Juu ya OIC na Mahakama ya Kadhi

Juu ya OIC na Mahakama ya Kadhi

OIC ni Jumuiya ya Wa-Islam, taifa lolote lisilo la Wa-Islam kujiunga huko ni wendawazimu, ambao sisi baadhi ya wananchi wa taifa hili tunapinga tena kwa nguvu zote, Maana ya uswahili uliyoitoa kama ni ya kweli, basi tunaongozwa na viongozi waswahili, ambao badala ya kutafuta njia zinakubalika kimataifa kutatua matatizo yetu, wanajaribu kutafuta njia za mkato,

OIC ni jumuiya ya Wa-Islam period, betweeen jana na leo nimeongea na wakubwa wengi sana wa taifa, na wakubwa huko UN wamenihakikishia kwamba OIC ni member wao as Jumuiya ya wa-Islam, ninarudia Tanzania sio taifa la ki-Islam we have no business kujiingiza huko, hatuhutaji mjadala wala anything on hilo.

Mkuu, nina kiu na majibu ya maswali ambayo kwa namna moja au nyingine unayakwepa kisiasa.

(1) OIC ni jumuia ya nchi za ki-islamu kama ulivyosema, je italeta madhara gani kimaendeleo endapo serikali yetu itaamua tujiunge?

(2) Maaskofu na watu wa dini nyingine wanapinga kujiunga na OIC; hawa wataathirika vipi kimaendeleo endapo serikali yetu itaamua kujiunga na OIC?

(3) Mimi mtanzania wakaiwaida nanayefuata dini yangu nitaathirika vipi kimaendeleo endapo Tz itajiunga na OIC?

Naamini JF ni sehemu ya kuelimishana na nitafurahi mkuu endapo utaelekeza responses zako kwenye maswali yangu.
 
Jambo moja ninalopenda kufahamu ikiwa nchi kama Tanzania inajiunga na OIC inaendelea kutumia charter ya UNIVERSAL DECLARATION OF HUMAN RIGHTS ya 1948 au ina adopt ile ya Cairo Declaration of Human Rights iliyotungwa na nchi wanachama wa OIC (mawaziri wa nchi za nje wa nchi wanachama wa OIC) 5 August 1990?
 
TzPride :TzPride has no status.
Senior Member Join Date: Wed Nov 2006

Re: Serikali yetu na Uanachama wa OIC: Tujiunge tusijiunge?

pendekezo;
Waislamiu wote wahamie zanzibar na tuvunje muungano ili Zanzibar ingine OIC na Tanganyika ibaki secular. Else, OIC isn't compatible to Tanzania comunity.

Field Marshall Es,

Mkuu nimekufuata wewe kwa sababu unayumba, ungekuwa wima wala nisingekufuata kwani wanihusu sana zaidi ya kuwa hapa Mtandaoni..Kesho naweza kuogopa kuomba maji ikiwa moyo wako umepigwa mhuri..

Mkuu, kama unazo hoja ziweke lakini kwanza rekebisha maneno yako kuunga mkono ati waislaam wote wahamie Zanzibar Tanganyika ibakie nchi yenu kama vile mlijua hata pa kuanzia kuutafuta Uhuru..

Bob hiyo hoja juu nafikiri ni wazi imesemwa na nani, sio yangu ingawa ninaiunga mkono, sasa yeye mwenyewe anaweza kuijibu na ninamuunga mkono kwa 100%. Lakini sio hoja yangu, ila nitajibu niliyoyasema tu on this ishu!
 
Jambo moja ninalopenda kufahamu ikiwa nchi kama Tanzania inajiunga na OIC inaendelea kutumia charter ya UNIVERSAL DECLARATION OF HUMAN RIGHTS ya 1948 au ina adopt ile ya Cairo Declaration of Human Rights iliyotungwa na nchi wanachama wa OIC (mawaziri wa nchi za nje wa nchi wanachama wa OIC) 5 August 1990?

