JamiiForums Usiku wa manane
Nyota huonekana njema
Nyota ya asubuhi ni njema
Asubuhi njema ina nyota
Asubuhi na nyota zote ni njema
Ah hivohivo ila hio methali ina asubuhi, nyota na njema ndani yake, utayapanga
🙂
 
Huko kwenu ni saa ngapi now? Hapa nilipo ni takribani saa 04:36 usikuuuuu…welcome to LA the sin city
 
Mazungumzo ya usiku

TUJENGE TABIA YA KUWASHUKURU NA KUWAPA SIFA WATU WETU WA KARIBU

Ni mara nyingi sana kama sio zote huwa tunawapa hongera na kuwakubali sana wanasiasa na watu mashuhuri kwa mambo wanayo yafanya iwe ya kisiasa au kijamii na mambo kama hayo

Pamoja na kuwakubali na kuwasifu kwa namna moja au nyingine ila wao hawatufahamu wala hawatujui,wanatuona ni watu tu miongoni mwa kikundi cha watu,kwahiyo kuna haja gani ya kuwapa kipaumbele sana

Lakini bahati mbaya sana,kuna watu ambao wapo kwenye maisha yetu ya kila siku,na wanamchango mkubwa kwetu lakini huwa hatuwapi sifa wanazo stahili

Dada wako wa kazi anasafisha nyumba yenu,anawapikia chakula,saa nyingine huwatayarisha watoto kwa kwenda shule,lakini haijatokea hata siku moja,ukampa sifa anayo stahili akajisikia vizuri na kuona mchango wake unatambulika

Wale wenye walinzi,mnajua jinsi kazi ya ulinzi ilivyo ngumu na ina risk kubwa,je mmeshawi walau mara moja moja kuwaambia ni kiasi gani mnajivuna kuwa nao hapo nyumbani?

Madereva wa serikali ni watu ambao kutwa kucha wapo na maboss wao tu,saa nyingine hadi wikiend,je nyie maboss mmeshawahi walau kuwapa maneno mazuri ya kushukuru kwa huduma yao?

Mlinzi wa zamu ninachotaka kusema ni kwamba,tujenge tabia ya kuwapenda na kuwapa sifa pia watu ambao wanatuzunguka na ambao wana mchango mkubwa sana katika maisha yetu

Tukiwaonyesha kwamba tunajivunia kuwa nao na tunatambua mchango wao,hakika itawapa hamasa kubwa sana ya kujituma zaidi na kufurahia majukumu yao

Mlinzi wa zamu!
 
2336

Kitu ambacho kinafurahisha au kinatia raha kuhusu uzi huu ni ile kutaja saa au mda wa usiku,tena ile mida mibovu ambayo wachawi wako kazini au wenye kuamka usiku kufanya ibada ya mola wao

Kwahiyo hata ukiamka kwenda wash room washa data fungua uzi chapisha mda hapo kisha zima data na endelea na mambo yako

Kwakufanya hivyo lindo litakuwa salama
 
Mazungumzo ya usiku


TOFAUTI YA MOOD YA WANAUME NA WANAWAKE


Wanawake mtambue kuwa wanaume wanapokuwa wamevurugwa na mambo yao au kuwa na mambo ambayo yanawashughulisha huhitaji kuingia ndani ya cave/Pangoni ili wapate kutulia na kufikiria namna ya kutatua changamoto zao,haimaanishi wanaenda Pangoni kiuhalisia Ila wanahitaji kuwa pekee Yao Kwa kipindi Fulani, kwahiyo mwanamke ukiona Hali kama hii,usipaniki na kutaka kumuuliza boy wako ''mbona hupigi Stori na Mimi tena, mbona unaonekana kama haupo kawaida nini tatizo'' na mambo kama hayo,San Sana mwanaume atakwambia nipo Sawa mke wangu wala usijali, so akishakwambia hivyo basi usiendelee kumgasi gasi mpe nafasi atatue changamoto zake akimaliza atarudi katika Hali yake ya kawaid,hapo sasa ukimuona yupo normal waeza muuliza nini lilikuwa tatizo,akiwa willing kukwambia Sawa asipotaka usipanic,jua ndio hulka za wanaume zilivyo, lakini wanawake wengi Kwa kutojua hili huanza kuwa wasumbufu na kutoa maneno kibao,'' naona hunipendi mbona huniambii nini kinakusumbua''? Mwanamke tambua kuwa mwanaume si Sawa na mwanamke katika kudili na mambo yake,wakati nyinyi mnapenda kushare mambo yenu basi wanaume hawako hivyo.

Wanaume nanyi tambueni kuwa Kwa kipindi Fulani Fulani huenda ikawa hata Kwa mwezi mara moja,mwanamke huwa ana bounce kama Mawimbi sometime anakuwa high na sometime low. Anapokuwa high ina maana anakuwa ktk full mood kila kitu kinaenda Sawa,mawasiliano mazuri,maelewano fresh na vitu kama hivyo. Na kinyume chake anapokuwa low basi ujue anakuwa hayupo katika mood nzuri,utamkuta kisirani kingi,huenda mawasiliano yasiwe mazuri na vitu kama hivyo, sio kwamba wanafanya makusudi ni asili Yao kutokana na maumbile Yao,na wakati mwingine anaenda sambamba na mzungo WA vipindi vyao vya kila mwezi,kwahiyo wanaume mkiona mazingira kama haya msipaniki Sana mjue kuwa ndio maumbile Yao na ndio walivyo,lkn muhimu ujue kutofautisha chuya na mchele,sio anakuletea jeuri kwakuwa kapata bwana mpya au ana michepuko anamtia kiburi halafu wewe ukawa bwege Tu kila siku dharau nyingi na kisirani au matusi juu hlf unadhani yupo low,no! Uwe Makini kumsoma je hapa ni mood swing au naibiwa?

Haya ni mambo ambayo watu wameyafanyia utafiti Kwa sample kubwa ya watu na kupata data hizi,ebu tafuta Kitabu Man are from Mars and Women from Venus, utakuja kunishukuri baadae kina madini Sana na ukikisoma sometime unaona kabisa kama mwandishi anaongea na wewe coz kuna mambo anakugusa kabisa kuhusiana na Maisha ya kimapenzi,kuna watu ndoa zao zilikuwa zinakufa lkn baada ya kusoma Hiki Kitabu na kujifunza wapi wanakosea na wapi PA kurekebisha wamejikuta ndoa zina nawiri na kustawi upya.

Mlinzi wa zamu!
 
20250506_090901.jpg
 
Back
Top Bottom