Juu ya OIC na Mahakama ya Kadhi

Juu ya OIC na Mahakama ya Kadhi

Mwankijiji,

Ndio sababu Makanisa ya Kiprotestanti Tanzania yanaweza kujiuna na Baraza la Makanisa Duniani (WCC) bila kulazimisha nchi nzima ya Tanzania kujiunga. Kuna taasisi mbalimbali duniani za Waislamu ambazo jumuiya za Kiislamu ni wanachama na hakuna mtu anayepinga wala mwenye haki ya kupinga hivyo.
Tanzania ni imo ktk baraza la Wanawake duniani na wanaotuwakilisha ni wanawake..Bado unatumia mifano ya Ukatoliki, mkuu waislaam na katoliki hawafanani hata kidogo!.. Ujenzi wa jumuiya zenu hauwezi kuwa sawa na waislaam hata kidogo na pengine katiba imeandikwa kwa misingi ya Ukristu, hivyo waislaam hawakutazamwa, Kumbuka wewe ni mwanaume huna shoga mkuu, na unapozungumzia mwili jaribu kuziona tofauti zako kwanza.

Kuhusu hizo Jumiya za Kiislaam, nakuomba unambie Jumuiya ya Kiislaam ambayo wewe unaifahamu tumejiunga nayo ama tunaruhusiwa kujiunga!..Ama kwa kukurahisishia nambie Jumuiya ya Kimataifa ya Kiislaam ambayo iko Tanzania..
Hapa umekosea kidogo. Mama Mongela alikuwa Katibu Mkuu wa Mkutano wa Wanawake kule Beijing. Mkutano huu ulikuwa ni wa Umoja wa Mataifa (nchi ambayo Tanzania ni mwanachama). Hivyo Tanzania haikuwa imejiunga na jumuiya mpya bali ni Jumuiya ya Umoja wa Mataifa.
Mkuu hili ni baraza (conference) ya wanawake na OIC ni baraza (Conference) la nchi za Kiislaam, tofauti hapa ni Wanawake na Waislaam kwa hiyo mipaka yake lazima haitakuwa sawa unapo address wasiohusika...Wanawake vs wanaume, Waislaam vs wasiokuwa Waislaam.
Hili ndilo kosa nadhani lililopo. Siyo jukumu la serikali kulinda value za ukristu au Uislamu wa mtu. HIlo ni jukumu la taasisi za kidini. Serikali inapoingilia kati na kufanya kazi ya makanisa na misikiti inavuka mpaka wa kuwa serikali isiyo na dini na kuingia kwenye anga zisizo zake.
Mkuu sheria inaposema kila mtu ana haki ya kuamini dini aitakayo unafikiria hilo ni jukumu la dini sio serikali? utaweza vipi kusimamisha sheria kama hiyo bila serikali kuweka mkono wake!
Wangefanya hivyo wengine tungeendelea kupinga tu; ni principle. Wewe unaangalia wingi wa watu kuhalalisha hili mimi naangalia principle. Nchi ya Uturuki ni nchi yenye waislamu wengi lakini kwa makusudi kabisa wamekataa kuifanya nchi hiyo kuwa ya Kiislamu na wakati wowote wanasiasa wanapoisogeza nchi kwenye masuala ya dini, wanapata onyo lililowazi kutoka Jeshi. Hiyo ni principle. Na wale wanajeshi wanaopinga hivyo ni Waislamu vile vile wanapenda maisha yao ya kuwa taifa secular.
Haya sasa maneno, Turkey wamekataa kuwa nchi ya kiislaam lakini wao ni Member wa OIC, kwa hiyo hapa umezidi kujenga hoja yangu. hakuna mtu aliyesema kujiunga kwetu na OIC kunaifanya nchi yako kuwa ya kiislaam. Turkey mfano mzuri sana, shukran!

