Nakumbuka mwaka 2020 nikiwa kwenye basi narudi nyumbani Dar kutokea Morogoro; kupitia spika za basi nilikuwa nasikia wimbo uliokuwa na maneno haya kwa uchache:🎶🎶 Unawasi wasi hofu na mashaka unahisi moyoni kama Mungu kakuacha maana unaona hausogei wala hauendelei uko pale pale kila siku uko vile vile,,,, Mungu alianzisha safari na ataimaliza ahadi zote alizo sema atazitimiza maana alikujua kabla haujazaliwa kabla haujajijua
Na Mungu hawezi kukuacha njiani, safari yako aliianzisha mwenyewe asingetaka angekuacha mwanzoni unapo kwenda yeye anajua...