Je, Rais Samia alikuwa haaminiki au ndiyo mfumo wa ulinzi na usalama ulivyo?

Shikamoo sana mtoa hoja.

Umeyaongea mengi sana kwenye aya chache

Kuna jambo moja naliona kwenye huu mfumo wetu. Mimi niliwahi kuwa kiongozi ngazi ya chini hukooo. Lakini upofu wangu ulinisaidia kujua how does system works. Kosa lipo kwenye eneo la uongozi, kuna viongozi wengi wamepachikwa kutoka kwenye system, wanakuwa loyal kwa mfumo na siyo kwa wananchi.

Sheria inayounda TISS ikiboreshwa iendane na mazingira tuliyonayo ya uchumi struggle tunaweza kufika mahala pazuri
Na ndio asilimia 75 ya viongozi wote..
 
Kifo cha Rais Magufuli kimefunua siri ambayo nadhani wengi hawakuwahi kuijua. Kifo cha Rais Magufuli kimeonyesha jinsi ambavyo Rais Samia alikuwa hajui siri za nchi ambazo kwa wadhifa wake kama Makamu wa Rais alitakiwa awe anajua!

Nakumbuka hata Rais Magufuli alipoingia madarakani alikuwa hajui siri nyingi za nchi lakini hili halikunishangaza sana kwa sababu alikuwa waziri tu kabla ya kuwa Rais wa Tanzania. Waziri hawezi kujua siri za ulinzi na usalama ambazo kwanza zinamfikia Rais kama Amiri Jeshi Mkuu.

Kwa wanaokumbuka vizuri, baada ya Rais Magufuli kuingia madarakani aliwaondoa wafanyakazi wengi hasa wa vyeo vya juu katika nafasi zao bila kujua baadhi yao ni sehemu ya watu wa usalama wa taifa(TISS). Mmoja wa wale waliondolewa ni Diwani Athumani Msuya ambaye alikuwa Mkurugenzi wa upelelezi wa makosa ya jinai(DCI) na kupelekwa kuwa Katibu tawala wa Mkoa wa Kagera.

Baada ya Rais Magufuli kuanza kupata classified intelligence briefings kutoka kwenye taasisi za ulinzi na usalama nchini ndio akajua alichokifanya pia kwa Diwani Athumani Msuya ni makosa ya bila kujua kwa sababu Diwani ni sehemu ya Usalama wa Taifa ndio maana akamrudisha na kumteua kuwa Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU.

Kwa wenye kumbukumbu, Rais Magufuli baada ya kuingia madarakani alianzisha mahusiano ya karibu na Rais Kagame lakini yalipungua sana baada ya kupata classified intelligence briefings kuhusu faida na athari zake kwa taifa.

Kilichonishangaza zaidi ni kuona kuwa Makamu wa Rais kwa zaidi ya miaka mitano ambaye kwa sasa amekuwa Rais wa Tanzania hana uelewa mkubwa wa mambo yanayoendelea hasa ya ulinzi na usalama nchini.

Rais Samia baada ya kuapishwa kuwa Rais alianza naye kusikiliza kelele za kwenye mitandao na kuanza kuondoa watu mbalimbali katika nafasi zao za kazi huku pia akiagiza wafanyiwe uchunguzi bila kujua kuwa baadhi ya watu hao ni sehemu ya usalama wa Taifa. Hii inaonyesha pamoja na kuwa alikuwa Makamu wa Rais wa zaidi ya miaka mitano lakini hajui kinachoendelea nchini hasa kwenye masuala ya ulinzi na usalama.

Kwa sasa nadhani baada ya kuanza kupata classified intelligence briefings kutoka katika vyombo vya ulinzi na usalama ameanza kuujua ukweli na kujikuta hata baadhi ya chunguzi ambazo alielekeza zifanyike zinakuwa ''redundant''.

Yanayoanza kutokea kwa sasa yanadhihirisha Rais Samia hakupata classified intelligence briefings wakati akiwa Makamu wa Rais. Kwa sasa baada ya kuanza kupewa hata aina tabia za kiuongozi zimeanza kubadilika. waliokuwa wanalia wameanza kucheka na waliokuwa wanacheka wameanza kulia!

Wanaoijua ''system ya utawala'' nchini hawawezi kushangaa kuona uchunguzi wa BOT na aliyekuwa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya usimamizi wa Bandari nchini(TPA) Deusdedit Kakoko ukiishia kwenye makabati ya Ikulu!

