Je, ni uchawi au saikolojia?

Je, ni uchawi au saikolojia?

Wallah nahisi ni chai kaka 😅
Mpaka nione kwa macho yaani
Sasa hivi maendeleo ya vitu, watu kustaarabika na mabadiliko ya kizazi hayo mambo ni ngumu kuyaona au kuyashuhudia. Lakini hizi mambo zimebakia kuwa history tu.
 
Lakini hiyo story ya Bibi kujigeuza fisi sio Chai ni kweli kabisa .😃😃😃
 
Sasa hivi maendeleo ya vitu, watu kustaarabika na mabadiliko ya kizazi hayo mambo ni ngumu kuyaona au kuyashuhudia. Lakini hizi mambo zimebakia kuwa history tu.
Sitakiii kuamini kaka😌
 
Hello jamii intelligence 👋

Wakuu hii habari ya uchawi nadhani sio jambo geni
Uchawi ulitajwa kwenye vitabu vya dini hasa hivi maarufu Bible&Qur'an

Kwa bible mfano Kutoka 22:18 inasema:

Usimwache mchawi kuishi
Huu ni ushahidi kua Bible inatambua uchawi



Uchawi umetajwa pia kwenye Qur’an, hasa Al-Baqarah 2:102 ambapo inazungumzia habari ya uchawi na watu kujifunza mambo hayo
Huu nao ni ushahidi Qur'an inatambua habari za uchawi

kwa mantiki hii dhana ya uchawi ni ya kale sana

Huku Africa watu bado wamekumbatia hii imani sana, sijui huko Ulaya ikoje

Utasikia mtu anasema
👇
Mtoto huyu karogwa, sio akili zake.

Hapa tunaona uchawi unatajwa kama kitu ambacho kinaweza kubadilisha hali ya mtu
Alikuwa mzima, ghafla akawa kichaa au mtu asie sawa kama alivyokua kabla

Mtu anaumwa, unaambiwa karogwa

Sasa najiuliza...

Uchawi umetengenezwa au umeundwa kwa kufanya vitu negative tu?

Hakuna namna huo uchawi kama upo unaweza kutumika kwa njia positive?

Yaani tukaamua kutumia akili ya mtu kilaza akawa genius, kama vile inavyoaminika kwamba uchawi unaweza kumbadilisha genius kuwa kilaza?

Kuna hii pia👇

Ooh, wachawi wanapaa usiku...

Kwanini sasa kama hiyo technology ipo tusiitumie kupunguza foleni?

Huo usafiri wa kupaa uwe official sasa

Nyie wachawi wa JF(jokes)
haiwezekani kuwa hivi yaani huu uchawi ukawa na tija?

Hivi uchawi unafanya kazi kweli au ni mambo ya nadharia tu?

Niliwahi kua na matatizo ya kupata maumivu ya kicwa nakizunguzungu

Basi kuna mtu akamwambia mama:

Huyu ShesRise_1 amelogwa asifanye vizuri shuleni na si haba shuleni nilikua najitahidi kwahiyo huyo mama akamuambia mama angu huenda nimelogwa ili nirudi nyuma kimasomo🤔

Heh! 🤔

Nikastuka

Nikawaza, haya yatakuwa mambo gani?

Basi nikaanza kufanyiwa zile zinazoitwa tiba za Kisunna, visomo na mambo mengine

Ajabu ni kwamba kuanzia pale ndiyo kwanza nikaanza kupata maruerue.

Usiku naogopa kulala mwenyewe.

Naota ndoto za ajabu, heh... tafrani mtindo mmoja

Kumbe ile issue ya kuanza kuota mauza uza ni kwa sababu
ya saikolojia bana
Yaani saikolojia kwa maana baada ya kusikia nimelogwa na kupelekwa kwenye visomo

Ndiyo ubongo ukaanza kuniundia mapicha picha

So nilivyoambiwa tu vile, akili yangu na ubongo wangu vikaanza kujishughulisha na hayo mambo

Mara nione hiki...

