Juu ya OIC na Mahakama ya Kadhi

Juu ya OIC na Mahakama ya Kadhi

Masuala ya wanawake yanatambulika rasmi serikalini. Tunao mawaziri na wizara zinazoshughulika na mambo ya wanawake. Leo hii tuna wizara inayoshughulikia mambo ya wanawake wizara ya Jinsia na Watoto. Sidhani kwa mtiririko huo tutahitaji kuwa na wizara inayoshughulikia mambo ya waislam!! Kwani sasa itakuwa rasmi na itabidi kuwe na idara ndani ya serikali itakayoshughulikia suala hilo.

Suala la wanawake ni rasmi serikalini ndio maana nchi inawakilishwa kama nchi.
 
1.
Field Marshall Es,

Kwa mtazamo wako nakuomba utazame vyombo vyote vya kimataifa ambavyo Tanzania ama nchi nyingine zimejiunga hali nchi zao sio ya watu ama kundi fulani la watu..Tazama wanawake, watoto Yatima, vilema na kadhalika..
Maswali ayko yote yaweke ktk vifungu hivyo pia pengine unaweza kunipa jibu tofauti na OIC ikiwa unakubali ni chombo cha waislaam lakini wakati huo huo unasema nchi yetu haina dini..

Bob kwenye hii ishu ya wanawake, vilema, na watoto au the rest huna hoja bro kwa sababu tunawakilishwa wananchi wote kwenye hizo Jumuiya, yaani wa-Tanzania wote na sio kikundi flani cha dini kama unavyotaka tuamini, kama ni wawake wanawakilishwa wanawake wote wa bongo sio wa dini flani tu!

2.
Kwanza una maana gani unaposema nchi yetu haina dini?..

Nina maana kwamba Tanzania, kama taifa hatuna officially dini ya kutuwakilisha taifa, kama Iran na Pakistan ambazo ni nchi za kii-Isilamu na pia hatutumii Sharia kama our guiding force behind our natinal laws, simply put ni kwamba Tanzania sio taifa la Wa-Isilam kama masharti ya OIC yanavyotaka ili kuwa member wao.

3.
Kumbuka mkuu Tanzania sio sawa na Urusi ama China ambao kutokuiwa na dini wao walikuwa wanaamini Ukomunist.. Sisis hatuna dini kwa maana hakuna dini moja inayokubalika zaidi ya nyingine ktk misingi ya Utawala. Hivyo Hata Bungeni huwezi kutumia misingi ya dini yako kupinga ama kutoa maamuzi dhidi ya muswada..
Kwa mfano mdogo tu Mashoga..
Ikiwa bungeni litakuja swala ama muswada unaohusiana na haki za mashoga haitakiwi mbunge ama kiongozi kubase judgemnet zake kwa kutumia imani yake ya dini, hata kama swala hilo linahusiana na imani ya dini yako..Kataa ushoga kwa kutumia culture yetu ama vitu vingine nje kabisa ya dini yako kwa sababu kila mmoja wetu akiingiza dini kutoa maamuzi hatuwezi kujenga kitu..
Kwa hiyo tusijaribu kupotosha maana ya Tanzania haina dini kwa maana kuwa hakuna dini ama dini haziruhusiwi isipokuwa mrengo fulani wa kisiasa. Dini zinaruhusiwa na zina kila haki ya kujiendeleza na mkono wa serikali ni lazima kuhakikisha haki hiyo inapatikana. Laa sivyo mkuu kila mmoja wetu atatumia Udini na tutavuana mashati kuhusiana na Ukatoliki nchini..kwa sababu nitajiuliza maswali kama yako kuhusiana na Vatican na mwisho wa yote ni kutokukubali wakristu wafuate dini yao ktk ibada zao..

Hakuna hoja hapa, Vatican sio shirika la dini kama OIC that is the bottom line, uamuzi wa kujiunga na hilo shirika ni wa serikali ya Jamhuri kikatiba yetu, sio kundi flani la dini, ya Vatican hayahusu anything na OIC shirika la wa-Isilamu,

Tanzania ni taifa lisilo la Wa-Isilamu, sasa hatuwezi kujiunga na shirika la dini ya Kii-Isilamu, sihitaji kuwa professor kuelewa hili kuwa ni haliwezekani kabisa tena hata kidogo, never!.
 
Ogah,
Mkuu kama kweli unafikiria hivyo basi mkuu wangu una ubaguzi ndani ya roho yako, kwa namna fulani unafikiria kwamba wanawake wanafanya njama fulani against wanaume na unapenda kujua kinachoendelea mle ndani hata kama vitu vyote viko wazi..At the same time wanawake hawa question kila wanaume wanalolifanya tunawaona wao wajinga ama watumwa wetu..

....hivi kuna sehemu nimesema hivyo Bob......!!!
 
Masuala ya wanawake yanatambulika rasmi serikalini. Tunao mawaziri na wizara zinazoshughulika na mambo ya wanawake. Leo hii tuna wizara inayoshughulikia mambo ya wanawake wizara ya Jinsia na Watoto. Sidhani kwa mtiririko huo tutahitaji kuwa na wizara inayoshughulikia mambo ya waislam!! Kwani sasa itakuwa rasmi na itabidi kuwe na idara ndani ya serikali itakayoshughulikia suala hilo.

