Mwanakijiji,
Mkuu wangu hapa umelewa! nakuaminia sana katika fikra huru lakini kusema kwamba Hatuwezi kujiunga na jumuiya fulani kwa "manufaa" ya sehemu moja ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Ni sawa na kusema hatuwezi kujiunga na jumuiya fulani kwa "manufaa" ya kundi moja la wananchi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania... yet tumejiunga na jumiya za wanawake duniani na Mama Mongella alikuwa secretary General.. Na ni katiba hiyo hiyo inaweza kutumiaka kupinga kitu kile lakini kwa sababu mazngira tunayoishi ndiyo yanasukuma baadhi ya ibara za katiba kuwa na nguvu na zenye msisitizo ktk haki za wananchi wake.
Hivyo hivyo katika swala la Muungano, values za Wazanzibar kama Waislaam ni lazima ziwe sababu kubwa kwao kuweza kuhakikisha hawapotezi values hizo ktk Jamhuri yetu..
Mkuu nina hakika kabisa kama Bara tungekuwa na asilimiam 99 ya wakristu na kuna baraza la wakristu duniani linalosajiri nchi za kikristu, tusingekuwa na mjadala huu hata kidogo. Rais, iwe Nyerere, Mwinyi, Mkapa ama Kikwete wote wangepitisha bila hata kumuuliza mtu..
Mkuu hili ni baraza tu la nchi za kiislaam ambalo lina malengo sawa kabisa na mabaraza mengine yanayokusudia kuendelea Umma wake kwa kupitia mijadala..
Sioni kitu kikubwa ambacho wewe unakizungumzia unaposema wakiondoa hiki ama kile.. Mkuu ni sawa kabisa na mkeo anayetaka kwenda ktk maandalizi ya Kitchen party unaanza kutazama orodha ya maandalizi kama Mwanaume na kutoa suggestion ambazo zinapinga women to be women..Ulichoombwa ni ruksa yako tu..Mkuu wewe hauhusiki na Kitchen party hivi kweli utaweza kuvaa khanga hata wakikualika?..
Ogah,
Bob,
Ndoa ni makubaliano........na mkishakubaliana...mnaweka mi/uongozo (katiba) ili kudumisha familia........ndoa nyingi zilizo na matatizo ni zile zilizokosa makubaliano ya miongozo.......sasa basi kama mume/mke anakuja na matakwa nje ya miongozo iliyopo inabidi tuelimishane na kufikia muafaka................
Hapa mkuu nipo nawe kuwa ndoa ni makubaliano lakini mkuu huwezi kufikiria yote ya kike isipokuwa yale yanayowahusu kwa wakati ule kudumisha ndoa hiyo kama Mume na Mke..
Hakuna ndoa ambayo inaanza na kusema hakuna mwanamme kwenda mpirani ama mwanamke kucheza Upatu...Haya ni mambo unakutana nayo ktk ndoa na utayategemea kuwepo, after all OIC imenzishwa baada ya muungano wetu..
Mara nyingi mkuu ndoa huvunjika nje ya makubalinao ambayo hugusia maswala ya msingi kama vile tutakuwa sote kwa mabaya na mazuri. shida na raha, uzima na Ugonjwa lakini pamoja na makubaliano haya sababu nyingi huwa zinatoka nje ya makubaliano. Tunafunga ndoa zetu kama wajibu kwanza kisha mategemeo ya ndoa zetu ni pamoja na kuanzisha familia mpya, security, kuondoa Upweke, na kadhalika hivyo kuna mipaka ya mtazamo krk ndoa. Na mara nyingi ndoa hutegemea (WATU) wahusika kiasi kwamba dini, kabila, elimu, afya vinaweza badilisha makubaliano ya ndoa moja hadi nyingine..