Hata kesi ya aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai inaweza kufia njiani, fikria eti kwa sasa mashitaka yamebadilishwa na anashitakiwa kwa kosa la kuiba kiasi cha Tsh 3,125,000 na simu aina ya Techno. Haya makosa yamefanyika siku moja katika duka moja! Yaani Sabaya huyu ambaye tuliaminishwa kwenye magazeti na mitandao anabaka, anachukua mamilioni ya shilingi kwa nguvu na kufisadi eti ameiba simu ya Techno!

Hii imenifanya nijiulize; Je, Rais Samia alikuwa haaminiki au ndio mfumo wa ulinzi na usalama ulivyo nchini?

Kama Rais Samia akiwa Makamu wa Rais hakupewa classified intelligence briefings ni kutokana na mfumo wa ulinzi na usalama basi kanuni zake inabidi zibadilishwe! Kama hakupewa kwa sababu alikuwa haaminiki, kwa nini hakuaminika wakati ni Makamu wa Rais?

Nchini Marekani tatizo hili la Makamu wa Rais kutojua kinachoendelea katika nchi hasa kwenye suala la ulinzi na usalama walilifanyia kazi mwaka 1945 baada ya Harry Truman ambaye alikuwa Makamu wa Rais kwa siku 82 tu na kujikuta anakuwa Rais wa nchi baada ya Rais Franklin Roosevelt kufariki. Wakati akiwa Makamu wa Rais hakujua kama kuna mradi uliojulikama kama ''Manhattan project'' ambao ulikuwa mahsusi kutengeneza bomu la atomiki.

Baada ya Harry Truman kuapishwa na kuwa Rais na kugundua udhaifu huo alijiapisha kuwa huo udhaifu hauwezi kutokea tena kwa Rais mwingine kuingia madarakani bila kuandaliwa kwanza kwa kupewa intelligence briefings. Utaratibu wa kupewa intelligence briefings umeendelea mpaka leo hasa pale vyama vikuu viwili vinapoteua wagombea Urais ambapo huanza kupewa intelligence briefings ili wakati wa kampeni wajue ni mambo gani wanatakiwa wayaseme kwenye mikutano ya hadhara ili kulinda maslahi ya taifa.

Watu au taasisi hujifunza kutokana na makosa, Kwa msingi huu yaliyotokea inabidi liwe ni funzo kwa vyombo vya ulinzi na usalama nchini kwa faida ya Taifa!
Mkuu, Inawezekana kwa sasa lakini hayati Nyerere alikuwa na huo utaratibu na ulikuwepo pia wakti wa Mwinyi, Kikwete na Mkapa.

Alipoingia hayati JPM palikuwepo vurugu na hivyohivyo alipoingia mama Samia.

Ila utaratibu wa SB umekuwepo siku zote.

Huanzia na magazeti muhimu ya siku hiyo kisha kuketi na DG au msaidizi.

Sasa hata haya magazeti yetu ya leo mengi si makini.

Zamani ukimsoma mtu kama Charles Kizigha au Lucas Liganga unafahamu utapata kitu muhimu.
 
The Presidency is not shared.

Commander in Chief ni mmoja kwa wakati mmoja, hata Marekani pamoja ni briefings wanazopewa, bado wanachopata ni peanuts ukilinganisha na anachopewa CiC. Ndio changamoto za kazi, Marais wote huwa wanaanza na blunder za hapa na pale.
 
Ndio maana sikutaka kujikita zaidi kwenye wagombea Urais kupata intel briefing kwa sababu siasa zetu bado ni changa sana!

Nimejikita kwa Makamu wa Rais kwa sababu kiuhalisia anakuwa ni Rais wa nchi wakati wowote kama la kutokea litatokea!

Sio unakuwa na Makamu wa Rais halafu la kutokea likitokea nchi inakuwa kama ndio imemaliza Uchaguzi Mkuu na inakuwa kwenye transition period!
Nadhan hz brief anapewa mgombea wa ccm km zp baadhi
 
Bro una hoja nzuri sana ila naona hutaki kukosolewa. naomba nikuulize kwa mazingira gani tuseme basi Sabaya yupo gerezani/ mahabusu kaenda kumhoji nani ambaye yupo kwenye top list ya ma files ya TISS

Nadhani Mkuu unapaswa kutulia na usome na kuelewa mantiki nzima ya bandiko la mtoa Mada.
 
