Kafulila,Tibaijuka live Star TV

Kafulila,Tibaijuka live Star TV

Kafulila anazo documents za sakata la ESCROW ACCOUNT kwa kuwa yeye ndiye aliyeleta hoja hiyo bungeni. Anayetakiwa kuzijibu hizo documents za Kafulila ni mtu mwenye documents kama hizo kutoka Wizara au Idara husika, mfano Wizara ya Nishati na Madini, Wizara ya Fedha, Ofisi ya Mwanasheria Mkuu, hao ndio wenye uwezo wa kuzungumzia au kujibu kuhusu documents za Kafulila.

Sawa! Lakini kwa mtu ambaye ni prof., tulitegemea aongee kiprofesa, na awe na uwezo wa kujicontrol, angeweza jieleza vizuri tu na watu wangeelewa kutokana na majibu yake ya kiprofesa licha ya kwamba hii si fani yake. Hapo ni Prof. Kapanic na kashindwa hata kuongea kama msomi. Hili nalo lilihitaji awe na uelewa wa mambo ya nishati? Okey, na je anapoulizwa swali kuhusu wahisani kusimamisha misaada, hilo jibu alilotoa mbona la shule ya msingi??
 
Tibaijuka hajui chochote yule,yeye ni waziri wa ardhi,kafulila angemtafuta hata ngeleja ndo waweke nae mechi.
hawa star tv nao

mama yenu ni mtumishi wa umma na ametumiwa fedha nyingi zilizopatikana kwa wizi na kukwepa kodi.
pia hii sio mechi bali ni mahojiano baina ya viongozi wawili wa umma.
 
Sidhani kama ni huyu FF, Prof. Hana elements za pwani, pia kaonyesha kuwa hawezi kujielezea na kugeuza uwongo kuwa kweli, FF ni bingwa wa kutetea hoja hata kama ni pumba asilimia 1000000. Ni mmama wa kuhororoja mpaka usiku saa saba, hana mme na ni mdini aliyepitiliza. Kama kweli ni huyu FF, basi ni actor mzuri sana wa kuvaa uhusika.


Mwenyee akiambiwa anajiona ni mwelevu kuliko yeyote katika jamvi
 
Prof Anna Tibaijuka ni waziri wa Ardhi ........hawezi kuzungumzia habari za IPTL ......apo ni kumlazimisha kuzungumza mambo asiyofahamu ..........mijadala lazima iwe na uwiano ..........

....Lakikini kupokea mgao kutoka IPTL anaweza......
 
Upuuzi tulioupokea kwa mikono miwili Waafrika ni ujinga unaoitwa Utawala Bora! Waafrika kama mazuzu, tukaupokea mfumo na kuanza kuupigia vigelegele bila wananchi wa kawaida kujiuliza kwamba inakuaje viongozi wetu wanaupiga sana upatu mfumo wa utawala bora wakati historia inaonesha wamekuwa ni wapinzani wa mifumo ya kimagharibi inayoletwa Afrika!

Waafrika wananchi tumefanya kosa kubwa sana kushadadia mfumo huu... huwezi kuwa na mfumo wa utawala bora kwenye jamii iliyojaa uovu... matokeo yake ndo haya hapa... tuatendelea kupiga keleke hapa but at the end of story no one will prove (utawala wa sheria... msingi wa utawala bora) beyond reasonable doubt kwamba Anna Tibaijuka amekula mlungula hata kama ni kweli amekula mlungula!!!

I believe this is a misconception. Tulipokea "mfumo wa utawala bora" kutoka wapi? Utawala bora ni "mfumo wa kimagharibi"? Kwamba ni kosa kwa kiongozi wa umma kupokea kickbacks kutoka kwa wafanyabiashara nchini Hispania au Marekani lakini ni sawasawa hapa Tanzania? And what is the alternative to good governance?

Wakati wa utawala wa Mwl. Nyerere, ilikuwa ni mwiko kwa kiongozi wa serikali kuwa mfanyabiashara. Lengo ni kuondoa "conflict of interests" na kuchochea utawala bora. Je, Mwl. Nyerere alipokea miiko hiyo kutoka nchi za Magharibi? Rasimu ya Katiba iliyopendekezwa na Tume ya Warioba imezungumzia mambo kama kiongozi kuwa na account nje ya nchi au waziri kuwa mbunge. Lengo likiwa kuweka mazingira yatakayochochea utawala bora. Je, hatupaswi kufanya hivyo kwa kuwa tutaonekana tumepokea "mifumo ya kimagharibi kama mazuzu"?

In fact, utawala bora is not about copying stuff from the West. It is about protecting basic human rights everywhere in the world. Nyerere alisema ili nchi iweze kusonga mbele, tunahitaji watu, ardhi, siasa safi,na uongozi bora. Kwa kufanya hivyo, hakupokea "mifumo ya kimagharibi kama zuzu".

Na utawala bora/maadili hauhitaji "proof beyond reasonable doubt". Ukishakuwa implicated, unapaswa kuwajibika na hatua nyingine kufuata baadaye.
 
Masikini unajua wamemwita Mama wa watu bila kumwambia kuwa na Kafulila atakuja!!
Hhahaha! Dah STAR TV noma sana!

Halafu wa washe AC, mama wa watu anazidi kutoa jasho tu halafu kashkaji kametuliaaaa!
Aibu tupu
 
huyo mama alikuwa anatetemeka na kigugumizi mpaka mtoto wangu wa darasa la sita akaniuliza huyo mama ndo Mwizi wa 1.6 billion:confused2:
 
Limama lina sweat vibaya kwan anabanwa na kashikaji,kajamaa kapo deep vibaya,eti limama linasema shule yake haifanyi biashara!,wizi mtupu!
Haifanyi biashara wakati anachaji karo milioni 3.5 huyu mama naona amechizi au anataka kutufanya wa Tanzania wajinga
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom