Kesi ya Babu Seya inaniumiza sana kichwa

Kesi ya Babu Seya inaniumiza sana kichwa

Katika vitu ambavyo vinanipa sana shida katika ubongo wangu ni ukweli kuhusu kesi ya Babu Seya, nakuwa natamani nijue ni kweli yeye na familia yake walihusika kulawiti watoto au ni kesi ya mchongo kutoka kwa mtu mkubwa..

Ni nani ambaye anaweza kunitatulia kitendawili hiki nafikiri hakuna mwenye jibu la uhakika. Nikifika mbinguni swali la kwanza nitamuuliza sir God anifunulie jambo hili.
Ila hii kesi hata mimi huwa inaniumiza kichwa mpaka kesho!
Cha kushangaza waliohukumiwa wenyewe, bado wapo! Hao watoto waliofanyiwa hicho kitendo (huenda wakawepo)!! Sasa inakuwaje tunashindwa kuupata ukweli!!

Na ilikuwaje wanasiasa wakaingilia kati kutaka kumtoa!! Alianza mgombea wa Urais wa UKAWA 2015 Mh. Edward Lowassa. Na Magufuli alipoingia madarakani, akawatoa kwa kutumia mamlaka yake!!


Kuna siri gani imejificha kwenye ile kesi? Mbona kuna wafungwa wengi tu wa ubakaji/ulawiti magerezani, lakini hawajawahi kupata msamaha wa Rais!!!
 
Kikwete alihusika,kwa nini mnapepesa macho?
Babu Seya na watoto wake walihukumiwa kifungo cha maisha mwaka 2004 kama sijakosea! Kipindi hicho Kikwete alikuwa ni Waziri wa Mambo ya Nje bila shaka, huku BM akiwa ndiyo Rais wa JMT!!

Tupe ufafanuzi namna alivyohusika, ili tusipepese hayo macho.
 
Ujasusi...halafu tena kuna ushahidi ?....umejichanganya

Kama ushahidi wa kutosha ulikuwepo hoja ya kuwa alifungwa sababu ni jasusi haina nguvu tena
Maneno yaliyosemwa ni mengi na mimi sija sema nime prove chochote nilichosikia
 
Maneno yaliyosemwa ni mengi na mimi sija sema nime prove chochote nilichosikia

..Babu Seya alitetewa na mawakili wazoefu wabobezi.

..alishindwa kesi ktk hatua zote mpaka Mahakama ya Rufani ya Tanzania.

..pia alikwenda Mahakama ya Afrika Mashariki huko nako alishindwa.

..nimeamua kuziamini Mahakama badala ya maneno ya mitaani.
 
..Babu Seya alitetewa na mawakili wazoefu wabobezi.

..alishindwa kesi ktk hatua zote mpaka Mahakama ya Rufani ya Tanzania.

..pia alikwenda Mahakama ya Afrika Mashariki huko nako alishindwa.

..nimeamua kuziamini Mahakama badala ya maneno ya mitaani.
Sawa mkuu. Ndo maana pia pale juu nilisema upande wa mahakama pia nilisikia kuwa kuna ushahidi wa video.
 
Wewe ni mjinga
Ile hukumu ya kisiasa ndio maana kuna jaji alienda kuhojiwa ili kufukia uongo
Usikimbilie sana kuita watu wajinga!

Unajua maana ya kesi ya kisiasa? Kwani Babu Seya alikuwa ni mwanasiasa? Unaiitaje ya kisiasa ilihali babu seya alikuwa hagombei cheo chochote cha siasa na wala hakuwa tishio kwa wanasiasa?

Wengi mnaropoka maneno ya vijiweni hata hamkufuatilia hiyo kesi. Hukumu zake zipo pamoja na rufaa zake lakini hamuwezi hata kusoma mnakariri upuuzi tu.

Ile kesi ni halali huyo Mwanamziki wenu alibaka. Walivyokuwa wanatoa ushahidi wale watoto, ukisikiliza mtiririko wa maelezo pamoja na 'emotions' zao kwenye maelezo utagundua kuwa walieleza ukweli..

Ni ngumu sana kuwakaririsha uwongo watoto wote wale halafu wasipishane maelezo.
 
Namfaham dada mmoja alikuwa anafundisha Mugabe primary school ni kweli watoto waliingiliwa na familia ya seya, unajua uchawi na mazindiko ndio yaliwalazimisha kuwaingilia.
Issue ya Salma ni uongo wa wazi, na Ingekuwa kweli wangepotezwa bila kesi
Inauma sana nikiwa kama mzazi
 
Tupende kusoma na kufanya tafiti watanzania.
Case ya Babu Seya@ Nguza Viking ina nakala nne za hukumu.
1. Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.
2. High Court of Tanzania Dar es Salaam
3. Court of Appeal of Tanzania
4. Review of court of appeal
Hapo utapata jibu kweli si kweli
Kangaroo Courts haziaminiki kabisa.
Ukweli na Uhalisia kuhusu sakata hili ni tofauti kabisa na yale yaliyopo kwenye rekodi za Mahakama.
Mungu aendelee kuilinda familia ya Babu Seya, dhuluma walizofanyiwa na Wadhalimu hapa duniani Malipo yake watalipwa na Mungu pekee.
 
Wale itakuwa walitenda huo uchafu. Na pamoja na kutolewa ndani na JPM ili kufurahisha jumuiya lakini laana imeendelea kuwatafuna na nyota yao kimuziki imegona kabisa kuwaka tena.
Wale wachachfu sana.

Yaani walishindwa kuchukua maraya wa Sinza wakaanza kuwinda watoto wa miaka 5
 
Kangaroo Courts haziaminiki kabisa.
Ukweli na Uhalisia kuhusu sakata hili ni tofauti kabisa na yale yaliyopo kwenye rekodi za Mahakama.
Mungu aendelee kuilinda familia ya Babu Seya, dhuluma walizofanyiwa na Wadhalimu hapa duniani Malipo yake watalipwa na Mungu pekee.
Ww naona huna uchungu w mtoto
 
Wale wachachfu sana.

Yaani walishindwa kuchukua maraya wa Sinza wakaanza kuwinda watoto wa miaka 5
Ww naona huna uchungu w mtoto
Usifikiri kwamba Watu wengine wote hapa mtandaoni hawana akili timamu sawa sawa kama ulivyo wewe.

Hivi unaamini kuwa ni KWELI mtoto Mdogo mwenye umri wa miaka mitano alawitiwe na Wanaume watatu watu wazima wenye umri wa kati ya miaka 18 hadi 50 Halafu mtoto huyo aendelee kubaki hai??? Hii inawezekana vipi????
 
Kesi ya Mchongo ile, nyuma ya pazia alikuwa anakula mke wa kiongozi mkubwa kwenye ule utawala. Ila hizo ni stori za vijiweni
Tanzania hakuna siri hata kidogo, usipuuze sana story za vijiweni kwani wanaotoa hizo siri ni hao hao watu wa usalama wenyewe. Utakuta kiongozi ana afya mbovu na gonjwa lake linajulikana na usalama lakini mtaani wanajuwa.
 
Back
Top Bottom