Mwita Maranya
JF-Expert Member
- Jul 1, 2008
- 10,565
- 7,993
Asema CHADEMA ipo tayari kwa uamuzi wowote
na Tamali Vullu = Tanzania Daima
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimesema kipo tayari kupokea maamuzi yoyote yatakayotolewa na Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho, Zitto Kabwe, ya kuamua kujiuzulu nyadhifa zote katika chama hicho ama la.
Kauli hiyo ilitolewa jana na Katibu Mkuu wa chama hicho, Dk. Willibrod Slaa, siku moja baada ya Zitto kukaririwa na vyombo vya habari jana kuwa amekuwa akiandaa barua ya kujiuzulu nyadhifa zote ndani ya chama hicho, ikiwamo na ya ubunge. Zitto pia alituma nakala ya maelezo hayo kwa gazeti hili.
Akizungumza na Tanzania Daima jana, Dk. Slaa alisema tangu Zitto aanze kunukuliwa katika baadhi ya vyombo vya habari kuwa anamuunga mkono aliyekuwa Ofisa Habari wa chama hicho, David Kafulula, amekuwa kimya licha ya kumtumia barua pepe kutaka kufahamu ukweli juu ya suala hilo.
"Zilipotolewa taarifa hizo kwenye vyombo vya habari mama yake Zitto, Shida Salum, alieleza kuwa mwanawe hausiki kwa kuwa e-mail yake imekuwa ikiingiliwa na watu na kutuma ujumbe huo," alisema.
Mama huyo pia aliwasilisha madai hayo katika kamati kuu iliyokutana Desemba 2 na kwamba kutokana na hali hiyo alilazimika kumtumia taarifa kwa barua pepe (e-mail) Zitto ili ampe ukweli wa suala hilo, lakini tangu wakati huo amekuwa kimya.
"Baada ya kutolewa kwa madai hayo na kuwasilishwa katika kamati kuu, Desemba 2, nilimtumia e-mail Zitto, lakini mpaka leo (jana) hajanijibu," alisema Dk. Slaa.
Alisema kutokana na hali hiyo, ameanza kupata wasiwasi kuwa huenda mama huyo anadanganywa na mtoto wake huyo (Zitto).
Hata hivyo, alisema asipopata majibu kutoka kwa Zitto atajua kuwa maelezo hayo yana ukweli na kusema kwamba CHADEMA ni taasisi, haitayumba kwa kuondoka kwa mtu yeyote.
"Wakati ule aliondoka Kabourou (Amani Walid Kabourou) na CHADEMA imeendelea kuwapo…anaweza kuondoka Freeman Mbowe na Dk. Slaa, lakini CHADEMA itabaki," alisema.
Aidha, alisema suala hilo linakuzwa ili chama hicho kiachane na ajenda ya kupigania ufisadi nchini na kujikita katika mizozo ya aina hiyo.
"CHADEMA haitaacha kupiga vita ufisadi na ndiyo maana hivi karibuni tumetoa tamko la kuitaka serikali ijibu hoja kuhusu ripoti ya Umoja wa Mataifa (UN) kuichafua Tanzania kuhusu kupeleka silaha kwa kundi la waaasi katika nchi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC)," alisema Dk. Slaa.
Jana, Zitto alikaririwa na gazeti moja (si Tanzania Daima) kupita barua pepe akieleza kuchukizwa na siasa chafu zinazoendelea ndani ya chama hicho na kwamba yupo tayari kujivua nyadhifa zote ndani ya chama hicho ikiwamo ubunge.
Mbunge huyo kijana, alikaririwa akieleza kuwa uamuzi wa kumfukuza Kafulila haukuwa wa haki na kwamba ataendelea kumuunga mkono kama atagombea ubunge katika Jimbo la Kigoma Kusini kwa tiketi ya NCCR - Mageuzi na si mgombea wa CHADEMA.
Hivi karibuni, chama hicho kilimtimua Kafulila na Danda Juju, ambao walikuwa wapambe wakuu wa Zitto katika uchaguzi mkuu wa chama hicho, akiwania nafasi ya uenyekiti wa taifa kabla ya kuamua kujitoa badaa ya vikao mbalimbali vya wazee wa chama hicho vilivyomsihi asigombee ili kutokigawa chama katika kipindi hiki kuelekea uchaguzi mkuu mwakani.
