UHURU JR
JF-Expert Member
- Jul 24, 2014
- 18,121
- 9,536
Uchawi yeyote yule anaweza kuutenda na si lazima hadi awe mchawi, hata waganga hufanya uchawi wa ubaya au uzuri na ndio maana hao wasio wachawi hutetea uchawi kwa sababu wanaweza kumroga mtu kupitia kwa mganga na waganga wapo wazi wanajitangaza ni tofauti na wachawi.Ungekua specific ni jambo gani hilo la kichawi limetoa hayo matokeo tungejadili vizuri
Kwa hapa kwetu Tz Imani ya uchawi ni jambo linalochukuliwa kama ni jambo BAYA sana………… uchawi unadhana kwamba mtu anatumia miujiza KUMDHURU mwingine
Sasa kumtafuta mtu “mchawi” akathibitisha huwa anawaroga kuwadhuru wengine inakua mtihani kidogo(labda wale wa mchongo kwa Manabii na mitume)
Kwahiyo utakuta burden of proof inaangukia kwa watu wanaodai wamerogwa………… hapa ndio pana viroja
Kama uchawi upo basi ni lazima iwe rahisi sana kuuthibitisha upo………….. lakini kwa bahati mbaya sana wasio “wachawi” ndio watu wa kwanza kutetea uchawi upo kwa kuweka ugumu kwamba uchawi hauthibitiki kirahisi kwa masharti yake as if wao ndio wachawi na wanajua kanuni zake
Kwahiyo kuthibitisha tu inawezekana ila utake uthibitisho wenye vigezo vya kisayansi.