Juu ya OIC na Mahakama ya Kadhi

Juu ya OIC na Mahakama ya Kadhi

Hizi ni allegations zinazotolewa bila umakini wala uthibitisho. Imefika wakati watu wakawekewa "luku" kwenye keyboard zao.

Swali dogo, have u got anything to back up ur story or u just throw allegations for the sake of it?

Siasa kali zilianza kipindi gani? Kuna mambo mengi nyuma ya pazia yalifanyika kipindi cha Mzee Ruksa(kuhusu kuupromote Uislamu kupitia serikali), nadhani hili halina upinzani. Na tutayasikia mengi tu usijali ..

Pia nakumbuka, ktk kipindi cha Mzee Mkapa, watu wa Iran bila haya walidai kutufutia deni letu kwa fedha za kigeni, ili sehemu ya deni seriakli yetu iitumie kuendeleza uislamu..Bahti nzuri wakakutana na kigingi.

Sasa kama una 'macho' anza kuyatumia..
 
Masatu wewe ni nani hasa hapa JF,na TZ?

Unashare zozote na huyu mzee?una udugu lamda?

Kaa pembeni basi,kama hujui hili,

Unataka ushaidi?ili nini sasa?

Sikuandika ili uamini,na huitajiki kufanya ivo.
 
Masatu wewe ni nani hasa hapa JF,na TZ?

Unashare zozote na huyu mzee?una udugu lamda?

Kaa pembeni basi,kama hujui hili,

Unataka ushaidi?ili nini sasa?

Sikuandika ili uamini,na huitajiki kufanya ivo.

Mimi ni mwanachama kama ulivyo wewe, sina share wala udugu na huyo mzee lakini haya madai yako yamekosa umakini na yamejikita kwenye chuki binafsi.
 
Siasa kali zilianza kipindi gani? Kuna mambo mengi nyuma ya pazia yalifanyika kipindi cha Mzee Ruksa(kuhusu kuupromote Uislamu kupitia serikali), nadhani hili halina upinzani. Na tutayasikia mengi tu usijali ..

Pia nakumbuka, ktk kipindi cha Mzee Mkapa, watu wa Iran bila haya walidai kutufutia deni letu kwa fedha za kigeni, ili sehemu ya deni seriakli yetu iitumie kuendeleza uislamu..Bahti nzuri wakakutana na kigingi.

Sasa kama una 'macho' anza kuyatumia..

The so called siasa kali zilianza wakati wa Nyerere. Kulikuwa kuna jumuiya Warsha ya waandishi wa kiislam na sheikh wao Ahmed pale Masijid Qubah. Haya jamaa ndio waliokuwa wakiandika makala na vipeperushi mbalimbali vyenye kuamsha hisia za waislam.
 
http://www.oic-oci.org/oicnew/member_states.asp

Waungwana badala ya hawa Masheikh na Maaskofu kutaka kuonyesha nani mbabe zaidi katika swala hili la umuhimu/kutokuwa na umuhimu wa Tanzania kujiunga na OIC ni bora ungefanywa utafiti wa kina kwa utumia balozi tatu katika nchi wanachama toka Afrika ambazo mimi naweza kusema huwezi kuziweka kwenye kundi la nchi za Kiislamu.

Nchi hizi kama zinavyoonekana katika link hiyo hapo juu ni Uganda ambayo ilijiunga OIC tangu mwaka 1974, Nigeria iliyojiunga mwaka 1986 na Msumbiji iliyojiunga mwaka 1994.
Serikali inaweza kabisa kwa kuwatumia balozi zetu katika nchi hizo ikakusanya athari na faida ambazo nchi hizo imezipata kutokana na kuwa wanachama wa OIC. Hizi zianikwe hadharani ili Watanzania walio ndani ya nje ya Tanzania tuzichambue kwa kina kabla ya kufanya uamuzi wa kujiunga au kutojiunga na OIC. Pia kama kuna masharti (nitayatafuta kwenye web site yao) yoyote ya kuwa mwanachama wa umoja huo basi pia nayo yawekwe hadharani kisha Watanzania tuamue kujiunga na umoja huo au kutojiunga.

Hili likifanyika litaondoa utata na ubabe unaotaka kuonyeshwa na pande zote mbili zinazounga na kutounga. Vinginevyo tunaweza kupigizana kelele bila ya kuwa na vigezo vyovyote muhimu na hatimaye kuingiza Tanzania katika matatizo makubwa zaidi na hasa ukitilia maanani Tanzania sasa hivi haijatulia kwa mambo mbali mbali yakiwemo mafisadi, uongozi duni n.k. tukiongeza na hili la udini basi nchi inaweza kulipuka tukabaki tunalia vilio vya mbwa mdomo juu, maana athari yake inaweza kuwa na matokeo mabaya sana.

Mkuu naungana na wewe kwa asilimia 100 kwenye hili suala la utafiti. Kama alivyosema Waziri Membe, suala hili litapelekwa kwa Watanzania wote, na wao ndio watakaokubali kujiunga ama la. Hivyo basi, tukipewa matokeo utafiti wa kina wa faida na madhara ya kujiunga na jumuia hii, basi itakuwa ni rahisi kwa wakristo na waislamu kufanya maamuzi ya busara kwa faida ya taifa zima.
 
The so called siasa kali zilianza wakati wa Nyerere. Kulikuwa kuna jumuiya Warsha ya waandishi wa kiislam na sheikh wao Ahmed pale Masijid Qubah. Haya jamaa ndio waliokuwa wakiandika makala na vipeperushi mbalimbali vyenye kuamsha hisia za waislam.

Mh nakusikiliza, endelea kutuhabarisha..mbona umeishia katikati?
I'm all ears..
 
Serikali ndio iliyoyataka haya, nchi bado iko katika hali tata juu ya muungano, ufisadi, rushwa n.k. Sasa wanaamsha na hili, sina uhakika kama wanajua wanachocheza nacho hapa. Eneo hili ni tete sana(dini), hata wale walioonekana kuwa kimya hawatakuwa kimya hapa.
 
Wale wote wenye nia njema na taifa letu, mnachotakwia kutusaidia hapa ni mawazo na maswali serious kuhusu this ishu, ya kafiri na the rest of the story hayawezi kutusaidia anything,

Tuambieni ni kwa nini Mwalimu alipokuwepo, Membe hakuwa na haya mawazo? Halafu kwa nini Waziri mzima wa Jamhuri anakwenda kuongea ishu very sensitive namna hii kwenye majukwaa ya media badala ya kuanzia bungeni kwanza? Why now tena baada ya kutoka Iran ambao historia ya siasa yetu iko very clear kua ndio waliowapa hela za uchaguzi the Mtandaos ambao yeye Membe was very much involved?

Hapa hapahitaji mabishano ya kidini kwa sababu historia iko very clear kuhusu vita vya hizi dini mbili kwamba mara ya mwisho huko Europe walioshinda ni wa-Kristo, na ni none ishu at all katika kuamua iwapo Tanzania tujiunge au hapana,

Binafsi ninapinga kwa nguvu zote hii idea ya Membe, ninaamini kwamba watawala wetu wa sasa wa hili taifa wameshindwa kutuaminisha wananchi kua wana nia njema na taifa letu, na hasa uwezo mdogo wa kuongoza waliouonyesha tayari. Katika kipindi kifupi cha utawala wao wametuingiza kwenye matatizo makubwa sana, hasa inapokuja ishu zinazohusu maamuzi ya taifa letu na mataifa mengine, la mwisho lilikuwa Richimonduli.

Matatizo ya Uganda, kimaendeleo hayakumalizwa na kujiunga kwao na OIC, kwa hiyo ni hoja finyu sana kwa waziri kutudanganya na hiyo hoja uchwara, Tanzania sasa hivi ni mwanachama wa jumuiya nyingi sana za kimataifa na tunashindwa kwenda popote kimaendeleo, sasa labda ifike mahali as a nation tujiangalie upya kama ni worthy sisi kuendelea na some of hizi international membership na hasa zile zinazohitaji yearly fee kuwa member, ikibidi tujitoe nazo, badala ya kulazimisha kujiunga na jumuiya hizi za kidini ambazo zina-guarantee mgawanyiko wa kisiasa na kidini kwa taifa lolote kama letu ambalo officially halina dini moja kama letu.

I do not care what hii ni jumuiya ya Wa-Islam period, Tanzania we have no business kujiunga na this kind of Jumuiya, kwa sababu sisi sio taifa la Kii-slam, na Membe should apologize to us the public for this nonesense ideas kama amezitoa under ministerial capacity. Incompetence ya utawala wa sasa it is just out of hand, I mean waziri mzima hajui kwamba this is a very sensitive political ishu ambayo haiwezi kurushwa tu kwenye media, badala ya sehemu maalum za kisiasa na kisheria?

Hiii incompetence na huu utawala where does it stops? Kwa sababu now karibu wananchi wote tunajua inapoanzia!
 
Tatizo la viongozi wa sasa 'usanii' wao wanaulekeza pabaya..Wanaona wanaoteza popularity wanakuja na mbinu za ajabuajabu ili kujipatia umaarufu bila kukaa chini na kufikiri kwa kina kila hatua na taathira yake kwa jamii.

Na kwa hali ilivyo hivi sasa jinsi watu walivyo hawana subira hivi sasa kutatokea mambo ambayo hatujawahi kuyashuhudia na yatakuwa irrevirsible and too late kuyacontrol.
 
Hiii incompetence na huu utawala where does it stops? Kwa sababu now karibu wananchi wote tunajua inapoanzia![/SIZE][/QUOTE]

"The only way to stop INCOMPETENCE is to get rid of Incompetence leaders starting with JK and his cabinet, he is such a shame to our country; he is too weak to be a President that' s for sure!"
 
Last edited:
Jamani JF mbona mnanishangaza, mnabishana kwenye kitu ambacho kimesemwa na mtu mdogo sana, au mmesahau kuwa hata salimini alilazimishwa kuitoa zanzibar OIC baada ya kugundua kuwa aliingiza wakati hana madaraka?

Hawa watu ni wajanja sana wanaona mmewakalia kooni kwa mambo ambayo ni ya kisiasa wanawaingizia dini ili mbishane kwenye dini msahau siasa wenyewe waendelee kupeta, Membe ana mamlaka gani ya kuiingiza tanzania OIC?

Hili swala ni sensitive sana kuliko hata mmuhafaka wa zanzibar watawezaje kuamua wenyewe bila kuuliza wananchi halafu muhafaka ndio waulize wananchi, angalieni pande zote wanatafuta likizo kidogo kutoka kwenu kwakuwa mmewakalia kooni.

Ukifikiria zaidi kuna mambo muhimu ambayo hawa maaskofu wangeweza kusema watayasimamia kwani yanategemea maamuzi ya viongozi zaidi kuliko wananchi mambo kama EPA, RICHMOND and now TTCL wanahitaji kusimamia haya zaidi kwani yana discreation ya viongozi na si wananchi lakini swala la OIC haiwezekani hata kidogo JK akaamua kuiingiza tanzania OIC bila ridhaa ya wananchi.

Hata hao maaskofu inabidi muwaulize uteuzi wa mungu umeishia wapi mbona kama ni washetani, au maono yao hayakuwa sahihi. waseme wasikae kimya kwani kukaa kimya kwa mambo ambayo yanafanywa na viongozi na kuja kuongelea kitu ambacho lazima wanchi washirikishwe ni uoga.

Afterall tutaacha kuomba lini tuanajiunga na OIC kufanya nini, tutapata nini huko OIC, je misaada itakayotolewa itawafikia wanchi kwa njia gani? hivi ndio vitu vya kujiuliza badala ya kupiga kelele na matusi yasiyo na msingi.
 
Baada ya ile documentary iliyoandaliwa kwa ushirikiano wa waislam na wakristo yenye kuonyesha jinsi wananchi wanavyoteseka na huku utajiri wao ukichotwa...Serikali ni wazi ilishtushwa....Serikali kuona kwamba sasa kwenye issue za masalahi a Taifa wananchi wanataka kuja pamoja.

Ni wazi kabisa kina Mama Masalakulangwa na watanzania wengine wasiojali tofauti zao za kidini wameishtuwa serikali yetu.
Na pia ni wazi kabisa kuwa Membe katumwa aseme yale aliyoyasema kuhusiana na OIC.

Rostam naona kaamua kuwa kimya lakini lazima ana mkono wake hapo maana yeye ndiye mwanasiasa mwenye kuwa na style za aina hiyo...Anajuwa sana ku counter balance na kusway news.
Sasa wakiona wananchi wanaungana...Wanatafuta cha kuwatenganisha by any means....Likishindikana utaona ukabila na muungano vinaibuliwa...Huu ni wakati wa kuzizika siasa za wanamtandao once and for all.

Mkuu Mtindio mchango wako ni mzuri hapa kwenye hoja hii na hivyo basi tunaendelea kusikilizia maoni yako na ukweli mzima kuhusu issue hii na ni kivipi tumefika hapa.
Nakubali kipindi cha Mwinyi mambo yalizidi kuvurugika na udini ilineemeka sana kipindi hicho....Mihadhara na bucha za nguruwe bongo ilikuwa vurugu tupu.

Wanaodai tujiunge na OIC simply eti kwasababu ya misaada ni wavivu wa kufikiri kwani tatizo si misaada bali viongozi wetu.

Kwanza nilidhani serikali sasa inataka kuwaandaa watanzania kutokutegemea wafadhili kwasababu tuna utajiri mkubwa sana ni uongozi tu wa hawa viongozi wetu ambao kusema ukweli saa nyingine tunajiuliza kama wana akili timamu ama ni just politics.
 
Kwani sasa tulivyo tunakosa nini?
Huoni tutavunja katiba yetu mabyo inasema nchi hii haina dini?
Au hujui OIC ni kwa nchi za Kiislamu na ni kwa ajili ya jamii ya kiislamu?
******.
]


Ndio maana tunaitwa waswahili: tunapinga kujiunga na OIC na tukiulizwa madhara ya Tz kujiunga na OIC hatuna jibu, badala yake tunauliza hasara za kutojiunga!!

Sasa kama faida za kujiunga = 0, na hasara za kutojiunga = 0 kwanini tunapinga kujiunga?

Narudia swali, mimi kama Mtanzania nadhurika vipi kwa nchi yangu kujiunga na OIC? Maaskofu na watu wa dini nyingine watadhurika vipi kwa Tz kujiunga na OIC? Haya ndio maswali ambayo wananchi wanataka kujuwa watakapokuwa wanatoa maoni yao.
 
Sasa hivi unadhurika nini Tanzania kutokuwemo OIC? Ni nani waliotuambia kuwa Salim hafai kua rais wetu kwa sababu ya rangi na dini yake sio hawa kina Membe na Mtandao?

Jamani naona sasa tumepatikana, hawa jamaa wanjanja sana wanajua wakiingiza huu mjadala kinachofuatia ni kubishana na kuacha mambo ya msingi, mimi binafsi sio tatizo la hili swala kwani serikali haiwezi hata kidogo kuamua kuingia OIC bila kuwashilikisha wananchi.

Siku hizi serikali yetu inampago mkubwa sana wa kushirikisha wananchi kama wananvyotaka mwafaka wa zanzibar upitie, wameongea hivi ili tuwape nafasi ya kupumua kidogo.

hakuna haja ya kutukanana hapa kwani wakati ukifika tutaamua kwa kura zetu kujiunga au kutojiunga.
 
Mkamap,
Hivyo kujenga hoja zako za OIC kulinganisha na VATICAN ni upotoshaji wa makusudi.ELEA HIVI vatican SIO tAASISI YA KIKATHOLIC bali ni nchi ya kikatholic na makao makuu ya kanisa katholic yapo ktk nchi ya VATICAN.
Tumia logic tu kidogo IMF ni taasisi hivyo makao makuu ya IMF hayawezi kuwa ktk IMF bali yapo ktk nchi fulani

Mkuu hata sijui niseme kitu gani...unapotumia IMF kuwa mfano wa Vatican. Yaani ni vitu viwili ambavyo havifanani kabisa..Kitumbua mkuu sio Andazi.
Kwa nini nasema hivyo IMF imeanzishwa kama Taasisi kisha ikatafutiwa makao makuu ambayo yanaweza kuhama kesho na kuwa nchi nyingine yoyote bila utata wowote..Lakini sio Vatican na Utawala wake, pengine ungenambia CCM ya Nyerere ya chama kimoja ni sawa na Ukatoliki na Vatican, chombo cha siasa ambacho kimeanzishwa na kuiendesha nchi - Tanzania..
Sasa huwezi kutenganisha CCM kama chama na Tanzania kama nchi kwani bila CCM Uhuru wa Tanzania ungekuwa na sura ama historia tofauti...Na Vatican kama CCM ya Nyerere haina Upinzani yaani mgombea huyo Papa anachaguliwa na Vatican wenyewe kina Pengo ambao ni raia wa Tanzania. Uliona wapi mfumo wa nchi namna hiyo! na hizo logic unazotumia..
Kwa hiyo tunapozungumzia kuwa Vatican ni nchi ni muhimu sana kutazama ni kitu gani kinaifanya nchi kuwa nchi kama mjadala huu unavyoendeshwa... Ikiwa kweli Vatican ni nchi iweje Pango na Makadinali wengine nchi tofauti duniani washiriki kupiga kura za uchaguzi wa rais wao na mtu yeyote toka sehemu yoyote duniani anaweza kuwa rais ama kiongozi wa juu wa nchi hiyo mnayotaka kuipa jina la NCHI!..Kesho Pengo, raia wa Tanzania anaweza kuchaguliwa kuwa Papa - rais wa Vatican how come?..Huyo aliyepo leo ni raia wa wapi? Vatican au Germany!..
Ukinijibu hayo tutaendelea..
Iran ni nchi ya waislaam kama vile Tanzania ni nchi ya weusi, lakini huwezi kusema mapinduzi ama kutokubaliwa kwa Utawala wa Somalia kimataifa kuna direct affect kwa watu weusi wote na kwamba pengine inaweza kufananishwa na swala la Vatican..
Nimekwisha kwambia hata kesho ondoa Uhusiano na Iran au Saudia haiwezi kuwa sababu ya waislaam kupiga kelele kwani hatuna ushirika kwa lolote zaidi ya kuwa makao makuu kama ilivyokuwa Adis Ababa, Ethiopia kuwa m makao makuu ya OAU enzi za Haile Marium. Kuondolewa kwake hakuna maana kunatuhusu Tanzania na nchi za Kiafrika..

Field marshall es,
Mkuu unazidi kuyumba hapa hujanijibu kitu kweli!
 
Ndio maana tunaitwa waswahili: tunapinga kujiunga na OIC na tukiulizwa madhara ya Tz kujiunga na OIC hatuna jibu, badala yake tunauliza hasara za kutojiunga!!

Sasa kama faida za kujiunga = 0, na hasara za kutojiunga = 0 kwanini tunapinga kujiunga?

Narudia swali, mimi kama Mtanzania nadhurika vipi kwa nchi yangu kujiunga na OIC? Maaskofu na watu wa dini nyingine watadhurika vipi kwa Tz kujiunga na OIC? Haya ndio maswali ambayo wananchi wanataka kujuwa watakapokuwa wanatoa maoni yao.

OIC ni Jumuiya ya Wa-Islam, taifa lolote lisilo la Wa-Islam kujiunga huko ni wendawazimu, ambao sisi baadhi ya wananchi wa taifa hili tunapinga tena kwa nguvu zote, Maana ya uswahili uliyoitoa kama ni ya kweli, basi tunaongozwa na viongozi waswahili, ambao badala ya kutafuta njia zinakubalika kimataifa kutatua matatizo yetu, wanajaribu kutafuta njia za mkato,

OIC ni jumuiya ya Wa-Islam period, betweeen jana na leo nimeongea na wakubwa wengi sana wa taifa, na wakubwa huko UN wamenihakikishia kwamba OIC ni member wao as Jumuiya ya wa-Islam, ninarudia Tanzania sio taifa la ki-Islam we have no business kujiingiza huko, hatuhutaji mjadala wala anything on hilo.
 
Mkuu unazidi kuyumba hapa hujanijibu kitu kweli!

Bob haiwezekani ukanirukia mimi ninaeyumba ukawaaacha wasioyumba, nimesema hoja unayojaribu kuniwekesha sio yangu hoja zangu on this ishu ziko wazi, ukitaka tunaweeza kuzichambua, sina noma,

Labda nirudie tena Tanzania sio nchi ya Kii-Islam, OIC ni Jumuiya ya wa-Islam, kwa maneno mafupi ni kwamba OIC haituhusu Tanzania.
 
Field Marshall Es,

Mkuu nimekufuata wewe kwa sababu unayumba, ungekuwa wima wala nisingekufuata kwani wanihusu sana zaidi ya kuwa hapa Mtandaoni..Kesho naweza kuogopa kuomba maji ikiwa moyo wako umepigwa mhuri..

Mkuu, kama unazo hoja ziweke lakini kwanza rekebisha maneno yako kuunga mkono ati waislaam wote wahamie Zanzibar Tanganyika ibakie nchi yenu kama vile mlijua hata pa kuanzia kuutafuta Uhuru..
Ni kweli kabisa kuwa OIC ni jumuiya ya Waislaam..sasa uinavyofikiria wewe Waislaam hawana haki ndani ya nchi isiyokuwa na dini?..Ikiwa wanazo haki kwa nini nchi isiwasaidie na kutambua haki zao wakati nchi inatambua hata haki za Mashoga Kwani nchi hii ni ya Mashoga! Tumejiunga na jumuiya za wanawake kwani nchi hii ni ya Wanawake watupu! yaani hata siwaelewi mnakojaribu kupeleka hoja hii.

Kitu kimoja tu mkuu wangu, kuna baadhi ya watu wanajaribu sana kuharibu uhusiano kati ya Waislaam na Wakristu kwa kutumia jina la dini.. sioni sababu kabisa ya sisi kupingana hapa kama vile Marekani leo hii wanavyojaribu kumkandya Obama kwa sababu iliyojificha - kuwa ni mweusi. Obama anakuwa sababu ya chuki walizokuwa wamepandikizwa miaka nenda, leo ktk uchaguzi huu chuki hizo zinatoka kwa sura tofauti. Wanajaribu kutumia kila Hila kumshusha hadhi wakati ukweli unabakia palepale -Wazungu hawataki kutaliwa na mweusi... hizi habari za Marekani ni nchi ya kila mtu na kuna Uhuru kwa wote ni Uongo mkubwa...Na hizi chuki naziona ktk mioyo yetu pamoja na kwamba sina uwezo wa kuchungulia ndani ya mioyo ya watu isipokuwa ndimi zetu zinatusuta..
 
Back
Top Bottom