Je, ni uchawi au saikolojia?

Je, ni uchawi au saikolojia?

Mola ameweka kila kitu

mola ameweka kila kitu kwa dalili na ushahidi mfano amesema miongoni mwa alama zangu ama uwepo wangu ni kuwepo kwa jua na mwezi usiku na mchana uwepo wa siku ya mwisho nikushauri dada yangu soma dini vizuri
Mola ameweka kila kitu

mola ameweka kila kitu kwa dalili na ushahidi mfano amesema miongoni mwa alama zangu ama uwepo wangu ni kuwepo kwa jua na mwezi usiku na mchana uwepo wa siku ya mwisho nikushauri dada yangu soma dini vizuri
Dini ipi nisome kaka?
 
Wewe unadhani sipendi kujielimisha?
Nasoma Bible na Qur’an
Hata hivyo vifungu sijavichukua kwa AI nimesoma hivyo vitabu viwili
Baada ya hapo nimefikia kuamini hivyo ninavyo amini

Issue za uchawi na majini
Nimeshuhudia watu wakisema wanapandisha majini
Nimeshuhudia watu wakilishwa chano nk.....
Sasa mbona hauelezi kwa kina ni vp ulifikia hilo hitimisho la kuamini hivyo unavyoamini baada kushuhudia na kujielimisha hayo mambo?

Ndio maana nikauliza hapo kwa mtu ambaye yeye mwenyewe ndio anafanya huo uchawi je huyu nae saikolojia inakaaje kwa upande wake? Maana mtu huyu baada ya kufanya aliyoyafanya anategemea kuona matokeo ya kile alichokifanya.
 
Wewe unadhani sipendi kujielimisha?
Nasoma Bible na Qur’an
Hata hivyo vifungu sijavichukua kwa AI nimesoma hivyo vitabu viwili
Baada ya hapo nimefikia kuamini hivyo ninavyo amini

Issue za uchawi na majini
Nimeshuhudia watu wakisema wanapandisha majini
Nimeshuhudia watu wakilishwa chano nk.....
Tupe uzowefu wako kwenye suala la watu kupandisha majini, umeshuhudia wakipandisha kwa hiari yao au yanapanda tu bila hiari yao? Na ni mazingira gani ya kawaida au kwa mganga?
 
Sasa mbona hauelezi kwa kina ni vp ulifikia hilo hitimisho la kuamini hivyo unavyoamini baada kushuhudia na kujielimisha hayo mambo?
Kaka hii ni mada nyingine
Niliweka kisa kifupi kama kuweka mfano ila yapo mambo mengine mengi
Ndio maana nikauliza hapo kwa mtu ambaye yeye mwenyewe ndio anafanya huo uchawi je huyu nae saikolojia inakaaje kwa upande wake? Maana mtu huyu baada ya kufanya aliyoyafanya anategemea kuona matokeo ya kile alichokifanya.
Hapa mwenye kufanya huo uchawi ndiyo mwenye majibu na si mimi
 
Tupe uzowefu wako kwenye suala la watu kupandisha majini, umeshuhudia wakipandisha kwa hiari yao au yanapanda tu bila hiari yao? Na ni mazingira gani ya kawaida au kwa mganga?
Sio kwa watu wengine mimi mwenyewe niliwahi kuambiwa nina majini 😂😂
Nikaambiwa yatapandishwa
But ni story ndefu tutaindikia uzi makhususi na nita ku tag bro
 
Kaka hii ni mada nyingine nimeweka kisa kifupi kama kuweka mfano ila yapo mambo mengine mengi
Hapa mwenye kufanya huo uchawi ndiyo mwenye majibu na si mimi
Lakini wewe si ndio mwenye kusema uchawi ni saikolojia na umefikia kusema hivyo baada kushuhudia na kujielimisha mambo kama hayo?
 
Lakini wewe si ndio mwenye kusema uchawi ni saikolojia na umefikia kusema hivyo baada kushuhudia na kujielimisha mambo kama hayo?
Sijui kwanini hunielewi bro
Sijui hutaki tu kunielewa au sieleweki kwako
 
Ahaa sawa
So kua na imani ni vibaya?
Sijamaanisha kwamba IMANI ni nzuri au ni mbaya…….. nimejaribu kufafanua Imani ni NINI.
Lakini mwanzoni ulisema unaamini kwanza sio?
Then baadae ndiyo ukathibitisha ukasema nyoka yupo baada ya kumuona right?

Niambie kuhusu neno (Imani) kama hutojali bro
Yes, Mwanzo ulikua HUJUI kama Nyoka yupo au hayupo……….. utakapo JUA yupo then IMANI inakwisha inabaki FACT kwamba nyoka yupo na sio ninaamini nyoka yupo.

IMANI ni kukubali jambo bila UTHIBITISHO
IMANI ni jambo ambalo HALIPO au HALINA UHAKIKA kama lipo ila wewe una train ubongo wako kukubali kwa dhati kwamba lipo
 
Sijamaanisha kwamba IMANI ni nzuri au ni mbaya…….. nimejaribu kufafanua Imani ni NINI.
Ahaa sawa
Yes, Mwanzo ulikua HUJUI kama Nyoka yupo au hayupo……….. utakapo JUA yupo then IMANI inakwisha inabaki FACT kwamba nyoka yupo na sio ninaamini nyoka yupo.