Kwa thread inazungumzia mambo ya OIC kama kila mtu anapost thread mpya za OIC we will end up kujadili OIC kila siku
 
1.
Ni kweli kabisa kuwa OIC ni jumuiya ya Waislaam..sasa uinavyofikiria wewe Waislaam hawana haki ndani ya nchi isiyokuwa na dini?..Ikiwa wanazo haki kwa nini nchi isiwasaidie na kutambua haki zao wakati nchi inatambua hata haki za Mashoga Kwani nchi hii ni ya Mashoga! Tumejiunga na jumuiya za wanawake kwani nchi hii ni ya Wanawake watupu! yaani hata siwaelewi mnakojaribu kupeleka hoja hii.

1. Great! unakubali kwamba OIC ni Jumuiya ya Wa-Islam, ndipo hoja yangu ya msingi ilipo kwamba Tanzania sio taifa la Wa-Islam, kwa hiyo hatuna sababu ya kujiunga nao.

2. Haki ya Wa-Islam ndani ya taifa letu ni kupractice imani yao bila kuingilia sheria za jamhuri, ya kujiunga na mashirika ya kimataifa ni la jamhuri sio la dini wala imani flani ndani ya jamhuri.

3. Kutambua haki za mashoga na the rest sijui yanahusu vipi na kujiunga na shirika la Wa-Isilamu, na sijui ni nani anayetambua hizo haki za mashoga kisheria bongo, hivi Tanzania ni wanachama wa shirika la mashoga duniani au?

4. Kama kuna any jumuiya ya wanawake duniani Tanzania ni member, basi tunawakilisha wanawake wote wa Tanzania kuanzia wa-Isilamu mpaka wa-Kritso na Wapagani, lakini sio kikundi kmoja tu ndani ya Jamhuri yetu ndio kinawakilishwa huko.

Ya US na Obama, hayahusu anything na sisi Tanzania kutojiunga na OIC, yaani shirika la Wa-Isilamu, kwa sababu sisi Tanzania sio taifa la W-Iisilamu period!.
 
Mkuu, nina kiu na majibu ya maswali ambayo kwa namna moja au nyingine unayakwepa kisiasa.

(1) OIC ni jumuia ya nchi za ki-islamu kama ulivyosema, je italeta madhara gani kimaendeleo endapo serikali yetu itaamua tujiunge?

(2) Maaskofu na watu wa dini nyingine wanapinga kujiunga na OIC; hawa wataathirika vipi kimaendeleo endapo serikali yetu itaamua kujiunga na OIC?

(3) Mimi mtanzania wakaiwaida nanayefuata dini yangu nitaathirika vipi kimaendeleo endapo Tz itajiunga na OIC?

Naamini JF ni sehemu ya kuelimishana na nitafurahi mkuu endapo utaelekeza responses zako kwenye maswali yangu.

Swali lako la msingi hapa bado ni lile lile, kwamba Tanzania taifa ambalo sio la Kii-Isilamu, litadhurika vipi na kujiunga na shirika la OIC ambalo ni shirika la Kii-Isilamu,

Hapo hakuna siasa wala intellectualism, taifa lisilo la Kii-Isilamu haliwezi kujiunga na shirika la Kii-Isilamu, ukiona taifa lisilo la Kii-Isilamu lina lilia kuijiunga na shirika la Kii-Isilamu, maana yake ni moja tu kwamba ni taifa lenye viongozi na wananchi wendawazimu, and some of us katika Tanzania we are not wendawazimu!

Ahsante Mkuu.
 
Kuna mwanaJF mmoja kashauri kuwa serikali yetu itafute modality ya kuwezesha wa-Islamu kujiunga na OIC.......ni wazo zuri...................najaribu kufikiria sijapata jibu bado.......on the modality

............In addition nafikri ni rahisi zaidi kwa OIC kurekebisha masharti yao ya uanachama na kuruhusu jumuiya za Kiislamu zinazokubalika na waislamu wa nchi husika ziruhusiwe kujiunga na OIC.........otherwise we will continue with this debate as a nation of differents beliefs to infinity............

