Hayo uliyoeleza hapo kuhusu imani si kila imani inaamini hayo, wakati wewe ulipokuwa unaamini hivyo kuna waumini wengine walikuwa wanakuona mjinga kwa hivyo ulivyokuwa ukiamini. Binaadamu ni kiumbe cha hisia na imani na hakuna asiyetumia logic ni sehemu ya ubongo wa mwanadamu.
Watu hutofautiana tu tunayoamini, hutofautiana logic zetu na tunapozitumia. Kwahiyo wewe kuacha kuamini Mungu,dini na uchawi sio kwamba ndio kipimo cha logic kwamba ukitumia logic lazima utafikia hitimisho la kuacha kuamini hivyo vitu, kuna watu wanatumia logic na hufikia hitimisho tofauti na hivyo.
"Kukosekana kwa uthibitisho sio uthibitisho wa kutokuwepo"
Shida ni kwamba mnafanya ushahidi na ukweli kuwa kitu kimoja ilhali hivyo ni vitu viwili tofauti, ushahidi unaweza ukawa hakuna kwa sababu kwa sasa bado haujapatikana au ni ngumu kupatikana huo ushahidi kutokana na aina ya huo ushahidi wenyewe, ila hiyo haiathiri ukweli bado ukweli utabaki kama ulivyo.
Ni kosa la kimantiki kutumia kukosekana kwa ushahidi kufanya kuwa ni ushahidi wa kutokuwepo, kwahiyo sisemi ukubali kitu bila ushahidi ila tusifanye kukosekana ushahidi kuwa ni ushahidi.