Mara nisikie kile...

Mara nianze kujiuliza, Hivi huu ni uchawi gani?

Asieee!

Nikakaa nikasema:

Hapana, hizi mbona kama fix?

Na mimi by nature nina kaubishi fulani sipendi kumezeshwa mambo japo mwanzo wali ni win

Nikaacha kabisa huo upuuzi

Nikaamua ku-clean akili yangu

Kuanzia hapo nikiambiwa

Njoo kwenye visomo

Nawaambia

Mimi sina tatizo lolote

Na kweli, nilifanya vipimo hospitali nikambiwa kicwa kilikuwa kinauma kwa sababu sikuwa na damu ya kutosha, na ndiyo maana nilikuwa naumwa kicwa na kizunguzungu

Na hata sijui ilikuaje na mama akaingia kwenye mtego wa rafiki yake akaacha kunipeleka hospital kwanza akaanzia kwenye imani huku

Nikatumia zangu dawa nikawa fresh

Sijaumwa tena kicwa, labda cha mafua tu

Sioni mauza mauza wala nini

Naishi vizuri kabisa

Ndipo nikaja kugundua kumbe mambo mengine ni saikolojia tu

Wala hakuna cha uchawi wala nini

Na kuna hii pia ya majini kutaja uchawi bila majini sio sawa ni mtu na shoga yake

Sasa imagine eti mtu anapandisha mashetani anataka dhahabu...

Heh! Dhahabu sasa inatoka wapi yani?

Mashetani wana migodi yao huko?

Nimetoa mtazamo wangu kuhusu hii dhana ya uchawi

Je, uchawi ni nguvu halisi?

Au wakati mwingine tunaita kitu uchawi kumbe kuna sababu za kiafya, kisaikolojia au mazingira ambazo hatujazijua?

Na kama kweli uchawi una uwezo wa kumbadilisha mtu kutoka kuwa genius mpaka kilaza...

Kwanini usitumike kinyume chake?

Au kama wachawi wanaweza kupaa...

Kwanini bado tunakaa kwenye foleni?

Kama hii dhana ya uchawi haina tija kwanini tuna ing'ang'ania?

ShesRise_1 ✋️

Ulichokieleza kuhusu maumivu ya kichwa na sababu za kiafya ni sawa: si kila tatizo ni uchawi, na ni muhimu kutafuta sababu za kiafya kwanza. Lakini Biblia na Qur’an hazisemi kwamba kwa sababu baadhi ya mambo yanaelezeka kisayansi au kisaikolojia, basi uchawi haupo kabisa.

Biblia:

Kutoka 22:18 inasema: “Usimwache mchawi kuishi.”
Hii yenyewe inaonyesha Biblia haikuchukulia uchawi kuwa hadithi tupu.

Pia Matendo 8:9-11 inamtaja mtu aliyeitwa Simoni ambaye alikuwa akifanya uchawi na kuwashangaza watu. Na Matendo 16:16-18 inasimulia msichana aliyekuwa na “pepo wa uaguzi” na watu walipata faida kupitia utabiri wake.

Qur’an:
Al-Baqarah 2:102 inasema kuhusu watu waliofundishwa uchawi na hata inaeleza kwamba uchawi huo unaweza kutumika kuleta madhara, kama kutenganisha mtu na mwenzi wake. Qur’an pia inasema:

Al-Falaq 113:4: “Na kutokana na shari ya wanaopuliza mafundoni.”

Kwa hiyo Qur’an haikanushi kuwepo kwa uchawi; inatuonya dhidi ya shari yake.

Lakini kuna jambo muhimu: Biblia na Qur’an hazifundishi kwamba kila ugonjwa, kila kushindwa shuleni, kila ndoto au kila tatizo ni uchawi. Huwezi kuchukua mfano wa mtu aliyegundulika ana upungufu wa damu, kisha ukatumia huo kuthibitisha kwamba uchawi wote haupo. Huo ni kama kusema, “Baadhi ya watu hudhaniwa wamepagawa lakini kumbe wana ugonjwa, kwa hiyo mapepo hayapo.” Hiyo haifuati.