.......kama masharti ya kujiunga na uanachama wa OIC unaruhusu jumuiya fulani fulani kujiunga........i don't see any fuss of this debate........
 
Kuna mwanaJF mmoja kashauri kuwa serikali yetu itafute modality ya kuwezesha wa-Islamu kujiunga na OIC.......ni wazo zuri...................najaribu kufikiria sijapata jibu bado.......on the modality

............In addition nafikri ni rahisi zaidi kwa OIC kurekebisha masharti yao ya uanachama na kuruhusu jumuiya za Kiislamu zinazokubalika na waislamu wa nchi husika ziruhusiwe kujiunga na OIC.........otherwise we will continue with this debate as a nation of differents beliefs to infinity............

.......kama masharti ya kujiunga na uanachama wa OIC unaruhusu jumuiya fulani fulani kujiunga........i don't see any fuss of this debate........

Sio rahisi sana kwa sababu na wao kuweka masharti ya kujiunga kuwa hivyo wana maana yao.....
 
....and what is that maana yao...........

Inabidi usome hizo charter, katiba yao etc ...utaipata tu.......lakini kukusaidia,

1. Kama lengo/goal mojawapo ni kuhakisha uislam unaenezwa ukiishika au kushirikisha serikali lengo linakuwa na nguvu zaidi ya kufanya kazi na jumuia za kiislam, meaning maazimio ya OIC yanachukuliwa kutekelezwa at governmental level sio NGO/community level.....

2. Kuna lengo/goal jingine linasema ku-defend sovereignty, independence and territory of member states ......meaning this is likely kuwa effective kama organization is composed of governments rather than NGO or jumuiya ndogo ndogo.

Na mengine mengi.....
 
Ogah,
Kwa mtazamo huo labda pia tuangalie pia wanawake wetu na pengine tuwaulize kwa vipi Mama Mongella alihusishwa kama Secretary-General wa Fourth World Conference on Women.
Kisha tuwaombe hawa wanawake na chombo chao wabadilishe katiba yao iweze kuwahusisha wanaume...ndipo Tanzania tunaweza kushiriki... Tanzania sio nchi ya wanawake!
 
Ogah,
Kwa mtazamo huo labda pia tuangalie pia wanawake wetu na pengine tuwaulize kwa vipi Mama Mongella alihusishwa kama Secretary-General wa Fourth World Conference on Women.
Kisha tuwaombe hawa wanawake na chombo chao wabadilishe katiba yao iweze kuwahusisha wanaume...ndipo Tanzania tunaweza kushiriki... Tanzania sio nchi ya wanawake!

1.....Yes i really want to know.......ni kwa vipi akina Mongella walihusishwa....

2......yes kama wanawake peke yao hawajitoshelezi kutafuta matakwa yanayowahusu wao wenyewe............hilo laweza kuwa pendekezo mojawapo
 
