Je, Kinachomponza Mbowe ni Anasa?

Je, Kinachomponza Mbowe ni Anasa?

Status
Not open for further replies.
Siwezi kusema mengi wenzetu mko home ground( JF) SIE tumeshapewa onyo na baba mwenye nyumba.ama kweli refa ana wabeba sana na bado tunawagalagaza.

vilio tu nani hakuwezi wewe na mental confusion zako hapa?

umegalagazwa jana kwenye udaku wako wa jana, leo umeleta hii pia umechemsha unaishia kulia lia kama mtoto!

kijiwe cha wakubwa hiki na ukishindwa unaenda darhotwire!
 
walipenda sana kuuliza pesa za EPA kurudishwa, sasa tuone JE ATAWEZA NA YEYE ?? Chadema fanatics pitisheni michango hapa mumsaidie mbowe kulipa deni ! opps, mabilioni ?? no we cant afford !
KADA
taratibu nimepewa tayari red card na na refa, hujui wenzetu wako HOME GROUND (JF) SIE TUKO AWAY.kubebwa na refa bado wanalia na moto wetu.
 
Heshima Zenu Wakuu !

Baada ya kuzipitia hizi exchange za hoja kuhusu Bwana Mbowe, Naanza kuogopa kuwa ile dhana kwamba JF ni FAIR & BALANCED kumbe ni MYTHICAL.

Hoja hii tulitakiwa tupate Evidence ili tuwe more objective, Lakini baadal yake Tunashuhudia jinsi UKADA wa CHADEMA kwa nguvu zote.

Kumbe huu ufisadi ni kosa to those in CCM kwa Kina CHADEMA ni ACCEPTABLE.

I beg to differ!!!

Unless we are prepared to be neautral when it comes to issues of national interest, the JF is simply a mouth piece of CHADEMA>

T U S I D A N G A N Y A N E. ITS a PITY.

ABSOLUTELY !!
 
hoja za chinga ktk hii jf zinanichefua sana na kama kuna namna yoyote ya kum delete ktk jf naomba wahusika wafanye hivyo haraka maana naweza hata kuibamiza hii lap top yangu chini kwa hasira,mwanaume mzima huwezi ukafikiri wenzako wanajadili nini halafu ukachangia cha maana!!!kudaadako
 
So far chinga na wenzake wamekosa uthibitisho kama walivyokosa uthibitisho jana kwenye ule udaku dhidi ya Mbowe!

Meanwhile, Nasubiria hii case mahakamani itolewe uamuzi au la sivyo tume huru ya bunge iundwe kuchunguza wote waliokopa kihalali na kiharamu (kikwete na mkullo) kutoka NSSF.

Thanks!
 
Kwa hiyo kilichoshindikana nini?

Kumfilisi mbowe au Mahakama kushindwa kutoa hukumu ya kumfilisi?

Watu wangapi wamefilisiwa mali zao Bongo?

Sasa huyu Mbowe anawashinda nini wakati hana pa kuegemea serikalini?

Serikali ina vyombo vya dola vya kuzuia maandamano tu?

Labda mahakama nazo siku hizi zimepungukiwa umaarufu!

Mtikila lishinda kesi ya mgombea binafsi hukumu hiyo haijatekelezwa mpka leo. Mbowe naye huku yake ilitolewa lakini haitekelezeki mpka serikali ije ilalamike huku kwetu walala hoi.

Serikali ime mbonji????

Huyu Mbowe ni mfanya biashara na ujanja wote wa biashara anaujua, kila alipoona mambo yamemkalia vibaya alikuwa anaomba wafanye majadiliano out of court and I dont know why NSSF were falling for it na hii ilizidi kumpa muda.

Nukuu..
NSSF iliamua kufungua kesi Mahakama Kuu. Kesi hiyo ya madai No. 277 ya mwaka 1996, ilikuwa ikidai Mkopaji alipe deni la msingi sh milioni 12 zilizokuwa zimesalia pamoja na riba.
Hatua hii iliwafanya wakurugenzi wa Mbowe Hotel kuomba suala hilo walimalize nje ya Mahakama. Hata hivyo, hawakuendelea kulipa hadi mwaka 1998, walipopewa tishio la kufungwa jela ndipo waliamua kulipa kwa mkupuo sh milioni 12.


