JamiiForums Usiku wa manane
Mazungumzo ya usiku

TUNA WAPENDA WANAWAKE WENYE KUSHUKURU


Wanaume huwa tunawathamini wanawake ambao huonesha kufurahishwa na hata yale mambo madogo tunayo wafanyia,Kwa kufanya hivyo huwa tunawapa thamani ya juu na kuzidi kuwapenda,chukulia mwanaume amekuletea kazawadi kadogo kutokana na uwezo wake au kutokana na choice yake ukaonyesha kufurahishwa nayo basi tambua mwanaume huyo siku zijazo atakufanyia kitu kingine kizuri zaidi,kwasababu amehisi umethamini kile alicho kufanyia na hivyo kumfanya akupende zaidi.

Na kinyume chake huwa hivyo hivyo,nimekuletea kapaseli ukaonyesha kutokufurahia au kutokujali,basi tambua itamkatisha tamaa mwanaume na huenda asifikirie tena kukufanyia kitu kama Hicho,hata kama hujapenda hiyo zawadi basi usimuonyeshe kuwa hujafurahishwa jizugishe ili mradi boy wako afeel okay,mbona kwenye orgasm huwa mnafeki hahahah! Mwanamke mjanja atamwambia boy wake,honey! Asante Kwa zawadi kpnz changu ila next time ukiamua kuninunulia zawadi basi nitapendelea zaidi unichukulie kitu flan,hapo utakuwa hauja humiza hisia zake, tena utakuwa umemsaidia kufanya kitu kizuri huko mbeleni.

Tunapenda wanawake ambao hata tukizingua basi hawafanyi iwe ishu kuuubwa! Trust me girls mkiwa hivyo mnatufanya tuwathamini Sana hata kama hatuta waonyesha hadharani lkn mnakuwa mashujaa wetu ktk nyoyo zetu. Nimezingua nambie babe sijapenda ulivyofanya pliz next time don't hurt my feelings! Daah tutaona aibu siku nyingine kuzingua,Kwanza tunaona kama zari kuwa hamjapanic kivile basi hapo unakuwa Queen ktk moyo WA mwanaume na hatokusahau.

Mwisho tunajua mnapenda hela waarabu wanaita fulusi,basi hata mwanaume akikupa kias kidogoi kutokana na uwezo wake Kwa Mda huo basi mshukuru,kwakufanya hivyo next time ataongeza digit zaidi,Ila mkileta zile zenu sasa honey hii hela itatosha nini? Daah hapo mnakuwa mnazingua! Unajua kwanini hiyo hela ambayo wewe unaona ndogo basi tukituma Kwa wazazi wanatuombea dua juu na kututakia baraka tele Kwa Mwenyezi Mungu,na tunabarikiwa Sana Tu.

Mlinzi wa zamu!
 
Mazungumzo ya usiku

WANANDOA NA HAKI YA TENDO LA NDOA


Leo kalamu ya mlinzi wa zamu inaangalia swala zima la tendo la ndoa kwa wanandoa

Hii ni haki ya msingi sana kwa wanandoa,maana hata msingi mzima wa ndoa umejengewa hapo,haki zote tulikuwa tunapata majumbani kwetu,lakini haki hii ndio ikawaunganisha mwanaume na mwanamke waishi pamoja ili kukidhi matamanio yao

Kwa maana kwamba baada tu ya kufunga ndoa kila mmoja anastahili kupata haki hiyo pasina masharti yoyote yale au bila vikwazo vyovyote vile

Lakini bahati mbaya iliyopo ni kwamba hutokea baadhi ya wanandoa kutumia silaha ya tendo la ndoa kukomoana pale inapotokea sintofahamu kati yao

Basi mwanandoa mmoja wapo hutumia silaha hiyo kumnyima mwenzake unyumba kwakuwa tu kuna haja au mambo fulani hayajatekelezwa

Hakika mbele ya Mungu hili ni kosa kubwa sana,sijui upande wa ukristo huko,lakini kwa ufahamu wa dini ya kiislamu,kwa mwanamke ambaye anaitwa na mumewe kitandani kisha akakataa basi hakika hulaaniwa na Malaika usiku kucha

Sasa usione hili ni jambo dogo,hawa viumbe hawana dhambi kwahiyo dua zao mbele ya Mola wao huwa ni zenye kupokelewa,kama ambavyo huwaombea watu wema dua kwa Mungu,na Mungu hupokea dua zao

Lakini lingine kuna hatar kubwa sana ya kuwa sababu ya mwenza wako kwenda nje kupata faraja huko,nawe utakuwa sehemu ya uovu huo,kwasababu umesababisha mwenza wako akazini kwakuwa wewe hukumpa haki yake

Kwahiyo mjue kwamba kinachowaunganisha wanandoa msingi wake ni hilo tendo,sasa iweje tena mnyimane mautamu wakati kwa hiari yenu wenyewe mmeamua muishi pamoja kama mume na mke

Kama kuna tokea sintofahamu yoyote basi zungumzeni na myamalize lkn msitumie haki yenu ya msingi kuanza kukomoana

Mlinzi wa zamu!
 
Back
Top Bottom