Juu ya OIC na Mahakama ya Kadhi

Juu ya OIC na Mahakama ya Kadhi

Hivi JK na Tume ndiyo utakuwa mchezo wake ama yuko serious ?Maana duh! zio kibao zilizopo na zinazo kuja
 
Hata wakiiondoa kwenye soft copy bado ipo kwenye hardcopy na tunazo.

ama kweli Ukitaka kujua Tanzania na watanzania angalia viongozi wake , hivi Shein naye hakushirikishwa kuandaa ilani?kwani huyu alikuwa mtaalamu wa kukariri ilani wakati wa mchakato, hebu naye ajitokeze kumwokoa JK kwani hawezi kujinasua pekeyake tena.


Na kweli namkumbuka makamu enzi hizo ilani yote ilikuwa kichwani alikuwa hazungumzi bila ilani, kama ukitaka kujua ilani ya ccm ilikuwa kuvuzia mikutano yake tu

Lakini kwa ninavoona ni kama kila mtu yupo yupo tu sijui kama wanakaa saa ngapi kushauriana au makamu sio mshuri wa Rais?
 
JAMANI INAKUWAJE MKUU WA NCHI ASEME HAUSIKI? INAMAANA KAMA WANAO KAANZISHA KITU KATIKA FAMILIA BABA UTASEMA SIHUSIKI KWASABABU MWANAO ALIANZISHA?

La hasha mambo yanazidi kuwa mambo, ni jambo la ajabu sana kuona suala la mahakama ya kadhi linajadiliwa kanisani. Mh JK angetumia fursa hii kujibu hoja hii akiwa katika moja ya siku kuu za kiislamu ajibie huko huko. Ili pengine angeweza kuona nini maana ya amani maana nadhani takbir zingeanza pale pale mbele yake. Ni suala la yeye kutoa tamko kwamba mjadala huu "STOP" akatoa sababu kama hizo wenzetu Kenya anasema wanaendesha kadhi huko kwao. Uganda iko ktk katiba lakini bado hawajaanza kutekeleza. South Afrca hakuna kabisa, tatizo letu sisi kama sitakosea tunajaribu kuiga bila kuona haja ya kuwepo mahakamka hiyo ama la, ndiyo maana unaona walienda kuangalia wenzetu wanaendesheje mahakama hizi. Uwepo wa mahakama hii mimi sipingi kabisa ninachopinga ni serikali kujiingiza. Mimi kama Mkristo siwezi nikachangia fedha yangu kwa jambo ambalo sina faida nalo, hiyo ni sawa na shughuli za kbra ambapo muumin hayamuhusu. waache hao waislamu waunde mahakama hizo ili wajihukumu wenyewe kwa sharia zao. Na kama utabiri kwa kuwa mahakama hizi zina athari kubwa sana zinapotekeleza majukumu yake ni dhahiri waislamu wengi watayakana hapo baadaye au la wengi wao wataamua kubatizwa.
 
Kisa cha JK kuikana Ilani ya Chama chake, kinatukumbusha hadithi ya Adam na Eva kule bustani ya Eden. Eva alimshawishi Adam kula tunda lilokatazwa na Mungu. Adam bila kufikiria mara mbili akala. Baadaye Mungu anamwita Adam (si Eva) Uko wapi? umekula lile tunda nililokukataza? Adam akajibu "Si huyu Mwanamke uliyenipa ndiye kanipa nami nikala" Adam kama Kiongozi hakuwajibika, hakukubali makosa, akamtupia Mungu lawama kwa kumletea Mwanamke.

Jk hataki kuwajibika yeye kama kiongozi wa nchi na chama chake. anawatupia lawama viongozi waliomtangulia anasahau kwamba naye alikuwa mmoja wao. katika hili amepotoka, anastahili kujifunja somo la Teamwork linasema nini. Inavyoonekana serikali inaongozwa kwa mtindo wa Competition zaidi, kila kiongozi anajiangalia yeye kama yeye, hii ni hatari kwa maendeleo ya nchi yetu.

Anatakiwa apate kichwa kizuri pale ikulu maana EL huenda anampoteza ili aonekane bomu mbele ya watz (my opinion)
 
Hivi JK na Tume ndiyo utakuwa mchezo wake ama yuko serious ?Maana duh! zio kibao zilizopo na zinazo kuja

Mkuu Mugishagwe,

Tume ndio mchezo wa wanasiasa wa kukwepa lawama. mtu anaunda tume inachukua muda mrefu mpaka watu wanasahau. Baada ya kutumbua pesa za kutosha za vikao na kuchapisha makaratasi.