Baada ya hapo wakaingia mitini tena hadi hili lilipotokea tena....

Nukuu...
Hata hivyo, kutokana na Mbowe kuona mambo yanaendelea kuchacha, Desemba 14, mwaka 2006, mmoja wa wakurugenzi wa Mbowe Hotel, Dk. Lilian Mtei Mbowe, aliamua kutoa malipo ya wastani wa sh milioni 50 kwa NSSF kwa hundi mba 298492, iliyoambatana na barua yenye Kumb. No. BGI/NSSF/MHL06/01, huku akitaka warejee kwenye meza ya majadiliano badala ya kufungwa jela.

SABABU ZA KUTOLIPA
-Anasema katika moja ya vielelezo kuwa fedha zilipotolewa na NSSF mwaka 1990, nchini Tanzania hakukuwapo vifaa vya ujenzi!
-Mbowe Hotel walilazimika kuagiza vifaa vya ujenzi kutoka nje ya
nchi, na lilijitokeza tatizo lingine kwamba benki nchini
hazikuwa na fedha za kigeni, hivyo Mbowe Hotel ililazimika
kusubiri kwa muda mrefu kupatiwa fedha hizo za kigeni.


Huhitaji kuwa msanii kujua kwamba huu ni usanii
 
hoja za chinga ktk hii jf zinanichefua sana na kama kuna namna yoyote ya kum delete ktk jf naomba wahusika wafanye hivyo haraka maana naweza hata kuibamiza hii lap top yangu chini kwa hasira,mwanaume mzima huwezi ukafikiri wenzako wanajadili nini halafu ukachangia cha maana!!!kudaadako

ziko nyingi sana kama unachefuka labda mjamzito tumia udongo.
ulipitia ile ya TRA na uchagga nimeweka hapo juu ipitie vizuri na ile ya mbowe kushindana na marehemu.
nakutea nyingie soon.
 
IF
IF
IF
IF

Mbowe doesnt come clean on this one ! let me repeat !
IF
IF
IF
IF
Mbowe doesnt come clean on this one,or doesnt publicly speak about it plus you put the other scandal he has on the way coming, NO MORE POLITICAL CAREER ! Trust me !!
 
sisi wana jf lengo letu ni kupambana na ufisadi wa namna yoyote ile lakini nakushangaa chinga unawatetea sijui wanakulipa ngapi.punguza njaa hiyo itakuua
 
IF
IF
IF
IF

Mbowe doesnt come clean on this one ! let me repeat !
IF
IF
IF
IF
Mbowe doesnt come clean on this one,or doesnt publicly speak about it plus you put the other scandal he has on the way coming, NO MORE POLITICAL CAREER ! Trust me !!

Tukia akili na busara yako kuchanganua mambo hili sio swala zito sana kama unavyodhani
Mbona Kikwete hanayo mascandal kibao na hamsemi lolote
Kuna Fisadi Mwizi na muhuaji kama Kikwete
Kama anaweza kukubali mahospitali yetu yakae bila madawa akiwashikilia nyie Mafisadi, huku sindo kuwauwa wa TZ sasa
 
sisi wana jf lengo letu ni kupambana na ufisadi wa namna yoyote ile lakini nakushangaa chinga unawatetea sijui wanakulipa ngapi.punguza njaa hiyo itakuua
NA VOLUNTEER TU KAMA WEWE.

MADELA WA MADILU,MWANAKIJIJI AU UKIINGIA NA MWAFRIKA WA KIKE.

