Bro kama umenisoma vizuri nimesema Rais Samia anaonekana alikuwa hajui kinachoendelea nchini ndiyo maana alipoingia madarakani akaanza kutoa maagizo ya kufanya chunguzi mbali mbali ambazo chanzo chake ni kwenye mitandao ya kijamii kwa watu ambao pia hawajui kinachoendelea nchini!Bro una hoja nzuri sana ila naona hutaki kukosolewa. naomba nikuulize kwa mazingira gani tuseme basi Sabaya yupo gerezani/ mahabusu kaenda kumhoji nani ambaye yupo kwenye top list ya ma files ya TISS
Why?Who are you by the way ??
Rejea kuondolewa kwa Gen Kombe...waliomwondoa Mzee Mkapa aliwapa msamaha kwa sababu ni state taskNeno ''wanavyojisia'' halipo kwenye majukumu ya ofisa wa Usalama wa Taifa!
Hoja ya msingi ni kuwa utajuaje kama alichofanya amekifanya kama ''anavyojisikia'' na sio kama ''alivyotumwa''.
Wenye historia ya nchi hii tunajua kuwa wakati wa vita vya uhujumu uchumi vilivyoongozwa na Marehemu Sokoine wakati wa utawala wa Nyerere, kuna watu wa usalama wa taifa ilibidi waonekane kama wamekamatwa na kupelekwa gerezani kama wahujumu uchumi lakini kiuhalisia walikuwa kazini kwenda kuwapeleleza mahabusu wengine waliokamatwa kwa kesi hizo.
Nimerejea!Rejea andiko lako.
Thanks!
Ndio maana sikutaka kujikita zaidi kwenye wagombea Urais kupata intel briefing kwa sababu siasa zetu bado ni changa sana!Nawaza wagombea wetu wote mfano hii ya 2020....wapewe intel briefing ili waweke sawa kampeni zao!. Hii kitu mkuu hakiwezi kunakiliwa kama kilivyo kisha kukitupa huku kwetu. Nina imani umejua ninachokimaaanisha.
Hata hilo unalosema alivamia hotel ya Mbowe, Kama kweli alivamia tutajuaje kama hakutumwa na ''system'' kufanya hivyo?
Kama nilivyosema kwenye mada yangu, inaonyesha Rais Samia hakujua yanayoendelea nchini na kwa mantiki hii hata kutaka kufanya uchunguzi alisema wakati hajapata picha halisi ya ulinzi na usalama nchini!
Watu wa system ya utawala kwa ivo watawala wafanye makosa yote wasiwajibishwe.Kifo cha Rais Magufuli kimefunua siri ambayo nadhani wengi hawakuwahi kuijua. Kifo cha Rais Magufuli kimeonyesha jinsi ambavyo Rais Samia alikuwa hajui siri za nchi ambazo kwa wadhifa wake kama Makamu wa Rais alitakiwa awe anajua!
Nakumbuka hata Rais Magufuli alipoingia madarakani alikuwa hajui siri nyingi za nchi lakini hili halikunishangaza sana kwa sababu alikuwa waziri tu kabla ya kuwa Rais wa Tanzania. Waziri hawezi kujua siri za ulinzi na usalama ambazo kwanza zinamfikia Rais kama Amiri Jeshi Mkuu.
Kwa wanaokumbuka vizuri, baada ya Rais Magufuli kuingia madarakani aliwaondoa wafanyakazi wengi hasa wa vyeo vya juu katika nafasi zao bila kujua baadhi yao ni sehemu ya watu wa usalama wa taifa(TISS). Mmoja wa wale waliondolewa ni Diwani Athumani Msuya ambaye alikuwa Mkurugenzi wa upelelezi wa makosa ya jinai(DCI) na kupelekwa kuwa Katibu tawala wa Mkoa wa Kagera.