Mwanakijiji, unaposema wengine tungeendelea kupinga tu ni vumbi la macho, mkuu nakufahamu vizuri sana inapofikia maswala haya..menigne tuyaache kama yalivyo. sina haja ya kuingia ndani zaidi
 
Mwankijiji,


Tanzania ni imo ktk baraza la Wanawake duniani na wanaotuwakilisha ni wanawake..Bado unatumia mifano ya Ukatoliki, mkuu waislaam na katoliki hawafanani hata kidogo!.. Ujenzi wa jumuiya zenu hauwezi kuwa sawa na waislaam hata kidogo na pengine katiba imeandikwa kwa misingi ya Ukristu, hivyo waislaam hawakutazamwa,

mzee una madai mengi kweli ya haya mambo "yanayowezekana". Jinsi ulimwengu ulivyo, mengi yanawezekana.

Kumbuka wewe ni mwanaume huna shoga mkuu, na unapozungumzia mwili jaribu kuziona tofauti zako kwanza.

silielewi hili katika maudhui ya mjadala huu.


Kuhusu hizo Jumiya za Kiislaam, nakuomba unambie Jumuiya ya Kiislaam ambayo wewe unaifahamu tumejiunga nayo ama tunaruhusiwa kujiunga!..Ama kwa kukurahisishia nambie Jumuiya ya Kimataifa ya Kiislaam ambayo iko Tanzania..

Hakuna jumuiya yoyote ya Kiislamu ambayo TAnzania kama serikali imejiunga kama vile hakuna jumuiya ya Kikristu ambayo Tanzania kama nchi imejiunga. Hili la OIC litakuwa la kwanza; sielewi kwanini.

Mkuu hili ni baraza (conference) ya wanawake na OIC ni baraza (Conference) la nchi za Kiislaam, tofauti hapa ni Wanawake na Waislaam kwa hiyo mipaka yake lazima haitakuwa sawa unapo address wasiohusika...Wanawake vs wanaume, Waislaam vs wasiokuwa Waislaam.

Kama jumuiya hiyo ingekuwa ni Wanawake Wakristu ningekuwa na tatizo. Nakushauri usome malengo ya OIC vizuri uweze kuona tofauti ya "mabaraza" haya.


Mkuu sheria inaposema kila mtu ana haki ya kuamini dini aitakayo unafikiria hilo ni jukumu la dini sio serikali? utaweza vipi kusimamisha sheria kama hiyo bila serikali kuweka mkono wake!

serikali haiwezi kuja na kuniambia "Mwanakijiji leo mkiri Yesu" au haiwezi kuja na kuniambia "Usiende kusali Pentekoste bali lazima usali Lutherani". Serikali ina nafasi yake lakini ya kutangaza dini siyo mojawapo.

Haya sasa maneno, Turkey wamekataa kuwa nchi ya kiislaam lakini wao ni Member wa OIC, kwa hiyo hapa umezidi kujenga hoja yangu. hakuna mtu aliyesema kujiunga kwetu na OIC kunaifanya nchi yako kuwa ya kiislaam. Turkey mfano mzuri sana, shukran!

Sijawahi hata mara moja kusema kuwa tukijiunga OIC TAnzania itakuwa nchi ya Kiislamu. NInachokataa ni kwa Tanzania kukubali malengo ya OIC ambayo yanaipendelea dini ya Kiislamu. Hilo tu ndio tatiz tu.


Mwanakijiji, unaposema wengine tungeendelea kupinga tu ni vumbi la macho, mkuu nakufahamu vizuri sana inapofikia maswala haya..menigne tuyaache kama yalivyo. sina haja ya kuingia ndani zaidi

sidhani kama unanifahamu vizuri; mimi siogopi kuwasema wakristu kama ninavyowasema wapagani. Hofu yangu ni kuwa mwenzangu linapokuja suala la Waislamu hakuna baya linaloweza kufanywa au kusemwa na jaribio lolote la kuonesha matatizo linakumbana na madai ya udini.
 
