James Comey
JF-Expert Member
- May 14, 2017
- 9,529
- 16,232
11:04 Pm
Location: Halmashauri ya wilaya ya Kiponjoroni, DSM.
Location: Halmashauri ya wilaya ya Kiponjoroni, DSM.
Mzee wa location,nimeipenda hii11:04 Pm
Location: Halmashauri ya wilaya ya Kiponjoroni, DSM.
Hahaha, kweli acha niendelee kusoma tuu 😅💯💯Nikikwambia utamu utakwisha,,Mwenyekiti wangu endelea kuvisoma hapa hapa,ipo siku utakuja kufahamu
😅😅😅Niamke nikatafute kazi wakuu,
Somo zuri sana Mkuu 💯Mastory ya Bey
Story: "Moyo wa Msamaha"
Kulikuwa na vijana wawili, Salim na Juma, waliokuwa marafiki wa karibu tangu utotoni. Walikulia mtaa mmoja, walishirikiana kila kitu — hadi walipokomaa, wakapenda msichana yule yule bila kujua.
Siku moja Juma aligundua kuwa Salim alikuwa akizungumza na msichana huyo kwa siri. Alihisi kusalitiwa. Urafiki wao ukavunjika ghafla, Juma akajaa chuki. Hakuzungumza na Salim kwa miaka mitano, hata salamu aliikataa.
Mwaka mmoja, Juma alipata ajali mbaya na kupelekwa hospitali. Alipopoteza fahamu, mtu aliyekuwa akimuuguza kila siku bila kuchoka alikuwa… Salim.
Alipofumbua macho, Juma aliuliza, “Mbona unanisadia baada ya yote yaliyopita?”
Salim alitabasamu na kusema:
“Chuki ni mzigo. Urafiki wetu ni wa thamani kuliko kinyongo cha moyo.”
Juma alilia. Akaomba msamaha. Wakarudisha urafiki wao — safari hii wakiwa na moyo wa kusamehe na kuachilia.
Somo:
Chuki huua ndani kwa ndani. Msamaha huponya moyo na hujenga maisha mapya.
Ohooo!!Satoh Hirosh tuhamie huku, tusiharibu uzi wa watukule. Kweli ni miaka mingi sana tumepoteana. Juzi tu nami nilikukumbuka, nikajiuliza ulipotelea wapi?
00:23