Baada ya Rais Magufuli kuanza kupata classified intelligence briefings kutoka kwenye taasisi za ulinzi na usalama nchini ndio akajua alichokifanya pia kwa Diwani Athumani Msuya ni makosa ya bila kujua kwa sababu Diwani ni sehemu ya Usalama wa Taifa ndio maana akamrudisha na kumteua kuwa Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU.
Kwa wenye kumbukumbu, Rais Magufuli baada ya kuingia madarakani alianzisha mahusiano ya karibu na Rais Kagame lakini yalipungua sana baada ya kupata classified intelligence briefings kuhusu faida na athari zake kwa taifa.
Kilichonishangaza zaidi ni kuona kuwa Makamu wa Rais kwa zaidi ya miaka mitano ambaye kwa sasa amekuwa Rais wa Tanzania hana uelewa mkubwa wa mambo yanayoendelea hasa ya ulinzi na usalama nchini.
Rais Samia baada ya kuapishwa kuwa Rais alianza naye kusikiliza kelele za kwenye mitandao na kuanza kuondoa watu mbalimbali katika nafasi zao za kazi huku pia akiagiza wafanyiwe uchunguzi bila kujua kuwa baadhi ya watu hao ni sehemu ya usalama wa Taifa. Hii inaonyesha pamoja na kuwa alikuwa Makamu wa Rais wa zaidi ya miaka mitano lakini hajui kinachoendelea nchini hasa kwenye masuala ya ulinzi na usalama.
Kwa sasa nadhani baada ya kuanza kupata classified intelligence briefings kutoka katika vyombo vya ulinzi na usalama ameanza kuujua ukweli na kujikuta hata baadhi ya chunguzi ambazo alielekeza zifanyike zinakuwa ''redundant''.
Yanayoanza kutokea kwa sasa yanadhihirisha Rais Samia hakupata classified intelligence briefings wakati akiwa Makamu wa Rais. Kwa sasa baada ya kuanza kupewa hata aina tabia za kiuongozi zimeanza kubadilika. waliokuwa wanalia wameanza kucheka na waliokuwa wanacheka wameanza kulia!
Wanaoijua ''system ya utawala'' nchini hawawezi kushangaa kuona uchunguzi wa BOT na aliyekuwa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya usimamizi wa Bandari nchini(TPA) Deusdedit Kakoko ukiishia kwenye makabati ya Ikulu!
Hata kesi ya aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai inaweza kufia njiani, fikria eti kwa sasa mashitaka yamebadilishwa na anashitakiwa kwa kosa la kuiba kiasi cha Tsh 3,125,000 na simu aina ya Techno. Haya makosa yamefanyika siku moja katika duka moja! Yaani Sabaya huyu ambaye tuliaminishwa kwenye magazeti na mitandao anabaka, anachukua mamilioni ya shilingi kwa nguvu na kufisadi eti ameiba simu ya Techno!
Hii imenifanya nijiulize; Je, Rais Samia alikuwa haaminiki au ndio mfumo wa ulinzi na usalama ulivyo nchini?
Kama Rais Samia akiwa Makamu wa Rais hakupewa classified intelligence briefings ni kutokana na mfumo wa ulinzi na usalama basi kanuni zake inabidi zibadilishwe! Kama hakupewa kwa sababu alikuwa haaminiki, kwa nini hakuaminika wakati ni Makamu wa Rais?
Nchini Marekani tatizo hili la Makamu wa Rais kutojua kinachoendelea katika nchi hasa kwenye suala la ulinzi na usalama walilifanyia kazi mwaka 1945 baada ya Harry Truman ambaye alikuwa Makamu wa Rais kwa siku 82 tu na kujikuta anakuwa Rais wa nchi baada ya Rais Franklin Roosevelt kufariki. Wakati akiwa Makamu wa Rais hakujua kama kuna mradi uliojulikama kama ''Manhattan project'' ambao ulikuwa mahsusi kutengeneza bomu la atomiki.
