Juu ya OIC na Mahakama ya Kadhi

Juu ya OIC na Mahakama ya Kadhi

Kuhani,
Mkuu Kuhani na wengine wote, kwanza tulitazame swala hili kama lilivyowakilishwa Bungeni. Swala hili limeanza toka miaka 10 na upuuzi uliopita, Zanzibar walipotaka kujiunga..

Kikatiba haikuwezekana kwa sababu Zanzibar sio nchi na swala hili lilikuwa la Muungano hivyo ilibidi uamuzi utolewe ktk bunge la Muungano mahala ambapo limekutana na Utata mkubwa.
Kwa hiyo, hoja bado haijabadilika zaidi isipokuwa ni sisi wananchi tumeshindwa kuelewa swali, kama tanzania inaweza kujiunga na OIC kwa sababu ya kikatiba ambayo inaikataza Zanzibar kujiunga kama nchi.

Kama utakumbuka hata mimi nilipinga vikali Zanzibar kujiunga na OIC kama nchi na hivyo kuwataka swala hili lifikishwe bunge la Muungano ambalo kusema kweli yawezekana Katiba haijitoshelezi.

Ni katiba hiyo hiyo tumeshindwa kutambua kwamba WaZanzibar ni distinct society ambayo imeingia ktk ndoa hii ya Muungano wakiwa na culture zao. Ni katiba hiyo hiyo imeshindwa kutambua kwamba Zanzibar ni sovereign country wakati Tanganyika isingekuwa Tanzania bila Muungano huo. Tanganyika iliondokewa nchi kama Rwanda na Burundi lakini bado tulibakia Tanganyika kwa sababu ile ilikuwa kama mikoa tu, hivyo hata leo tunaweza kuvunja mikoa lakini bado Tanzania ikasimamisha jina lake lakini sivyo kama Zanzibar itaondoka...
Nilichokuwa nikitazama mimi ni haki ya kimsingi ya waislaam ambao wanatengeneza asilimia 99 ya wananchi wa Zanzibar. Hii ndio chulture waliyokuja nayo (Uislaam) ktk Muungano wetu na hatuwezi kuipuuza kwa sababu tu sisi bara tuna dini nyingi na tofauti.
Ndio maana nikatumia mifano mingi ya ndoa kama nchi mbili na hata ndugu kama kigezo cha wananchi wa pande hizi mbili ili kutoa mawazo yangu kwa sababu Muungano wetu ni sawa na ndoa ama udugu wa kaka na dada.

Kuna watu humu wanafikiria kwamba mimi nazungumza kama Muislaam ama natoa hoja zangu kwa sababu ni muislaam, wanafanya makosa ya wazi kabisa kwani hata kama ningekuwa mkristu ningependekeza Tanzania kujiunga na OIC kwa sababu ya Zanzibar.
Hata kama Zanzibar ingekuwa na asilimia 99 ya Wakristu na wakataka kujiunga na baraza lolote la Kikristu ningeunga mkono isipokuwa tu kama wangetaka kutoa maamuzi wao wenyewe bila kuihusisha Bara wakati wanatumia bendera ya Taifa ningepinga. Kwa hiyo utaona kwamba sina upande, lakini waulize wengi humu maswali hayo watakuwa na majibu tofauti..

Tatizo jingine lililojitokeza ni pale tunapotaka kuziangalia faida za Tanzania kujiunga na OIC.. wakuu wangu hili sio swala letu, kama mimi Muislaam nimefunga ndoa na Mkristu inabidi nikubali yanayokuja na Ukristu.. isipokuwa hoja yoyote inayohusu nyumba yetu ni lazima nihusishwe kama mume ktk maamuzi..

Kwa hiyo wakuu, swala bado lipo pale pale na pengine tunajichanganya sisi wenyewe kufikiria kwamba swala hili ni la Bara maadam limekuja ktk bunge la Muungano..!..Zaidi ya yote hayo kuna mambo mengi sana Bara tunawaburuza Zanzibar tukitumia jina na bendera ya Taifa bila wao kuhusishwa wala kupata hata mapato ya Ubalozi tuliotumia..

