshot_20230522_044221_Facebook.jpg
    63.5 KB · Views: 45
Watamzania msiogope Hawa majama matapeli Kama wale tuna kwenye namba hii huwezi mkopesha mtu elfu ishirini Kisha alipe na riba ellfu ishirini na tano ndani ya siku Saba

Kibaya zaidi kipindi Cha marejesho kikaribia unapigiwa sm mteja wetu tumeona tukuongeze kiwango Cha kukopa na siku za marejesho kwaiyo tuambie unaweza kukopa bei gani na mda upi unaweza rudisha ili tukupe mkopo wako ukowambia mda unaoweza kufanya rejesho na kiasi unachotaka wanakwambia sawa fanya rejesho la kwanza ili uweze kukopa hicho kiwango kipya maana mfumo wetu hauwezi kuhudumia Mara mbili ukiwa bado una deni la kwanza basi mteja akifanya rejesho la kwanza tu akitaka kufanya mhamala mpya hapo ndio kituko anakutana nacho akikopa elfu ishirini arudishe elfu 25, ndani ya siku nane kutokana na kupigiwa sm kushawishiwa akarudisha hiyo elfu 25 ndani ya siku sita kwa ahadi atapewa mkopo mpya kwa siku aaliyotaka mteja na kiwango alichotaka mteja sasa mteja akikopa tu akiingia kweye huduma anakuta wamemuongezea elfu kumi tu😂😂😂 Yani akope elfu 30 arudishe elfu 35 kwa siku zile zile nane mteja akipiga sm wamemblock haya ni PESAX wahuni sana dawa yao nini sasa

Mtanzania mwenzangu wewe chukua hiyo pesa arafu usiwallipe sm zaoo pokea jibu sina pesa hata wakutishe vipi usiogope maana ni wahuni so na wewe kuwa mhuni acha wajinga waliwe Ila wewe usikubali
Ndugu zangu watanzania kopa kuanzia elfu ishirini warudishie riba Yao kubwa ,kopa Tena rudisha riba Yao ya kinyonyaji mpaka kiwango chako kifike laki Tano Kisha usirudishe chochote wala kuogopa yoyote maana wanakiuka misingi ya Sheria ya mikopo.Kopeni ikifika kiasi kikubwa msirudishe hawana uwezo wa kuwafanya chochote watakimbia wenyewe kurudi kwao Kenya.
 
Ndugu zangu watanzania kopa kuanzia elfu ishirini warudishie riba Yao kubwa ,kopa Tena rudisha riba Yao ya kinyonyaji mpaka kiwango chako kifike laki Tano Kisha usirudishe chochote wala kuogopa yoyote maana wanakiuka misingi ya Sheria ya mikopo.Kopeni ikifika kiasi kikubwa msirudishe hawana uwezo wa kuwafanya chochote watakimbia wenyewe kurudi kwao Kenya.
Shida inakuja pale wanapohitaji taarifa muhimu sana za mtu!, lengo ni kutoa mikopo tu au kuna lingine nyuma ya pazia?
 
Shida inakuja pale wanapohitaji taarifa muhimu sana za mtu!, lengo ni kutoa mikopo tu au kuna lingine nyuma ya pazia?
Kiongozi hakuna tasisi imara dunia ya leo ikaitaji number yako ya sm, namba ya kitambulisho na picture vyako Kisha uingilie mifumo yao hakuna wale wababaishaji wanajua dunia hii wajinga hawaishi so wanawaoiga wahu kajisajiri uchukue pesa utulie ununue hata bia nne upoze koo
 
Kiongozi hakuna tasisi imara dunia ya leo ikaitaji number yako ya sm, namba ya kitambulisho na picture vyako Kisha uingilie mifumo yao hakuna wale wababaishaji wanajua dunia hii wajinga hawaishi so wanawaoiga wahu kajisajiri uchukue pesa utulie ununue hata bia nne upoze koo
Duh
 
Binafsi nimeshakumbana na kisa kama hicho kutoka kwa kampuni inayojiita Pesa X.

Niliona tangazo lao mtandaoni nikashawishika kujiunga nao,nikatimiza vigezo vyao vyote walivyo taka kama vile; Majina matatu,kitambulisho cha nida,namba ya nyumba na mahali ninapoishi,picha yangu,wadhamini wawili na namba zao za simu,kazi yangu,na makisio ya mapato yangu kwa mwezi.

Baada ya kukamilisha mlolongo wote huo maajabu ya mwaka yanatokea kwa wao kunitumia Tsh 15,000/ ambayo natakiwa kurejesha Tsh 19,200/ baada ya siku saba!!!.

Binafsi nikajawa na maswali kichwani,je Tsh 15,000 nafanyia biashara gani?,nachoma maandazi au nauza karanga?,mbona kwenye matangazo na promo zao walisema naweza kupata Tsh 300,000/ - 1,000,000/- sasa imekuaje tena?

Basi siku zikaenda na muda wa marejesho ukafika,zikaanza kumwagika simu zisizo na idadi kwangu na kwa wadhamini wangu!!!.

Na deni limepanda hadi kufikia Tsh 22,000/ na vitisho juu kwamba watakuja kwenye makazi yangu kuchukua samani za ndani!!!

Jibu langu hadi muda huu wanipigiapo,ni kwamba nawaomba wanithibitishie kwa nyaraka juu ya usajili wao,maana siwezi kushiriki kwenye mikopo ya batili na ya kinyonyaji kama huu halafu nisijue serikali inapata nini!!

Kiufupi ni wezi na matapeli wa mitandaoni
 
Binafsi nimeshakumbana na kisa kama hicho kutoka kwa kampuni inayojiita Pesa X.

Niliona tangazo lao mtandaoni nikashawishika kujiunga nao,nikatimiza vigezo vyao vyote walivyo taka kama vile; Majina matatu,kitambulisho cha nida,namba ya nyumba na mahali ninapoishi,picha yangu,wadhamini wawili na namba zao za simu,kazi yangu,na makisio ya mapato yangu kwa mwezi.

Baada ya kukamilisha mlolongo wote huo maajabu ya mwaka yanatokea kwa wao kunitumia Tsh 15,000/ ambayo natakiwa kurejesha Tsh 19,200/ baada ya siku saba!!!.

Binafsi nikajawa na maswali kichwani,je Tsh 15,000 nafanyia biashara gani?,nachoma maandazi au nauza karanga?,mbona kwenye matangazo na promo zao walisema naweza kupata Tsh 300,000/ - 1,000,000/- sasa imekuaje tena?

Basi siku zikaenda na muda wa marejesho ukafika,zikaanza kumwagika simu zisizo na idadi kwangu na kwa wadhamini wangu!!!.

Na deni limepanda hadi kufikia Tsh 22,000/ na vitisho juu kwamba watakuja kwenye makazi yangu kuchukua samani za ndani!!!

Jibu langu hadi muda huu wanipigiapo,ni kwamba nawaomba wanithibitishie kwa nyaraka juu ya usajili wao,maana siwezi kushiriki kwenye mikopo ya batili na ya kinyonyaji kama huu halafu nisijue serikali inapata nini!!

Kiufupi ni wezi na matapeli wa mitandaoni
Pole sana mkuu
 
Mimi wamenipa 20000 eti niludishe 25000 sikuludisha mpaka leo nawaambia riba yenu ya wizi kama wanataka niwatumie pesa yao upande wa namba za Jamaa niliweka namba zangu za mitandao mingine kwanza mfumo wao wa kijinga
 
Back
Top Bottom