Kafulila,Tibaijuka live Star TV

Prof Anna Tibaijuka ni waziri wa Ardhi ........hawezi kuzungumzia habari za IPTL ......apo ni kumlazimisha kuzungumza mambo asiyofahamu ..........mijadala lazima iwe na uwiano ..........
 
Huyu mama ana temper za ajabu yani hawezi kujenga hoja zaidi yakupanic yani alikuwa anajichanganya changanya
Unajua ni vigumu kujenga hoja kwenye uongo! Yani ukibanwa na una hatia ni ngumu sana kutokupanic, hasa kama jamaa anae ku accuse unamdharau.

Hujawahi kuzuiliwa na ka mlinzi uchwara tu kuingia sehemu ukaanza kupanic. Pale sababu unajua kale ka mlinzi kana haki ya kukuzuia ila unakadharau sababu unahisi hakana status ya kukuzuia!

Hivyo hivyo kwa AT, anahisi haka katumbili hakana haki ya kuni accuse wakati nilianza siasa kakiwa kanajinyea tu. Hehehehe. Hence hasira!
 
Nimemuelewa kiundani mno Kafulila kwenye hii issue ya Escrow.
 
Kafulila anazo documents za sakata la ESCROW ACCOUNT kwa kuwa yeye ndiye aliyeleta hoja hiyo bungeni. Anayetakiwa kuzijibu hizo documents za Kafulila ni mtu mwenye documents kama hizo kutoka Wizara au Idara husika, mfano Wizara ya Nishati na Madini, Wizara ya Fedha, Ofisi ya Mwanasheria Mkuu, hao ndio wenye uwezo wa kuzungumzia au kujibu kuhusu documents za Kafulila.
STAR TV hapo walichemsha
 
Maelezo yako marefu yanavunjwa na maneno machache sana,''fedha za escrow hazikua za umma".

Kama hazikua za umma kwanini walifuata mchakato WA kiserikali kuzi draw ukiwa Ni pamoja Na Katibu WA rais kuamtaka mwanasheria mkuu kijiridhisha kabla ya kulipwa? Mnahangaika lakini ndio hivyo pesa mmeshazipiga. Tutaonana mwakani kwenye uchaguzi mkuu.
 
Wakuu hali ni tete sana hapa nchini, kwa watu wenye akili timamu na uwezo wa kufikiri vizuri ndo tunaojua au kuona utete huo.
 
Maelezo yako marefu yanavunjwa na maneno machache sana,''fedha za escrow hazikua za umma".

Misingi ya utawala bora inatufundisha kuwa kiongozi wa umma kupokea donations au kickbacks kutoka kwa wafanyabiashara tena wenye mikataba ya kibiashara na serikali ni TATIZO. Hili halihitaji mjadala na Tibaijuka anafahamu na ndio maana unaona anajisikia vibaya. Na hii haijalishi kama pesa zilikuwa escrow account, za umma au si za umma. Hoja ya msingi ni uadilifu. Je, unajua ni kwa nini Rugemalira aliamua kuchangia Barbro na akaacha shule nyingine za sekondari Mkoani Kagera pengine zenye mahitaji zaidi? Au utasema hizi shule hazikuwasilisha maombi?
 
Back
Top Bottom