Tume inakuja na very simpo solution ambayo mara nyingi huwa ina maneno yafuatayo.... to the best of our knowledge....
 
Miaka michache iliyopita iliundwa tume/kamati maalumu kujaribu kutafuta ni jinsi gani watu watapunguza intake ya chumvi ya mezani. Baada ya research na fedha karibu dola milioni mbili, tume ilikuja na mapendekezo yake. Pendekezo la kwanza na kubwa zaidi lilikuwa KUPUNGUZA MATUNDU YA SALT SHAKERS!..
 
Miaka michache iliyopita iliundwa tume/kamati maalumu kujaribu kutafuta ni jinsi gani watu watapunguza intake ya chumvi ya mezani. Baada ya research na fedha karibu dola milioni mbili, tume ilikuja na mapendekezo yake. Pendekezo la kwanza na kubwa zaidi lilikuwa KUPUNGUZA MATUNDU YA SALT SHAKERS!..

...kama kawaida yako hapo,najua kuna kitu unataka kusema ila hutabiriki...Jenerali alisema sifa moja ya kiongozi mzuri lazima awe predictable
 
ni wakati sasa wa vyombo vyetu vya habari kuacha kunukuuu maneno ya mpendwa raisi wetu,kwani kuendelea kufanya hivyo ni kushushia hadha na kumfanya aonekane hafai mbele wa wapigakuru wake.

Raisi anaitaji kuombewa ili mapepo wabaya wanaomwandana washindwe na walegee,haya madudu yamemfikisha mahali hata kusahau alipotoka na ndio kila analosema linakuwa pumba na safari kwa wingi.
 
...kama kawaida yako hapo,najua kuna kitu unataka kusema ila hutabiriki...Jenerali alisema sifa moja ya kiongozi mzuri lazima awe predictable


nina habari mbaya kwako, Jenerali was wrong; kiongozi mzuri hatabiriki, akitabirika siyo kiongozi mzuri. Kiongozi mzuri anasababisha watu wasijue move yake inayofuata ni nini. Kiongozi mzuri ni kama Grand Master wa Chess ambaye licha ya kuwa mnaweza kuona pawns, king na queen wake, you can never guess his coming move.. na wakati akikuweka kwenye "check mate" hutajua alifika fikaje hapo...
 
Yaani huyu jamaa is so cheap.Yaani kwa kauli kama hizi hafai kuwa hata kiongozi wa kaya.
Hawa ndo wale watu wasio na uwezo na uongozi bali nia yao ni kuwa katika kumbukumbu za kuwahi tawala.
 
Raisi anaitaji kuombewa ili mapepo wabaya wanaomwandana washindwe na walegee,haya madudu yamemfikisha mahali hata kusahau alipotoka na ndio kila analosema linakuwa pumba na safari kwa wingi.

duh, haya bwana labda itasaidia!
 
Watanzania,
tukubali yaishe kwamba Kikwete ni bomu,kilaza,zero, hana uwezo wa kufikiri na kuongoza.

nimeshangaa kwanini airuke Ilani ya CCM namna ile. Nadhani Mwalimu wake wa siasa Mzee Kingunge anasikitika. Lowassa naye anatukuwa anacheka kwa mkenge kwa jinsi alivyoturubuni mpaka tukamchagua Kikwete.

Alichopaswa kueleza Kikwete ni nini CCM ilimaanisha kwa kuliweka suala la KADHI ktk ILANI yake. Chimbuko la suala hilo si la msingi hapa. Sasa atayakana mambo mangapi ktk Ilani ya CCM kwa kisingizio kwamba hakushiriki kuiandaa.

Mwanakijiji,
observation yako kwamba suala la Kadhi lipo kwenye Ilani na siyo sera za CCM ni nzuri. Nafikiri tulipaswa kuzama ndani zaidi na kujiuliza kama suala hilo linakinzana au halikinzani na sera za CCM.
 
Watanzania,
tukubali yaishe kwamba Kikwete ni bomu,kilaza,zero, hana uwezo wa kufikiri na kuongoza.

nimeshangaa kwanini airuke Ilani ya CCM namna ile. Nadhani Mwalimu wake wa siasa Mzee Kingunge anasikitika. Lowassa naye anatukuwa anacheka kwa mkenge kwa jinsi alivyoturubuni mpaka tukamchagua Kikwete.

Alichopaswa kueleza Kikwete ni nini CCM ilimaanisha kwa kuliweka suala la KADHI ktk ILANI yake. Chimbuko la suala hilo si la msingi hapa. Sasa atayakana mambo mangapi ktk Ilani ya CCM kwa kisingizio kwamba hakushiriki kuiandaa.

Mwanakijiji,
observation yako kwamba suala la Kadhi lipo kwenye Ilani na siyo sera za CCM ni nzuri. Nafikiri tulipaswa kuzama ndani zaidi na kujiuliza kama suala hilo linakinzana au halikinzani na sera za CCM.

Hivi niulize, kuna uwezekano mtu akaweka kwenye ilani kitu ambacho sio sera ya chama hicho?
Najaribu kufikiria kama CCM waliliweka kwenye ilani katika muktadha upi....wa kulitafutia 'ufumbuzi'.....? Lakini je wahusika wanaelewa kuwa 'ufumbuzi' unaweza kuwa iwepo ama isiwepo, au wanaodhani kuwa 'ufumbuzi' unaotafutwa ni wa kuiweka hiyo mahakama ya kadhi?

Naomba kuelimishwa wakuu
 
Hii inaonyesha ni jinsi gani watu walivyochoshwa na utendaji wa mahakama zetu nchini.Mimi naona kama tunataka haki itendeke kwa wananchi wote basi tuboreshe mahakama zilizopo ili zifanye kazi kwa ufanisi zaidi.Kama kuna watu au kundi linaloona kuwa ufumbuzi wa matatizo ya vyombo vyetu vya mahakama ni kuongeza mahakama za kidini mimi naona hilo si ufumbuzi wa kumpatia haki mwananchi. Kwa mtazamo wangu naona litazidi tu kuongeza malumbano kwenye jamii yetu kwa kuwa si watanzania wote wanaamini dini moja.
Hebu fikiria watu kama sisi ambao ni mabudha na ambao tuanaamini kwa dini yetu ya kibudha, tuwe na mahakama yetu ya kibudha na kuwahukumu wasabato kwa sheria za kibudha tutafika??
Wembe.
 
Mungu isaidie Tanzania ili igeuzie mawazo yake kwenye maswala ya kujenga uchumi na sio mahakama za talaka na urithi. AMEN
 
Nitaweka sehemu ya pili na ya mwisho baadaye leo na nitaunganisha sehmu zote mbili.
 
Tunapomchagua mtu wa kutuongoza inabidi tuangalie na IQ zake zimekaaje hata kwa kuwashirikisha wataalamu maaanake duh!
 
Ben umesema kweli,nadhani safari hii mpaka hapa tulipo watanzania wamejifunza vizuri tu.May be next time watabadilika, lakini nina wasiwasi tatizo kubwa pia ni watu kusahau!!
 
Mkandara ,

Heshima mbele mkuu , mimi nakubalina na wewe kabisa kwamba kuna mapungufu makubwa katika sheria zetu epecially inapokuja kwenye masuala ya mirathi. Lakini lazima tukubali ya kuwa CONSITUTION ndio supreme law of the land , na kama kuna sheria yoyote inayokuwa na conflict na katiba ni lazima ipingwe na wakati huo huo kubatlishwa.

Suala hapa sio la uislamu au ukristo , suala hapa ni conflict kati ya mahakama kadhi na katiba yetu ya Jamhuri . Kitu kingine ninachokiona hapa kama tukiruhusu dini fulani iwe na mahakama yake , then tutakuwa na mahakama ngapi ? mind you tuna dini nyingi sana hapo nyumbani .Na jee mahakama ipi itakuwa na nguvu kuliko mahakama nyingine ? Mimi nadhani ni muhimu kuwa na separation kati ya dini na serikali .
 
Jamani naona kuna tatizo moja ambalo lazima tulisahihishe. Binafsi sijaona mahali popote ambapo Jumuiya ya Waislamu wanataka Marekebisho ya Katiba (niko tayari kusahihishwa kwa hilo), ila wanataka sheria ibadilishwe au itungwe ili uwepo wa mahakama za kadhi utambulike kisheria.

Suala la Kikatiba linakuja pale ambapo watu walio nje ya wanamwamko wa vuguvugu hili wanapoamini kuwa endapo sheria kama hiyo itatungwa basi itavunja Katiba kwa kuipendelea dini fulani rasmi wakati serikali haina dini.

Upande wa Jumuiya hiyo wao wanasema hivi kuhusu suala la sheria:

a. Endapo sheria itatambua uwepo wa makadhi basi maamuzi yao yataheshimika na kukubalika.

b. Sheria itaweka mipaka rasmi ya mahakama hizo kufanya watakalo.

c. Mahakama ya Kadhi iko Zanzibar na inatambulika kisheria na ina mipaka yake.

Kwenye hilo la pili kuna hoja ya msingi. Endapo Waislamu watajianzishia mahakama yao wenyewe nani atawawekea mipaka ya kisheria?
 
Back
Top Bottom