Field Marshall Es,

Kwa mtazamo wako nakuomba utazame vyombo vyote vya kimataifa ambavyo Tanzania ama nchi nyingine zimejiunga hali nchi zao sio ya watu ama kundi fulani la watu..Tazama wanawake, watoto Yatima, vilema na kadhalika..
Maswali ayko yote yaweke ktk vifungu hivyo pia pengine unaweza kunipa jibu tofauti na OIC ikiwa unakubali ni chombo cha waislaam lakini wakati huo huo unasema nchi yetu haina dini..
Kwanza una maana gani unaposema nchi yetu haina dini?..
Kumbuka mkuu Tanzania sio sawa na Urusi ama China ambao kutokuiwa na dini wao walikuwa wanaamini Ukomunist.. Sisis hatuna dini kwa maana hakuna dini moja inayokubalika zaidi ya nyingine ktk misingi ya Utawala. Hivyo Hata Bungeni huwezi kutumia misingi ya dini yako kupinga ama kutoa maamuzi dhidi ya muswada..
Kwa mfano mdogo tu Mashoga..
Ikiwa bungeni litakuja swala ama muswada unaohusiana na haki za mashoga haitakiwi mbunge ama kiongozi kubase judgemnet zake kwa kutumia imani yake ya dini, hata kama swala hilo linahusiana na imani ya dini yako..Kataa ushoga kwa kutumia culture yetu ama vitu vingine nje kabisa ya dini yako kwa sababu kila mmoja wetu akiingiza dini kutoa maamuzi hatuwezi kujenga kitu..
Kwa hiyo tusijaribu kupotosha maana ya Tanzania haina dini kwa maana kuwa hakuna dini ama dini haziruhusiwi isipokuwa mrengo fulani wa kisiasa. Dini zinaruhusiwa na zina kila haki ya kujiendeleza na mkono wa serikali ni lazima kuhakikisha haki hiyo inapatikana. Laa sivyo mkuu kila mmoja wetu atatumia Udini na tutavuana mashati kuhusiana na Ukatoliki nchini..
kwa sababu nitajiuliza maswali kama yako kuhusiana na Vatican na mwisho wa yote ni kutokukubali wakristu wafuate dini yao ktk ibada zao..
 
Ogah,
Mkuu kama kweli unafikiria hivyo basi mkuu wangu una ubaguzi ndani ya roho yako, kwa namna fulani unafikiria kwamba wanawake wanafanya njama fulani against wanaume na unapenda kujua kinachoendelea mle ndani hata kama vitu vyote viko wazi..At the same time wanawake hawa question kila wanaume wanalolifanya tunawaona wao wajinga ama watumwa wetu..
 
Kuna madhara kujiunga na OIC. Hii ni taasisi au jumuiya ya nchi za kiislam. Inasema na katiba yake inajiainisha hivyo. Tanzania kuna waislam, kwa nini wasiwakilishwe? Wana haki ya kuwakilishwa ikiwa wataunda nchi ya kiislam ndani ya Tanzania. Kwa sababu OIC hawawakilishwi mwislam mmoja mmoja. Ni lazima wawakilishwe kama nchi. Tatizo sasa liko wapi ikiwa Nchi ya Tanzania yenye waislam itajiunga?

Tatizo ni kuwa katika Tanzania serikali italazimika kuangalia dini za watu katika utendaji wake. Itakuwa imeingiza rasmi dini ndani ya serikali. Mkuu wa nchi ni rais. Uwakilishi wa Tanzania katika mikutano ya OIC itakuwa ni lazima ateuliwe mwislam. Kiutendaji rais atalazimika kuuliza hivi furani dini gani? Kama kutakuwa na kamati au taasisi ya kuratibu mahusiano yetu na OIC itakuwa lazima taasisi hiyo iwe na composition ya waislam. Ikiwa uteuzi utatakiwa, rais si Mwislam, akamteua Mwislam ambaye hakubaliki kwa baadhi ya makundi ya waislam tayari kiutendaji rais atakuwa amefanya maamuzi yahusuyo imani yatakayo mwingiza katika mgogoro wa kiimani. Hilo ni tatizo ingawa sasa hivi hatulioni kwa kuwa ajenda ni kuingia. Sema utaundwa mfumo wa uwakilishi ambao hautahusisha watendaji wa selikali moja kwa moja, lakini kumbuka wanaenda kuwakilisha nchi! Maazimio yatakayopitishwa yataridhiwa na nchi, vipi ikiwa maazimio yenye madhara kwa makundi mengine ya kidini yatakapopitishwa na kuridhiwa na nchi? Si yatakuwa sheria?