Kwa hiyo jamani kuwanyima waislaam ama niseme Zanzibar haki yao ya kimsingi ambayo ni moja ya culture yao waliyoingia nayo ktk Muungano kusema kweli tutafanya Udikteta. Na sasa hivi kuna hatari kubwa sana maadui wa Muungano na pengine hao fundamentalist wakaitumia hoja kama hii kubomoa kile mwalimu alikijenga kwa miaka 20 na upuuzi..bahati mbaya ni kuwa fundamentalist toka upande wa pili (Ukristu) ndio wanaoendesha hoja hii ktk Upinzani hali Zanzibar leo wameweza kufungua hata mipaka yao wa Wakristu kufungua makanisa ndani ya nchi yao.

Mwisho, mimi Mkandara pamoja na kuwa Muislaam sintakubali OIC kujenga sheria za Bara ama serikali nzima ya Muungano. Na sidhani kama inawezekana kwa sababu zipo nchi kibao zilizoungana zina toifauti kama zetu na wameweza kuishi kwa amni maadam unafahamu mipaka ya sheria hizo..

Kwa hiyo waungwana swali hapa halijapinda wala kugeuzwa kuwa swala la Tanzania nzima (nilivyoelewa mimi) isipokuwa majibu yake yatatoka kwa mawasilino ya sehemu zote mbili (bungeni) na muhimu zaidi ni sisi kutazama kujiunga huko kutaleta madhara gani Bara!.. Hizo faida wakuu wangu sio kazi yetu hata kidogo, unless tuna hakika kuwa Mwanamke/ mwanaume huyu anataka ku cheat!..

Ahsante sana Mheshimiwa Mukandara. Naona umeeleza kabisa yanayojiri. Pamoja na hayo kwa kujalizia tu. OIC wanaihitaji Zanzibar hivi sasa kujiendeleza kiuchumi. Kuna investments kutoka Vyombo (mabenki) yanayofungamana na OIC na Investors wanaofungamana na vyombo hivyo amabayo hayawezi ku-materialise bila ya Zanzibar kujiunga na OIC. Nayo basi kwa sababu ya Muungano haiwezi kujiunga ila ipitie kwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Enyi ndugu zetu wa Bara- Please do the needfull- Wacha Jamhuri iingie kuiwezesha Zanzibar kunufaika. Zanzibar imeyakubalia mangapi yenye maslahi na Tanganyika yafanyike kwa Jina na nguvu za Jamhuri ya Muungano. Nasema tena Thank you Mheshimiwa Mukandara for the post.
 
Tatizo lliloibuka karibuni la OIC lilitokana na uwongo wa baadhi ya waislamu ambao walikuwa wakiwaibia wafadhili wa nchi za kiislamu zilizomo katika OIC.
Hizi ni moja ya taarifa nilizookota jalalani waweza ziamini au kuzitupilia mbali.

Mjadala wa kuingia OIC ulianza hivi:

Enzi za Raisi Nyerere sensa ilikuwa ikisema Wakristo walikuwa wengi kuliko waislamu.Baadhi ya Matapeli wa kidini wa kiislamu wakaanzisha mradi wa mihadhara kwa kusingizia kuwageuza wakristo waingie Uislamu wakati Raisi Mwinyi alipoingia madarakani.

Kila mhadhara uliokuwa ukifanyika wakawa wanapeleka taarifa za kupika kuonyesha kuwa idadi ya wakristo wanaosilimu kuingia uislamu ni wengi hivyo pesa zinatakiwa kuwasaidia na kuwajengea misikiti inayolingana na idadi ya hao waisilamu hwa waliosilimu.Taarifa hizo kila zikienda misaada ya ujenzi wa misikiti,madrasa n.k ikawa inamiminika kote Zanzibar na Tanzania bara.

Misikiti ikajengwa mingi mno mfano Zanzibar kila hatua chache unakuta msikiti na upande wa Tanzania bara wakajenga mingi mno ambayo ukisafiri barabarani waweza iona hata maporini lakini hata haina watu wa kuisali na waliweka barabarani makusudi ili wafadhili waliowatapeli wakipita waione waende na picha kuwa uislamu uko kila sehemu hadi maporini wakati si kweli.