IMANI ni kukubali jambo bila UTHIBITISHO
IMANI ni jambo ambalo HALIPO au HALINA UHAKIKA kama lipo ila wewe una train ubongo wako kukubali kwa dhati kwamba lipo
Kwa maana hii usipoamini uchawi huwezi kuuona ukifanya kazi?
 
Ahaa sawa
Kwa maana hii usipoamini uchawi huwezi kuuona ukifanya kazi?
Mkuu kinacho tatiza kwenye Imani ya UCHAWI ni UTHIBITISHO kwamba uchawi ndio umefanya kazi kwa sababu hiyo inayo aminiwa imefanyika huwa ndio matokeo ya kawaida kutokea

Labda uwe specific jambo gani wewe umethibitisha ni matokeo ya uchawi
 
Mkuu kinacho tatiza kwenye Imani ya UCHAWI ni UTHIBITISHO kwamba uchawi ndio umefanya kazi kwa sababu hiyo inayo aminiwa imefanyika huwa ndio matokeo ya kawaida kutokea

Labda uwe specific jambo gani wewe umethibitisha ni matokeo ya uchawi
Mimi sikubaliani na hii dhana ya uchawi
Sasa hapo nathibisha je sasa bro?
Wa ku thibitisha ni wale wanaoamini uchawi
 
Sijamaanisha kwamba IMANI ni nzuri au ni mbaya…….. nimejaribu kufafanua Imani ni NINI.

Yes, Mwanzo ulikua HUJUI kama Nyoka yupo au hayupo……….. utakapo JUA yupo then IMANI inakwisha inabaki FACT kwamba nyoka yupo na sio ninaamini nyoka yupo.

IMANI ni kukubali jambo bila UTHIBITISHO
IMANI ni jambo ambalo HALIPO au HALINA UHAKIKA kama lipo ila wewe una train ubongo wako kukubali kwa dhati kwamba lipo
Kipi sasa kinachofanya mtu achague cha kuamini na kipi akatae kuamini?
 
Mkuu kinacho tatiza kwenye Imani ya UCHAWI ni UTHIBITISHO kwamba uchawi ndio umefanya kazi kwa sababu hiyo inayo aminiwa imefanyika huwa ndio matokeo ya kawaida kutokea

Labda uwe specific jambo gani wewe umethibitisha ni matokeo ya uchawi
Nadhani kama anaweza kukusudia apate matokeo fulani endapo akufanya hiko anachosema ni uchawi na kweli baada ya kufanya yakapatikana hayo matokeo, je hilo halitoshi kuthibitisha?
 
Kipi sasa kinachofanya mtu achague cha kuamini na kipi akatae kuamini?
Sio jambo moja mkuu.

Mara nyingi sana IMANI yoyote ile ni MATOKEO ya kihistoria, Kijiografia, mila/tamaduni, makuzi/malezi na uelewa binafsi wa mtu…………. Hivi kwa sehemu kubwa ndio vina mtengeneza mtu aamini nini.

Tunacho amini kuhusu mambo ya Uchawi Tanzania kuna utofauti na Wachina wanavyo amini kuhusu uchawi na hata kwenye mambo mengi ya KIIMANI kuna tofauti pia

Kwa mfano Kijiongrafia/malezi/mila/tamaduni mtoto aliyezaliwa viunga vya Nazaret pale Israel na wazazi waisrael kwa 90+% ATAAMINI katika Uyahudi same applied kwa mtoto atakayezaliwa Pyong Yang China na wazazi mabudha au Mtoto atakayezaliwa na Chabaa pale Udzabeni Arusha, au atakaye zaliwa Teheran na wazazi washia pale Iran, au atakaye zaliwa Kashmir India na wazazi Wahindu………….. hata watoto wako binafsi kwa kiasi kikubwa Imani yao ya dini itatokana na wewe mlezi wao

So imani INATENGENEZWA na mfumo tajwa
 
Nadhani kama anaweza kukusudia apate matokeo fulani endapo akufanya hiko anachosema ni uchawi na kweli baada ya kufanya yakapatikana hayo matokeo, je hilo halitoshi kuthibitisha?
Ungekua specific ni jambo gani hilo la kichawi limetoa hayo matokeo tungejadili vizuri

Kwa hapa kwetu Tz Imani ya uchawi ni jambo linalochukuliwa kama ni jambo BAYA sana………… uchawi unadhana kwamba mtu anatumia miujiza KUMDHURU mwingine

Sasa kumtafuta mtu “mchawi” akathibitisha huwa anawaroga kuwadhuru wengine inakua mtihani kidogo(labda wale wa mchongo kwa Manabii na mitume)

Kwahiyo utakuta burden of proof inaangukia kwa watu wanaodai wamerogwa………… hapa ndio pana viroja

Kama uchawi upo basi ni lazima iwe rahisi sana kuuthibitisha upo………….. lakini kwa bahati mbaya sana wasio “wachawi” ndio watu wa kwanza kutetea uchawi upo kwa kuweka ugumu kwamba uchawi hauthibitiki kirahisi kwa masharti yake as if wao ndio wachawi na wanajua kanuni zake
 
Back
Top Bottom