Juu ya OIC na Mahakama ya Kadhi

Juu ya OIC na Mahakama ya Kadhi

Mkuu, hapo ndio utambue kuwa hii ajenda ya OIC ni kwa ajili ya maslahi ya watu fulani. haiwezekani nchi huru kama Tanzania tukae tunabishana kuhusiana na suala hili eti tu kisa tunataka kupata misaada wakati kial siku, hao hao wanaotushawishi kuwa tutapata misaada OIC, ndio waliokuwa wakituhutubia kuwa maendeleo yetu hayataletwa na wajomba

sasa kwa nn tanzania imejiunga UN au common wealth au sadc au AU kama haihitaji misaada? na jee kujiunga huko kumepoteza uhuru wa tanzania ?

unataka kutuimbisha tuamini kuwa waliojiunga na OIC wameuza uhuru wao ?

sisi mara hii tumeamua lolote liwalo na liwe ila haturudi nyuma
 
sasa kwa nn tanzania imejiunga UN au common wealth au sadc au AU kama haihitaji misaada? na jee kujiunga huko kumepoteza uhuru wa tanzania ?

unataka kutuimbisha tuamini kuwa waliojiunga na OIC wameuza uhuru wao ?

sisi mara hii tumeamua lolote liwalo na liwe ila haturudi nyuma

Nafikiri kujaribu kufananisha OIC na SADC au AU ni kama kujaribu kulinganisha maji na mafuta. Kama kweli kujiunga kwa TZ kwenye hiyo jumuia hakuna uhusiano wowote na dini mbona unasema safari hii hakubali. Hamkubali ninyi akina nani????

Kama TZ ingekuwa inafaidika mbona kwenye kipindi chote cha BWM hii issue haikuibuliwa tena??? Au kwa vile mmemuona rais wa sasa ni legelege.
 
Wale wapenda UDINI poleni sana. Mahakama ya kadhi inaweza isiwe tatizo sana ila la kujiunga na OIC ni ' pure'UDINI maana lengo mojawapo ni kuendeleza uislamu na hatimaye kuwa na taifa la kiislamu. wapenda udini pitieni vizuri malengo ya OIC.

Kama suala ni kuendeleza waislamu kiuchumi basi ije kama NGO na kuna NGO nyingi sana za kusaidia waislamu, WHY they want to subject our loved country OIC?
Nina aamini wale wote wanaoshabikia kwa nguvu eti TZ ijiunge OIC ni wale wenye siasa kali na malengo ya udini na hawaitakii nchi yetu mema, kama wapo ambao wanashabikia lakini si wenye msimamo mkali basi hawana uwezo wa kuchambua na kuona mambo ya mbali
 
sasa kwa nn tanzania imejiunga UN au common wealth au sadc au AU kama haihitaji misaada? na jee kujiunga huko kumepoteza uhuru wa tanzania ?

unataka kutuimbisha tuamini kuwa waliojiunga na OIC wameuza uhuru wao ?

sisi mara hii tumeamua lolote liwalo na liwe ila haturudi nyuma

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inapaswa kujiunga na OIC, kwa ajili ya manufaa ya Zanzibar na watu wake (hili si suala la dini). Sasa tuone safari hii ama Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ikidhi haja na matakwa ya Zanmzibar (na watu wake) au ikatae. Kwa nini kila siku tuburuzwe kukubali ya Wa Bara tu yetu sisi N'go!!! Msijitie sababu za dini- bileshi. Kanisa la kwanza la Afrika Mashariki la Anglican lipo pale Mkunazini (Mjini Zanzibar)- jee limevunjwa?
 
Last edited:
Nafikiri kujaribu kufananisha OIC na SADC au AU ni kama kujaribu kulinganisha maji na mafuta. Kama kweli kujiunga kwa TZ kwenye hiyo jumuia hakuna uhusiano wowote na dini mbona unasema safari hii hakubali. Hamkubali ninyi akina nani????

Kama TZ ingekuwa inafaidika mbona kwenye kipindi chote cha BWM hii issue haikuibuliwa tena??? Au kwa vile mmemuona rais wa sasa ni legelege.
Kwani Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni ya kina nani?
 
Nafikiri kujaribu kufananisha OIC na SADC au AU ni kama kujaribu kulinganisha maji na mafuta. Kama kweli kujiunga kwa TZ kwenye hiyo jumuia hakuna uhusiano wowote na dini mbona unasema safari hii hakubali. Hamkubali ninyi akina nani????