Hivi kumbe kabla ya Mrema kujiunga na NCCR na TLP vilikuwa ni vyama tishio kwa CCM...., naomba ufafanuzi? nijuavyo mie NSSR kilikuwa ni Chama dhaifu sana kilichokuwa hakina ata uwezo wa kushinda jimbo moja la ubunge, na umaarufu wa NSSR 1995 mpaka kuwa chama tishio kwa CCM uliletwa na Mrema, na leadership failure baada ya 1995 ndiyo iliyokiua NCCR na kisha Mrema mwenyewe baadae.
Huu mtindo wa kubadili heading unaanza kuniboa! We moderator anzisha thread zako kama hii ni 'jamii forums' sioni ni kwanini uondoe baadhi ya articles zenye maslahi ya taifa au kuzibadili vichwa vya habari kuku-suit wewe madhalani hazimkashifu mtu!Jamani nimeona article inayosema Zitto yuko mbioni kujiuzulu Chadema katika Mwananchi! Cha kushangazwa article hiyo wameitoa ghafla! Sasa najiuliza kulikoni?
tukiwa "ndani ya kumi na mbili" hawa watatu watapata kazi sana kufanya kazi pamoja kuelekea uchaguzi mkuu mwakani. Mbowe, Slaa, na Zitto. Hawawezi kulima shamba pamoja kama hawajafungwa kongwa pamoja. Ningekuwa na uwezo ningewafungia hawa watatu kwenye kisiwa kimoja mahali fulani na hawarudi hadi wawe wamekumbatiana na kukubaliana.
Huu mtindo wa kubadili heading unaanza kuniboa! We moderator anzisha thread zako kama hii ni 'jamii forums' sioni ni kwanini uondoe baadhi ya articles zenye maslahi ya taifa au kuzibadili vichwa vya habari kuku-suit wewe madhalani hazimkashifu mtu!
NB: Pls dont use my name kuweka article yako au heading that's a crime dont put words in my mouths! Kuwa mstaarabu!!
1.mwalimu j k nyerere aliwahi kusema kuwa chama cha kweli cha upinzani kitatoka ccm,yaani pale itakapomeguka.na hili ndilo linalokuja....
2.pima uone nccr ilipoanzishwa akina marando na wenzie,alipojiunga mrema nccr ikadorora mpaka leo na akina marando wakasepa
3.mrema alipomaliza kazi ya pale nccr akaenda kudororesha tlp sasahivi na chenyewe hoi
4.muulize mrema wapi na lini alrudisha kadi ya ccm kama utajibiwa
zito nae ni walewale tu
https://www.jamiiforums.com/members/asha-abdala.html
Omar;
Usimzushie Mwenyekiti wa CHADEMA kwa kadri ya taarifa ambazo zililetwa hapa JF na hata magazetini huyo Bwana Kafulila alianguka ghorofani mwezi Disemba 2008, wakati huo uchaguzi wa CHADEMA umefanyika Septemba 2009; vipi useme alikuwa na chuki nae? Umekuwa ukisema hapa kwamba Mdee na Mnyika wapo kundi la Mbowe; mbona imeelezwa hapa kwamba hawa ndio wamekwenda kumtibu na kulipia matibabu yake? Kama ingekuwa chuki ya unachokiita kambi ya Mbowe si wangemuacha tu ili apelekwe hospitali na kambi ya Zitto ambayo mama yake alikuwepo eneo la tukio?