Na swali lako la: “Kama uchawi upo, kwa nini usitumike kufanya genius awe genius zaidi au kupunguza foleni kwa kupaa?” — hilo ni dhana yako kuhusu uchawi, si mafundisho ya Biblia wala Qur’an. Vitabu hivyo havisemi kwamba uchawi ni teknolojia yenye matumizi yoyote tunayoyataka. Vinauhusisha na mambo ya siri, udanganyifu na madhara.

Hata Biblia inatofautisha uchawi na miujiza ya Mungu. Kwa mfano, Kutoka 7:11-12 inataja waganga/wachawi wa Misri waliweza kufanya mambo yao, lakini nguvu zao hazikuwa sawa na uwezo wa Mungu.

Kwa hiyo hoja sahihi si: “Kwa nini mchawi hapandishi watu angani?”
Hoja sahihi ni: Biblia na Qur’an zote zinatambua uchawi kama jambo lililokuwepo, lakini zinakataza kuufuata na kuutumia. Na pia si sahihi kuita kila tatizo la kiafya au kisaikolojia “uchawi.”
 
Ulichokieleza kuhusu maumivu ya kichwa na sababu za kiafya ni sawa: si kila tatizo ni uchawi, na ni muhimu kutafuta sababu za kiafya kwanza. Lakini Biblia na Qur’an hazisemi kwamba kwa sababu baadhi ya mambo yanaelezeka kisayansi au kisaikolojia, basi uchawi haupo kabisa.

Biblia:

Kutoka 22:18 inasema: “Usimwache mchawi kuishi.”
Hii yenyewe inaonyesha Biblia haikuchukulia uchawi kuwa hadithi tupu.

Pia Matendo 8:9-11 inamtaja mtu aliyeitwa Simoni ambaye alikuwa akifanya uchawi na kuwashangaza watu. Na Matendo 16:16-18 inasimulia msichana aliyekuwa na “pepo wa uaguzi” na watu walipata faida kupitia utabiri wake.

Qur’an:
Al-Baqarah 2:102 inasema kuhusu watu waliofundishwa uchawi na hata inaeleza kwamba uchawi huo unaweza kutumika kuleta madhara, kama kutenganisha mtu na mwenzi wake. Qur’an pia inasema:

Al-Falaq 113:4: “Na kutokana na shari ya wanaopuliza mafundoni.”

Kwa hiyo Qur’an haikanushi kuwepo kwa uchawi; inatuonya dhidi ya shari yake.

Lakini kuna jambo muhimu: Biblia na Qur’an hazifundishi kwamba kila ugonjwa, kila kushindwa shuleni, kila ndoto au kila tatizo ni uchawi. Huwezi kuchukua mfano wa mtu aliyegundulika ana upungufu wa damu, kisha ukatumia huo kuthibitisha kwamba uchawi wote haupo. Huo ni kama kusema, “Baadhi ya watu hudhaniwa wamepagawa lakini kumbe wana ugonjwa, kwa hiyo mapepo hayapo.” Hiyo haifuati.

Na swali lako la: “Kama uchawi upo, kwa nini usitumike kufanya genius awe genius zaidi au kupunguza foleni kwa kupaa?” — hilo ni dhana yako kuhusu uchawi, si mafundisho ya Biblia wala Qur’an. Vitabu hivyo havisemi kwamba uchawi ni teknolojia yenye matumizi yoyote tunayoyataka. Vinauhusisha na mambo ya siri, udanganyifu na madhara.

Hata Biblia inatofautisha uchawi na miujiza ya Mungu. Kwa mfano, Kutoka 7:11-12 inataja waganga/wachawi wa Misri waliweza kufanya mambo yao, lakini nguvu zao hazikuwa sawa na uwezo wa Mungu.