Shedafa,
Kero zote za Muungano zinatokna na maswala haya haya tunayozungumzia. Kwa maana kwamba ni katiba hiyo inayokataa OIC kwa Zanzibar kuwa ni nchi, hivyo wakalileta swala Kitaifa. bado limekataliwa ama limegandishwa kiasi kwamba frustartion zao zimefikia kutotambua kipengele kinachosema Zanzibar sio nchi wakiwa na maana zaidi ya Bendera bali soveignty na distinct society kama walivyo Scotland ndani ya Great Britain. Hata hiyo tumeshindwa kuwapatia jibu tumebakia kusema Zanzibar sio nchi lakini hatuelezi wao ni kitu gani kama sio Mkoa tukijua wazi kwamba kukubali kwamba wao ni nchi ama Taifa - tafsiri yoyote itakayo tumika kuwapa uhuru kama Scotland utasababisha maamuzi yanayowagawa wao Kitaifa..
Kwa hiyo hakuna swala la Muafaka wa Muungano zaidi ya maswala haya kuwa wazi pande zote mbili na kila tunapokawiza majibu kama vile kesi za Ufisadi ndivyo tunavyozidi kujenga hali mbya zaidi ktk Muungano kiasi kwamba Muakfdaka wa aina yoyote ile hauwezi kuwa dawa.
 
Mwanakijiji,
Mkuu wangu mbona unazidi kujichanganya?..
Wewe ndiye uliandika kuwa jumuiya za kikristu zinaweza kujiunga na ukatoa mfano wa Makanisa ya Kiprotestanti Tanzania yanaweza kujiuna na Baraza la Makanisa Duniani bila kulazimisha nchi nzima ya Tanzania kujiunga. Na ukasema pia, Kuna taasisi mbalimbali duniani za Waislamu ambazo jumuiya za Kiislamu ni wanachama na hakuna mtu anayepinga wala mwenye haki ya kupinga hivyo.
Kutokana na maneno hayo nimekuuliza ni Taasisi gani za Kiislaam duniani ambazo waislaam ni wanachama wake ama kurahisisha swali ni Taasisi gani ya kiislaam ya dunia, waislaam wa Tanzania wamejiunga nayo ama wanaruhusiwa.
Na ndio ukafuatia mfano ambao hukuelewa umetoka wapi kwa sababu huelewi tofauti za Uislaam na Ukristu bali wewe unaona suriali inaweza valiwa kama shati.

Sijawahi hata mara moja kusema kuwa tukijiunga OIC TAnzania itakuwa nchi ya Kiislamu. NInachokataa ni kwa Tanzania kukubali malengo ya OIC ambayo yanaipendelea dini ya Kiislamu. Hilo tu ndio tatiz tu.
Sasa Turkey umeizungumzia hapa kwa maana gani ikiwa wao ni wanachama wa OIC!

sidhani kama unanifahamu vizuri; mimi siogopi kuwasema wakristu kama ninavyowasema wapagani. Hofu yangu ni kuwa mwenzangu linapokuja suala la Waislamu hakuna baya linaloweza kufanywa au kusemwa na jaribio lolote la kuonesha matatizo linakumbana na madai ya udini.
Hapana mkuu hii sio mara ya kwanza, niliwahi kuuliza nambie hata moja baya la jumuiya za kikristu ambalo wewe umewahi kulizungumzia.. sizungumzii mtu fulani ambaye ni mkristu!..Mkuu nakufahamu vizuri ktk swala la imani ya dini yako... uko bias kishenzi!
Mimi naweza kusema mambo millioni yanaona mabaya au makosa ktk Uislaam na jumuiya zake (nje ya Kuran na Hadith) lakini wewe nambie hata moja toka dhehebu lako na umewahi kuliandika wapi..
 
Mwankijiji,


Tanzania ni imo ktk baraza la Wanawake duniani na wanaotuwakilisha ni wanawake..



Mkuu hili ni baraza (conference) ya wanawake na OIC ni baraza (Conference) la nchi za Kiislaam, tofauti hapa ni Wanawake na Waislaam kwa hiyo mipaka yake lazima haitakuwa sawa unapo address wasiohusika...Wanawake vs wanaume, Waislaam vs wasiokuwa Waislaam.

