DOKEZO Taarifa Binafsi zinakusanywa na "Kampuni za Mikopo Mtandaoni" ni Hatarishi kwa Faragha ya Mtu

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'

Makamura

JF-Expert Member
May 19, 2022
356
550
Siku hizi kumekuwa na Kampuni nyingi za Mikopo Online kama PesaX, Twiga Loan, Mloan, Cash X.

Na watu bila kuwa makini mtakuja jikuta mnaingia matatizoni kutoka na taarifa zinazokusanywa na Kampuni hizi.

Nimejaribu kadhaa na hakuna ya afadhali, unakuta inakusanya taarifa hizi:-
  • SMS - yan wanaweza kusoma sms zote zilizoingia katika namba yako uliyosajilia, hii ikujumuisha sms za miamala, mapenz, siri za familia na kadharika je unahisi upo salama?
  • CONTACTS - wanaweza kuona majina na namba zote ulizosave kwenye simu yako unahisi watu wako watakuwa salama?
  • CAMERA - hii wanaweza kurekodi au kupiga picha bila wewe kujua na hapa ndo linapokuja swala zima la connections kuvuja
  • STORAGE - wanaweza ku-access picha, video, na files zote zilizoseviwa kwenye simu yako, je unahisi wataacha kushare na wwngine siri zako?
  • APPS - wanaweza kuona app zote kwenye simu na kuzifikia, hii ikijumlisha WhatsApp, IG, app za kutunz afaragha zako n.k
  • TAARIFA BINAFSI - kama Vyeti, elimu, kazi, mahala pa kuishi, urefu, picha zako, unadhan utakuwa salama mtu kuwa na taarifa zako zote..
Ikatokea mfanyakaz akatoka hapo tayar anajua siri za wengi, na ni rahisi kuzitumia kuscam watu mitandaoni
Watanzania tuweni makini na maamuzi yetu, hizi ndo huchangia watu kudhalilika mitandaoni, na kutoa siri za watu kama history za bank, miamala, chati za siri na faragha za watu, je unahisi utakuwa salama wewe na uwapendao?.

Mamlaka ishughulikie hawa watu wanapata wapi dhamana ya kukusanya taarifa za watu kama Sensa ya Kidigitali?

Mdau weka screen ya App ya Mikopo tuone taarifa wanazokusanya kwenye Simu yako

Screenshot_20240319-183509.jpg
 
dawa yao una nunua ile laini za tuma namba hii za matapeli unaombea mkopo alafu contact unasave na picha unaweka namba za serikali,polisi, mawaziri na wakubwa tiss binafsi na kwenye storage weka picha za viongozi paspport size na mapolisi.

wakikudai niite babu wa shetani
 
dawa yao una nunua ile laini za tuma namba hii za matapeli unaombea mkopo alafu contact unasave na picha unaweka namba za serikali,polisi,mawaziri na wakubwa tiss binafsi na kwenye storage weka picha za viongozi paspport size na mapolisi.
wakikudai niite babu wa shetani
Shida kwenye hizo app wanakusanya taarifa hata ambazo hujawapa,labda hio simu uwe unaitumia kwa hilo jambo tu,, hizi app naona ni za kupeleleza sema wanawaingiza mtegoni watu kwa mikopo ila wanakusanya taarifa nyingi sana sensitive na wanajua waTanzania wengi sio watu wakusoma ,kikubwa yeye kaambiwa ni mkopo anapata bas hajiumizi kichwa
 
dawa yao una nunua ile laini za tuma namba hii za matapeli unaombea mkopo alafu contact unasave na picha unaweka namba za serikali,polisi,mawaziri na wakubwa tiss binafsi na kwenye storage weka picha za viongozi paspport size na mapolisi.
wakikudai niite babu wa shetani
Kijana Mhuni sana wewe 🤣🤣🤣
 
Kiwango cha juu wanakopesha kiasi gani? Pamoja na huuu ujinga wao wooote, mimi nikiamua leo nikope na wasiweze kuni-trace naweza, na fedha hawatazipata kamwe.
Ndio inawezekana ila Kunaraia hawajui kabisa hili swala, hatusomagi kabisa Privacy & Policy kwenye hizi app tunazo Install kwenye simu zetu
 
Shida kwenye hizo app wanakusanya taarifa hata ambazo hujawapa,labda hio simu uwe unaitumia kwa hilo jambo tu,, hizi app naona ni za kupeleleza sema wanawaingiza mtegoni watu kwa mikopo ila wanakusanya taarifa nyingi sana sensitive na wanajua waTanzania wengi sio watu wakusoma ,kikubwa yeye kaambiwa ni mkopo anapata bas hajiumizi kichwa
Hii Point ndugu.. wanakusanya taarifa nyingi sana bila mtumiaji kujua
 
Back
Top Bottom