Kama TZ ingekuwa inafaidika mbona kwenye kipindi chote cha BWM hii issue haikuibuliwa tena??? Au kwa vile mmemuona rais wa sasa ni legelege.

Siyo halikuibuliwa. Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ilikuwa imepewa muda kulitafakari hilo suala. Na imeshaelezwa kuwa suala hilo halina uhusiano na agenda za kidini- Bali ni maslahi ya Wazanzibari na Uchumi wao chini ya uongozi wa SMZ. Kulikoni Bwana!!. Hakuna dini hapo!!. Nyinyi mnaolumbana kwa misingi ya dini ndio mnaotushangaza.Lakini hata mkitaka hivyo. Misahafu ikija isiende Sumbawanga na iende Zanzibar, Si basi yameisha.
 
Last edited:
Pakacha.. tusaidieni kuona hizo faida za kujiunga na OIC kwa kutolea mifano ya nchi zilizonufaika hivyo.
 
Hakuna mwenye mfano wa nchi ambayo imefaidika na misaada ya OIC?

Mheshimiwa hakuna. Lakini nakuomba wewe mweledi tafuta hiyo. Uganda haiwezi kunufaika . Lakini Zanzibar(as a Zanzibar per see) ni tofauti hapo. Sasa tufupishe maneno. Mimi sikubali hata siku moja Tanganyika iingie OIC (kwa mazingira yake). Lakini kuna Zanzibar-hiyo inacheleweshwa kuingia OIC.Zanzibar ina faida kibao hapo(usiiifananishe na Uganda au Gabon au Somali au Sudan) Wajarislamali wa Zanzibar watakuwa na "close access" na vyombo vya mshiko (mabenki) yanayofungamana na OIC. Ukitaka zaidi Mzee MKKJ wasiliana na SMZ. Sisi huku Znz hili suala tunaliona ni la kiuchumi zaidi (sio la kidini wala siasa). Hakuna mtu anaekataa OIC kwa sababu ee eti ni ya Waarabu (Mahizbu, ZNP, ma CUF) NO. Uchumi mbele. Sasa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, plse. kubalini kujiunga na OIC, for the sake of Zanzibar. Acheni hiyo ---Misahafu ikija itafika Makunduchi (Zanzibar) lakini asilan isifikishwe Kunduchi (Dar es salaam)
 
Hakuna mwenye mfano wa nchi ambayo imefaidika na misaada ya OIC?

Mwanakijii niliipata hii kwenye internet....Lakini inaingia akilini tangu 1974 ndio haya tu Uganda iliyofanikiwa kupata kutoka OIC?....au labda sababu ya vita na misukosuko iliyopitia ilisababisha kutonufaika na uanachama wa OIC?....


Since joining the OIC, Uganda has received various funds and grants to finance development projects including construction of roads, sugar and coffee production, hydro-power generation, teacher and technical education and health service rehabilitation, among others.

Another tangible benefit is the Islamic University, located east of Kampala. It was established in 1988 and is known to be one of the most successful OIC-funded institutions. The university serves the English-speaking African Muslim community in east and southern Africa and has so far produced more than 3,000 graduates in the various fields of arts and social sciences, 70% of whom are Ugandans.

Uganda also hopes to benefit from the ten-year program of action adopted by the OIC summit. The program establishes, among other things, a poverty alleviation fund to help member states provide additional resources including support for the eradication of diseases and epidemics like HIV/AIDS, malaria and tuberculosis.


source: Agence de Presse Africaine - Article



Link nyingine you can learn more ....Malaysia, Turkey & Saudi Arabia Driving Increased Intra-OIC Trade: Dinar Standard
 
Mwanakijii niliipata hii kwenye internet....Lakini inaingia akilini tangu 1974 ndio haya tu Uganda iliyofanikiwa kupata kutoka OIC?....au labda sababu ya vita na misukosuko iliyopitia ilisababisha kutonufaika na uanachama wa OIC?....

Since joining the OIC, Uganda has received various funds and grants to finance development projects including construction of roads, sugar and coffee production, hydro-power generation, teacher and technical education and health service rehabilitation, among others.

Another tangible benefit is the Islamic University, located east of Kampala. It was established in 1988 and is known to be one of the most successful OIC-funded institutions. The university serves the English-speaking African Muslim community in east and southern Africa and has so far produced more than 3,000 graduates in the various fields of arts and social sciences, 70% of whom are Ugandans.