Tuwekane sawa kidogo kwenye hili kama njia ya kuelimishana.Hakuna kitu kama hicho unachokiita " baraza" au " conference" ya wanawake, ambayo Tanzania imejiunga.Kama unazungumzia Beijing conference huu ni mkutano kama mikutano mingine yote ya UN ambayo huchagua theme au maudhui.Ipo mingine kama:
1991 - Mkutano wa Mazingira uliofanyika Rio De Janeiro; 1992 UN Conference on Social Development uliofanyika Copenhagen Denmark, 1993 UN Conference on Human Rights uliofanyika Vienna,1994 -UN Conference on Population uliofanyika Cairo na hatimaye 1995 UN Conference on women uliofanyika Beijing China.
Ni dhahiri kuwa haihusiani na suala zima la OIC au Mahakam za Kadhi.
 
Serikali ya Jamhuri ya Muungano iwe inaisikiliza Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, hiyo ndiyo ina sera na mipango yake ya kiuchumi ikiwa ni pamoja na hiyo ya kuwa katika (OIC) Sasa suala la OIC ni la SMZ ikiwa na mandate ya Zanzibar(Wananchi wa Zanzibar) ndio wanaotaka huko. Msijitie kulitia katika medani ya kidini -kubabaisha- haliko hivyo. Kuwa mkweli Bwana.

Nakubaliana nawe. Kabisa.
 
yakhe....swali langu ni kuhusu hiyo sentensi yako hapo juu.........hebu tuwekee hayo matakwa ya Tanganyika tu...........

Yakhe wewe upo hapa nchini lakini? Hebu angalia katika miaka hii yetu 44, nini ambacho Tanganyika imetaka kukifanya kwa kupitia Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania au Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imeshindwa kukifanya? kwa maslahi ya Tanganyika( na Wa-Tanganyika). Na angalia mangapi Zanzibar(iwe ama kwa kupitia Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, au Baraza la wawakilishi) imeyataka na kubembeleza (nasikitika -na hii kubembeleza) Bunge la Jamhuri au Serikali ya Jamhuri iyape legal mandate imeshindikana na kuishia katika malumbano yanayovishwa ngozi ya udini au makorokoro mengine pasipo na sababu za msingi? Do a fair analysis-yakhe!!
 
Mwanakijiji,
Ogah,
Bara tunatumia sana bendera ya taifa (jina la Tanzania) kuchukua misaada kibao nje na uwekeshaji wake unakwenda bara..ziko kibao na wala hatuna aibu..

Sasa kwa nini linapokuja suala la kugeuza upande wa pili wa shilingi (Zanzibar wanapotaka kutumia angalau kiduchu tu hiyo bendera ya Taifa(jina la Tanzania) kukidhi maslahi na matakwa yao kama Zanzibar -mnakuwa walalamishi?
 
JK aende kisha awaeleze idadi ya WATANZANIA WAKATOLIKI ambao wamekufa kwa sababu ya msimamo wa VATICAN kuwaambia wafuasi wao wasitumie CONDOM hilo la MAPADRE WALAWITI awaahie hao waamerika watadela na vatican

Siamini kama kondomu ndizo zinazozuia ukimwi! Kwani Kanisa kusema watu wasiue kumewazuia baadhi ya Wakatoliki kutoua au kusema wasiibe kumewazuia baadhi ya waumini kutoiba?

Kanisa linatoa mwongozo wa jumla, watu wanaamua wafanye nini kulingana na mahitaji au mazingira waliyomo. Have you ever read something called the Church's Pastoral Approach? So, there are general rules but it is up to the person's faith and informed conscience that lead him or her to choose under the circumstances.

The Church never chooses for her members!
 
Mkandara,
Naona unasogeza magoli. Mwanzo hii OIC haikuwa ya kidini bali ya mambo ya uchumi. Sasa unataka kweli kutuambia kuwa tujiunge kwa ajili ya Zanzibar? Hao waislamu lukuki walio bara jee? Tusisogeze magoli katika kutafuta ushindi. Kwa mantik, hiyo hiyo, basi Zanzibar wanahaki ya kujitangaza nchi ya kiislamu ndani ya Muungano! Si tumeishaelezwa kuwa wao ni nchi tukiwa nyumbani. Sasa kwa nini kwa vile kwao, waislamu ni wengi, wasijitangaze kuwa ni taifa la kiislamu? Tujiunge katika jumuia hii kwa maslahi ya jamii yote ya watanzania na si vinginevyo.

