Mazungumzo ya usiku
WANANDOA NA HAKI YA TENDO LA NDOA
Leo kalamu ya mlinzi wa zamu inaangalia swala zima la tendo la ndoa kwa wanandoa
Hii ni haki ya msingi sana kwa wanandoa,maana hata msingi mzima wa ndoa umejengewa hapo,haki zote tulikuwa tunapata majumbani kwetu,lakini haki hii ndio ikawaunganisha mwanaume na mwanamke waishi pamoja ili kukidhi matamanio yao
Kwa maana kwamba baada tu ya kufunga ndoa kila mmoja anastahili kupata haki hiyo pasina masharti yoyote yale au bila vikwazo vyovyote vile
Lakini bahati mbaya iliyopo ni kwamba hutokea baadhi ya wanandoa kutumia silaha ya tendo la ndoa kukomoana pale inapotokea sintofahamu kati yao
Basi mwanandoa mmoja wapo hutumia silaha hiyo kumnyima mwenzake unyumba kwakuwa tu kuna haja au mambo fulani hayajatekelezwa
Hakika mbele ya Mungu hili ni kosa kubwa sana,sijui upande wa ukristo huko,lakini kwa ufahamu wa dini ya kiislamu,kwa mwanamke ambaye anaitwa na mumewe kitandani kisha akakataa basi hakika hulaaniwa na Malaika usiku kucha
Sasa usione hili ni jambo dogo,hawa viumbe hawana dhambi kwahiyo dua zao mbele ya Mola wao huwa ni zenye kupokelewa,kama ambavyo huwaombea watu wema dua kwa Mungu,na Mungu hupokea dua zao
Lakini lingine kuna hatar kubwa sana ya kuwa sababu ya mwenza wako kwenda nje kupata faraja huko,nawe utakuwa sehemu ya uovu huo,kwasababu umesababisha mwenza wako akazini kwakuwa wewe hukumpa haki yake
Kwahiyo mjue kwamba kinachowaunganisha wanandoa msingi wake ni hilo tendo,sasa iweje tena mnyimane mautamu wakati kwa hiari yenu wenyewe mmeamua muishi pamoja kama mume na mke
Kama kuna tokea sintofahamu yoyote basi zungumzeni na myamalize lkn msitumie haki yenu ya msingi kuanza kukomoana
Mlinzi wa zamu!