JamiiForums Usiku wa manane
Mastory ya Bey

Je ni sahihi kuendelea kuwa na namba ya ex wako?

Jibu linaweza kuwa ndio au hapana itategemeana na mahitaji ambayo yanaweza kuwepo baada ya mahusiano kufa

Ila jibu la kwanza si sawa kuendelea kuwa na namba ya ex wako,kwanza unakuwa nayo ili iweje? Unatarajia nini toka kwa ex wako?

Je haupo tayar kumove on na mahusiano mapya? Au bado upo njia panda huku unataka na huku unataka

Sikia msomaji wangu,lililo la busara ni kumove on,futa namba ya simu,na liepuke lolote ambalo bado linaweza kuwa kikwazo kwako cha kusonga mbele,kumbu kumbu yoyote ambayo itakuwa sababu ya kukufanya ushindwe kumove basi malizana nayo mara moja ili uwe free kusonga mbele

Heshimu hisia zako na songa mbele,kwani mlivyoamua kuachana si mlikuwa na akili timamu bila kushurutishwa na yeyote yule mpaka mkayafikia hayo maamuzi? Sasa kinachokufanya ushindwe kumove on nini?

Fanya maamuzi ya busara na songa mbele kamwe usiangalie nyuma

Upande wa pili kwa nini uwe na namba ya ex wako,hii itategemeana na mko matured kiasi gani,kwa maana ya kwamba now ni stickly business that's all na si vinginevyo,na mtatafutana kwa mambo nje ya mapenzi

Mfano nijizungumzie mie binafsi,nina ex wangu ambaye yupo kwenye fani ya huduma za kiafya,huyu huwa namtafuta pale ninapotaka huduma hiyo na kupata huduma ya VIP. na nje ya hapo hakuna la ziada,ni just business

Kwahiyo huenda ukawa na namba ya ex ambaye akawa msaada kwako kwa huduma fulani lkn hakikisha hakuna zaidi ya hapo,hakuna kuchekiana time to time,ni pale tu unapo hitaji msaada fulani basi

Hapo unaweza kuwa na namba ya ex wako,kama analeta leta shobo basi fasta malizana nae mapemaaaa.
 
LEO KATIKA HISTORIA

Hapa kuna baadhi ya matukio muhimu yaliyotokea tarehe 14 Septemba katika historia:


---

Matukio

1741 – Ufalme wa Uingereza ulipitisha mfumo wa kalenda ya Gregorian; tarehe 2 Septemba ikabadilishwa moja kwa moja kuwa 14 Septemba.

1812 – Napoleon na majeshi yake waliingia Moscow, ambayo ilikosa maafisa wa serikali na watu wengi walikuwa wameondoka kabla ya kuingia kwake.

1814 – Francis Scott Key aliandika wimbo uliokuwa baadaye kuwa himno ya taifa la Marekani “The Star-Spangled Banner” baada ya kuona bendera ya Marekani ikibaki juu ya Fort McHenry baada ya shambulio la Uingereza.

1959 – Probe ya Sovieti, Luna 2, ilikuwa kitu cha kwanza kilichotengenezwa na binadamu kufika uso wa mwezi.

1960 – OPEC (Organization of the Petroleum Exporting Countries) ilianzishwa.

1901 – Rais wa Marekani William McKinley alifariki kutokana na jeraha la risasi alilopata, na Makamu wake wa Rais Theodore Roosevelt akachukua nafasi akiwa na miaka 42, akiwa Rais mchanga kuliko wote wakati huo.



---

Wazaliwa na Wafu

Wazaliwa

Margaret Sanger, mwanzilishi wa klini ya kwanza ya udhibiti wa uzazi nchini Marekani.

Dmitry Medvedev, mwanasiasa wa Urusi.


Wafu

Grace Kelly, mwigizaji maarufu wa filamu na baadaye Malkia wa Monaco, alifariki kutokana na ajali ya gari mwaka 1982.

William McKinley, Rais wa Marekani wa 25.






 
Back
Top Bottom