Naona tena Mkuu unachanganya Conference (Mkutano) ya Wanawake kule Beijing ambao ulikuwa ni one-off na Conference ( jumuia) ya OIC ambayo ni ya kudumu. Sisi kule Beijing hatukujiunga na Conference ya Wanawake bali tulishiriki na tulihudhuria mkutano huo. Hapa tunachokusudia ni kujiunga na chombo na si kuhudhuria mkutano.

Mimi bado naunga mkono sisi kujiunga katika OIC kwa manufaa ya taifa letu ambamo waislamu ni sehemu muhimu. Napinga kujiunga katika OIC ili kuwaridhisha Zanzibar.
 
Mkandara,
Naona unasogeza magoli. Mwanzo hii OIC haikuwa ya kidini bali ya mambo ya uchumi. Sasa unataka kweli kutuambia kuwa tujiunge kwa ajili ya Zanzibar? Hao waislamu lukuki walio bara jee? Tusisogeze magoli katika kutafuta ushindi. Kwa mantik, hiyo hiyo, basi Zanzibar wanahaki ya kujitangaza nchi ya kiislamu ndani ya Muungano! Si tumeishaelezwa kuwa wao ni nchi tukiwa nyumbani. Sasa kwa nini kwa vile kwao, waislamu ni wengi, wasijitangaze kuwa ni taifa la kiislamu? Tujiunge katika jumuia hii kwa maslahi ya jamii yote ya watanzania na si vinginevyo.

Naona tena Mkuu unachanganya Conference (Mkutano) ya Wanawake kule Beijing ambao ulikuwa ni one-off na Conference ( jumuia) ya OIC ambayo ni ya kudumu. Sisi kule Beijing hatukujiunga na Conference ya Wanawake bali tulishiriki na tulihudhuria mkutano huo. Hapa tunachokusudia ni kujiunga na chombo na si kuhudhuria mkutano.

Mimi bado naunga mkono sisi kujiunga katika OIC kwa manufaa ya taifa letu ambamo waislamu ni sehemu muhimu. Napinga kujiunga katika OIC ili kuwaridhisha Zanzibar.


Kama inakuwa hivyo ni sawa, hakuna tatizo. Naomba urudi nyuma elewe chanzo cha hili suala. SMZ ikiwa na mandate ya wananchi wa Zanzibar (kupitia Baraza la Wawakilishi) ndio walioona ni busara kuiingiza Zanzibar katika OIC kwa malengo ya kiuchumi na wakafanya hivyo (kiharamia). Serikali ya Jamhuri ya Muungano na Jamhuri ya Muungano yenyewe (kupitia Bunge la Jamhuri )ikahoji hatua hiyo kuwa si sahihi. Zanzibar(na SMZ) wakatanabahi kosa na wakajitoa uanachama mara moja. Jamhuri ya Muungano ikaahidi kulifuatilia suala hilo ili kuingiza Jamhuri kwa manufaa ya wananchi wote wa Jamhuri. Zanzibar ikawa mvumilivu na ikaa kusibiri huo mchakato. Mchakato ndio huu-unaishia katika malumbano yasiyo miguu wala mikono. Verdict- Kama Jamhuri ya Muungano inashindwa kulielekeza suala hili katika mtizxamo wa manufaa ya Watanzania wote, basi na ijuiunge ili iiwezeshe Zanzibar kuendelea mbele na sera zake. Kugwaya kwa nini SASA?Jamhuri ya Muungano isiiyumbishe (na kuikwaza) Zanzibar, fahamu imeshakuwa stahamilivu (tokea ilipojitoa) hadi leo hakuna follow up ya maana ya kukidhi matakwa yao. Kulikoni Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kama faida ya Jamhuri nzima sasa kwa nini inasita?
 
Mkandara,
Naona unasogeza magoli. Mwanzo hii OIC haikuwa ya kidini bali ya mambo ya uchumi. Sasa unataka kweli kutuambia kuwa tujiunge kwa ajili ya Zanzibar? Hao waislamu lukuki walio bara jee? Tusisogeze magoli katika kutafuta ushindi. Kwa mantik, hiyo hiyo, basi Zanzibar wanahaki ya kujitangaza nchi ya kiislamu ndani ya Muungano! Si tumeishaelezwa kuwa wao ni nchi tukiwa nyumbani. Sasa kwa nini kwa vile kwao, waislamu ni wengi, wasijitangaze kuwa ni taifa la kiislamu?