Suala la wanawake ni rasmi serikalini ndio maana nchi inawakilishwa kama nchi.

......nafikri Kipima pembe hili suala la wanawake kulinganishwa ktk hii issue umeliweka sawia kabisa....its very clear......tofauti ni kubwa mno
 
Kuna madhara kujiunga na OIC. Hii ni taasisi au jumuiya ya nchi za kiislam. Inasema na katiba yake inajiainisha hivyo. Tanzania kuna waislam, kwa nini wasiwakilishwe? Wana haki ya kuwakilishwa ikiwa wataunda nchi ya kiislam ndani ya Tanzania. Kwa sababu OIC hawawakilishwi mwislam mmoja mmoja. Ni lazima wawakilishwe kama nchi. Tatizo sasa liko wapi ikiwa Nchi ya Tanzania yenye waislam itajiunga?

Tatizo ni kuwa katika Tanzania serikali italazimika kuangalia dini za watu katika utendaji wake. Itakuwa imeingiza rasmi dini ndani ya serikali. Mkuu wa nchi ni rais. Uwakilishi wa Tanzania katika mikutano ya OIC itakuwa ni lazima ateuliwe mwislam. Kiutendaji rais atalazimika kuuliza hivi furani dini gani? Kama kutakuwa na kamati au taasisi ya kuratibu mahusiano yetu na OIC itakuwa lazima taasisi hiyo iwe na composition ya waislam. Ikiwa uteuzi utatakiwa, rais si Mwislam, akamteua Mwislam ambaye hakubaliki kwa baadhi ya makundi ya waislam tayari kiutendaji rais atakuwa amefanya maamuzi yahusuyo imani yatakayo mwingiza katika mgogoro wa kiimani. Hilo ni tatizo ingawa sasa hivi hatulioni kwa kuwa ajenda ni kuingia. Sema utaundwa mfumo wa uwakilishi ambao hautahusisha watendaji wa selikali moja kwa moja, lakini kumbuka wanaenda kuwakilisha nchi! Maazimio yatakayopitishwa yataridhiwa na nchi, vipi ikiwa maazimio yenye madhara kwa makundi mengine ya kidini yatakapopitishwa na kuridhiwa na nchi? Si yatakuwa sheria?

OK watu wanasema nchi so and so ni wanachama na hayo madhara hayajatokea kwa nchi hizo. kumbuka katika uendeshaji wa nchi kuna mambo mengi hatuyaoni, hasa yanayozihusu nchi zingine. Jiulize kwa nini ukabila inakuwa tatizo Burundi kwenye makabila mawili usiwe tatizo Tanzania kwenye makabila 120? Kila nchi inatofautiana na nyingine. Dini katika uendeshaji wa nchi inaweza isiwe tatizo Kenya lakini ikawa tatizo Tanzania, Kama vile ukabila ulivyo Tatizo Kenya na si Tanzania. Ni lazima kuchukua tahadhari hasa unapodeal na mambo yanayogawa watu kama dini.

OIC wanataka wanachama kutoka nchi za kiislam, wanajadili masuala yanayowahusu waislam. Tanzania kuna waislam lakini si nchi ya waislam pekee.

Hili suala la Vatican sijui kwa nini kila hoja hii inapojadiliwa lije. Kwanza Vatican haisajili wanachama. Vatican in Ubalozi tanzania kama walivyo na Ubalozi nchi zingine. Hivi kuna mikutano Vatican huwa Tanzania tunawakilishwa kama nchi? Hivi kuna maazimio ya mikutano ya Vatican ambayo yakitolewa huko Tanzania kama nchi inayaridhia? Hivi Tanzania kama nchi inashiriki kutunga katiba na taratibu zinazoendesha Vatican? Kwa nini hili liwe linajitokeza linapojadiliwa OIC. Kuna nchi nyingine wanachama wa Vatican? Hivi Vatican kuwa na Ubalozi Tanzania ina maana Tanzania kama nchi ni Mwanachama wa Vatican. Pengo akienda Vatican anawakilisha serikali au anatumia bajeti ya serikali? Hivi muundo wa vatican ni kitu ambacho Tanzania kama nchi imehusika? Kweli raia wa Tanzania anaweza siku moja akawa papa, Lakini atakuwa anaiwakilisha Tanzania kwenye upapa? Hivi ni vitu visivyofanana.

Vatican siyo Conference of Catholic States. Vatican ina muundo wake ambao unawahusu wakatoliki kama wakatoliki. Balozi wa Vatican ni Balozi kama walivyo mabalozi wengine. Labda ikiwa kuna mtu atasema yule hadhi yake inayotambuliwa serikalini ni tofauti na mabalozi wengine. Ikiwa Tanzania tuna Balozi vatican je yule balozi ana hadhi tofauti na balozi aliyeko Urusi au Uchina?


Kudos to Kipimapembe........this is one piece from you Kipimapembe ambacho Membe na wabunge inabidi wakisome na kuelewa.....na sio ushabiki...............
 
About OIC

The Organization of the Islamic Conference (OIC) is the second largest inter-governmental organization after the United Nations which has membership of 57 states spread over four continents.

The Organization is the collective voice of the Muslim world and ensuring to safeguard and protect the interests of the Muslim world in the spirit of promoting international peace and harmony among various people of the world.

