Mastory ya Bey
Hello My people
Mapenzi ndio yana run dunia kwahiyo hatuwezi ishi bila mapenzi au kuzungumzia mapenzi
Tuangalia namna ya kuponya majeraha ya kuumizwa kimapenzi,kama hujaumia leo basi tarajia kesho utaumizwa yan iko hivyo siku zote
Kwanza kubali hisia zako kwamba umeumizwa, jisikie vibaya na lia hata ukiweza,usijifanye upo okay wakati haupo okay,kubali maumivu ambayo umeyapata
Zungumza na mtu unayemwamini anaweza kuwa mshauri wa mapenzi,best yako wa ukweli na mwingine yoyote yule ambaye atakufanya uyaone mambo katika namna tofauti na kukufanya ujisikie gud
Jiepushe kumrudia ex wako kwa muda mfupi,wakati mwingine kutokana na mazoea waeza jikuta kama unataka kurudiana nae tena kwa haraka, kumbuka huyu ndio aliyekuumiza na kukupa machungu hivyo gangamala
Jipe kipaumbele katika nyakati hizi,fanya mambo ambayo unayafurahia,kama kusoma,michezo kutembea,kucheki movie,kutalii na kadhalika,give yourself a gud time
Epuka kujilaumu,mapenzi huvunjika kwasababu nyingi sana,na wakati mwingine sio makosa yako,kwahiyo usijilaumu kwa yaliyotokea
Jifunze kupitia maumivu ya mapenzi unayoyapata,jitathimini wapi unakosea,wapi unatakiwa uboreshe,je ni redflags gani uliziona toka awali lakini ulizichukulia poa na mambo kama hayo
Jipe muda kabla hujaingia kwenye mahusiano mapya,usikurupuke eti kumuonnyesha ex wako kwamba ukisema cha nini wenzio wanasema nitakipata lini, aisee hapo utajikomoa mwenyewe bila kujijua,baada ya muda si rmrefu utakuja kujua kwamba umefanya makosa makubwa sana
Toa msamaha au samehe yaliyo pita,kusamehe haimaanishi kwamba unarudiana nae laa! Ni kuponya moyo wako,unapokuwa na chuki dhidi ya mtu mwingine basi tambua unabeba mzigo mkubwa mgongoni mwako na utavunjika usipokuwa makini
Tambua unapotoa msamaha ni kwa ajili ya kuponya nafsi yako mwenyewe,kwahiyo fanya si kwa ajili ya aliyekukosea ila kwa ajili yako.
Bey