Hospitali ya Amana: Daktari abainika kutumia Vifaa Tiba vya Serikali kutibu Wagonjwa na kujilipa binafsi

Miss Zomboko

JF-Expert Member
May 18, 2014
4,501
9,280
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Dorothy Gwajima ameagiza Daktari aliyejimilikisha hospitali ya Amana kwa lengo la kujitajirisha achukuliwe hatua kali

Daktari huyo mwenye jina kapuni amebainika kutumia Vifaa vya Hospitali hiyo ambavyo vinamilikiwa na Serikali ili kuwatibu Wagonjwa lakini malipo yote alikuwa akiyapokea binafsi

Tuhuma dhidi yake zimetolewa na Mgonjwa kwa Wizara hiyo ambaye alilipishwa laki 7 na kuhudumiwa na Nesi huku akiwa amelazwa Gesti badala ya kulazwa kwenye Wodi za Wagonjwa na wala hakuambiwa anaumwa nini

Waziri wa Afya ameagiza hatua zote za kinidhamu zifuatwe katika kumshughulikia Daktari huyo. Ametoa agizo hilo akiwa katika ziara ya kikazi Mkoani Dar es Salaam alipotembelea Hospitali ya Amana kujionea utendaji kazi.
 
Hii ni habari ya propaganda.
Imeandaliwa ili kuwahadaa wananchi waendelee kuwa mazuzu.
Hivi alilazwaje guest na kisha kulipishwa laki 7?
Alishikiwa bunduki ili alipishwe hiyo fedha?
Kama yalikuwa makubaliano yao ilikuwaje atoe malalamiko kwa wizara/Waziri?.
Mtuhumiwa jina kapuni😁😁😁😁😁.
Kwahiyo wakitaja jina wanaona watafuta ushahidi au watamdhalilisha?.
Kama fedha cash laki 7 alikuwa nazo alikubali vipi kulazwa guest house?
Je, mgonjwa wa kulazwa hospitali alijipeleka yeye mwenyewe?
Hapakuwa na ndugu waliokuwa wakija kumjulia hali?
 
Hahaha yani badala kuchunguza kwanza upate ushahidi halafu ndio utoke na habari kwa umma, yeye anatoka na habari kwa umna isiyokuwa na uhakika,kisha ndio anaagiza uchunguzi.

Kweli ccm wanejaa wajinga.

Huyu pia ni daktari na anaelewa jinsi wagonjwa tulivyo, tukishindwa kuelewana na madaktari ndio tunalalamika, kwani hakuziona hospitali zingine hadi akubali kulazwa guest house.
 
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Dorothy Gwajima ameagiza Daktari aliyejimilikisha hospitali ya Amana kwa lengo la kujitajirisha achukuliwe hatua kali

Daktari huyo mwenye jina kapuni amebainika kutumia Vifaa vya Hospitali hiyo bavyo vinamilikiwa na Serikali ili kuwatibu Wagonjwa lakini malipo yote alikuwa akiyapokea binafsi

Tuhuma dhidi yake zimetolewa na Mgonjwa kwa Wizara hiyo ambaye alilipishwa laki 7 na kuhudumiwa na Nesi huku akiwa amelazwa Gesti badala ya kulazwa kwenye Wodi za Wagonjwa na wala hakuambiwa anaumwa nini

Waziri wa Afya ameagiza hatua zote za kinidhamu zifuatwe katika kumshughulikia Daktari hiyo. Ametoa agizo hilo akiwa katika ziara ya kikazi Mkoani Dar es Salaam alipotembelea Hospitali ya Amana kujionea utendaji kazi.
Sikuamini mpaka unitajie jina la huyo mpuuzi Daktari wa Amana.
 
Hii ni habari ya propaganda.
Imeandaliwa ili kuwahadaa wananchi waendelee kuwa mazuzu.
Hivi alilazwaje guest na kisha kulipishwa laki 7?
Alishikiwa bunduki ili alipishwe hiyo fedha?
Kama yalikuwa makubaliano yao ilikuwaje atoe malalamiko kwa wizara/Waziri?.
Mtuhumiwa jina kapuni😁😁😁😁😁.
Kwahiyo wakitaja jina wanaona watafuta ushahidi au watamdhalilisha?.
Kama fedha cash laki 7 alikuwa nazo alikubali vipi kulazwa guest house?
Je, mgonjwa wa kulazwa hospitali alijipeleka yeye mwenyewe?
Hapakuwa na ndugu waliokuwa wakija kumjulia hali?
Majibu yanaweza kuwa rahisi sana katika maswali yako, kwanza tayari umeambiwa ni mfanyakazi wa wizara hivo huenda alikuwa undercover kwa maana nyingine huenda alikuwa katika uchunguzi wa kuthibitisha tuhuma za Daktari husika. Mimi swali langu ni kwa Dr husika alipataje ujasiri wa kwenda kumtibu mgonjwa clinic ktk zama hizi?
Au ndo kuonja nyama ya binadamu kwamba huwezi acha tena?
 
