A
Anonymous
Guest
Ni muda sasa kumekuwepo na hili wimbi la watu wanaojiita kamchape kiboko ya kutoa uchawi katika wilaya ya kasulu.
Mwanzoni Serikali kupitia jeshi la polisi walitoa maonyo kuhusu hawa watu lakini wananchi wengi waliyapuuza.
Kinachotokea sasa wanadhalilisha watu, wanatengeneza chuki dhidi ya wanajamii kupitia ramli yao chonganishi, Wanadhulumu watu pesa zao kidogo kwa ahadi watawasafishia nyumba zao zisiwe na uchawi, wanasambaza magonjwa ya zinaa ikiwemo kaswende na gono.
Kinachotokea katika kata ya Nyakitonto
Watu wanadhalilishwa, wanaibiwa pesa zao ,ndoa zinavunjika, maelewano katika familia yanapotea, raia wasio na hatia wanapigwa, watu wanavunjiwa nyumba zao.
Askari polisi kama walinzi wa usalama wako kimya kuhusu hali hii. Juzi kuna raia asiye na hatia kutokea Kitema kapigwa manusura ya kufa, jana mwananchi asiye na hatia kidogo avunjiwe nyumba yake.
Jeshi la Polisi liko wapi kupinga dhulma hii na uonevu huu au na wenyewe ni sehemu ya kamchape?
Waziri wa Mambo ya Ndani, sikiliza kilio cha hawa wanachi wasio na hatia. Kinachopaliliwa sasa hivi ipo siku kitatoa matunda na matunda hayo itakua ngumu kuyateketekeza.
RPC Kigoma angalia suala hili ni jipu linaloiva litakua kidonda ndugu siku moja. OCD Kasulu umewatelekeza raia wema ambao kila siku wanakupa ushirikiano kudhibiti uhalifu
Mwanzoni Serikali kupitia jeshi la polisi walitoa maonyo kuhusu hawa watu lakini wananchi wengi waliyapuuza.
Kinachotokea sasa wanadhalilisha watu, wanatengeneza chuki dhidi ya wanajamii kupitia ramli yao chonganishi, Wanadhulumu watu pesa zao kidogo kwa ahadi watawasafishia nyumba zao zisiwe na uchawi, wanasambaza magonjwa ya zinaa ikiwemo kaswende na gono.
Kinachotokea katika kata ya Nyakitonto
Watu wanadhalilishwa, wanaibiwa pesa zao ,ndoa zinavunjika, maelewano katika familia yanapotea, raia wasio na hatia wanapigwa, watu wanavunjiwa nyumba zao.
Askari polisi kama walinzi wa usalama wako kimya kuhusu hali hii. Juzi kuna raia asiye na hatia kutokea Kitema kapigwa manusura ya kufa, jana mwananchi asiye na hatia kidogo avunjiwe nyumba yake.
Jeshi la Polisi liko wapi kupinga dhulma hii na uonevu huu au na wenyewe ni sehemu ya kamchape?
Waziri wa Mambo ya Ndani, sikiliza kilio cha hawa wanachi wasio na hatia. Kinachopaliliwa sasa hivi ipo siku kitatoa matunda na matunda hayo itakua ngumu kuyateketekeza.
RPC Kigoma angalia suala hili ni jipu linaloiva litakua kidonda ndugu siku moja. OCD Kasulu umewatelekeza raia wema ambao kila siku wanakupa ushirikiano kudhibiti uhalifu