HAYA NI MANENO YA CHACHA WANGWE KUWA CHADEMA NI CHAMA CHA WACHAGGA NA MBOWE ANAWEKA VIMADA WAKE KWENYE VITU MAALUM.
PITIA VIZURI KAMA UNA MAKENGEZA UTASAIDIWA MIWANI.

http://www.dailynews-tsn.com/habarileo/page.php?id=6170
 
Tukia akili na busara yako kuchanganua mambo hili sio swala zito sana kama unavyodhani
Mbona Kikwete hanayo mascandal kibao na hamsemi lolote
Kuna Fisadi Mwizi na muhuaji kama Kikwete
Kama anaweza kukubali mahospitali yetu yakae bila madawa akiwashikilia nyie Mafisadi, huku sindo kuwauwa wa TZ sasa

trust me ! someone's career is on the blink of .................. !
 
sisi wana jf lengo letu ni kupambana na ufisadi wa namna yoyote ile lakini nakushangaa chinga unawatetea sijui wanakulipa ngapi.punguza njaa hiyo itakuua
Ufisadi ni mpana sana, sio lazima uwe chama tawala ili uwe fisadi. Unaweza kuwa chama cha upinzani, unaweza kuwa mfanyabiashara, unaweza kuwa mfanyakazi katika asasi,na bado ukawa fisadi vilevile...
 
Yani kumbe tuna safari ndefu ya ukombozi wa kweli. Kama kweli hili la Mbowe kukopa hela NSSF nalo watu wanataka kuita ufisadi basi kazi ipo.Hebu nyie mnaomkomalia mbowe nitajieni mfanyabiashara yeyote wa TZ au yeyote unaemjua ambae hadaiwi na institute ya hela nchini kwake au nje ya nchi.Hii ni biashara.Mabenki yako kwa ajili ya biashara na yanategemea wakopaji.Kuna mabenki sasa yanaanzishwa hapo TZ ya mortgage na yanalilia kupata wakopaji.Kama mkopaji ameshindwa ama yuko kwenye mchakato wa kulipa hilo ni suala lingine na si ufisadi.Au hatujui maana ya ufisadi??

Sasa kali ni hiyo eti mbowe anaishi maisha ya anasa,kisa eti ukienda kwake KILA HATUA MOJA MBELE,TAA ZINAWAKA UNAKOELEKEA NA KUZIMA UNAKOTOKA!!! Jamani????? yani kweli sisi ni washamba kiasi hicho??Taa kuwaka kwa ku-sense nalo ni tatizo au tuite anasa??? mwishowe mtasema chumbani kwake anazima taa za sebuleni akiwa hukohuko chumbani kwake.Kwi kwi kwi.Tuache ushamba
 
usinikumbushe habari ya madawa hospitalini maana inanitia uchungu kwani kuna mtanzania gani asiyejua kuwa kwa mzalendo kuagiza dawa nje ya nchi haiwezekani kabisa maana serikali hii ya ajabu ina watu wake spesho wahindi ambao wana uwezo wa kutoa ten pasent kwa hao wapenda rushwa wazandiki, hata kama dawa zimekwisha wako tayari kushuhudia wa tz wakifa kwa kukosa dawa kuliko kuruhusu wazalendo kuingiza,kwani tumesahau yule mhindi aliyepewa tenda ya kusaply zile dawa za kifua kikuu alivyowateketeza wa tz? nani alijali?
 
MAJITA.

UFISADI MWINGINE CHADEMA.



Makala Habari nyingine zaidi!
Uchaguzi wa Makamu Mwenyekiti na jinsi ulivyoitikisa CHADEMA
Theopista Nsanzugwanko
HabariLeo; Tuesday,January 08, 2008 @00:02


Makamu Mwenyekiti wa Chadema,Chacha WANGWE.
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) ni moja ya vyama vikubwa vya siasa nchini. Kilianzishwa kwa juhudi za waasisi kadhaa wa chama hicho, ambao ni pamoja na Edwin Mtei na Bob Makani. Mkutano mkuu wake wa kwanza wa chama hicho, ulifanyika katika kituo cha Msimbazi Dar es Salaam kuanzia Desemba 15-17, 1992.

Mkutano huu ulihudhuriwa na wajumbe kutoka mikoa yote ya Tanzania na ulichagua viongozi wa kwanza wa chama hicho, majina na vyeo vyao kwenye mabano ni: Edwin Mtei (Mwenyekiti), Ali Suleiman Ahmed (Makamu Mwenyekiti upande wa Zanzibar), Brown Ngwilulupi (Makamu Mwenyekiti Bara), Bob Makani (Katibu Mkuu), Mustafa S. Simba (Naibu Katibu Mkuu Zanzibar) na Eric Mchatta (Naibu Katibu Mkuu Bara).