Mawazo yako potofu. Zanzibar inajifunga na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Zanzibar ni Nchi ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Zanzibar haina dini, lakini Waananchi wa Zanzibar wana dini (asilimia 99 inakadiriwa kuwa ni Waislamu na asilimia isiyozidi 1 ni dini nyengine zikiwemo Dini ya Kikristu-madhehebu yote, na Dini ya Hindu (mabaniani). Si nchi ya kiislamu na haiwezi kutangazwa kuwa nchi ya kiislamu, lakini wananchi wake walio wengi ni wasilamu na itabakia kuwa hivyo (ndani ya Muungano) au ikiwa peke yake. suala la OIC halipo hapo kidini (kwa mtizamo wa Zanzibar na watu wake)
 
[BVerdict- Kama Jamhuri ya Muungano inashindwa kulielekeza suala hili katika mtizxamo wa manufaa ya Watanzania wote, basi na ijuiunge ili iiwezeshe Zanzibar kuendelea mbele na sera zake. Kugwaya kwa nini SASA?Jamhuri ya Muungano isiiyumbishe (na kuikwaza) Zanzibar, fahamu imeshakuwa stahamilivu (tokea ilipojitoa) hadi leo hakuna follow up ya maana ya kukidhi matakwa yao. Kulikoni Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kama faida ya Jamhuri nzima sasa kwa nini inasita?

Fair points, lakini kama unavyozungumza maamuzi yeyote yale ya kujiunga au kutokujiunga ni lazima yafanywe kwa misingi ya manufaa ya kiuchumi ambayo nchi inaweza pata au la. Vile vile pia kumbuka sio lazima nchi ijiunge kwa mantiki hiyo Zanzibar isiiyumbishe na kuikwaza Jamhuri ya Muungano pia maana nayo pia imeshakuwa mstahimilivu wa kuruhusu mjadala na kusamehe makosa ya kiharamia yaliyopita.

Matakwa ya Jamhuri ya Muungano yapewe kipaumbele zaidi kushindwa yale ya Zanzibar au Tanganyika
 
Mawazo yako potofu. Zanzibar inajifunga na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Zanzibar ni Nchi ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Zanzibar haina dini, lakini Waananchi wa Zanzibar wana dini (asilimia 99 inakadiriwa kuwa ni Waislamu na asilimia isiyozidi 1 ni dini nyengine zikiwemo Dini ya Kikristu-madhehebu yote, na Dini ya Hindu (mabaniani). Si nchi ya kiislamu na haiwezi kutangazwa kuwa nchi ya kiislamu, lakini wananchi wake walio wengi ni wasilamu na itabakia kuwa hivyo (ndani ya Muungano) au ikiwa peke yake. suala la OIC halipo hapo kidini (kwa mtizamo wa Zanzibar na watu wake)

Kigezo kinachotumiwa sasa ni wingi wa waislamu Zanzibar ili kujenga hoja ya kujiunga kwa manufaa yao. Sio mimi niliyeingiza suala la udini wa Zanzibar katika mjadala huu bali ni nyie mnaotetea. Kwangu mimi suala hili lingeangaliwa bila ya kujali wingi wa waislamu Zanzibar bali tuangalie na kuzingatia kuwa waislamu ni sehemu ya jamii yetu. Mimi leo baniani wakiomba tujiunge kwenye chombo chao (kama kipo) nitawaunga mkono bila kuangalia wingi wao. Kwa kuifanya hii hoja iegemee uinchi wa Zanzibar na idadi ya waislamu huko ndiko kunakoingiza suala la upendeleo wa dini na sehemu ya Muungano. Ndio maana nikauliza kama wingi wa waislamu huko ndiyo kigezo, kikichangiwa na uinchi wa zanzibar ni kitu gani kitakachowazuia kutangaza kuwa Zanzibar ni nchi ya kiislamu ndani ya Muungano? Si ground work imeshafanywa katika suala hili la O.I.C? Kusema kuwa suala hili haliko kidini ni kujaribu kutudanganya maana ni wingi wa waislamu Zanzibar ndiyo unaotumiwa kama kigezo. Kigezo ni zanzibar kama nchi yenye waislamu wengi haitendewi haki na serikali ya Muungano ambayo haina dini. Kwa kufanya hivi mnageuza kuwa identity nchi ya Zanzibar ni uislamu. Kwa maneno mengine ni de facto nchi ya kiislamu. Ni hatua fupi kugeuza hili kuwa de jure!
 
