JamiiForums Usiku wa manane
Huyu baba Ambwene mwasonge ni kama ana sauti ya uponyaji kwenye nyimbo zake,, Nyimbo zote ni nzuri na nina zipenda mnooo ila huu "Nimeachilia" nina upenda mara miamoja

siku ukiwa na machungu hautamani kuzungumza wala kumshirikisha mtu unayo yapitia kaa mahali then sikiliza huu wimbo kwa utulivu utapata relief ya moyo na akili
 
🎶🎶 Sio kila kinachokuja kwako ni chako na sio kila kiondokacho kwako ni chako hata kama unavipenda sio vyako", vingine Mungu huviondoa ili wew ubaki salama iwe kazi nafasi mahusiano au cheo, japo vyaondoka kwa maumivu ila jifunze kuviacha viende na nafasi ya moyo wako mpe Mungu

Jifunze kuviacha viende jifunze kusema bai bai maana sio vyote vyakwako,, walitoka kwetu hawakua wa kwetu maana wangekua wetu wangelikaa nasi walifunuliwa ili tujue sio wote wa kwetu🎶🎶
 
Nyimbo ni nyingiiii ila kwa leo tuishie na huu wimbo wa paul Clement: Mwaminifu

Huu wimbo alinidedcate rafiki angu wa kipindi hichoo anaitwa Eva niliupenda toka siku ya kwanza nausikiliza mpaka kesho nitaendelea kuupenda,, na mimi leo nausimulia hapa labda utafanyika baraka kwa watu wengine pia 🙏👇
 
🎶🎶 Unawasi wasi hofu na mashaka unahisi moyoni kama Mungu kakuacha maana unaona hausogei wala hauendelei uko pale pale kila siku uko vile vile,,,, Mungu alianzisha safari na ataimaliza ahadi zote alizo sema atazitimiza maana alikujua kabla haujazaliwa kabla haujajijua

Na Mungu hawezi kukuacha njiani, safari yako aliianzisha mwenyewe asingetaka angekuacha mwanzoni unapo kwenda yeye anajua...
 
🎶🎶 Unawasi wasi hofu na mashaka unahisi moyoni kama Mungu kakuacha maana unaona hausogei wala hauendelei uko pale pale kila siku uko vile vile,,,, Mungu alianzisha safari na ataimaliza ahadi zote alizo sema atazitimiza maana alikujua kabla haujazaliwa kabla haujajijua

Na Mungu hawezi kukuacha njiani, safari yako aliianzisha mwenyewe asingetaka angekuacha mwanzoni unapo kwenda yeye anajua...
Nakumbuka mwaka 2020 nikiwa kwenye basi narudi nyumbani Dar kutokea Morogoro; kupitia spika za basi nilikuwa nasikia wimbo uliokuwa na maneno haya kwa uchache:
"Akisema atakubariki,
Hakuna atakayezuia,
Kwani yeye ndiye Mungu,
Mwenye baraka zote."

Muimbaji ni yule aliyeimba pia
"Naliaaa 'pole'
Naliaaa 'pole sana!'"

Haikuwa mara ya kwanza nasikia huo wimbo ila hiyo siku ulinibariki na kunifariji mno. Nilikuwa nimepoteza matumaini na mipango yangu ilikuwa imefeli pakubwa.. lakini baada ya kuusikiliza ule wimbo nilijikuta napata nguvu mpya ya kuendelea kupambana.
 
Back
Top Bottom