Tangu mwaka huo 1992, chama hicho kimeendelea kukua na kufanya uchaguzi wa viongozi wake kila inapobidi. Pia, tangu mwaka huo kimekuwa kikishiriki katika uchaguzi wa serikali za mitaa na uchaguzi mkuu wa madiwani, wabunge na Rais. Matokeo ya kura katika chaguzi hizo yamekuwa ya kuridhisha na hali ya utulivu imekuwa pia inaridhisha.

Hata hivyo, hivi karibuni chama hicho kimetikiswa sana na suala la uchaguzi wa Makamu Mwenyekiti wa Chadema upande wa Tanzania Bara. Hali hiyo ilijitokeza dhahiri katika vikao vya Kamati Kuu na Baraza Kuu vilivyofanyika Dar es Salaam, ambapo baada ya mvutano wa muda mrefu hatimaye alipatikana mshindi, ambaye ni Mbunge wa Tarime kwa tiketi ya chama hicho, Chacha Wangwe.

Wakati wa kampeni ya kugombea nafasi hiyo, madai mengi yalitolewa na baadhi ya wanachama wao, kuhusiana na chama hicho hadi ikafika mahali Katibu Mkuu wao, Dk.Wilbrod Slaa na Naibu Katibu Mkuu, Zitto Kabwe, kudaiwa kutaka kujiuzulu nyadhifa zao. Wanadaiwa walitaka kujiuzulu baada ya kuchukizwa na kitendo cha Chacha Wangwe, ambaye alikuwa mgombea wa nafasi hiyo ya Makamu Mwenyekiti, kukishutumu chama kupitia vipeperushi vilivyosambazwa nchi nzima.

Katika vipeperushi hivyo, Wangwe anadaiwa kusema kwamba chama kimegeuzwa kuwa mali ya ukoo na baadhi ya viongozi wa makao makuu. Vipeperushi hivyo vilisambazwa na wafuasi wa chama hicho, waliokuwa wakimuunga mkono Wangwe katika kinyang'anyiro hicho. Habari kutoka ndani ya kikao cha Kamati Kuu ya chama hicho, zinadai Dk Slaa ambaye ni Mbunge wa Karatu na Zitto ambaye ni mbunge wa Kigoma Kaskazini, walifikia uamuzi huo, baada ya hoja kuhusu vipeperushi hivyo kujadiliwa katika kikao hicho.

Hata hivyo, waasisi wa chama hicho, Edwin Mtei na Bob Makani walifanya kazi ya ziada kuwashawishi Dk Slaa na Zitto kubadili uamuzi wao wa kujiuzulu na kuendelea na nyadhifa zao ili kulinda chama kisigawanyike. Chanzo chetu kilichokuwa ndani ya kikao hicho cha Kamati Kuu, kilisema kuwa "Ni kweli Zitto na Slaa walitangaza kujiuzulu nyadhifa zao kutokana na vipeperushi vya Wangwe, lakini baada ya mambo kuwekwa sawa na waasisi hao wa chama, walikubali kurejea kwenye nyadhifa zao."

Kutokana na kitendo hicho, Kamati Kuu ilimuonya Wangwe na pia Kamati Kuu ilitishia kufuta uchaguzi huo. Hata hivyo, baadaye Kamati Kuu iliridhia kuwa uchaguzi huo ufanyike. Ilitoa uamuzi huo baada ya wajumbe wa kamati hiyo kupiga kura, ambapo 14 walisema ufanyike na 11 wakasema usifanyike.

Ndipo kikao hicho kilifanyika chini ya Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe ili kuandaa ajenda ambazo zingejadiliwa katika kikao cha Baraza Kuu. Nalo Baraza Kuu baada ya kujadili ajenda hizo, liliendelea na ajenda ya kumchagua mwanachama atakayejaza nafasi ya Makamu Mwenyekiti, iliyoachwa wazi na Amani Walid Kabourou, aliyejiunga na Chama Cha Mapinduzi (CCM) mwaka jana.