Jamhuri ya Muungano ikaahidi kulifuatilia suala hilo ili kuingiza Jamhuri kwa manufaa ya wananchi wote wa Jamhuri. Zanzibar ikawa mvumilivu na ikaa kusibiri huo mchakato. Mchakato ndio huu-unaishia katika malumbano yasiyo miguu wala mikono. Verdict- Kama Jamhuri ya Muungano inashindwa kulielekeza suala hili katika mtizxamo wa manufaa ya Watanzania wote, basi na ijuiunge ili iiwezeshe Zanzibar kuendelea mbele na sera zake. Kugwaya kwa nini SASA?Jamhuri ya Muungano isiiyumbishe (na kuikwaza) Zanzibar, fahamu imeshakuwa stahamilivu (tokea ilipojitoa) hadi leo hakuna follow up ya maana ya kukidhi matakwa yao.

Kwani JMT iliahidi kujiunga na OIC kwa manufaa ya wananchi wote hao kufanya uchambuzi wa kina na baadae kuamua kama iingie au isiingie? Je JMT ikiona kuwa kujiunga huko hakuna maslahi kwa taifa kwa jumla basi ijiunge tu kwa kuogopa kuikwaza Zanzibar?
 
Kwani JMT iliahidi kujiunga na OIC kwa manufaa ya wananchi wote hao kufanya uchambuzi wa kina na baadae kuamua kama iingie au isiingie? Je JMT ikiona kuwa kujiunga huko hakuna maslahi kwa taifa kwa jumla basi ijiunge tu kwa kuogopa kuikwaza Zanzibar?
Zanzibar ni Nchi ndani ya Jamhuri ya Muungano (nukuu ya Jakaya Kikwete). Jee ni zipi haki za nchi hiyo (Zanzibar) ndani ya Jamhuri?
 
Zanzibar ni Nchi ndani ya Jamhuri ya Muungano (nukuu ya Jakaya Kikwete). Jee ni zipi haki za nchi hiyo (Zanzibar) ndani ya Jamhuri?

Ninachofahamu mimi kuwa wana haki ya kutendea watakavyo machogo tukiwa ndani ya JMT. Kutuambia tubebe pasi kuingia kwao maana sisi ni vibaka. Kutuwekea vigingi kwenye ajira n.k. Lakini inapokuja mahusiano na nchi za nje au vyombo vya nje, hamna tofauti kati ya chogo na mzanzibari! Wote ni watanzania, raia wa nchi moja. Maslahi yao yataangaliwa kwa ujumla wao na si vinginevyo.
 
Mimi ningependa tuangalie mojawapo ya matatizo ya mahakama hizi za kadhi kama yaliyompata huyu binti wa miaka 13. Hii iliwasilishwa na KITIA kwenye mada zake hapa jamvini,,,, Je tukubaliane na hizi "sharia"?

Somalia: Girl stoned was a child of 13

31 October 2008

Contrary to earlier news reports, the girl stoned to death in Somalia this week was 13, not 23, Amnesty International can reveal.

Aisha Ibrahim Duhulow was killed on Monday, 27 October, by a group of 50 men who stoned her to death in a stadium in the southern port of Kismayu, in front of around 1,000 spectators.

Some of the Somali journalists who had reported she was 23 have told Amnesty International that this age was based upon a judgement of her age from her physical appearance.