Uganda also hopes to benefit from the ten-year program of action adopted by the OIC summit. The program establishes, among other things, a poverty alleviation fund to help member states provide additional resources including support for the eradication of diseases and epidemics like HIV/AIDS, malaria and tuberculosis.


source: Agence de Presse Africaine - Article



Link nyingine you can learn more ....Malaysia, Turkey & Saudi Arabia Driving Increased Intra-OIC Trade: Dinar Standard

Waeleze Mheshimiwa. Hayo ni mafanikio ya Uganda. Lakini kama tunayatathmini kuwa ni asilimia 10, basi kuwa na hakika Zanzibar (ikiwa ndani ya Jamhuuri ya Muungano wa Tanzania ) inapata mafanikio kama hayo kwa asilimia 75. Tanganyika (as Tanganyika katika Jamhuri ya Muungano) nafasi yake!!!!!! -wacha tulumbane hapo. HUU NI UCHUMI SIO DINI WALA SIASA.
 
Last edited:
Since joining the OIC, Uganda has received various funds and grants to finance development projects including construction of roads, sugar and coffee production, hydro-power generation, teacher and technical education and health service rehabilitation, among others.


Barabara, kilimo cha miwa, kahawa, na umeme wa maji, walimu na elimu ya ufundi, na kuboreshwa kwa sekta ya afya kumeifanya Uganda kuwa tofauti na sisi tusiopokea misaada kutoka OIC?

Tumekuwa tukipokea misaada ya aina mbalimbali kutoka nchi za Kiarabu/Kiislamu kwa muda mrefu tu je tunaweza kusema kuwa hatujanufaika na na kuhusiana na nchi ambazo tayari ni wanachama wa OIC.


Another tangible benefit is the Islamic University, located east of Kampala. It was established in 1988 and is known to be one of the most successful OIC-funded institutions. The university serves the English-speaking African Muslim community in east and southern Africa and has so far produced more than 3,000 graduates in the various fields of arts and social sciences, 70% of whom are Ugandans.

Tanzania imeweza kutoa majengo ya iliyokuwa Chuo cha Tanesco kuanzisha Chuo Kikuu cha Waislamu nchini je hilo halihesabiki hadi hicho Chuo kiwe kimeanzishwa na OIC?

Uganda also hopes to benefit from the ten-year program of action adopted by the OIC summit. The program establishes, among other things, a poverty alleviation fund to help member states provide additional resources including support for the eradication of diseases and epidemics like HIV/AIDS, malaria and tuberculosis.

Tayari tunapokea misaada ya mabilioni kwenye hilo eneo na inawahusu watanzania wote. Tumepokea toka Uingereza, Marekani, Ubelgiji, Iran n.k kwanini hii mingine lazima tujiunge kwanza? Hizo nchi wanachama wa OIC haziwezi kusaidia katika masuala hayo hadi tuwe wanachama?

Lakini Uganda ni mfano mmoja tu;

Tujiulize:

Comoro imefaidika vipi kwa kuwa mwanachama wa OIC? Kwanini OIC haikupeleka vikosi vyake kwenda kuinganisha nchi hiyo baada ya Bakari kuivunja?

Somalia imenufaika vipi sasa (mwaka wa kumi na zaidi haina serikali) na ni taifa lenye waislamu wengi na makundi ya "Mahakama za Sharia" yanaongoza sehemu mbalimbali. Kama suala la dini lina influence maendeleo kati ya Tanzania na Somalia ni nchi gani hasa inahitaji msaada kutoka Ummah wa Waislamu duniani kama Somalia?

Sudan: OIC imeweza kufanya nini kuhakikisha mauaji ya halaiki yanayoendelea Darfur yanakoma. Mauaji yanayofanywa na kundi la wanaodai ni waumini wa Uislamu dhidi ya Waislamu wengine? Je, mwanamama wa Darfur ambaye amebakwa mara kibao na Janjaweed utamueleza vipi faida ya nchi yake kuwa mwanachama wa OIC?

Guinea na Niger: Imetajwa mara nyingi kuwa chini kabisa katika kila aina ya vipimo vya dunia vya maendeleo. Kama Tanzania nchi isiyo mwanachama wa OIC iko juu ya Guinea ambayo imekuwa mwanachama wa OIC kuanzia 1969, ni kwa sababu gani watanzania waaamini kuwa OIC itasababisha maendeleo? Kwanini hawajaleta hayo maendeleo tunayoahidiwa sisi huko Guinea kwanza?