The Organization was established upon a decision of the historical summit which took place in Rabat, Kingdom of Morocco on 12th Rajab 1389 Hijra (25 September 1969) as a result of criminal arson of Al-Aqsa Mosque in occupied Jerusalem.


In 1970 the first ever meeting of Islamic Conference of Foreign Minister (ICFM) was held in Jeddah which decided to establish a permanent secretariat in Jeddah headed by the organization's secretary general. Prof Ekmeleddin Ihsanoglu is the 9th Secretary General who assumed the office in January 2005 after being elected by the 31st ICFM.

The present Charter of the Organization was adopted by the Eleventh Islamic Summit held in Dakar on 13-14 March 2008 which laid down the objectives and principles of the organization and fundamental purposes to strengthen the solidarity and cooperation among the Member States. Over the last 38 years, the membership has grown from its founding members of 30 to 57 states.

The Organization has the singular honor to galvanize the Ummah into a unified body and have actively represented the Muslims by espousing all causes close to the hearts of over 1.5 billion Muslims of the world.

The Organization has consultative and cooperative relations with the UN and other inter-governmental organizations to protect the vital interests of the Muslims and to work for the settlement of conflicts and disputes involving Member States.

In safeguarding the true values of Islam and the Muslims, the organization has taken various steps to remove misperceptions and have strongly advocated elimination of discrimination against the Muslims in all forms and manifestations.


The Member States of the OIC face many challenges in the 21st century and to address those challenges, the third extraordinary session of the Islamic Summit held in Makkah in December 2005, laid down the blue print called the Ten-Year Program of Action which envisages joint action of Member States, promotion of tolerance and moderation, modernization, extensive reforms in all spheres of activities including science and technology, education, trade enhancement, and emphasizes good governance and promotion of human rights in the Muslim world, especially with regard to rights of children, women and elderly and the family values enshrined by Islam.
 
The Organization is the collective voice of the Muslim world and ensuring to safeguard and protect the interests of the Muslim world in the spirit of promoting international peace and harmony among various people of the world.

The Organization was established upon a decision of the historical summit which took place in Rabat, Kingdom of Morocco on 12th Rajab 1389 Hijra (25 September 1969) as a result of criminal arson of Al-Aqsa Mosque in occupied Jerusalem.

Tanzania hatuwezi kujiunga na hii Jumuiya, we just can't.
 
Labda nianze na mmoja mmoja kuweza kuyajibu yote pamoja na kwamba nimeandika karibu kurasa mbili hakuna mtu alojibu langu isipokuwa kuongezea maswali juu..

Field Marshall Es,
Unaweza kunambia maswala ya wanawake yanawahusu vipi wanaume na imekuwaje wanaume hawahusishwi ktk jumuiya hiyo ya wanawake lakini bado ni swala la Kitaifa.

Kipimapembe,
Mkuu nimekuuliza kuhusu wanawake bado hujanijibu zaidi ya kusema rais atahusika. Sikuona maswali hayo hayo yakijibiwa kuhusiana na wanawake..unless unataka kunambia Wanawake ni swala tofauti na kwa zipi zinafanya kuwa tofauti ikiwa mimi ninayepinga kujiunga kwao kunatokana na Uume wangu. Ndivyo navyoelewa kuwa unapinga kwa sababu wewe sio Muislaam kwa hiyo unatumia zaidi imani yako dhidi ya Uislaam..
Labda nikuongezee kidogo swali hapa, hivi papa alipotembelea nchi yetu na fungu la serikali lilitengwa kwa ajili ya msafara wake nchini, hii ilikaa vizuri kweli kwa Waislaam... na inakuwaje rais Kikwete atembelee viongozi wa dini kama kina Pengo, shughuli za kidini hata kupewa ushauri hali nchi yetu sio ya kidini?. Huoni kwamba rais wetu pia amejihusisha na maswala ya dini moja kwa moja ikiwa ni pamoja na kutoa misaada kujengwa makanisa ama misikiti!..Wewe ulitaka rais awe mbali kiasi kipi maana kutojihusisha kwako kuna mengi!

Ogah,
Mkuu soma bandiko lako lililotangulia umesema utapenda kuelewa kuhusiana na Mama Mongella na hicho chombo cha Wanawake au nime quote vibaya sio wewe!

Wakuu, nafikiri mgonjwa Ukimwi aliuliza swali zuri sana.. kujiunga kwetu na OIC kutapunguza nini haki za watu wengine na kuna ubaya gani?..
 
Ni kweli kabisa kuwa OIC ni jumuiya ya Waislaam..sasa uinavyofikiria wewe Waislaam hawana haki ndani ya nchi isiyokuwa na dini?..Ikiwa wanazo haki kwa nini nchi isiwasaidie na kutambua haki zao wakati nchi inatambua hata haki za Mashoga Kwani nchi hii ni ya Mashoga! Tumejiunga na jumuiya za wanawake kwani nchi hii ni ya Wanawake watupu! yaani hata siwaelewi mnakojaribu kupeleka hoja hii...

Mkuu Mkandara,

Ni kweli waislamu wanayo haki ya kujiunga na jumuiya yao. Ingekuwa hiyo OIC ni jumuiya ambayo waislamu wanajiunga wenyewe katika taasisi zao, wala hakuna ambaye angepiga kelele. Kwa mfano, Christian Council of Tanzania (CCT) ni mwanachama wa World Council of Churches (WCC), na hakuna anayepiga kelele, kwa sababu dola ya Tanzania haijajiunga huko, ni CCT ndio imejiunga. Sasa kama mtu angezuia chombo cha waislamu kujiunga na OIC mimi pia ningepiga kelele sana, kwamba jamani waacheni wenzetu wajiunge katika chombo chao chenye manufaa kwao kiimani. Kwa hiyo jumuiya ya kiislamu kujiunga kwenye jumuiya pana zaidi ya kiislamu, hapo ni sawa kabisa. Lakini suala la OIC ni nchi isiyokuwa ya kidini inazungumziwa kujiunga na jumuiya ya kidini, hili si sawa hata kidogo. Kinachopingwa hapa ni nchi (dola) yenye waislamu na wasio waislamu kuingizwa kwenye chombo ambacho msingi wake ni kusimamia imani na maslahi ya kundi moja tu la waislamu. Hilo ndilo tunalopinga.

Ningekuwa na uwezo wa kuishauri OIC ningewaambia katika nchi ambazo si za kidini kama Tanzania, waruhusu jumuiya zinazowakilisha waislamu kujiunga huko OIC badala ya kusisitiza uanachama wa nchi. Yaani iwe uanachama huko ni wa waislamu, na si lazima iwe dola. Katika zile nchi za kiislamu, waendelee na utaratibu wa uanachama kama ilivyo sasa. Nadhani suala kama hili serikali zenye nia za kutetea maslahi ya waislamu kama sehemu ya wananchi wake zingepeleka mapendekezo kama hayo. Mtu kama Bernad Membe katika nafasi yake kama Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje, badala ya kauli sumbufu hizi anazotoa sasa hivi, angeweza kushauriana na nchi nyingine zenye waislamu ambazo si wanachama wa OIC wakapeleka wazo kama hili huko OIC. Wawaambie tu jamani waislamu wa nchi zetu wanapenda kujiunga nanyi, lakini serikali zetu hazina dini, serikali zetu haziwezi kujiunga, mnaonaje mkawaruhusu wakajiunga kupitia taasisi zao? Ninaamini OIC ina wasomi wengi waliobobea, hawashindwi kutafakari jambo kama hili na kulipatia suluhisho. Na hapo assumption yangu ni kwamba hakuna jumuiya nyingine ya kimataifa inayounganisha waislamu wote duniani (nahitaji kusahihishwa hapa, maana sijui kama ipo au haipo). Lakini hata kama zipo jumuiya nyingi tu za namna hiyo, waislamu bado wanayo haki ya kujiunga na jumuiya yoyote ile wapendayo.

Kuhusu mashoga, kwa ufahamu wangu bado Tanzania haitambui kinachoitwa "haki" za watu hao, maana bado katika sheria zetu ni kosa la jinai kufanya ulawiti hata kama wahusika wameridhiana.

Sijawahi kusikia jumuiya ya wanawake watupu ambayo Tanzania kama nchi imejiunga, lakini hata ingekuwepo kweli ingefaa kuungwa mkono kwa sababu wanawake ni sehemu ya jamii ambao masuala yao yanawabeba wanaume pia, yaani wanabeba jamii nzima. Kwa hiyo ukizungumzia wanawake ni sawa na kuzungumzia watu wote maana hawa wanatuzaa na kutulea sote, wake kwa waume. Ndio maana nchi nyingi zina wizara za masuala ya wanawake. Maslahi ya wanawake yanabeba maslahi ya wanaume pia. Na humo ndani ya jumuiya za wanawake kuna wanawake wa dini zote. Kwa hiyo hapa mfano wa jumuiya ya wanawake na hiyo OIC haviendani hata kidogo.
 
Field Marshall Es,

Unaweza kunambia maswala ya wanawake yanawahusu vipi wanaume na imekuwaje wanaume hawahusishwi ktk jumuiya hiyo ya wanawake lakini bado ni swala la Kitaifa.

OIC: The Organization has the singular honor to galvanize the Ummah into a unified body and have actively represented the Muslims by espousing all causes close to the hearts of over 1.5 billion Muslims of the world.

Ni kwa sababu wanawakilishwa wanawake wa taifa letu zima la Tanzania, Wakristo, Waisilamu, Wapagani, na tunaye waziri wa kina mama na watoto lakini hatuna waziri wa wanaume.
 
Kithuku,
tatizo la hoja yako ni kwamba unataka Waislaam WAIGE walichofanya Wakristu wakati hizi ni dini mbili tofauti zenye utawala tofauti...
Mnachoshindwa kutazama hapa ni kwamba Uislaam ni kitengo kimoja cha jumuiya ya Watanzania na wana mambo ambayo sio lazima yawemo ktk Ukriostu ama dini nyingineyo..
Jumuiya za Kikristu zimepangwa ktk mifumo ambayo tayari nchi zimekwisha ukubali Ukristu na wameweza kuingiza dini kabla hata Taifa halijaundwa. kwa hiyo vyombo vyote vya dola vinautambua Ukristu na mumeweza kuunda Tawala kwa kutumia dini.