OK watu wanasema nchi so and so ni wanachama na hayo madhara hayajatokea kwa nchi hizo. kumbuka katika uendeshaji wa nchi kuna mambo mengi hatuyaoni, hasa yanayozihusu nchi zingine. Jiulize kwa nini ukabila inakuwa tatizo Burundi kwenye makabila mawili usiwe tatizo Tanzania kwenye makabila 120? Kila nchi inatofautiana na nyingine. Dini katika uendeshaji wa nchi inaweza isiwe tatizo Kenya lakini ikawa tatizo Tanzania, Kama vile ukabila ulivyo Tatizo Kenya na si Tanzania. Ni lazima kuchukua tahadhari hasa unapodeal na mambo yanayogawa watu kama dini.

OIC wanataka wanachama kutoka nchi za kiislam, wanajadili masuala yanayowahusu waislam. Tanzania kuna waislam lakini si nchi ya waislam pekee.

Hili suala la Vatican sijui kwa nini kila hoja hii inapojadiliwa lije. Kwanza Vatican haisajili wanachama. Vatican in Ubalozi tanzania kama walivyo na Ubalozi nchi zingine. Hivi kuna mikutano Vatican huwa Tanzania tunawakilishwa kama nchi? Hivi kuna maazimio ya mikutano ya Vatican ambayo yakitolewa huko Tanzania kama nchi inayaridhia? Hivi Tanzania kama nchi inashiriki kutunga katiba na taratibu zinazoendesha Vatican? Kwa nini hili liwe linajitokeza linapojadiliwa OIC. Kuna nchi nyingine wanachama wa Vatican? Hivi Vatican kuwa na Ubalozi Tanzania ina maana Tanzania kama nchi ni Mwanachama wa Vatican. Pengo akienda Vatican anawakilisha serikali au anatumia bajeti ya serikali? Hivi muundo wa vatican ni kitu ambacho Tanzania kama nchi imehusika? Kweli raia wa Tanzania anaweza siku moja akawa papa, Lakini atakuwa anaiwakilisha Tanzania kwenye upapa? Hivi ni vitu visivyofanana.

Vatican siyo Conference of Catholic States. Vatican ina muundo wake ambao unawahusu wakatoliki kama wakatoliki. Balozi wa Vatican ni Balozi kama walivyo mabalozi wengine. Labda ikiwa kuna mtu atasema yule hadhi yake inayotambuliwa serikalini ni tofauti na mabalozi wengine. Ikiwa Tanzania tuna Balozi vatican je yule balozi ana hadhi tofauti na balozi aliyeko Urusi au Uchina?
 
Kipimapembe,

Sawa mkuu nakubaliana na wewe sana tu.. sasa katika maandishi yako pale ulipoandika Waislaam weka Wanawake kisha nambie kama jibu lako bado litabakia hivyo hivyo ktk msimamo wako!

Halafu ni wapi ktk katiba ya nchi yetu imesema Rais wetu atalazimika kuihusisha OIC ktk uongozi wake.
 
Kuna wanaofananisha OIC na Beijing ya wanawake kuwa Tanzania kama nchi iliwakilishwa wakati ule ulikuwa ni mkutano wa wanawake! Hili mbona rahisi sana. Tanzania tulikuwa na waziri wa wanawake na watoto. Leo hii masuala ya wanawake ndani ya serikali yanashughulikiwa na wizara ya Jinsia. Hili la wanawake lipo ndani ya serikali.

Kwa hiyo itabidi tuwe na wizara inayoshughulikia masuala ya waislam kwa kuwa tuna wizara inayoshughulia mambo ya wanawake?

...... this is too low!
 
Kiutendaji, lazima nchi itawakilishwa na watu. Utaweka mfumo gani ambao hatimaye hautamgusa raisi kwenye suala linalohusiana na sera ya mambo ya nje? Hata tukiunda wizara itakuwa na waziri. Ikiundwa idara ya kuwateua watakaokuwa wanawakilisha nchi itakuwa chini ya wizara fulani. Au tuseme itakuwa idara huru itakayoshughulikiwa moja kwa moja na Bunge? Bajeti ya idara hiyo ipitishwe na Bunge!!!
 
Back
Top Bottom