Ni wapi mimi nilisema kuwa Heche alitaka kumchoma kisu Zitto Kabwe. Angalia sasa unajikuta ukisema hata yale yaliyofunikwa. Unataka nikuletee ushahidi kwani wewe umeshajiona ni Mwanasheria na JF ni mahakama siku hizi? Ni lini uliwahi kuleta mashahidi wa wawili ama watatu wanaothibitisha kuwa ROSTAM anahusika na WIZI wa EPA? Hivi hayo aliyoyafanya Heche aliyafanya kwa Kificho na sio kwenye uwanja w wazi kabisa akizungukwa na mamia ya WANACHADEMA? Yaani kitendo cha Heche kusema magazetini kuwa hakufanya hilo tayari kimeshathibitisha kuwa hilo halikufanyika. Unataka kutuambia kuwa kwa kuwa ROSTAM alishasema magazetini kuwa hakuhusika na RICHMOND, DOWANS na EPA basi tayari ni thibitisho kuwa yeye ni innocent?Hilo tukio la John Heche kutaka kumchoma kisu Zitto Kabwe lilitokea wapi? Ulilishuhudia wewe mwenyewe au umehadithiwa? Maana tukio la Mbunge kuchomwa kisu lilipaswa kuwa tukio kubwa ambalo lingekuwepo vyombo vyote vya habari na hata taarifa zingekuwa polisi? Kama ni Kafulila, unaweza kutuambia ni lini na wapi alitishiwa na walau ukataja mashahidi wawili watatu? Unaweza kujikuta unaeneza uzushi wa gazeti la Mwananchi. Nakumbuka Bwana Heche aliwahi kuhojiwa na magazeti mbalimbali akaeleza uzushi wa habari ile kumchafua, akataka ajitokeze yoyote hata kama ni Kafulila aseme kama ni kweli yeye ametishia yoyote kwa kisu.
Hata kipofu asiyesoma magazeti wala mitandao kama JF atakushangaa. Mlianza kutumia majina vivuli na sasa mmefikia hata kutumia majina yenu kama alivyofanya KINABO na hata magazeti yenu bila hata kujificha mkiiamini kuwa mnanafasi ya kushinda. Acheni kujidanganya, vita dhidi ya Zitto hamtaiweza kamwe…..Kuhusu Zitto kuchafuliwa, unaweza kututajia ni viongozi gani, wamemchafua wapi kuhusu nini? Sana sana mimi nakumbuka Zitto aliwahi kukukanya hapa kwa tabia yako hii ya kuendelea kuzusha mambo ambayo yanamfanya awe na malumbano na viongozi wenzake. Je, amekupa ruhusa urudi tena kuanzisha malumbano?
Huna tofauti na kina SOPHIA SIMBA na MAKAMBA. Badala ya kujibu hoja unakimbilia kudai MATUSI na UASI. Ni wapi mimi nimetukana CHADEMA ama hata kiongozi wenu? Uweje niwe muasi wakati kamwe sijawahi kuwa MWANACHAMA wenu….Mnadhani ninyi tu mna haki ya kusema mapungufu ya CCM lakini yakisemwa yenu basi inakuwa ni WIVU, MATUSI na UASI? Nasikia wewe ndio unajiona kuwa MASTER OF SPINING wa CHADEMA.Umerudia tena kutoa tuhuma kwa Mwenyekiti wa chama ambacho wewe umekuwa ukisema hapa hutaki kujiunga nacho. Halafu unajiita rafiki wa Zitto na mshauri wake wa kisiasa. Unakuwaje mshauri wa Naibu Katibu Mkuu wakati huo huo unasambaza matusi na uasi dhidi ya CHADEMA ambayo yeye anaiongoza?
Hili nakubali nilikosea. Ni kweli Muslim Hassanali amefanya kazi ya kisiasa Kigoma Kusini lakini pia Kafulila amekuwa na mchango mkubwa pia….tatizo wewe si mwanaCHADEMA kwa hiyo huijui CHADEMA. Kamwambie Zitto akueleze kuhusu CHADEMA. CHADEMA kwa kawaida wanagawana maeneo ya kukijenga chama, ndio maana unaona kuna watu wamepewa kazi ya kujenga maeneo mbalimbali na ruzuku ya chama na michango mingine inatumika kwa ajili hiyo. Zitto Kigoma Kaskazini; Kafulila na Muslim Hassanal Kigoma Kusini, Mama Kiwanga Kilombero, Benson Kibakwe, Msafiri Mtemelwa Urambo Mashariki nk. Kwa hiyo huwezi kuwalaumu viongozi wa chama kutokwenda huko kama ambavyo huwezi kuwalaumu kwa kutokwenda Kilombero. Lakini kukiwa na Operesheni za pamoja si unawasikia wanazunguka wote? Kwa hiyo Sangara ikienda Kigoma viongozi wote hao watakwenda huko Kigoma Kusini.