On the other hand Waislaam hawana nchi, hawana chombo ambacho kinaweza kutawala maswala ya dini kwani hakuna imani hiyo ndani ya Uislaam kwa sababu Uislaam ni IMANI sio chombo kinachoweza kuundwa na Binadamu..
Na kama ungekuwa msdomi mzuri wa Uislaam ungeelewa kwamba Muislaam ni yule anayefuata ibada za mwenyezi Mungu, hapo wewe unaweza kuwa Muislaam bora hata kuliko mimi..Hakuna Mungu mtu na hakuna kiranja isipokuwa kitabu Kuran.
Haya ndio aliyoyafanya Nyerere na Bakwata na ndio maana hadi leo tuna matatizo makubwa pamoja na kwamba ni Idea nzuri sana..
Pili, Hili swala la OIC limetokana na Umaskini wa Waislaam, limetazama dola nyingi duniani zinavyo wadunisha Waislaam na kuwanyima haki zao kiasi kwamba wamekuwa lebelled kama mtu mweusi ktk maswala ya race..Hivyo, wameamua kuunda chombo cha kusaidia nchi ambazo kwa lugha nzuri zinakubali Uislaam kama ni dini ya mwenyezi Mungu...
Ni kitu kama IMF vile isipokuwa inalenga nchi ambazo zina hesabu kubwa ya Waislaam..Ukitazama IMF inalenga nchi maskini na ni lazima kuwepo na hesabu kubwa ya wananchi maskini pamoja na kwamba wanaweza kabisa kusaidia nchi ambazo sio maskini..Sasa nikitumia mtazamo wako nchi tajiri kila siku zinapiga kelele kwa nini wanasaidia nchi maskini, mawazo ambayo ninayaona hapa kutoka upande wa pili..Cha ajabu ni kwamba fedha hizo zinatoka kwa nchi za Kiislaam ingekuwa kodi za wananchi ningesema kweli hapa kuna Utata lakini hata hivyo kuna mengi ya kidi9ni tunatumia mifuko ya serikali na hakuna matatizo..
Muslim wanahitaji imani zenu, msaada yenu ni kuwakubali, kudumisha udugu kama tulikuwa nao ktk mila zetu kiasi kwamba humtazami jirani yako kwa dini yake...
Humkaribishi mgeni kwa kutazama dini yake.. familia zetu zimeundwa kwa mchanganyiko wa imani za dini na itakuwa kupoteza Utamaduni ambao tayari tumekwisha ujenga tukianza kutazama mgeni anayekuja nyumbani kwetu ni dini gani na kwa nini ndugu yako anamleta rafiki yake nyumbani hali wewe dini tofauti.. Ati hiyo nyumba sio ya Waislaam kuja kusoma kuran..Haya sio malezi yetu na hatukulelewa hivyo kabisa.
Mbona zamani wazee wetu walifanya haya bila matatizo?.. ilikuwa sii ajabu kumwona malecela akimwita Sheikh kuja kusoma dua nyumbani wala padre fulani kuja kumbatiza mtoto ama kutoa mashetani nyumba ya Muislaam...
Kama kuna tiba ya mmoja wetu iwe hata inatoka kwa mtu tusiyempenda baadhi yetu nadhani ndio hoja yangu kubwa hapa.. yaani kupona kwa mgonjwa huyo na sio nani amekuja kumtibu.
 
Field Marshall Es,
Na hiyo OIC ni kwa sababu inawakilisha Waislaam wetu wa Tanzania kama hao wanawake!
Umesema tunaye waziri wa wanawake lakini hatuna waziri wa wanaume! Je, huoni kama hii haikukaa vizuri? kama unaikubali then itakuwa hivyo hivyo Wakristu ni sawa na wanaume na sisi kina Yakhe waislaam ni wanawake zenu!... Tunahitaji msaada..
 
Mkamap,


Mkuu hata sijui niseme kitu gani...unapotumia IMF kuwa mfano wa Vatican. Yaani ni vitu viwili ambavyo havifanani kabisa..Kitumbua mkuu sio Andazi.
Kwa nini nasema hivyo IMF imeanzishwa kama Taasisi kisha ikatafutiwa makao makuu ambayo yanaweza kuhama kesho na kuwa nchi nyingine yoyote bila utata wowote..Lakini sio Vatican na Utawala wake, pengine ungenambia CCM ya Nyerere ya chama kimoja ni sawa na Ukatoliki na Vatican, chombo cha siasa ambacho kimeanzishwa na kuiendesha nchi - Tanzania..
Sasa huwezi kutenganisha CCM kama chama na Tanzania kama nchi kwani bila CCM Uhuru wa Tanzania ungekuwa na sura ama historia tofauti...Na Vatican kama CCM ya Nyerere haina Upinzani yaani mgombea huyo Papa anachaguliwa na Vatican wenyewe kina Pengo ambao ni raia wa Tanzania. Uliona wapi mfumo wa nchi namna hiyo! na hizo logic unazotumia..
Kwa hiyo tunapozungumzia kuwa Vatican ni nchi ni muhimu sana kutazama ni kitu gani kinaifanya nchi kuwa nchi kama mjadala huu unavyoendeshwa... Ikiwa kweli Vatican ni nchi iweje Pango na Makadinali wengine nchi tofauti duniani washiriki kupiga kura za uchaguzi wa rais wao na mtu yeyote toka sehemu yoyote duniani anaweza kuwa rais ama kiongozi wa juu wa nchi hiyo mnayotaka kuipa jina la NCHI!..Kesho Pengo, raia wa Tanzania anaweza kuchaguliwa kuwa Papa - rais wa Vatican how come?..Huyo aliyepo leo ni raia wa wapi? Vatican au Germany!..
Ukinijibu hayo tutaendelea..
Iran ni nchi ya waislaam kama vile Tanzania ni nchi ya weusi, lakini huwezi kusema mapinduzi ama kutokubaliwa kwa Utawala wa Somalia kimataifa kuna direct affect kwa watu weusi wote na kwamba pengine inaweza kufananishwa na swala la Vatican..
Nimekwisha kwambia hata kesho ondoa Uhusiano na Iran au Saudia haiwezi kuwa sababu ya waislaam kupiga kelele kwani hatuna ushirika kwa lolote zaidi ya kuwa makao makuu kama ilivyokuwa Adis Ababa, Ethiopia kuwa m makao makuu ya OAU enzi za Haile Marium. Kuondolewa kwake hakuna maana kunatuhusu Tanzania na nchi za Kiafrika..

