Mazungumzo ya usiku
TOFAUTI YA MOOD YA WANAUME NA WANAWAKE
Wanawake mtambue kuwa wanaume wanapokuwa wamevurugwa na mambo yao au kuwa na mambo ambayo yanawashughulisha huhitaji kuingia ndani ya cave/Pangoni ili wapate kutulia na kufikiria namna ya kutatua changamoto zao,haimaanishi wanaenda Pangoni kiuhalisia Ila wanahitaji kuwa pekee Yao Kwa kipindi Fulani, kwahiyo mwanamke ukiona Hali kama hii,usipaniki na kutaka kumuuliza boy wako ''mbona hupigi Stori na Mimi tena, mbona unaonekana kama haupo kawaida nini tatizo'' na mambo kama hayo,San Sana mwanaume atakwambia nipo Sawa mke wangu wala usijali, so akishakwambia hivyo basi usiendelee kumgasi gasi mpe nafasi atatue changamoto zake akimaliza atarudi katika Hali yake ya kawaid,hapo sasa ukimuona yupo normal waeza muuliza nini lilikuwa tatizo,akiwa willing kukwambia Sawa asipotaka usipanic,jua ndio hulka za wanaume zilivyo, lakini wanawake wengi Kwa kutojua hili huanza kuwa wasumbufu na kutoa maneno kibao,'' naona hunipendi mbona huniambii nini kinakusumbua''? Mwanamke tambua kuwa mwanaume si Sawa na mwanamke katika kudili na mambo yake,wakati nyinyi mnapenda kushare mambo yenu basi wanaume hawako hivyo.
Wanaume nanyi tambueni kuwa Kwa kipindi Fulani Fulani huenda ikawa hata Kwa mwezi mara moja,mwanamke huwa ana bounce kama Mawimbi sometime anakuwa high na sometime low. Anapokuwa high ina maana anakuwa ktk full mood kila kitu kinaenda Sawa,mawasiliano mazuri,maelewano fresh na vitu kama hivyo. Na kinyume chake anapokuwa low basi ujue anakuwa hayupo katika mood nzuri,utamkuta kisirani kingi,huenda mawasiliano yasiwe mazuri na vitu kama hivyo, sio kwamba wanafanya makusudi ni asili Yao kutokana na maumbile Yao,na wakati mwingine anaenda sambamba na mzungo WA vipindi vyao vya kila mwezi,kwahiyo wanaume mkiona mazingira kama haya msipaniki Sana mjue kuwa ndio maumbile Yao na ndio walivyo,lkn muhimu ujue kutofautisha chuya na mchele,sio anakuletea jeuri kwakuwa kapata bwana mpya au ana michepuko anamtia kiburi halafu wewe ukawa bwege Tu kila siku dharau nyingi na kisirani au matusi juu hlf unadhani yupo low,no! Uwe Makini kumsoma je hapa ni mood swing au naibiwa?
Haya ni mambo ambayo watu wameyafanyia utafiti Kwa sample kubwa ya watu na kupata data hizi,ebu tafuta Kitabu Man are from Mars and Women from Venus, utakuja kunishukuri baadae kina madini Sana na ukikisoma sometime unaona kabisa kama mwandishi anaongea na wewe coz kuna mambo anakugusa kabisa kuhusiana na Maisha ya kimapenzi,kuna watu ndoa zao zilikuwa zinakufa lkn baada ya kusoma Hiki Kitabu na kujifunza wapi wanakosea na wapi PA kurekebisha wamejikuta ndoa zina nawiri na kustawi upya.
Mlinzi wa zamu!