Sasa taarifa za uongo zilizokuwa zikipelekwa zikionyesha wakristo wengi kuslimu kuingia uislamu zilipoenda ikaja kuonekana kuwa ukijumlisha taarifa hizo na idadi za watu Tanzania ilionyesha waislamu sasa ni wengi kuliko wakristo nchini Tanzania kutokana na hizo taarifa za kupika walizopika ili wapate misaada waile.

Sasa taarifa zilipofikia kuonyesha kuwa waislamu ni wengi kuliko wakristo basi waislamu wenzao wakawabana kule wakawaambia kama ninyi ndio wengi ni kwa nini basi msijiunge na OIC na kwa nini msiwe na kadhi wa kiislamu wa kuwaamulia mambo yenu kiislamu? Wakawabana barabara.

Walipowabana ndipo wakaanza kuhangaika kujaribu kuingiza suala la kadhi na OIC kuanzia kipindi cha Mwinyi.

Kipindi kile kukawa na Sensa ya kuhesabu watu.Sensa zote kwa kawaida ilikuwa wakihesabu watu wanahesabu watu wakiweka na vigezo vya kujua watu wa dini fulani wako kiasi gani.Wakristo ni wangapi,waislamu,wapagani n.k.
Wakapigania kufa na kupona kuwa Sensa ikifanyika watu wasihesabiwe kwa dini wakaogopa siri itafichuka ikitokea Sensa kusema Wakristo ni wengi kuliko wapagani.Wakafuta haraka kipengele cha kuhesabu watu kwa kuuliza dini zao.
Lakini masheikh na waumini wakaendelea kuimba wimbo ule ule wa kusema Waislamu ni wengi kuliko wakristo misikitini,kwa wafadhili n.k

Kama usemi usemavyo njia ya mwongo ni fupi .Kukwama kwa suala OIC na kadhi kutawaweka pabaya matapeli fulani wanaotumia uislamu kutapeli wafadhili Uarabuni.Na sasa nafikiri hawalali kwa kuota mwarabu mwislamu wa siasa kali akiwa kabeba jambia kuja kuwararua kwa kuwatapeli kwa kisingizio cha Uislamu.

Kama ni misaada waislamu wa mataifa ya nje walikuwa wakitoa mamilioni kwa waislamu binafsi na taasisi zake hapa nchini hata kabla ya suala la OIC na kadhi hadi waliposhtuka na kughundua kuwa kumbe wanashughulika na wengi matapeli wanaotumia dini kuwaibia.
 
Unajua kuna mambo mengi sana japo mengine utayaona ni madogo madogo lakini wenzetu wamekuwa wakitumia kwa makusudio maalum kuwabagua waislam na hasa wale walio waumini.
Nitakupa moja dogo ili kukupanua upeo wa kuoni ni jinsi gani mambo yameandaliwa kiustadi ili kumbagua muislam, angalia taarifa za Habari katika Redio na TV, zimeandaliwa maalum waumini wa kiislam wasiweze kuziona/kuzisikia. angalia timings zimepangwa muda ambao muumini atakuwa msikitini. ya saa nne asubuhi ili aipate maana yake asifanye kazi na ya saa nne/tano usiku ili asilale mapema ila achelewe swala ya Alfajiri. kwa wepesi unaweza kuona si jambo zitu lakini limefanywa strategically. ah kwani taarifa ya habari inaumuhimu gani????. ila wangeweza kupanga muda tofauti na wa swala kwa mfano saa sita mchana saa tisa alasiri saa moja usiku na saa tatu usiku. yapo mengi ila leo niko hapa tu ilikukufahamisheni kwamba hata mambo madogo ambayo hayaonekani umuhimu wao wanayafanyia mkakati.


