Nadhani Rais ambaye kwa dini ni mwislamu alilazimika kuonyesha mbele ya jamii ya wakristo kwamba chimbuko la wazo lenyewe lilitoka wapi? Na sasa nini kinafanyika, kwa mkristo wa kawaida anadhani hili linakuja kwa kuwa rais ni mwislamu.
Ilikuwa ni muhimu kuonyesha kwamba yeye sio mwasisi wa hiyo mahakama ya kadhi... Lakini hata hivyo hebu tuangalie CCM iliahidi nini?
Sura ya Nane "MAENEO MENGINE MUHIMU", IBARA 108 (b) ya Ilani ya Uchaguzi wa CCM 2005. inasema na ninanukuu!!!
Ukisoma vizuri hii sio ahadi kwamba Mahakama ya Kadhi itaanzishwa; hii ni ahadi kwamba suala hili litajadiliwa, litachambuliwa na kwa pamoja kuwa na msimamo mmoja na kuweza aidha kuanzisha au kutoanzisha, huu ndio uelewa wangu, naomba musome hayo maneno ya Ilani ya Uchaguzi hapo juu!!!
Na kwa kweli nadhani mchakato ulishaanza ikiwa ni pamoja na tume ya kurekebisha sheria kuwa hiyo ni agenda yao... what else was needed guys!!!
Sasa tume haijasema kitu... ndio hivyo tena ramli zimeanza... au hili suala mlitaka JF ndio wapewe walifanyie kazi?
Kulipatia ufumbuzi maana yake ni kutatua tatizo sio kulizungumza,
Huyu JK anaonyesha alivyo na uwezo mdogo, pia serikali ya awamu ya nne wanaonyesha jinsi walivyo na ubongo mdogo, kwani wakati wa tatizo la umemem LOWASSA alisema kuwa hilo sio tatizo la serikali yao ila lilitokana na awamu ya tatu.
Leo JK naye anasema kuwa hilo sio la kwake, hapa kuna tatizo la kimsingi kama JK haijui ilani iliyomweka madarakani ,basi hawezi kamwe kuitekeleza na hivyo hafai kuendelea kutekeleza kitu ambacho hakijui ama hajashiriki kukiandaa,
Namlaumu rais wetu kwa kusema kitu ambacho ni zaidi ya uwongo kwani alishawahi kusema kuwa atatekeleza ahadi zote zilizoko kwenye ilani ya CCM na zile alizoziita ahadi za papo kwa hapo.
Mahakama ya kadhi ni ahadi ya ccm kama zilivyo ahadi nyingine , na kama tukisema kuwa hii sio ahadi basi hakuna haja ya kudai ahadi nyingine zitekelezwe kwani pia zimo ndani ya ilani.
Kusema ni hoja ya Mrema ni kufilisika kimawazo, na je?Mrema alishiriki kuandaa ilani ya CCM? ama yeye ni consultannce wa CCM?
Mwenyekiti wa ccm hana budi kufafanua kuwa ilikuwaje hoja ya mrema ikaingizwa kwenye ilani ,wakati yeye kwa wakati huo alikuwa ni mjumbe wa kamati kuu ya CCM aseme kuwa hajui na hakushiriki kuandaa ilani wakati wao ndio walipitisha ilani hiyo?
Inamaana kuwa vikao vya ccm alikuwa anaenda kusinzia ama alikuwa anafuata nini hadi asikijue kitu alichokuwa anakipitisha kwenye vikao?
Naendelea kuuona uwezo wa ubongo wa rais wetu na majukumu tuliyompa naona hawezi kama huku ndio kufikiri kwake na kuona hii ni kauli ya kutoa mbele ya maaskofu na waumini wa kkt basi kuna haja ya uchunguzi wa kina juuu ya uwezo wake.