Mbona hayo maendeleo hatujayaona yakimiminika huko Guinea kama kweli kuwa mwanachama tu inatosha kupata maendeleo?

Mauritania: Nchi hii imekuwa mwanachama wa OIC kwa miaka mingi (tangu 1969) hivi karibuni tumeshuhudia utawala wa kijeshii ukiingia tena kama ilivyowahi kutoka kwa Uganda (nchi mwanachama pia). Ni kwa kiasi gani OIC ilijitahidi kuwaletea maendeleo watu wa Mauritania kiasi cha kuwafanya wafurahie kuwa wanachama na kuepusha mapinduzi ya kijeshi?

Hayo maendeleo ambayo Tanzania haiwezi kuyapata bila OIC ni yapi hayo?
 
The link below could be a starting point for discussion on FDI inflows between and among OIC countries. A quick look shows like most beneficiaries aren't countries in Africa........what could be wrong?

-Are our countries too risk to invest?
-We don't have good incentives for investors?
-Payback duration is too long in our countries?... (Uganda, Cameroun, Senegal etc...)

Let us discuss, because otherwise if Tanzania will join OIC possibility of experiencing the same laxity on investment flow from to be OIC investors is also likely to be the same....Tusipotibu ugonjwa hata kujiunga OIC hakutasaidia kitu. Tutabakia kupokea masalio au makombo tu.

Foreign Direct Investment (FDI) on the Rise in OIC Economies: Dinar Standard
 
deny all..

sisi hatuangalii FDI... ingekuwa hivi mjadaala ungekuwa tofauti sana. Kinachoangaliwa ni Misaada.
 
deny all..

sisi hatuangalii FDI... ingekuwa hivi mjadaala ungekuwa tofauti sana. Kinachoangaliwa ni Misaada.

Hakuna mtu anayetoa misaada tu kila siku bila siku moja kutegemea kufaidika kwenye dunia ya leo.....Kama serikali yetu na wananchi tunawaza hivyo tumeliwa.
 
Mwanakijii niliipata hii kwenye internet....

Another tangible benefit is the Islamic University, located east of Kampala. It was established in 1988 and is known to be one of the most successful OIC-funded institutions. The university serves the English-speaking African Muslim community in east and southern Africa and has so far produced more than 3,000 graduates in the various fields of arts and social sciences, 70% of whom are Ugandans.


Kwa hiyo kumbe misaada ya OIC inawalenga waislamu tu?? sio wana inji wote??-

someone help

waberoya
 
Hivi hii mijadala ya nini wakati Kikwete kasema wananchi tusiingile ila ni ofisi ya Membe ndio itatuamulia ?
 
Kuhani,
Unajua Kikwete ameshindwa kabisa kutoa maamuzi ktk swala hili kwa sababu moja kubwa - Hafahamu jibu lake...sawa na wengi wetu humu ktk mjadala huu tumeshindwa kabisa kutazama swali kisha kutoa majibu yanahusiana na swali lenyewe..Na kibaya zaidi tumeshindwa kukaa nje ya sanduku la Udini kufikiria swali. Kama ni mtihani wakuu wangu wengi wetu tumeshindwa na sio kwamba hatukufahamu jibu isipokuwa hatukufahamu swali!

Binafsi nimesikia mawazo mengi sana na mengine hadi yametufikisha ktk Udini na hakika mimi mwenyewe nilivutwa na hali hiyo kiasi kwamba niliacha kulitazama swali nikajibu hoja za watu ambazo zilikuwa nje kabisa ya swali..zilinivuta ktk sanduku hilo..

Mkuu Kuhani na wengine wote, kwanza tulitazame swala hili kama lilivyowakilishwa Bungeni. Swala hili limeanza toka miaka 10 na upuuzi uliopita, Zanzibar walipotaka kujiunga..

Kikatiba haikuwezekana kwa sababu Zanzibar sio nchi na swala hili lilikuwa la Muungano hivyo ilibidi uamuzi utolewe ktk bunge la Muungano mahala ambapo limekutana na Utata mkubwa.
Kwa hiyo, hoja bado haijabadilika zaidi isipokuwa ni sisi wananchi tumeshindwa kuelewa swali, kama tanzania inaweza kujiunga na OIC kwa sababu ya kikatiba ambayo inaikataza Zanzibar kujiunga kama nchi.

