JamiiForums Usiku wa manane
Mastory ya Bey

Changamoto nyingi sana za wanaume zinasababishwa na wanawake,naweza Sema asilimia 80 chanzo ni wanawake

Tunapambana sana na tunatumia nguvu nyingi kwa ajili ya hawa viumbe,ambao mwisho wa siku hawaoni thamani yetu,yani akija mwanaume mwenzako na dau kubwa anaonekana wa thamani kuliko wewe ambaye umesapoti kwa mda mrefu

Anakuja mwamba mmoja na hela zake kwa siku moja tu anapindua Meza na unaonekana si lolote

Kwa kutaka kupambania penzi lako ndio unajiiongezea changamoto zaidi,maana itategemea na mshindani wako ana nguvu kiasi gani ana uwezo kiasi gani

Tunaumiza familia zetu kwasababu ya wanawake,hatuwajali watoto wetu kwa sababu ya wanawake,hela ambayo ingesaidia familia yako na mkeo,unaenda kumhonga mwanamke

Wengine wanapoteza kazi kwasababu ya wanawake,unakimendea king'asti cha boss,mara paap boss anashtukia mchezo kibarua huna

Vipato vyetu kweli havitoshi lakini hali inakuwa mbaya zaidi pale tunapo tumia vipato hivyo hivyo vidogo kuhonga wanawake

Tuje kisaikolojia, tuna athirika sana, kwanza kibarua kinakuja kubalance mapenzi ya wife na mchepuko,wakati mwingine mchepuko ndio anataka awe juu zaidi ya wife,je hapo imekaaje?


Unashindwa kuwa na utulivu kwakuwa wewe ni mmoja lakini unataka kuishi maisha ya watu wawili tofauti, huku unataka kuishi kama innocent husband ambaye huna makando kando,na huku unataka kuishi kama mwanaume ambaye hajaoa

Kiroho nafsi yako ina tapa tapa,huku unajiona mkosefu mbele ya muumba wako,upande wa pili unajipa moyo kwamba utabadilika soon,lakini mwisho wa siku upo pale pale

Unaweza ongea mengi sana,lakini kama wanaume tukifanikiwa kudhibiti tamaa zetu na uchu wetu na kujiweka mbali na wanawake naamini kabisa tutakuwa tumepunguza asilimia 80 ya changamoto zetu

Ni juu yako kuchukua hatua.
 
LE0 KATIKA HISTORIA

🗓️ Leo katika Historia – Septemba 12 (Dunia kwa ujumla)

Hapa kuna matukio muhimu yaliyowahi kutokea siku kama ya leo duniani:


---

🔹 490 K.K. – Vita vya Marathon

Wanajeshi wa Kigiriki walishinda dhidi ya Waajemi katika vita vya Marathon, ushindi uliyoimarisha ustaarabu wa Ugiriki na demokrasia ya Athene.

🔹 1940 – Ugunduzi wa Pango la Lascaux (Ufaransa)

Vijana waligundua michoro ya kale ya mapango huko Lascaux, ambayo sasa ni miongoni mwa hazina kubwa za sanaa ya kale duniani.

🔹 1953 – John F. Kennedy aoa Jacqueline Bouvier

Seneta wa Marekani, John F. Kennedy (baadaye rais), alifunga ndoa na Jacqueline Bouvier, tukio lililovutia vyombo vya habari vya kimataifa.

🔹 1959 – Urusi Yazindua Luna 2

Chombo cha anga cha Kisovieti, Luna 2, kikawa cha kwanza kugonga uso wa Mwezi, hatua kubwa katika mbio za anga.

🔹 1974 – Ethiopia: Mapinduzi ya Derg

Mfalme Haile Selassie I wa Ethiopia aliondolewa madarakani baada ya utawala mrefu, na baraza la kijeshi (Derg) likachukua mamlaka.

🔹 2005 – Israel Yakamilisha Kuondoa Walowezi Gaza

Jeshi la Israel lilimaliza rasmi mpango wa kuondoa walowezi wa Kiyahudi katika Ukanda wa Gaza.
 
Mastory ya Bey

Changamoto nyingi sana za wanaume zinasababishwa na wanawake,naweza Sema asilimia 80 chanzo ni wanawake

Tunapambana sana na tunatumia nguvu nyingi kwa ajili ya hawa viumbe,ambao mwisho wa siku hawaoni thamani yetu,yani akija mwanaume mwenzako na dau kubwa anaonekana wa thamani kuliko wewe ambaye umesapoti kwa mda mrefu

Anakuja mwamba mmoja na hela zake kwa siku moja tu anapindua Meza na unaonekana si lolote

Kwa kutaka kupambania penzi lako ndio unajiiongezea changamoto zaidi,maana itategemea na mshindani wako ana nguvu kiasi gani ana uwezo kiasi gani

Tunaumiza familia zetu kwasababu ya wanawake,hatuwajali watoto wetu kwa sababu ya wanawake,hela ambayo ingesaidia familia yako na mkeo,unaenda kumhonga mwanamke

Wengine wanapoteza kazi kwasababu ya wanawake,unakimendea king'asti cha boss,mara paap boss anashtukia mchezo kibarua huna

Vipato vyetu kweli havitoshi lakini hali inakuwa mbaya zaidi pale tunapo tumia vipato hivyo hivyo vidogo kuhonga wanawake

Tuje kisaikolojia, tuna athirika sana, kwanza kibarua kinakuja kubalance mapenzi ya wife na mchepuko,wakati mwingine mchepuko ndio anataka awe juu zaidi ya wife,je hapo imekaaje?


Unashindwa kuwa na utulivu kwakuwa wewe ni mmoja lakini unataka kuishi maisha ya watu wawili tofauti, huku unataka kuishi kama innocent husband ambaye huna makando kando,na huku unataka kuishi kama mwanaume ambaye hajaoa

Kiroho nafsi yako ina tapa tapa,huku unajiona mkosefu mbele ya muumba wako,upande wa pili unajipa moyo kwamba utabadilika soon,lakini mwisho wa siku upo pale pale

Unaweza ongea mengi sana,lakini kama wanaume tukifanikiwa kudhibiti tamaa zetu na uchu wetu na kujiweka mbali na wanawake naamini kabisa tutakuwa tumepunguza asilimia 80 ya changamoto zetu

Ni juu yako kuchukua hatua.
Kiufupi kataa ndoa linda maisha yako.
 
Back
Top Bottom