Lakini, pamoja na kuonywa, Wangwe aliendelea kushikilia msimamo wake ulioko kwenye vipeperushi vyake katika kikao hicho pia. Vipeperushi hivyo vinawatuhumu baadhi ya viongozi wa Chadema kuendesha chama kwa upendeleo, hasa katika mgawo wa ruzuku. Pia, kinawatuhumu viongozi wa Chadema kwa ubaguzi wa misingi ya kidini na Kikanda. Katika vipeperushi hivyo, Wangwe anadai kuwa kutokana na kasoro hizo, atahakikisha analeta mabadiliko ya kweli ndani ya chama ili kukiepusha kuendeshwa kama shirika lisilo la kiserikali (NGO).

"Tunataka kiwe chama cha siasa chenye lengo la kuking'oa madarakani Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010," anasema Wangwe. Anasisitiza kuwa jambo kubwa linalokitia dosari CHADEMA ni ofisi za wilaya na kata kutokuwa na mawasiliano na makao makuu, hasa katika mgawo wa ruzuku na uteuzi wa wabunge wa viti maalumu.

Wangwe anadai mgawo wa ruzuku na uteuzi wa wabunge wa viti maalumu, vimekuwa vikitolewa na uongozi wa Chadema kwa kuangalia upande mmoja wa wanachama wanaotoka Kanda ya Kaskazini hapa nchini. "Chama kimekuwa mali ya koo na familia fulani. Tunataka kiwe cha wanachama," anadai Wangwe, ambaye baadaye alifanikiwa kupata nafasi hiyo ya Makamu Mwenyekiti. Alimshinda Mbunge wa Mpanda Kati kwa tiketi ya Chadema, Said Arfi.

Wafuasi wa chama hicho wanaomuunga mkono Wangwe katika kinyang'anyiro hicho, waliendelea kusambaza vipeperushi hivyo vinavyotuhumu kuwapo na upendeleo katika mgawo wa ruzuku za chama na ubaguzi wa kidini na kikanda katika chama hicho. Vipeperushi hivyo vilitawanywa makao makuu ya Chadema, mikoani, wilayani na katika eneo ambalo Kamati Kuu ilikutana na vinadai kwamba chama hicho kimekuwa kikipata ruzuku ya Sh milioni 60 kila mwezi, lakini fedha hizo zimekuwa zikiishia makao makuu huku matumizi yake hayawekwi bayana.

"Tunasema inawezekana kila mkoa ukapata Sh milioni 1.5 kila mwezi na makao makuu itabaki na zaidi ya Sh milioni 10 ambazo zinawatosha kwa shughuli za chama," inaeleza sehemu ya kipeperushi hicho. Kipeperushi kinadai kuwapo kwa "ubinafsi" katika chama, ambao umesababisha karibu wabunge wote wa viti maalumu kuteuliwa kutoka katika mkoa mmoja uliopo eneo la Kaskazini mwa nchi.

"Tumchague Chacha ili aweze kubeba majukumu hayo na kuyavalia njuga ili ruzuku igawanywe katika mikoa yote. Chacha pambana kama unavyopambana na CCM katika Jimbo lako la Tarime," kinaeleza kipeperushi hicho. Kipeperushi hicho kinawataka wajumbe wa Kamati Kuu na Baraza Kuu kutoingia kwenye mtego wa kidini, kwa madai kwamba chama hicho siyo msikiti wala kanisa.

"Ni chama cha siasa kinachotaka kuendelezwa na kiongozi jasiri kama Chacha (Wangwe). Hatusemi kwa ushabiki, angalia ukweli hapo makao makuu. Chadema ni chama chetu siyo kampuni ya watu binafsi, tubadilishe hali hii," kilieleza kipeperushi hicho. Baada ya kutolewa kwa malalamiko hayo yaliyopo katika vipeperushi, Dk.Slaa alikanusha madai yaliyotolewa na kusema kuwa pesa zote za ruzuku, hutumika kutokana na maamuzi ya vikao vya chama.