Mahala (MAZINGIRA) mnapoishi pia kunaweza kutofautisha ndoa moja hadi nyingine kwani Ukimuoa Msukuma Usukumani maswala la kulima, ufugaji na kadhalika yanaingia moja kwa moja kisha jioni kuna Chimpumu ama gongo, hakuna bills za umeme wala maji..Kama mwanaume ukirudi nyumbani lazima unaimba sana kwa kusikifia, kuita mali zako ukiwa mita 100, tofauti na wakazi wa mjini ambao mnatumia usanii mwingine..
Tatizo langu kubwa ktk swala hili la OIC halihusiani na yote haya isipokuwa sehemu moja tu.. Pale unapoweka vikwazo kwa mke/mme kushiriki ktk vikao vya imani yake ya kidini kwa sababu tu wao ni dini tofauti na wewe hali mkeo ni dini hiyo..kisha unadai kwamba huna ubaguzi wa dini na ati kama ungekuwa na ubaguzi usingemuoa!..
Sababu kubwa unayotumia kupinga inatokana na malengo ya dini yake kutokana na mwongozo wa kitabu cha dini hiyo kuanza kuchambua yale usiyokubaliana nayo wakati hakuna hata sehemu moja inakushirikisha wewe kama mlengwa wa mikutano hiyo...Zaidi ya yote haya ndio maana wewe hukuwa dini hiyo in the first place kutokana na kutokubali imani ya dini hiyo iweje leo utake kubadilisha sura za dini hiyo wakati huna imani nayo!
Ogah,
Bara tunatumia sana bendera ya taifa (jina la Tanzania) kuchukua misaada kibao nje na uwekeshaji wake unakwenda bara..ziko kibao na wala hatuna aibu.. Chukulia mfano mdogo tu wa Richmond,(sijui kama nimekosea) fedha iliyotumika sio fungu la halmashauri ya mkoa wa Dar na uzembe umefanyika na viongozi wa bara, yet deni la Taifa linapohesabiwa Zanzibar wamo na bado wanakatiwa umeme kutwa kila wanapopiga kelele!..Miradi kibao ya Kitaifa imetazama Bara kuliko Zanzibar na bado wao wamefungwa ktk Muungano kutoweka deal za nje...
Mkuu kama utasoma vizuri yote yaliytotangulia ktk mada hii utaona chuki na udini mkubwa ambao umefikia hata watu kuutazama Muungano kwa jicho la kidini..
Cha ajabu zaidi watu wanatumia neno misaada kuwa ndio sababu kubwa ya Zanzibar kujiunga, let me tell them something, hakuna maendeleo yoyote ya nchi yoyote duniani kama haina mikopo hata Marekani leo hii inadaiwa mabillioni na China..
Neno misaada lisitumike kama Tanzania itapata fedha ama mafuta bure isipokuwa tunakuwa na mipango ya biashara kati ya nchi zinazohusika hata kama zimepatikana kwa njia tofauti..
Msaada (Aid) inaweza kuwa mtaji ambao utarudishwa kama vile sisi tunavyopata ama kutoa mikopo kwa mtu unayemfahamu na kumwamini (jumuiya)..Lakini wakati huo huo akija mtu usiyemfahamu mkopo wako unakuwa na masharti magumu kuhakikisha fedha yako itakuwa salama na ndio hali inayotukuta toka nchi za Magharibi...
Tatizo la wengi hapa tumezoea kibongo Bongo yaani neno Msaada ni fedha ya Bure!..
Ukimpa mtu usimuulize hata kaitumia vipi unatafuta ugonvi..Na ni kwa sababu hatuna Utaratibu kama huo ndio maana Unaona Mafisadi nchini wakiiba fedha kutafuta mtaji, hakuna njia nyingine zaidi ya kuiba kama hujajaliwa.
Hivyo basi Zanzibar wanataka kuingia chama, pengine niseme Upatu ambao sisi wanaume wa bara tunataka kujua hizo Khanga, wanja na heleni zina faida gani kwetu!... wakuu mambo ya kike haya mnataka ku reason vitu ambavyo mwanamke hatakuelewa kabisa!.. Mkeo akiwa na furaha ndani ya nyumba, ndoa huzidi kuboreka.