Mastory ya Bey
Part 1
Story: “Mzigo wa Zamani”
Fatma alikuwa msichana mchangamfu, mwenye ndoto ya kuwa mwalimu. Lakini siku moja, alipokosea kusahihisha mtihani akiwa msaidizi wa mwalimu, mwanafunzi mmoja alipata adhabu kwa kosa ambalo halikuwa lake. Fatma alipojua ukweli, aliogopa kusema. Muda ukapita, na akahisi lawama kubwa moyoni.
Miaka ilivyopita, alikosa kujiamini, alijilaumu, na kujihisi hastahili mafanikio. Kila alipopata nafasi, alijiambia: “Nakumbuka nilivyomuumiza yule mtoto, siwezi kuwa mwalimu bora.”
Siku moja kwenye kongamano la walimu, alimkuta yule mwanafunzi akiwa mtu mzima na mfanikio makubwa. Kwa aibu na huzuni, Fatma alimuomba msamaha. Yule mwanafunzi akacheka kidogo na kusema:
“Nilishasahau hilo kitambo. Mengine ni changamoto za maisha tu. Usijichomee moto wa zamani, Fatma.”
Fatma alilia kwa hisia. Toka siku hiyo, aliamua kuachilia mzigo wa kujilaumu na kuanza upya.
Somo: Kujilaumu ni kama kubeba mzigo wa mawe — haukusaidii kufika mbele. Ukishatubu au kuomba msamaha, jikubalie, jifunze, na songa mbele kwa matumaini.
Part 2
Story: “Usijilaumu Milele”
Zuhura alikuwa msichana mwerevu sana, lakini siku moja alipata matokeo mabaya shuleni. Alijilaumu kwa miezi kadhaa: “Ningeamka mapema,” “Nisingefungua simu,” “Nilikuwa mzembe.” Polepole alianza kujiona hana thamani. Alijitenga, akaacha ndoto zake za kuwa daktari.
Mwalimu wake mmoja alipoona hali hiyo, alimuita na kumuuliza:
“Zuhura, kama mtoto mdogo ateleza na kuanguka, utamkemea au utamsaidia kuinuka?”
Zuhura akajibu: “Nitamsaidia ainuke.”
Mwalimu akasema: “Hivyo ndivyo unavyopaswa kujiangalia. Umeanguka, sasa inuka na ujisamehe.”
Maneno yale yalimgusa. Alianza kujifunza tena taratibu, akapata marafiki wapya waliomtia moyo, na miaka miwili baadaye alifaulu na kujiunga na chuo cha udaktari.
Somo:
Kosa moja si mwisho wa safari. Kujilaumu kupita kiasi hukufunga. Lakini kujifunza, kutubu, na kuendelea mbele ndio ushindi wa kweli.
Methali ya leo: “Aliyeanguka si aliyeshindwa, bali ni yule anayekataa kusimama tena.”