Pia, alizungumza kuhusu wabunge wa viti maalumu karibu wote kutoka upande mmoja wa Kaskazini, ambapo alisema kutokana na chama hicho kuwa na wabunge wachache, inawabidi kutafuta wenye uwezo katika kutoa hoja za msingi bungeni. “Wabunge huteuliwa kwa kuangalia utendaji wa kazi zao ambazo zinaonekana wakiwa bungeni. Kule bungeni hatupeleki sura, bali watendakazi ambao ndio jeuri ya chama chetu,” anasema.

Dk Slaa anasema shutuma zilizotolewa na Wangwe, ambaye alikuwa anagombea umakamu mwenyekiti, ni maneno tu ya kumtaka apate nafasi hiyo. Alizungumzia baadhi ya matumizi yaliyoamuliwa katika vikao vya chama, kuwa ni pamoja na kuzunguka nchi nzima kukitambulisha chama kwa Watanzania, ambazo ukiacha usafiri na gharama nyingine zimetumika zaidi ya Sh milioni 200 kutengeneza bendera, kadi na vipeperushi.

Dk. Slaa anasema matumizi kama hayo siyo kwa manufaa ya makao makuu pekee, bali kwa mikoa yote waliyotembelea, ukiacha Mtwara na Lindi, ambayo bado hawajaitembelea kwa lengo la kuwajulisha Watanzania walioko mikoani sera za chama hicho. “Hakuna chama kingine cha siasa ukiacha chama tawala kilichoweza kuzunguka mikoani na kujitambulisha kwa wananchi kama tulivyofanya sisi kwa shilingi milioni 60 kila mwaka,” anasisitiza.

Akifungua Baraza Kuu la chama hicho, Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, alidai suala la kusitishwa kwa mjadala wa Katiba ni ukiritimba. Anasema katiba inapaswa kujadiliwa wakati wowote kwa kuwa ni mali ya wananchi. Pia, alisema baada ya kutimiza miaka miwili, Rais Jakaya Kikwete inabidi afanyiwe tathmini ya uongozi wake na pia alidai kuwa wananchi wamechoka na kauli za kutia matumaini huku hali ya maisha ikizidi kuwa ngumu.

Pia, Mbowe anawataka Waziri wa Fedha, Zakia Meghji, kutoa ripoti ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT), kwani kampuni iliyopewa kazi ya kuichunguza ilipewa siku 28 tu kukamilisha uchunguzi na kutoa ripoti. Anadai kuwa siku zimeisha, lakini wananchi bado hawajapewa ripoti hiyo. Baada ya kumalizika kwa kikao hicho cha Baraza Kuu, Mbowe alikanusha kuwa kuna migogoro katika chama chake hicho.

Pia, alisema kuwa Chadema itaendelea kutumia helikopta katika awamu nyingine ya ziara zake, baada ya kutafakari gharama za ziara za helikopta. “Baraza Kuu limetafakari gharama za ziara za helikopta na kuwianisha na ziara nyingine na kuazimia kwa kauli moja kuendelea kutumia usafiri huo katika awamu nyingine ya ziara,” anasema.

Mbowe anasema maazimio mengine waliyoyafikia ni pamoja na kuweka hadharani hesabu ya mapato na matumizi, kwani kila mwanachama wa chama hicho ana uhuru wa kufahamu hilo. Alitaka wengine wanaotaka kujua hesabu hizo wafike makao makuu. Pia, Baraza Kuu liliamua kuendeleza ushirikiano wa vyama kwa lengo la kudumisha demokrasia nchini na kuunganisha nguvu katika kutetea maendeleo na hatimaye upinzani uweze kuchukua dola. Baraza hilo lilipitisha azimio la kutangaza ratiba ya uchaguzi wa chama hicho, utakaofanyika kuanzia mwezi Januari hadi Desemba.

Anasema uchaguzi huo utaanzia katika vitongoji, kata, jimbo, wilaya, mikoa na Kanda. Pia, kutakuwa na uchaguzi wa wajumbe wa Kamati Kuu, Baraza Kuu na Mkutano Mkuu wa Taifa. Katika uchaguzi wa Makamu wa Mwenyekiti upande wa Tanzania Bara, Baraza Kuu lilimchagua Chacha Wangwe kushika nafasi hiyo, baada ya kupata kura 56 kati ya 94 zilizopigwa.