Baada ya Harry Truman kuapishwa na kuwa Rais na kugundua udhaifu huo alijiapisha kuwa huo udhaifu hauwezi kutokea tena kwa Rais mwingine kuingia madarakani bila kuandaliwa kwanza kwa kupewa intelligence briefings. Utaratibu wa kupewa intelligence briefings umeendelea mpaka leo hasa pale vyama vikuu viwili vinapoteua wagombea Urais ambapo huanza kupewa intelligence briefings ili wakati wa kampeni wajue ni mambo gani wanatakiwa wayaseme kwenye mikutano ya hadhara ili kulinda maslahi ya taifa.
Watu au taasisi hujifunza kutokana na makosa, Kwa msingi huu yaliyotokea inabidi liwe ni funzo kwa vyombo vya ulinzi na usalama nchini kwa faida ya Taifa!
Hajui anachoandika huyo hajui ethics na miikoKuwa Usalama unaruhusiwa kufanya mambo ya hovyo kwa kigezo cha wewe n mlinzi wa Taifa?
Tuanze hapo kwanza.
Utawala wa Magufuli ulikuwa ni utawala wa aina yake. Samia alikuwa ni kama mtu wa pembeni na hakuaminiwa na Magufuli kwa siri nyingi, hivyo hata kama kungekuwa na briefying kwa vice president bado tu angebaniwa. Samia alikuwa anaonekana kama ni informer wa kambi ya Msoga ambayo nayo haikuwa ''inaiva'' sana na marehemu. Mpaka Magufuli kuugua Samia alikuwa hajui undani wa kinachoendelea na mpaka siku alipofariki hakupata habari mapema. Mwisho: nina uhakika wa 100% Magufuli angejua kuwa hatamaliza kipindi chake cha pili, uchaguzi wa 2020 angechagua makamu mwingine au angebadili katiba ili makamu wa mgombea wa urais wa jamhuri atoke bara pia!Ndio maana sikutaka kujikita zaidi kwenye wagombea Urais kupata intel briefing kwa sababu siasa zetu bado ni changa sana!
Nimejikita kwa Makamu wa Rais kwa sababu kiuhalisia anakuwa ni Rais wa nchi wakati wowote kama la kutokea litatokea!
Sio unakuwa na Makamu wa Rais halafu la kutokea likitokea nchi inakuwa kama ndio imemaliza Uchaguzi Mkuu na inakuwa kwenye transition period!
Amewapoteza maboyaThread hii ina mashiko sana..umechambua vizuri sana. Umewafungua macho na wengine. Good job
Na watanzania wanapenda conspiracy kama hizi hakuna mfano.Watu wa system ya utawala kwa ivo watawala wafanye makosa yote wasiwajibishwe.
Acha kuandika conspiracy zisizo na maana na kuwajaza wafu misinformation ambazo hazina misingi yeyote. When a President is A President. Bahati mbaya sana Tanzania tuna Vice President na si Deputy President
Sent from my SM-G9350 using JamiiForums mobile app
Wewe kausha humjui Sabaya unamdhania na kumwandika kwa sababu ya cheo chake alichokuwa nacho. Tabia ni ngozi,Kwamba Sabaya anaenda kuiba simu aina ya Techno kwa kutumia silaha! Nchi hii kuna sanaa na maigizo ya aina yake!
Tunaambiwa mahakamani kuwa Sabaya alienda kuibaTechno kwa kutumia silaha za moto!Sabaya atatoka na kesi hii haina ushahidi wa kutosha kumfunga jela niliwambia toka mwanzo
Nani alikwambia hakuiva? Equivocal unamanisha pia JPM hakuwa ameiva alipokua Rais tayari?...manake umefanya judgement ya maamuzi yake alipokua rais kuwa hakujua mfumo blah blah, Once you're a President You Are The President acha kabisa kudanganya watuMsingi wa hoja yangu alitakiwa aive wakati akiwa Makamu wa Rais!