This is serious!
1.Tupeni uzoefu wa vyombo vya habari vya kiislam au vyenye kumilikiwa na waislamu utaratibu wa vipindi ukoje.
2. Je vyombo vya habari vya kiislam vinachukua hatua gani kusawazisha kwa kupanga vipindi muda muafaka?
 
huu ni upuuzi mtupu

ukweli ni kuwa waislamu wanadai haki yao na wapewe kwani na wao ni sehemu ya ya watanzania


Ndugu yangu ina elekea wewe hufahamu nini maana ya haki. kwako wewe kudai haki ni pamoja na kuvunja katiba. lakini uliouita upuuzi wakati ukifika wa mabomu utanikumbuka, mtatumia neno hilo hilo la kudai haki huku mnaua watu wasio na hatia. Wakati wa nyerere OIC ilikuwepo mbona hamkudai? mlisubiri afe ndio muanze kusumbua watanzania wenzenu tusio na udini kwa kudai mahakama ya kadhi na OIC, sisi tumezoea amani tuliyonayo nyinyi waislamu mnataka kuivunja kwa kisingizio cha kudai haki. katika watu wapuuzi wewe ni mmoja wao kwani mwishowe utakabidhi familia yako kwa jirani kwa kisingizio cha kutaka misaada. Watawala wa kiislamu wakiingia madarakani ndio tuna kumbana na issues za IOC na Mahakama ya Kadhi, mnataka kutumia udhaifu wa kiimani kutuingiza kwenye udini,watu mmeletewa mpaka katiba ya OIC lakini bado hamuelewi kuwa hiyo kwa Tanzania iliyojengwa kwa misingi imara ya kutokuwa na udini haifai. kwa hiyo mnachotafuta sasa ni roho za watanzia wenzenu?
 
Ahsante sana Mheshimiwa Mukandara. Naona umeeleza kabisa yanayojiri. Pamoja na hayo kwa kujalizia tu. OIC wanaihitaji Zanzibar hivi sasa kujiendeleza kiuchumi. Kuna investments kutoka Vyombo (mabenki) yanayofungamana na OIC na Investors wanaofungamana na vyombo hivyo amabayo hayawezi ku-materialise bila ya Zanzibar kujiunga na OIC. Nayo basi kwa sababu ya Muungano haiwezi kujiunga ila ipitie kwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Enyi ndugu zetu wa Bara- Please do the needfull- Wacha Jamhuri iingie kuiwezesha Zanzibar kunufaika. Zanzibar imeyakubalia mangapi yenye maslahi na Tanganyika yafanyike kwa Jina na nguvu za Jamhuri ya Muungano. Nasema tena Thank you Mheshimiwa Mukandara for the post.

......ni vyombo gani hivyo.......unaweza kutuwekea hapa......?
 
Thanks MAMA nimekulewa UK’s first official sharia courts na wanatakiwa wengine waisome vizuri kabisa

Pia nataka kumwambia OPAQUE kwamba tuelewe uzuri Serikali sio itabeba mzigo wa OIC itapata manufaa
hichi chama pia ni kwaajili ya kusaidi wailsamu ina wadhamini wa kiislamu huko mbele wananapesa za kutosha na sio mzigo kwa serikari ni kama Roman catholik wanavyopata pesa kutoka Romapia tusiifanye nchi kuwa na migongano ya kidini kutokana na Maaskofu kuwa wanasikilizwa na Serikali je Waislamu waki simamsha jambo wanalotaka kufanya Maaskofu Serikali itakuba?

sahihisho!
Roman Catholic hapa Tanzania hawategemei kupata pesa kutoka Roma kama unavyofikiria bali kanisa lina fund raise internally kutoka kwa waumini.Hicho unachokisema wewe ni historia - mambo ya kale wakati kanisa likiwa changa! Hakuna tena hand-outs!
 
Ndugu yangu ina elekea wewe hufahamu nini maana ya haki. kwako wewe kudai haki ni pamoja na kuvunja katiba. lakini uliouita upuuzi wakati ukifika wa mabomu utanikumbuka, mtatumia neno hilo hilo la kudai haki huku mnaua watu wasio na hatia. Wakati wa nyerere OIC ilikuwepo mbona hamkudai? mlisubiri afe ndio muanze kusumbua watanzania wenzenu tusio na udini kwa kudai mahakama ya kadhi na OIC, sisi tumezoea amani tuliyonayo nyinyi waislamu mnataka kuivunja kwa kisingizio cha kudai haki. katika watu wapuuzi wewe ni mmoja wao kwani mwishowe utakabidhi familia yako kwa jirani kwa kisingizio cha kutaka misaada. Watawala wa kiislamu wakiingia madarakani ndio tuna kumbana na issues za IOC na Mahakama ya Kadhi, mnataka kutumia udhaifu wa kiimani kutuingiza kwenye udini,watu mmeletewa mpaka katiba ya OIC lakini bado hamuelewi kuwa hiyo kwa Tanzania iliyojengwa kwa misingi imara ya kutokuwa na udini haifai. kwa hiyo mnachotafuta sasa ni roho za watanzia wenzenu?
Nawe nawe. Wacha ushabiki wa kidini. Tafadhali rudi juu soma post ya Bw. Mkandara- uielewe. Halafu tafuta Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania uielewe. Halafu rudia ile kadhia ya Zanzibar kuchukua uamuzi(wa kiharamia) kuingia OIC kivyake vyake (ambao Mwalimu Nyerere aliukemea). Ndipo Zanzibar ikajitoa (mara moja) kusubiri utaratibu muafaka wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ambao haujafanyika (nasikitika kueleza hili) mpaka hii leo.
 