Mpinzani wake Mbunge wa Mpanda Kati, Said Amour Arfi, alipata kura 38. Akitoa shukrani zake baada ya kutambulishwa rasmi kuwa Makamu, Wangwe anasema atatumia nafasi hiyo kurudisha demokrasia iliyoanza kupotea katika chama hicho. Anasema atafanya hivyo kwa kutumia vikao vya viongozi wa ngazi za juu. Wangwe anasema kutokana na chama hicho kuwa cha kidemokrasia, mambo yote yaliyotokea ni harakati za kuimarisha demokrasia, hivyo yalikuwa ni sehemu ya midahalo tu; na wala sio migogoro, kama wengi walivyodhania.
 
Yani kumbe tuna safari ndefu ya ukombozi wa kweli. Kama kweli hili la Mbowe kukopa hela NSSF nalo watu wanataka kuita ufisadi basi kazi ipo.Hebu nyie mnaomkomalia mbowe nitajieni mfanyabiashara yeyote wa TZ au yeyote unaemjua ambae hadaiwi na institute ya hela nchini kwake au nje ya nchi.Hii ni biashara.Mabenki yako kwa ajili ya biashara na yanategemea wakopaji.Kuna mabenki sasa yanaanzishwa hapo TZ ya mortgage na yanalilia kupata wakopaji.Kama mkopaji ameshindwa ama yuko kwenye mchakato wa kulipa hilo ni suala lingine na si ufisadi.Au hatujui maana ya ufisadi??

Sasa kali ni hiyo eti mbowe anaishi maisha ya anasa,kisa eti ukienda kwake KILA HATUA MOJA MBELE,TAA ZINAWAKA UNAKOELEKEA NA KUZIMA UNAKOTOKA!!! Jamani????? yani kweli sisi ni washamba kiasi hicho??Taa kuwaka kwa ku-sense nalo ni tatizo au tuite anasa??? mwishowe mtasema chumbani kwake anazima taa za sebuleni akiwa hukohuko chumbani kwake.Kwi kwi kwi.Tuache ushamba

Majita,

Kama ni kweli Mbowe alikopa NSSF na anadaiwa mpaka kupelekwa mahakamani, hiyo ni issue. Sio sawa na case nyingine ya kukopa na kulipa ambako watu wengi wanafanya kila siku.

Kukopa pesa za walalahoi na kushindwa kulipa kunaweza kuwa issue kubwa tu.

Tusipoangalia TZ tutaendelea kuongozwa na mafisadi, kuanzia huyo waziri wa fedha mpaka hao watu wake aliokuwa anawakopesha.

Kuna mtu wa kawaida gani amewahi kukopeshwa NSSF? Kwanini hawa viongozi wasiende kukopa kwenye mabank?

Sumaye alikopa na kulipa lakini bado aliandamwa kweli kweli, kwanini mnaona
Mbowe kukopa NSSF na kushindwa kulipa on time mpaka case iende mahakamani haiwezi kuwa issue?

Acheni double standards zenu. Sioni tofauti kati ya hii case na Sumaye, tena huenda Sumaye ilikuwa hata nafuu.
 
usinikumbushe habari ya madawa hospitalini maana inanitia uchungu kwani kuna mtanzania gani asiyejua kuwa kwa mzalendo kuagiza dawa nje ya nchi haiwezekani kabisa maana serikali hii ya ajabu ina watu wake spesho wahindi ambao wana uwezo wa kutoa ten pasent kwa hao wapenda rushwa wazandiki, hata kama dawa zimekwisha wako tayari kushuhudia wa tz wakifa kwa kukosa dawa kuliko kuruhusu wazalendo kuingiza,kwani tumesahau yule mhindi aliyepewa tenda ya kusaply zile dawa za kifua kikuu alivyowateketeza wa tz? nani alijali?

USAHAU NA PENSENI ZA WAZEE WETU KALA MBOWE.
HALAFU KODI ALIZOKWEPA KWENYE MATANGAZO YA WASTAFU EAST AFRICA NITAKULETEA.
UNAJUA MRAMBA ALIMPA MATANGAZO YA ZAIDI YA BILLIONI MOJA KWA NJIA ZA KIKABILA?
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom