........... Kama kukipata ni lazima serikali yetu ijiunge, so be it. Tukiona kubaya si tutajitoa na kuwaeleza wenzetu kwa nini tumefanya hivi. Viongozi wa kikristu kwa kulishikia bango suala hili ndiyo kunazidisha imani kuwa wakristu hawawatakii mema wenzao. Kichuguu tunakigeuza mlima sisi wenyewe.
Kuna ishu za kusimamia kidete ( Mahakama ya Kadhi ikiwa ni mojawapo) lakini si hili. Tujiunge tu na chombo hiki kwa faida ya wenzetu. Hatutabadilika kuwa nchi ya kiislamu kwa kufanya hivyo.
Amandla.......
Sikiliza Fundi. Kitu ambacho huna uhakika ni sumu au la, hakijaribiwi kwa kukionja! Kinapelekwa maabara kuchunguzwa. Maabara zetu za masuala ya kijamii ni majukwaa kama haya ya JF.
Maswali muhimu ya kujiuliza kabla ya kupendekeza kujiunga kwenye hiyo OIC ni haya: Je sisi watanzania kama taifa tunayaamini na kuyakubali malengo ya OIC kama yalivyoainishwa kwenye OIC charter? Na je tuko tayari kama taifa kushiriki kutekeleza malengo hayo? Hebu isome kwanza hiyo charter, inapatikana kirahisi tu kwenye google.
Mimi binafsi siiamini wala siikubali hiyo OIC charter kwa ujumla wake, na hivyo siko tayari kuwa sehemu ya utekelezaji wake. Na ninaamini kuwa kama hiyo kitu ikiwekwa wazi watanzania wote wakaijua, wako wengi tu watakaokuwa na msimamo kama wangu. Na zaidi ni kwamba malengo ya charter ile kwa nchi kama yetu yenye mchanganyiko wa kiimani, hayawezi kutekelezwa na nchi maana yatakuwa yanapingana na katiba ya nchi ya kutofungamana na dini yoyote.
Lakini ninakubali na ninaheshimu haki ya waislamu kushiriki mambo ambayo wanayaamini, ikiwamo ya kujiunga na jumuiya kama hizo. Ndio maana nasema hiyo OIC itoe nafasi kwa waislamu wa nchi ambazo si za kiislamu kujiunga nao katika nafasi yao ya uislamu na si kupitia kwa serikali. Lakini hii ya kutaka misimamo ya kidini ipewe nguvu za kiserikali (ndilo linalotafutwa kwa kudai serikali ijiunge na OIC) kamwe haliwezi kukubalika katika nchi ya utawala usio wa kidini.