Ahsante sana Mheshimiwa Mukandara. Naona umeeleza kabisa yanayojiri. Pamoja na hayo kwa kujalizia tu. OIC wanaihitaji Zanzibar hivi sasa kujiendeleza kiuchumi. Kuna investments kutoka Vyombo (mabenki) yanayofungamana na OIC na Investors wanaofungamana na vyombo hivyo amabayo hayawezi ku-materialise bila ya Zanzibar kujiunga na OIC. Nayo basi kwa sababu ya Muungano haiwezi kujiunga ila ipitie kwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Enyi ndugu zetu wa Bara- Please do the needfull- Wacha Jamhuri iingie kuiwezesha Zanzibar kunufaika. Zanzibar imeyakubalia mangapi yenye maslahi na Tanganyika yafanyike kwa Jina na nguvu za Jamhuri ya Muungano. Nasema tena Thank you Mheshimiwa Mukandara for the post.

......ni vyombo gani hivyo.......unaweza kutuwekea hapa......?

Tafadhali wasiliana na SMZ Wizara ya Fedha na Uchumi au Wizara ya Biashara , Viwanda na Uwekezaji. Sio mimi.


.......kwani wewe ni Ndivyo Ilivyo?..........
 
Hii si ajabu kuona siku zijazo moja ya mbiu ya kampeni kwa rais ni kuwa

''Ndugu zangu, mkinichagua kuwa rais nitahakikisha ninawaombea misaada nchi za nje''

Hasa inapotokea wananchi na akili zao, wanaona wananyimwa haki kutokupata misaada, hii fikra duni na potofu ukiiweka personal ni aibu.

Ni aibu ukiwa na kila kitu, kwenda kuomba misaada, huu ni mtindio wa ubongo, inakuwa kama unamlazimisha mwanaume mwezio akupe fedha!!

waberoya
 
sahihisho!
Roman Catholic hapa Tanzania hawategemei kupata pesa kutoka Roma kama unavyofikiria bali kanisa lina fund raise internally kutoka kwa waumini.Hicho unachokisema wewe ni historia - mambo ya kale wakati kanisa likiwa changa! Hakuna tena hand-outs!

Lets assume R.C wanategemea misaada toka ROMA, je misaada yao waliombea kupitia serikalini??

waberoya
 
Kwa manufaa ya Zanzibar, ambayo ni sehemu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. JMT ijiunge na OIC.
Kama mnapendana na rafiki yako na anapenda kwenda mpirani na angependa mwende wote mridhishe kwa wote kwenda mpirani hata kama hutauangalia. Iko siku utamwomba akupeleke usipopenda pia. Ndio urafiki wa dhati. Vivyo hivyo na Muungano wetu. Zanzibar waislamu ni wengi. Maadamu Zanzibar sio nchi basi JMT ijiunge ili iwaridhishe. Ndio Muungano huo. hebu angalia arctcle 3.2 ya OIC charter :-
Any State, member of the United Nations, having Muslim majority and
abiding by the Charter, which submits an application for membership may
join the Organisation if approved by consensus only by the Council of Foreign
Ministers on the basis of the agreed criteria adopted by the Council of Foreign
Ministers.
 
Jambo hili linashangaza sana. Kila wakati hoja inabadilika, nadhani wanaobadilisha hoja wanajaribu kutafuta pa kukamata. Sasa hivi hoja imekuwa ZANZIBAR! What a pseudo politics?