She was accused of adultery in breach of Islamic law but, her father and other sources told Amnesty International that she had in fact been raped by three men, and had attempted to report this rape to the al-Shabab militia who control Kismayo, and it was this act that resulted in her being accused of adultery and detained. None of men she accused of rape were arrested.

“This was not justice, nor was it an execution. This child suffered a horrendous death at the behest of the armed opposition groups who currently control Kismayo,” said David Copeman, Amnesty International's Somalia Campaigner.

“This killing is yet another human rights abuse committed by the combatants to the conflict in Somalia, and again demonstrates the importance of international action to investigate and document such abuses, through an International Commission of Inquiry.”

Amnesty International has learnt that:

* Aisha Ibrahim Duhulow was reported as being 23, based upon a judgement on her physical appearance, according to one of the journalists who had reported the stoning. Her actual age was confirmed to Amnesty International by other sources, including her father.
* Her father said she had only travelled to Kismayo from Hagardeer refugee camp in north eastern Kenya three months earlier.
* She was detained by militia of the Kismayo authorities, a coalition of Al-shabab and clan militias. During this time, she was reportedly extremely distressed, with some individuals stating she had become mentally unstable.
* A truckload of stones was brought into the stadium to be used in the stoning.
* At one point during the stoning, Amnesty International has been told by numerous eyewitnesses that nurses were instructed to check whether Aisha Ibrahim Duhulow was still alive when buried in the ground. They removed her from the ground, declared that she was, and she was replaced in the hole where she had been buried for the stoning to continue.
* An individual calling himself Sheik Hayakalah, was quoted on Radio Shabelle saying:``The evidence came from her side and she officially confirmed her guilt, while she told us that she is happy with the punishment under Islamic law.'' In contradiction to this claim, a number of eye witnesses have told Amnesty International she struggled with her captors and had to be forcibly carried into the stadium.
* Inside the stadium, militia members opened fire when some of the witnesses to the killing attempted to save her life, and shot dead a boy who was a bystander. An al-Shabab spokeperson was later reported to have apologized for the death of the child, and said the milita member would be punished.

Background
Amnesty International has campaigned to end the use of the punishment of stoning, calling it gruesome and horrific. This killing of Aisha Ibrahim Duhulow demonstrates the cruelty and the inherent discrimination against women of this punishment.

The reports on this killing should be understood within the climate of fear that armed insurgent groups such as al-Shabab have created within the areas they control in Somalia. As Amnesty International has documented previously, government officials, journalists and human rights defenders face death threats and killing if they are perceived to have spoken against al-Shabab, who have waged a campaign of intimidation against the Somali people through such killings.

Since the death, a number of individuals have told Amnesty International they have fled from Kismayo out of fear of suffering a similar fate to Aisha Ibrahim Duhulow.


Nawasilisha
 
To JF,
please find the attached supposedly OIC charter,
lets digest it, then be the judges of our own destiny. The question being do we really want to subject our Tanzania to such????????
 
Mimi ningependa tuangalie mojawapo ya matatizo ya mahakama hizi za kadhi kama yaliyompata huyu binti wa miaka 13. Hii iliwasilishwa na KITIA kwenye mada zake hapa jamvini,,,, Je tukubaliane na hizi "sharia"?
Sheria ya kiislam hairuhusu hukumu ya kupiga mawe kwa alie repiwa na pia kwa mtu ambae haja olewa/owa,

TUELEWE tafauti kati ya sheria za kiislam na wavunjaji sheria, Somalia kwa sasa hakuna sheria na wananchi wake wametelekezwa na so called International community, Wa-Ethiopia na Wamarikani wote wanawapipiga mabomu mazitomazito hakuna Amnesty wala yoyote anae watetea, Wanaibuka tu wanaposikia chochote kinachoweza kuchafua Wislam bila kutafakari. Tumewafaamisha sheria Halisi zote kuusu Islam lakini wana-ignore iliwakamilishe agenda zao.

MAHAKAMA YA KADHI HAITODILI NA MAKOSA YA JINAI BALI ITADILI NA MASWALA YA JAMII, TUMESHA SEMA SANA HAYA NAKURUDIA KILA SIKU, HATUTACHOKA TUTENDELEA KUWASOMESHA
 
Back
Top Bottom