Field marshall es,
Mkuu unazidi kuyumba hapa hujanijibu kitu kweli!

Mkuu
Hoja yako dhaifu,wewe unataka kulazimisha mfumo wa serikali unaouelewa wewe basi ndio mfumo sahihi.Kumbuka mfumo ni jinsi ya makubaliano ya wananchi na si wewe unavyotaka lazima iwe.

Mfano sisi watanzania tunaweza kubaliana kabisa kuwa nchi yetu imepoteza mwelekeo hivyo basi tunataka RAIS awe mzungu na atoke SWEDEN na watakao mteuwa ni mapadri na mashehe kote duniani tunapitisha ktk katiba na inakuwa.

Wenda hata NENO katiba linakupa utata kidogo ama vipi?

Kama unakumbu kumbu kipindi kile PAPA alipo sema maneno fulani kuhusu Mtume mhamed aliwaita mabalozi wa nchi za kiislamu na akaongea nao.Swali hao mabolizi wa nchi za kiislamu ?? wewe unapata picha gani?

Elewa Tz haiwezi kujiunga na VATICAN ila zitashirikiana ktk mambo ya kidiplomasia.
VATICAN sio taasisi ila catholic ndiyo taasisi,
 
Na hiyo OIC ni kwa sababu inawakilisha Waislaam wetu wa Tanzania kama hao wanawake!
Umesema tunaye waziri wa wanawake lakini hatuna waziri wa wanaume! Je, huoni kama hii haikukaa vizuri? kama unaikubali then itakuwa hivyo hivyo Wakristu ni sawa na wanaume na sisi kina Yakhe waislaam ni wanawake zenu!... Tunahitaji msaada..

The present Charter of the Organization was adopted by the Eleventh Islamic Summit held in Dakar on 13-14 March 2008 which laid down the objectives and principles of the organization and fundamental purposes to strengthen the solidarity and cooperation among the Member States. Over the last 38 years, the membership has grown from its founding members of 30 to 57 states.

Ili uwe member wa hii OIC ni lazima uwe State sio kundi flani ndani ya taifa, Bob betweeen jana na leo, nimewatumia ujumbe wabunge karibu nusu ya bunge letu, kuwaonya sana kuhusu hili suala kwamba wasilifanyie mchezo, ninajua kua Membe sasa anahaha hajui pa kuanzia wala kuishia toka atoe hayo amneno yake mufilisi,

Hawa viongozi kumbe tukiwachezea watatufikisha pabaya zaidi ya hapa tulipo.

Mungu Ibariki Tanzania.
 
Mkamap,

Bado hujainibu kitu hapa.. Nimeuliza kuhusiana na rais wa Vatican, sikuuliza Papa kama kiongozi wa katoliki na hiyo Taasisi kama unavyojaribu kutenganisha. Kama Vatican ni nchi huyo rais wa Vatican ni raia wa nchi gani! -Vatican au Germany!.. ndilo swali langu..
 
Mkandara

Nadhani umeelewa hoja yangu kuwa sipingi waislamu kujiunga na OIC, bali napinga nchi yetu kujiunga humo, maana tukifanya hivyo itakuwa na maana hata sisi wengi tu ambao hatukubaliani na OIC charter tutakuwa tumelazimishwa kujiunga na kufungwa na maazimio mbalimbali yatakayokuwa yanatolewa na OIC. Ndipo nikasema ingefaa kwa OIC kuruhusu waislamu kujiunga huko bila kulazimisha nchi kujiunga.

Inafaa pia kutofautisha suala la OIC na jumuiya kama za wanawake ambazo umetolea mfano mara nyingi. Ni kwamba sisi kama taifa tunayakubali malengo ya jumuiya hizo na tuko tayari kushiriki kuyatekeleza, lakini hiyo OIC charter haijawahi kukubaliwa nasi kama taifa kiasi cha kutosha kutufanya tukubali kuwa sehemu ya utekelezaji wake. Suala ni malengo gani jumuiya hiyo inasimamia, na je yana muundo wa kitaifa? Yako katika vipaumbele vya taifa?

Baada ya kuisoma OIC charter nimeridhika kuwa malengo yake hayana maslahi kwa Tanzania kama taifa, hayana sura ya kitaifa kwa upande wetu, na zaidi yana hatari ya kutugawa hasa kama serikali itasimama upande wa kundi moja dhidi ya mengine mengi yaliyoko nchini. Serikali inapaswa kuwa impartial, iwaache waumini wa makundi mbalimbali wajiunge na jumuiya wanazotaka, na si yenyewe kuwaburuza wananchi wote kujiunga katika malengo ya dini moja ambayo aghalabu yatakinzana na yale ya dini nyingine ndani ya nchi hiyohiyo.
 