OK Mkandara anasema Zanzibar ina tamaduni zake ambazo ni lazima ijiunge OIC. Katiba inasema Zanzibar inawakilishwa na JMT katika mambo ya nje. Kwa hivyo JMT ijiunge ili kuridhisha interrest za Zanzibar. Hata hivyo mwishowe ni JMT itakayo kuwa imejiunga. Kama Zanzibar wanadhani kuwepo ndani ya muungano ni tatizo linalowafanya washindwe kuridhisha "their foreign policy interrests - Kujiunga OIC", hili ni Tatizo. Hivi Zanzibar ni sehemu ya muungano au ni nchi? Ikiwa Zanzibar ni sehemu ya muungano hawana budi kukubaliana na serikali ya muungano kwani hakuna serikali ya muungano kama Zanzibar haipo! Vikwazo vinavyoikwamisha JMT, vitaikwamisha Zanzibar unless Zanzibar iseme is not part of JMT!

Tuambieni kuwa sasa Zanzibar inataka kuendesha sera yake ya nje kama Zanzibar. Jambo litakuwa ni rahisi. Ni kureview UNION MATTERS ndani ya katiba. Sera ya nje Zanzibar ijitegemee, ili hatimaye kile hawa "pseudo politicians" wanachokitaka kitokee, kuvunjika kwa muungano.

Kama Zanzibar ingekuwa ni true partner ndani ya muungano isingekuwa "hellbent" kutafuta vitu ambavyo inajua serikali ya muungano haiviwezi kwa muundo uliopo. Kung'ang'ania huku kwa Zanzibar ni hidden agenda. Hivi unadhani Nyerere angekubali kuunganisha Tanganyika na Zanzibar ikiwa Mambo ya nje si sehemu ya muungano?? Asilani asingefanya hivyo. Suala hili ni one of the pillars of union. Vunjeni hilo mvunje muungano!
 
Nadhani watanzani wengi watakubali nchi yao ijiunge na OIC endapo:

a. Katiba ya OIC itabadilishwa na kutotambua Uislamu kama kiunganishi cha nchi hizo.
b. Itatoa nafasi za ajira kwa mtu yeyote mwanachama na mtu huyo si lazima awe Muislamu
c. Haitaweka kipaumbele cha kulinda, kuhifadhi, na kutetea tunu za Kiislamu tu
d. Haitataka maamuzi yake kuongozwa na mafundisho ya dini ya Kiislamu
e. Haitalazimisha nchi zote wanachama kukubali Yerusalemu (al Quds) kuwa Makao makuu ya Palestina
f. Itaondoa Bismillah kwenye ufunguzi wa Katiba hiyo na hivyo kuzifanya nchi zinazokubali kujiunga nayo kusema Bismillahi.
g. Kuondoa references zozote zile za dini ya Kiislamu kwenye Katiba na kuifanya jumuiya hiyo iwe ni jumuiya misaada tu isiyounganishwa na dini moja.
h. Kama hayo yote hayawezekani, basi Katiba hiyo iutambue Ukristu na kuweka malengo yenye kulinda, kutunza, na kutetea tunu za Kikristu pia.

Wakifanya hivyo Tanzania inawea kujiunga.
 
Kwa manufaa ya Zanzibar, ambayo ni sehemu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. JMT ijiunge na OIC.
Kama mnapendana na rafiki yako na anapenda kwenda mpirani na angependa mwende wote mridhishe kwa wote kwenda mpirani hata kama hutauangalia. Iko siku utamwomba akupeleke usipopenda pia. Ndio urafiki wa dhati. Vivyo hivyo na Muungano wetu. Zanzibar waislamu ni wengi. Maadamu Zanzibar sio nchi basi JMT ijiunge ili iwaridhishe. Ndio Muungano huo. hebu angalia arctcle 3.2 ya OIC charter :-
Any State, member of the United Nations, having Muslim majority and
abiding by the Charter, which submits an application for membership may
join the Organisation if approved by consensus only by the Council of Foreign
Ministers on the basis of the agreed criteria adopted by the Council of Foreign
Ministers.[/QUOTE
Wewe achana na philosophy hiyo. Kimsingi unayosema ni ok. Lakini hatuendi hivyo ndiyo maana Zanzibar imekwezwa katika hili la OIC. Sasa tuiangalie Katiba tuweke misingi itakayoshughulikia suala kama hili linapojitokeza.
 