Kama utakumbuka hata mimi nilipinga vikali Zanzibar kujiunga na OIC kama nchi na hivyo kuwataka swala hili lifikishwe bunge la Muungano ambalo kusema kweli yawezekana Katiba haijitoshelezi.

Ni katiba hiyo hiyo tumeshindwa kutambua kwamba WaZanzibar ni distinct society ambayo imeingia ktk ndoa hii ya Muungano wakiwa na culture zao. Ni katiba hiyo hiyo imeshindwa kutambua kwamba Zanzibar ni sovereign country wakati Tanganyika isingekuwa Tanzania bila Muungano huo. Tanganyika iliondokewa nchi kama Rwanda na Burundi lakini bado tulibakia Tanganyika kwa sababu ile ilikuwa kama mikoa tu, hivyo hata leo tunaweza kuvunja mikoa lakini bado Tanzania ikasimamisha jina lake lakini sivyo kama Zanzibar itaondoka...

Nilichokuwa nikitazama mimi ni haki ya kimsingi ya waislaam ambao wanatengeneza asilimia 99 ya wananchi wa Zanzibar. Hii ndio chulture waliyokuja nayo (Uislaam) ktk Muungano wetu na hatuwezi kuipuuza kwa sababu tu sisi bara tuna dini nyingi na tofauti.

Ndio maana nikatumia mifano mingi ya ndoa kama nchi mbili na hata ndugu kama kigezo cha wananchi wa pande hizi mbili ili kutoa mawazo yangu kwa sababu Muungano wetu ni sawa na ndoa ama udugu wa kaka na dada.

Kuna watu humu wanafikiria kwamba mimi nazungumza kama Muislaam ama natoa hoja zangu kwa sababu ni muislaam, wanafanya makosa ya wazi kabisa kwani hata kama ningekuwa mkristu ningependekeza Tanzania kujiunga na OIC kwa sababu ya Zanzibar.
Hata kama Zanzibar ingekuwa na asilimia 99 ya Wakristu na wakataka kujiunga na baraza lolote la Kikristu ningeunga mkono isipokuwa tu kama wangetaka kutoa maamuzi wao wenyewe bila kuihusisha Bara wakati wanatumia bendera ya Taifa ningepinga. Kwa hiyo utaona kwamba sina upande, lakini waulize wengi humu maswali hayo watakuwa na majibu tofauti..

Tatizo jingine lililojitokeza ni pale tunapotaka kuziangalia faida za Tanzania kujiunga na OIC.. wakuu wangu hili sio swala letu, kama mimi Muislaam nimefunga ndoa na Mkristu inabidi nikubali yanayokuja na Ukristu.. isipokuwa hoja yoyote inayohusu nyumba yetu ni lazima nihusishwe kama mume ktk maamuzi..

Kama amechaguliwa kwenda Vatican ktk kisomo ni muhimu swala zima tulijadili kama familia lakini haina maana nitamkatalia kwa sababu tu ni swala la dini yake ama kujaribu kuelewa faioda yeye kwenda Vatican..

Nimewapeni mfano wa nchi kama canada ambao wameweza kupitisha bill nzito kama Quebec kujiunga na Jumuiya ya nchi za Kifaransa, Quebec kupitisha Kirfaransa kuwa lugha ya mawasiliano ktk jimbo lao (province) haya yote ukiyatazama bila kuelewa swali utafikiria kwamba kukubali kwa miswada ile kutaifanya canada nzima iwe nchi ya Kifaransa.. lakini sivyo ila kisheria (Kikatiba) ni lazima maswala yanayohusu Taifa zima yatajadiliwa na bunge la muungano hata kama uwezekano wa kupitisha ni mkubwa.

Leo hii Quebec ni mwanachama wa jumuiya hiyo na hakuna madhara sehemu nyingine na wala hakuna mtu aliyetaka kujua faida za kujiunga kwao.. wanazijua wenyewe.. Bill 101 ya mwaka 1990 (kama sikosei) kuhusiana na lugha ya mawasiliano Quebec ilikuwa mshike mshike kwa sababu bill hiyo ingeua kabisa Kiingereza huko Quebec, yet walifikia maamuzi kuwaachia wafanye hivyo kutokana na kwamba lugha ni moja ya tamaduni walizokuja nazo ktk muungano wa nchi hizo..