Kithuku,
Mkuu, nakuelewa vizuri sana unachopinga na wengi wote waliotangulia..
Binafsi naitazama OIC kama vile Sullivan ikataliwe na nchi za kiarabu kama Egypt na Tunisia kwa sababu inalenga watu weusi ati kwa sababu raia wake ni mchanganyiko..Naiona kama FWWC ya wanawake kwa sababu tu inawahusu wanawake...
Kitu kinachofahamu mimi tatizo lenu wengi sio OIC isipokuwa jina lake na Uislaam, kitu ambacho hadi sasa hivi sijapata mtu wa kunifahamisha vizuri, chombo hiki kinasaidia nchi zenye waislaam..

Kifupi ni kwamba hakuna mtu humu anakubali kuwa Waislaam wana matatizo, yet ni wakristu hao hao kila siku husema waislaam nao wanatakiwa kujipanga waweze kujiendeleza. leo wamepata kitu kama walivyoanza Wanawake kulilia haki, kusaidiwa na hata kufikia UN kutambua haki hizo imekuwa nongwa tunatafuta sababu za Udini.
Kama kuna Mapungufu ya OIC kama tulivyoona kwa Sullivan basi ni bora tuzungumzie hali ya OIC yenyewe badala ya mipango ya Waislaam hali tuna haki za kimsingi..
Huyo Mkamap, amefikia hata ku question kama naelewa katiba ni kitu gani wakati ni maswala kama haya ndio huunda katiba..Kutazama swala hili kwa kutumia imani zetu za dini ni makosa kabisa!..
 
YNIM,

Nawe umekosa objectivity. Nimeuliza kwa kuwa tumeambiwa kuwa maslahi ya Waislamu ni duni na hivyo kulinda na kujenga maslahi yao ni kujiunga OIC. Ama tumeambiwa kuwa Waislamu wana unyonge na njia ya kufungamana na kujenga umoja ni kujiunga OIC.

Nimeuliza, je Waislamu wa Saudi na kwingineko ambao ni predominantly Islamic state (or declared to be Islamic state and they are rich) wamefanya nini kuhudumia adha za Umasikini na Unyonge wa jamii zilizoko katika nchi zao ambao ni Waislamu?

Kwangu mimi, vita dhidi ya Umasikini na Unyonge haina rangi, dini, kabila, umri au jinsia. Ni vita Universal ambayo ni shurti kila mtu aifanye na atumie bidii zake kuvunja nguvu zinazolea Umasikini na Unyonge.

Kwa mantiki hiyo, historia inatuonyesha kuwa kukua kwa jamii kulitokana na ubaguzi, nako kukazaa Umasikini na Unyonge. Ubaguzi huu haukujifunga kwa Mzungu dhidi ya mweusi tuu au Mwarabu dhidi ya Mwasia, ni hata Mwafrika kwa Mwafrika, Mwarabu kwa Mwarabu, Mkristo kwa Mkristo, Muislamu kwa Muislamu, Wanaume kwa Wanaume, Wanawake kwa Wanawake na kadhalika.

Sasa tukisema Tanzania ijiunge OIC ili kudhibiti Unyonge na Umasikini wa Waislamu, swali linakuja, jee ni jukumu la nani kuangalia na kudhibiti kwa nchi yetu Unyonge na Umasikini wa Wakristo, Wapagani, Wahindu na Mabudha? Je tutasema ni Jukumu la Vatican ambayo ni Nchi? what about Lutherans, Anglicans, Baptists, Pentecostal who are not Catholics or believe in Vatican and Papacy?

Kama Serikali yetu inajiunga kama nchi katika umoja kama huu ambao ni shirikisho la nchi za Kiislamu lenye kukaribisha nchi na jumuiya za Kiislamu kujiunga, basi iwe ni haki kwa Tanzania kama nchi (si taasisi binafsi na za Kidini) kujiunga na World Council of Churches, World Council of Pagans, Atheists na Agnostics!

Nafahamu, kuwa CCT (Church Council of Tanzania) ni mwanachama wa World Council of Churches, TEC ya Wakatoliki iko chini ya Universal Roman Catholic Church, ELCT (Evangelical Lutheran Church of Tanzania) ni mwanachama wa Lutheran World Federation na Uanachama wa Taasisi hizi katika jumuiya hizi ambako maslahi ya kawaida ya kiroho na kimwili ya Wakristo wa madhehebu haya huzungumzwa na si kutumia mwavuli wa Nchi.

Labda niulize, kwa nini Bakwata haijajiunga OIC independently bila kutaka Serikali ya Jamhuri wa Muungano wa Tanzania iwe mwanachama wa OIC?

Mnaposema kuwa Vatican ni nchi ya Kidini, je mnasahau kuwa Saudi Arabia ni Nchi ya Kidini?

