JamiiForums Usiku wa manane
Repost from nala

Alhamdulilah mshukuru mungu amekupa pumzi, tumia kila dakika kujiepusha na upuuzi/

Amekupa leo amekupa jana alikunyima juzi, mshukuru sana mshukuru maulana ye ndo mwenye maamuzi/

Ameshusha viumbe, dunia duara ndo maana binadamu tunazungukana kumbe/

Mwema wa sasa mbaya baada ya sekunde, kua na msimamo simama imara usiyumbe/

Watakuja wawili kwa muda tofauti, watakufanya ufikiri ujiulize we ni yupi/

Wakwanza atakuambia we ni boya sana, akija wapili atakuambia we ni bora mwana/

Kaa mbali na wanaoumiza moyo wako, ishi na wale ambao watatimiza ndoto zako/

umezaliwa kwenye mwanga hilo giza sio lako, unaweza jiamini fanya miujiza yako/

It's Scars
 
Back
Top Bottom