Kwa hiyo wakuu, swala bado lipo pale pale na pengine tunajichanganya sisi wenyewe kufikiria kwamba swala hili ni la Bara maadam limekuja ktk bunge la Muungano..

Na kusema kwamba waislaam wanaounga mkono OIC waende zanzibar na kama Muungano uvunjike wakati hili swala dogo kabisa na haliwahusu Bara waislaam kwa wakristu..Mnapotoa maneno mazito kama haya mnajenga fear ambayo binafsi naogopa kwamba inaweza kujenga chuki kati ya Waislaam na wakristu, leo hii Tayari waislaam wa Bara wameisha anza kuingilia na vyombo kama Ansar Sunni wanapata sababu ya kusema mnaona? tulisema kwamba nchi hii inaendeshwa kikristu!..Zaidi ya yote hayo kuna mambo mengi sana Bara tunawaburuza Zanzibar tukitumia jina na bendera ya Taifa bila wao kuhusishwa wala kupata hata mapato ya Ubalozi tuliotumia..

Kwa hiyo jamani kuwanyima waislaam ama niseme Zanzibar haki yao ya kimsingi ambayo ni moja ya culture yao waliyoingia nayo ktk Muungano kusema kweli tutafanya Udikteta. Na sasa hivi kuna hatari kubwa sana maadui wa Muungano na pengine hao fundamentalist wakaitumia hoja kama hii kubomoa kile mwalimu alikijenga kwa miaka 20 na upuuzi..bahati mbaya ni kuwa fundamentalist toka upande wa pili (Ukristu) ndio wanaoendesha hoja hii ktk Upinzani hali Zanzibar leo wameweza kufungua hata mipaka yao wa Wakristu kufungua makanisa ndani ya nchi yao.

Mwisho, mimi Mkandara pamoja na kuwa Muislaam sintakubali OIC kujenga sheria za Bara ama serikali nzima ya Muungano. Na sidhani kama inawezekana kwa sababu zipo nchi kibao zilizoungana zina toifauti kama zetu na wameweza kuishi kwa amni maadam unafahamu mipaka ya sheria hizo..

Kwa hiyo waungwana swali hapa halijapinda wala kugeuzwa kuwa swala la Tanzania nzima (nilivyoelewa mimi) isipokuwa majibu yake yatatoka kwa mawasilino ya sehemu zote mbili (bungeni) na muhimu zaidi ni sisi kutazama kujiunga huko kutaleta madhara gani Bara!.. Hizo faida wakuu wangu sio kazi yetu hata kidogo, unless tuna hakika kuwa Mwanamke/ mwanaume huyu anataka ku cheat!..
 
Hi salaam,

Mimi nafikiri kuwa wapo watu wanaopaswa kuelimishwa na wapo watu wanaopaswa kusoma. Tembelea web hii upate kujua nini kuhusu OIC www.oic-oci.org. pia malengo na wanachama. wewe kama msomi hupaswi kusubiri kuamabiwa wakati unaweza kutafuta info hata zilizo jificha. Tatizo kubwa la watanzania wengi wamewaachia viongozi wa makanisa kuelimisha watu juu ya OIC kuliko kutafuta habari za kweli kuhusu hili jambo.

Uganda toka1974 na Msumbiji toka 1994 ni nchi zenye wakristo wengi kuliko waislam lakini ni wanachama . Je ninini umesikia matatizo yawalio wapata waganda ou wananchi wa Msumbiji.

Pia fikiria kanisa katoliki kuwa na balozi hapa nini nini tataizo kwa waislam? Usiwe chongo wakati macho kam chechengo kwa kuangalia upande wakati macho yako yako yanaona. Uepuke upofu na uzikizi waakili kwa kuto jielimisha. kujielimisha.

Wewe unamshinda elimu katekista nau mchungaji pia umesoma inter-reginal organization 4m4 nini kinakushinda kutambua OIC?

Sishabikii Tanzania kujiunga na OIC ila naamsha hisia za kufikiri zaidi kuliko kutegemea viongozi wa dini wakuambie masuala ambayo unaweza kuyajua bila kushindikizwa.

Jua mambo uwe huru kuwa na msimamo wake kuliko kuwa bendera ya wasiojua ila washabiki.
 
Back
Top Bottom