OIC na Vatican are two different things. One is an organisation of Islamic Countries, similar to AU for African Countries and the other one is a Country, yes the head of Country is Pope who is the leader of Catholic church, Similar to the King of Saudi Arabia a Muslim country who is the defender and protector of Islam and its holy places in Saudi Arabia!
REVEREND hapo umepapasa.huwezi kulinganisha saudi arabia na vatican.Vatican huwezi kulinganisha na nchi yeyote.saudi arabia unaweza kulinganisha na uingereza. mbona tuna uhusiano na vatican kwa mujibu wa kiroho na tunapinga uhusiano na OIC kwa mujibu wa kiuchumi .Lakini kinachonikera kule kwa maaskofu na Bakwata kuingilia mjadala ukiwa bado uko mitaani sijui viongozi wa kidini wa kileo wamekosa busara za kitakaifu. watuachie tulumbane ndipo tuwaendee kuomba ushauri.Nadhani reverend umenielewa
 
Mkamap,

Bado hujainibu kitu hapa.. Nimeuliza kuhusiana na rais wa Vatican, sikuuliza Papa kama kiongozi wa katoliki na hiyo Taasisi kama unavyojaribu kutenganisha. Kama Vatican ni nchi huyo rais wa Vatican ni raia wa nchi gani! -Vatican au Germany!.. ndilo swali langu..

Pope sio rais wa Vatican City bali ni mfalme. Ingawa anachaguliwa na makadinali wenzake lakini uongozi wake ni wa maisha na hamna bunge la kushirikiana nae katika utawala wake. In other words, Vatican City ni Monarchy na sio republic. Makadinali wote wa kanisa katoliki ni raia wa nchi ya Vatican City. Uraia wa Vatican City unatokana na nafasi uliyonayo na si kuzaliwa. Ndiyo maana walinzi wa Pope wanahesabiwa kama raia wa Vatican City wakati wa utumishi wao. Utumishi wao ukiisha, uraia wao nao unakoma. Pope ni raia wa Vatican City toka pale alipokuwa Kadinali. Kwa vile nchi anayotoka inakubali uraia wa zaidi ya nchi moja, basi bila shaka ni raia wa ujerumani na Vatican. Kama sheria za nchi yake kadinali haziruhusu uraia wa nchi mbili bila shaka wahusika wanapewa permanent residency katika Vatican ambayo inampa haki sawa na raia bila kuwa na haja ya pasi.

Waislamu mara nyingi wanakosea kufananisha miundo ya uongozi wa baadhi ya madhehebu ya wakristu na yale waliyonayo. Madhehebu makubwa makubwa uongozi uko institutionalised na kila aliyekuwemo katika hilo dhehebu nafasi yake inaeleweka kuanzia muumini wa kawaida hadi kiongozi mkuu. Waislamu ukiondoa, wa madhehebu ya washia, hawana hilo. Kila Imam na Sheikh anasimama mwenyewe na hawajibiki kwa kiongozi yeyote juu yake bali kwa wale anaowaongoza. Hawana nafasi kama ya maaskofu, makadinali na kadhalika. Hii ndiyo inayopelekea vyombo kama bakwata kukwama maana hamna kitu kinacholazimisha waislamu kutambua na kuheshimu uongozi wake. Hii ni tofauti na wakristu ambao dini yao inakulazimisha kumtambua na kumnyenyekea yule aliye na jukumu la kukuhudumia kiroho. Madhehebu mengine yanawaita hawa baba. Sasa waislamu wanapolalamika rais kumtembelea Mfalme wa Vatican, basi watuambie kwao aende wapi kumtembelea kiomgozi wao? Aende Pakistan, kumtembelea Aga Khan? Aende Iran kumtembelea Ayatollah? Au Mumbai kwa mabohora? Sasa mbona wote hawa mmeishawakana!

Kosa kubwa linalofanywa na pande zote mbili ni kulitazama suala hili kupitia darubini la dini yao. Waislamu kwa kujaribu kukifananisha chombo hiki na Vatican, wakisahau kuwa ni vitu viwili tofauti kabisa. Wakristu kwa kushindwa kuelewa kuwa mfumo walionao unawapa advantage katika sehemu kadhaa. Wao hawana haja na kitu kama OIC kwa sababu dini zao zina institutions kamili nje ya muundo wa serikali. Wao walitakiwa kuwa sympathetic na kuelewa kwa nini wenzao wanahitaji chombo mbadala ambacho kitawaunganisha katika imani yao. Kama kukipata ni lazima serikali yetu ijiunge, so be it. Tukiona kubaya si tutajitoa na kuwaeleza wenzetu kwa nini tumefanya hivi. Viongozi wa kikristu kwa kulishikia bango suala hili ndiyo kunazidisha imani kuwa wakristu hawawatakii mema wenzao. Kichuguu tunakigeuza mlima sisi wenyewe.

Kuna ishu za kusimamia kidete ( Mahakama ya Kadhi ikiwa ni mojawapo) lakini si hili. Tujiunge tu na chombo hiki kwa faida ya wenzetu. Hatutabadilika kuwa nchi ya kiislamu kwa kufanya hivyo.

Amandla.......
 

Makadinali wote wa kanisa katoliki ni raia wa nchi ya Vatican City.

...Kama sheria za nchi yake kadinali haziruhusu uraia wa nchi mbili bila shaka wahusika wanapewa permanent residency katika Vatican ambayo inampa haki sawa na raia bila kuwa na haja ya pasi.

Kwa hiyo, sio makadinali wote ni raia wa Vatican City. Au ?
 
Back
Top Bottom