JUAN MANUEL
JF-Expert Member
- Nov 26, 2010
- 6,835
- 14,213
Sijaona Cha maana ulichoeleza zaidi ya maneno Mengi kama mzaramo,Hapo vip!!
Binafsi tokea mwanzo niliamini jamuhuri wapo sahihi na ni wakweli dhidi ya Mbowe,na hii inadhihirishwa katika maeneo haya.
Kwanza upeleleze wa Kingai sio wa mchezo mchezo ni mtaalam mwenye udhoefu wa muda mrefu katika maswala ya upelelezi na hii kesi ya Mbowe upelelezi wake ni umeanza muda mrefu sana sio juzi tokea mwa 2020.
Pili, ushahidi ya wakina Mahita ni ushahidi mzito sana...ni watu ambao ni mapapa wa system kwa muda..na serikali imewaanda hawa watu kwa pesa nyingi sana na kwa muda mrefu ili waweze kuisaidia taifa.
Tatu,Tanzani ni nchi bora sana Duniani kwa upelelezi na wapelelezi ni hawa waliompeleleza Mbowe..hivyo upelelezi wao ni wakitaalamu kama majibu ya Dactari
Nne,hukumu ndogo dhidi ya kesi ya mbowe ni ushahidi tosha ya kwamba upelelezi ni wakitaalam na u.efuata sheria.
Tano..gaidi sio mpaka mtu alipue bomu au ateke watu ndio anakuwa guidi...juzi uingereza jamaa mmoja alikuwa na mikakati ya kumteka mbunge tu basi akatuhumiwa kama gaidi.
Nimalize kwa kusema acheni ushabiki wa itikadi kwenye hili..wakina Kingai na wengine hawana interest yeyote dhidi ya kesi ya mbowe bali wanamshughulikia kama muhalifu yeyote mwenye makosa.
Kama Huyo Kingai na Mahita ni makachelo waliobobea kama ulivyosema,weka CV zao tuone kama wamewahi kupata mafunzo nje,kwenye nchi kama Israel,UK,USA,au Cuba