Jambo hili linashangaza sana. Kila wakati hoja inabadilika, nadhani wanaobadilisha hoja wanajaribu kutafuta pa kukamata. Sasa hivi hoja imekuwa ZANZIBAR! What a pseudo politics?

OK Mkandara anasema Zanzibar ina tamaduni zake ambazo ni lazima ijiunge OIC. Katiba inasema Zanzibar inawakilishwa na JMT katika mambo ya nje. Kwa hivyo JMT ijiunge ili kuridhisha interrest za Zanzibar. Hata hivyo mwishowe ni JMT itakayo kuwa imejiunga. Kama Zanzibar wanadhani kuwepo ndani ya muungano ni tatizo linalowafanya washindwe kuridhisha "their foreign policy interrests - Kujiunga OIC", hili ni Tatizo. Hivi Zanzibar ni sehemu ya muungano au ni nchi? Ikiwa Zanzibar ni sehemu ya muungano hawana budi kukubaliana na serikali ya muungano kwani hakuna serikali ya muungano kama Zanzibar haipo! Vikwazo vinavyoikwamisha JMT, vitaikwamisha Zanzibar unless Zanzibar iseme is not part of JMT!

Tuambieni kuwa sasa Zanzibar inataka kuendesha sera yake ya nje kama Zanzibar. Jambo litakuwa ni rahisi. Ni kureview UNION MATTERS ndani ya katiba. Sera ya nje Zanzibar ijitegemee, ili hatimaye kile hawa "pseudo politicians" wanachokitaka kitokee, kuvunjika kwa muungano.

Kama Zanzibar ingekuwa ni true partner ndani ya muungano isingekuwa "hellbent" kutafuta vitu ambavyo inajua serikali ya muungano haiviwezi kwa muundo uliopo. Kung'ang'ania huku kwa Zanzibar ni hidden agenda. Hivi unadhani Nyerere angekubali kuunganisha Tanganyika na Zanzibar ikiwa Mambo ya nje si sehemu ya muungano?? Asilani asingefanya hivyo. Suala hili ni one of the pillars of union. Vunjeni hilo mvunje muungano!
Punguza munkar. Punguza jazba. Umepiga ndipo. Hivi Muungano ni kukidhi haja na matakwa ya Tanganyika tu. Ikija matakwa na haja ya Zanzibar tubeze?
 
Nawe nawe. Wacha ushabiki wa kidini. Tafadhali rudi juu soma post ya Bw. Mkandara- uielewe. Halafu tafuta Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania uielewe. Halafu rudia ile kadhia ya Zanzibar kuchukua uamuzi(wa kiharamia) kuingia OIC kivyake vyake (ambao Mwalimu Nyerere aliukemea). Ndipo Zanzibar ikajitoa (mara moja) kusubiri utaratibu muafaka wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ambao haujafanyika (nasikitika kueleza hili) mpaka hii leo.


Mimi naielewa katiba kuliko unavyofikiri, kwani hoja yangu imeelemea kwenye katiba hiyo hiyo, suala la kujiunga OIC au Mahakama ya Kadhi linahitaji marekebisho katika katiba yetu. Ndugu yangu kwa taarifa yako ni ushabiki wa kidini ndio uliofanya haya mambo ya OIC na Mahakama ya Kadhi yakaibuka tena na si maendeleo kama unavyofikiria wewe,kama ni maendeleo tungeshabikia kufanya kazi kwa bidii zaidi na sisi tuwe kama nchi nyingine zilizoendelea kwani raslimali tunazo nyingi tatizo ni uongozio,na si kuwaza misaada,msitake kuufanya uafrika kama laana, bali ni watu kama nyie kila kukicha mnagonga hodi kwenye taasisi za misaada kuomba kusaidiwa wakati mvua zinanyesha, ardhi tunayo ,madini tunayo pamoja na maliasili nyingine kama si ujinga ni nini?
 
Back
Top Bottom