Af mdau inaonekana hataki kukosolewa yaani

Tatizo siyo kukosolewa,nachokiona hapa wewe binafsi ndiyo hujaelewa mantiki nzima ya bandiko lake.Ukielewa unaweza kuja na hoja za msingi pia za kumkosoa,wewe hapa unakwenda kushoto wakati mada inakwenda kulia.Hapo ndipo tatizo la “ukosoaji” wako linapoanzia.
 
Umeandika utumbo mtupu. Usalama wa taifa sio tiketi ya kufanya maovu. Huyo mumeo Sabaya unayemtetea kafanya maovu yasiyohitaji maelezo mengi zaidi ya kumfikisha mahakamani. Kamati ya maadili ya CCM ndo kila kitu nchi hii. Muulize Lowassa atakupa jibu sahihi kuhusu hiyo kamati.
kamati ya maadili? Maadili gani ya kimaku ya kuwateuwa majangili kuwa maDC ?Nani anafanya vetting? Anyway time I'll tell.
 
Ulevi wa Madaraka hauendani kabisa na mambo ya kiusalama.
Jamaa alikua mlevi wa Madaraka na asiingizwe/asiusishwe kabisa kwenye mfumo maana atachafua taswira nzima ya mfumo Bora na msafi wa kiusalama wa Nchi yetu Tanzania.
 
Kwa nini huwa unamtetea huyo kibaka mwenye tuhuma za kijingajinga? Halafu unataka kutueleza kwamba "Ole Mungiki" mwenye tabia sugu za uhalifu(rejea alivyojifanya TISS halafu akakwama) kwamba hawezi kuiba simu?Ulitaka aibe,apore nini weye ndiyo ingekuingia akilini kwamba amefuzu ukibaka?
Unajua kwamba kuna watu wazima,kwa sababu wana tabia za udokozi,hawajaacha kudokoa mboga hadi wanafika late 50's?
Na tumkumbushe tu kuna mmiliki wa mabasi fulani hadi leo ni mwizi wa simu kwenye ma grocery
 
Kwa Marekani hata raisi aliyestaafu ana aceess ya kupewa intelligence briefing. kwa hapa TZ bado sana
 
Kwamba Sabaya anaenda kuiba simu aina ya Techno kwa kutumia silaha! Nchi hii kuna sanaa na maigizo ya aina yake!
Hata mimi nashangaa jambo hilo lilivyovurugwa kitaalamu!

Uzushi tuliosadikishwa raia na namna mashitaka yalivyoandaliwa na wanaojiita wanasheria wabobezi ni mambo mawili tofauti na ni ya kustaajabisha sana.

Hivi kiongozi kutenda makosa katika kutekeleza majukumu yake kisheria(kuchukua na kuomba rushwa), waweza kumuandika mashitaka ya ujambazi wa kutumia silaha?

Ninadhani hapa kuna namna ya kulimaliza suala hili bila hatua yoyote kuchukuliwa!

Ni yale yale ya Zombe na genge lake.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nini unataka kusema?
Kwamba Sabaya ni afisa wa usalama wa taifa? Kama ni ndio kuna kipindi alishawahi kushtakiwa kwa kujifanya usalama wa taifa?
Taifa hili usalama wa taifa ni watu wa hovyo tu isipokuwa wachache sana wanaoijua vyema kazi yao.
Tunaweza kuamini hivyo kwamba ni 'Tiss', sababu kwenye kesi hiyo ya kitambulisho ambacho alikamatwa nacho red handed, mwisho wa siku serikali ilinywea!

Eti haioni faida ya kuendelea na kesi ya mtu aliyefoji nyaraka muhimu za serikali!

Vichekesho sana.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Utaratibu wa kupewa intelligence briefings umeendelea mpaka leo hasa pale vyama vikuu viwili vinapoteua wagombea Urais ambapo huanza kupewa intelligence briefings ili wakati wa kampeni wajue ni mambo gani wanatakiwa wayaseme kwenye mikutano ya hadhara ili kulinda maslahi ya taifa.

Kama ni hivyo kwa nini wanasubiri mpaka chama kikuteue mgombea ndio wakupe briefings?

kwani siku unapopanda jukwaani na kutangaza nagombea huwezi kuanza kuropoka mambo yasiyo na maslahi ya Taifa ?

Acha kutuongopea hapa wewe bana...
 
Back
Top Bottom