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Dorothy Gwajima ameagiza Daktari aliyejimilikisha hospitali ya Amana kwa lengo la kujitajirisha achukuliwe hatua kali

Daktari huyo mwenye jina kapuni amebainika kutumia Vifaa vya Hospitali hiyo bavyo vinamilikiwa na Serikali ili kuwatibu Wagonjwa lakini malipo yote alikuwa akiyapokea binafsi

Tuhuma dhidi yake zimetolewa na Mgonjwa kwa Wizara hiyo ambaye alilipishwa laki 7 na kuhudumiwa na Nesi huku akiwa amelazwa Gesti badala ya kulazwa kwenye Wodi za Wagonjwa na wala hakuambiwa anaumwa nini

Waziri wa Afya ameagiza hatua zote za kinidhamu zifuatwe katika kumshughulikia Daktari hiyo. Ametoa agizo hilo akiwa katika ziara ya kikazi Mkoani Dar es Salaam alipotembelea Hospitali ya Amana kujionea utendaji kazi.
Namshauri waziri afike Tumbi awatume tena watu wake huko wajifanye wagonjwa, hosptali unaambiwa gloves kuanzia atakazotumia Dr utakayemwona, umnunulie Gloves nesi atayekuja kukuchukuwa sampli. Yaaani shida tupu.
 
Majibu yanaweza kuwa rahisi sana katika maswali yako, kwanza tayari umeambiwa ni mfanyakazi wa wizara hivo huenda alikuwa undercover kwa maana nyingine huenda alikuwa katika uchunguzi wa kuthibitisha tuhuma za Daktari husika. Mimi swali langu ni kwa Dr husika alipataje ujasiri wa kwenda kumtibu mgonjwa clinic ktk zama hizi?
Au ndo kuonja nyama ya binadamu kwamba huwezi acha tena?

Soma vizuri, taarifa inasema "Tuhuma dhidi yake zimetolewa na Mgonjwa kwa Wizara hiyo ambaye alilipishwa..."

Hapo kuna kwa badala ya wa.
 


Kumchukulia hatua tu huyo daktari sio suluhisho la kudumu. Inabidi uchunguzi zaidi how was that possible inawezekana hiyo sio isolated case ni culture yao hapo Amana.

Weka tangazo kama kuna watu wengine washafanyiwa utaratibu huo wajitokeze, kuna vijana wengi wamehitimu mpaka leo awajapangiwa kazi useless Dr wafukuzwe tu.

Huyu mama ata sort hii wizara kuna tatizo kubwa sana supervision and control measures za HR, nurse anatokaje bila ya senior kwenye ward kujua one of the staff is missing kama sio muda wa break. Lazima ni culture ya wengi hapo Amana aliekamatwa ni mmoja tu.

Sisi watanzania tuna utamaduni mmoja wa kishamba sana kila sehemu tukifika tunachofikiria ni kupiga deals tu.
 
Kama alilazwa Gest na kupatiwa matibabu huko, huyo ahesabiki kama ni mgonjwa wa Amana Hospitali.
Kesi ya kujieleza apo ni kutumia vifaa vya hospitali ya Amana kwenda kumtibia mgonjwa wako nyumbani. Na kama hivyo vifaa vilirudishwa hospitali, hamna kesi apo ni onyo la mdomo tu asirudie tena.
 
Mgonjwa anakwenda hospitali ajapewa diagnosis yoyote ndiyo wataalamu wanavyotakiwa kufanya kazi ivyo?

Achilia mbali swala la theft kuchukua mapato ya hospitali, kutumia vifaa vyao kujipatia faida (embezzlement) na unsafe practice kutoa huduma sehemu isiyo sahihi kitendo kinachohatarisha usalama wa mgonjwa? Vipi angezidiwa usiku wa manane wakati hakuna muuguzi.
Tuache kutetea upuuzi, muhusika anatakiwa anyang’anywe practice licence na jela juu ili liwe somo kwa wengine. You can’t put patients lives at risk like that halafu uachiwe.
 
Hii ni habari ya propaganda.
Imeandaliwa ili kuwahadaa wananchi waendelee kuwa mazuzu.
Hivi alilazwaje guest na kisha kulipishwa laki 7?
Alishikiwa bunduki ili alipishwe hiyo fedha?
Kama yalikuwa makubaliano yao ilikuwaje atoe malalamiko kwa wizara/Waziri?.
Mtuhumiwa jina kapuni.
Kwahiyo wakitaja jina wanaona watafuta ushahidi au watamdhalilisha?.
Kama fedha cash laki 7 alikuwa nazo alikubali vipi kulazwa guest house?
Je, mgonjwa wa kulazwa hospitali alijipeleka yeye mwenyewe?
Hapakuwa na ndugu waliokuwa wakija kumjulia hali?

Huyu mgonjwa huenda alikuwa afusa kipenyezo!
 
Back
Top Bottom