Kwa hiyo hoja sahihi si: “Kwa nini mchawi hapandishi watu angani?”
Hoja sahihi ni: Biblia na Qur’an zote zinatambua uchawi kama jambo lililokuwepo, lakini zinakataza kuufuata na kuutumia. Na pia si sahihi kuita kila tatizo la kiafya au kisaikolojia “uchawi.”
Nani alianzisha uchawi ?
Alikusudia nini?
Tuanzie hapa ili twende taratibu
 
Ila katika kitu chenye kunishangazaga humu kuhusu watu wenye kudai hakuna uchawi ni kwamba ukijadiliana nao humu unaweza kusema hawa jamaa wote hawaishi africa, yani kana kwamba toka utoto wao hadi utuuzima hawana experience yoyote na matokeo yenye kuhusu na uchawi katika maisha yao hivyo ni kama unajadiliana na watu waliyozaliwa na kukulia nchi za ulaya huko ambako uchawi kwa kiasi kikubwa ni kama masimulizi tu.
 
Ila katika kitu chenye kunishangazaga humu kuhusu watu wenye kudai hakuna uchawi ni kwamba ukijadiliana nao humu unaweza kusema hawa jamaa wote hawaishi africa, yani kana kwamba toka utoto wao hadi utuuzima hawana experience yoyote na matokeo yenye kuhusu na uchawi katika maisha yao hivyo ni kama unajadiliana na watu waliyozaliwa na kukulia nchi za ulaya huko ambako uchawi kwa kiasi kikubwa ni kama masimulizi tu.
Nimezaliwa Africa na nimekulia hapa pia sijawahi kuona mama yangu akitupeleka kwa waganga zaidi ya hicho kipindi alivyoambiwa na rafiki yake na alinipeleka kwa sheikh tu sijawahi kuona tukiogeshwa madawa wala kuchanjwa sijawahi kuona athari yoyote kuhusu uchawi achilia mbali faida
 
Nimezaliwa Africa na nimekulia hapa pia sijawahi kuona mama yangu akitupeleka kwa waganga zaidi ya hicho kipindi alivyoambiwa na rafiki yake na alinipeleka kwa sheikh tu sijawahi kuona tukiogeshwa madawa wala kuchanjwa sijawahi kuona athari yoyote kuhusu uchawi achilia mbali faida
Wala sijazungumzia faida,hasara wala ukweli na uongo hapo mkuu. Ulaya tunajua kule idadi ya watu kuamini uchawi ndogo na hiyo hupelekea kutokuwa na matukio yenye kuhusishwa na uchawi ama watu kujihusisha na matendo yenye kuaminika ni uchawi.

Sasa humu watu wenye kueleza experience zao kwenye mambo yenye kuhusishwa na uchawi ni watu wenye kuamini uchawi tu ila wenye kudai hakuna uchawi wao hawajawahi hata kushuhudia hayo matukio yenye kuhusishwa na uchawi yani hawajawahi hata kusikia tu matukio hayo hata kwa ndugu ama rafiki zao.

Na hapo ndipo panapo nishangaza, najiuliza wote tunaishi afrika hii hii ama?
 
Wala sijazungumzia faida,hasara wala ukweli na uongo hapo mkuu. Ulaya tunajua kule idadi ya watu kuamini uchawi ndogo na hiyo hupelekea kutokuwa na matukio yenye kuhusishwa na uchawi ama watu kujihusisha na matendo yenye kuaminika ni uchawi.

Sasa humu watu wenye kueleza experience zao kwenye mambo yenye kuhusishwa na uchawi ni watu wenye kuamini uchawi tu ila wenye kudai hakuna uchawi wao hawajawahi hata kushuhudia hayo matukio yenye kuhusishwa na uchawi yani hawajawahi hata kusikia tu matukio hayo hata kwa ndugu ama rafiki zao.

Na hapo ndipo panapo nishangaza, najiuliza wote tunaishi afrika hii hii ama?
Tupo hapa hapa mkuu
 
Back
Top Bottom