Tafadhali usinipeleke huko. Unajua wazi kuwa ninakujua wewe, namjua Kinabo na connection zenu wote na CHADEMA, mmefikaje huko, mnaoperate vipi na kadhalika. Kinabo alikuja na jina lake na kutoa madai yake ambayo kwangu niliona kuwa ni mwendelezo wa vita ya kimakundi dhidi ya Zitto. Kama alivyotoa madai yake na mtazamo wake nami nina haki ya kutoa madai yangu na msimamo wake. Ukitaka ushahidi hata wa kimazingira ni kunipush mimi kumwaga mchele kwenye viapanga wengi. I am not as insensitive and reckless as u r.Umemtuhumu tena mwandishi wa habari kuwa anagenge laki lenye vita dhidi ya Zitto, unaweza kutupa ushahidi wa tuhuma zako hata kama ni wa kimazingira
Hata nikukueleza siamini kama umeshafikia ukomavu wa kisiasa wa kuweza kuelewa. Natambua kuwa ni hamasa na sio dira, itikadi na mitizamo mipana na endelevu iliyokuvutia kuingia katika siasa na zaidi CHADEMA. Na huu ndio upungufu mkubwa ambao vijana wengi tunao na kushindwa kujenga aina ya siasa itakayotusaidia sisi kutekeleza wito wa kizazi chetu ambao wote tulipaswa kutilia mkazo na sio hizi petty, egoistic and selfish short term interests. .Unaweza kuyaeleza hayo maono ya mbali?
Hili na mengine ambayo nimeyaacha kwa makusudi, nakupa muda ujirudi kabla name sijachagua kufuata mkondo huo kukujibu. Jana nimewasialiana nawe kistaarabu na kuzungumza na Mnyika na viongozi wako wengine kwa undani sana. Naamini wamekutumia ujumbe. Nikirudi tena na kukuona unaendelea na haya matusi ya wazi na kuwahusisha wasio husika nami sitakutukana lakini ni wazi nitawahusisha pia watu wa karibu wako. Nakuapia kuwa sio tu itawaumiza wao bali hata chama chako kitu ambacho bado najizuia kukifanya hata katika hali mliyofikia…..Kama unadhani kwamba Zitto pekee ndio Kafara ya umaarufu wa CHADEMA nitaanza kufikiri kwamba urafiki wenu ni zaidi ya maneno unayoyaandika hapa JF, inawezekana mnaurafiki wa vitendo ambao mimi siwezi kuuingilia. Ila ushauri wangu kwako, usipende sana kumzungumzia mtu mmoja tu, na kuwaona watu wengine hawana maana duniani; hizo ni tabia za wanaume kama mabinti.
Kwa hiyo mh Zitto ameukabidhi muskakabali wake mikononi mwa mafisadi? Maana kwa kauli hii mafisadi ndio wanaoonekana kuratibu ubaadae wa Zitto.Ambacho nakijua , taarifa toka ndani ya chumba fulani cha habari katika haya magazeti ya mafisadi , ni kwamba habari ya kujiuzuru zito Imeisha pewa kichwa cha habari, wanasubiri huyo jamaa aamue kujiuzulu waijazie jazie maneno tu basi.
KABISA ...!! WATANZANIA WAMESHAUMIA VYA KUTOSHA ..KUWABEBA WATU...KUWAUNGA MKONO...MWISHO WANAWAACHA SOLEMBA!! SI VEMA.....ikiwa ni kweli kuna wazo kama hilo kwa zitto na ikiwa kweli yeye ni mpenda mageuzi itapendeza kama atahama bila kuyumbisha wananchi wa kawaida....lakini sitaki tukio la NCCR LIRUDI kwani kuna wananchi walijiapiza kuwa hawatakaa tena waunge mkono wapinzani ...kwa kuwa waliwadanganya ...wakawaunga mkono mwisho wakapewa pesa wakawakimbia ......na huo ndio umekuwa mtaji wa ccm siku zote .....kuwa WAPINZANI WANAGOMBANA NA HAWANA MSIMAMO!!....kumbukeni ya MSABAH SALUM na kisa cha kutekwa nyara....!!