Hospitali ya Amana: Daktari abainika kutumia Vifaa Tiba vya Serikali kutibu Wagonjwa na kujilipa binafsi

Mchawi wa Mwalimu==Mwalimu mwenyewe
Mchawi wa Dakitari== Dakitari mwenyewe
Mchawi wa Mhasibu == Fedha/Pesa/Mshiko/Talanta/Hela/mafuba

Kuna mdau kashauri kitu kizuri sana kuhusu hili sakata, waziri yupo kwenye strategic level, ni muhimu hili suala likaangaliwa kwa mapana, inawezekana ni practice nchi nzima na inawezekana kuna kisababish of which ucheleweshwaji wa malipo yaweza kuwa sababu etc. Dakitari ni kada ya mtu anayepaswa kufanya kazi bila msongo wa mawazo, nadhani wizara iliangalie hili suala ki changamoto ili ma Dakitari waweze kufanya kazi kwa ufanisi.

Nakumbuka Dkt Magufuli aliwahi kufukuza degree holders kwenye mizani baada ya hao vijana kuwa wezi sana, lakini hakukurupuka bali mfumo ulifanya kazi na kuja na suluhusho la kudumu ambapo mpaka leo mla rushwa mizani hudakwa ka digidigi kimya kimya.

Hivyo waziri waafya kafanya vizuri ila wizara iende beyond kumuwajibisha tu mhusika
 
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Dorothy Gwajima ameagiza Daktari aliyejimilikisha hospitali ya Amana kwa lengo la kujitajirisha achukuliwe hatua kali

Daktari huyo mwenye jina kapuni amebainika kutumia Vifaa vya Hospitali hiyo ambavyo vinamilikiwa na Serikali ili kuwatibu Wagonjwa lakini malipo yote alikuwa akiyapokea binafsi

Tuhuma dhidi yake zimetolewa na Mgonjwa kwa Wizara hiyo ambaye alilipishwa laki 7 na kuhudumiwa na Nesi huku akiwa amelazwa Gesti badala ya kulazwa kwenye Wodi za Wagonjwa na wala hakuambiwa anaumwa nini

Waziri wa Afya ameagiza hatua zote za kinidhamu zifuatwe katika kumshughulikia Daktari huyo. Ametoa agizo hilo akiwa katika ziara ya kikazi Mkoani Dar es Salaam alipotembelea Hospitali ya Amana kujionea utendaji kazi.
Mgonjwa alilazwa;
Mgonjwa alilazwa guest;
Mgonjwa alilipa TZS700,000;
Mgonjwa hajui anaumwa nini;
Mgonjwa alihudumiwa na nesi




But tuhuma ni za daktari⁉️⁉️⁉️⁉️⁉️⁉️
MSINICHANGANYE

ILA

HAPPY NEW YEAE
 
Mchawi wa Mwalimu==Mwalimu mwenyewe
Mchawi wa Dakitari== Dakitari mwenyewe
Mchawi wa Mhasibu == Fedha/Pesa/Mshiko/Talanta/Hela/mafuba

Kuna mdau kashauri kitu kizuri sana kuhusu hili sakata, waziri yupo kwenye strategic level, ni muhimu hili suala likaangaliwa kwa mapana, inawezekana ni practice nchi nzima na inawezekana kuna kisababish of which ucheleweshwaji wa malipo yaweza kuwa sababu etc. Dakitari ni kada ya mtu anayepaswa kufanya kazi bila msongo wa mawazo, nadhani wizara iliangalie hili suala ki changamoto ili ma Dakitari waweze kufanya kazi kwa ufanisi.

Nakumbuka Dkt Magufuli aliwahi kufukuza degree holders kwenye mizani baada ya hao vijana kuwa wezi sana, lakini hakukurupuka bali mfumo ulifanya kazi na kuja na suluhusho la kudumu ambapo mpaka leo mla rushwa mizani hudakwa ka digidigi kimya kimya.

Hivyo waziri waafya kafanya vizuri ila wizara iende beyond kumuwajibisha tu mhusika
Mchawi wa Mhasibu= TAKUKURU, PCCB, nk.
 
Soma vizuri, taarifa inasema "Tuhuma dhidi yake zimetolewa na Mgonjwa kwa Wizara hiyo ambaye alilipishwa..."

Hapo kuna kwa badala ya wa.
SOMA VIZURI JIBU LANGU, Utaelewa au google maana ya Agent undercover huenda nimetumia maneno ambayo huelewi yanawakilisha nini, Majibu yanaweza kuwa rahisi sana katika maswali yako, kwanza tayari umeambiwa ni mfanyakazi wa wizara hivo huenda alikuwa undercover kwa maana nyingine huenda alikuwa katika uchunguzi wa kuthibitisha tuhuma za Daktari husika
 
SOMA VIZURI JIBU LANGU, Utaelewa au google maana ya Agent undercover huenda nimetumia maneno ambayo huelewi yanawakilisha nini, Majibu yanaweza kuwa rahisi sana katika maswali yako, kwanza tayari umeambiwa ni mfanyakazi wa wizara hivo huenda alikuwa undercover kwa maana nyingine huenda alikuwa katika uchunguzi wa kuthibitisha tuhuma za Daktari husika

Hakuna mahali ilipoandikwa kwamba ni mfanyakazi wa wizara.
 
Hii ni habari ya propaganda.
Imeandaliwa ili kuwahadaa wananchi waendelee kuwa mazuzu.
Hivi alilazwaje guest na kisha kulipishwa laki 7?
Alishikiwa bunduki ili alipishwe hiyo fedha?
Kama yalikuwa makubaliano yao ilikuwaje atoe malalamiko kwa wizara/Waziri?.
Mtuhumiwa jina kapuni😁😁😁😁😁.
Kwahiyo wakitaja jina wanaona watafuta ushahidi au watamdhalilisha?.
Kama fedha cash laki 7 alikuwa nazo alikubali vipi kulazwa guest house?
Je, mgonjwa wa kulazwa hospitali alijipeleka yeye mwenyewe?
Hapakuwa na ndugu waliokuwa wakija kumjulia hali?
Logical questions
 
Majibu yanaweza kuwa rahisi sana katika maswali yako, kwanza tayari umeambiwa ni mfanyakazi wa wizara hivo huenda alikuwa undercover kwa maana nyingine huenda alikuwa katika uchunguzi wa kuthibitisha tuhuma za Daktari husika. Mimi swali langu ni kwa Dr husika alipataje ujasiri wa kwenda kumtibu mgonjwa clinic ktk zama hizi?
Au ndo kuonja nyama ya binadamu kwamba huwezi acha tena?
Majibu marahisi wakati huna majibu, umeandika huenda, huo ni mtazamo wako Wala sio uhalisia.
 
Hivi kiswahili ni kigumu sana? sijasema majibu ni marahisi nimesema yanaweza kuwa, narudia tena yanaweza kuwa....
Sasa marahisi vipi huku unaweka huenda??? Hiii sentensi yako umeweka neno huenda, ikimaanisha hauna uhakika, ingekuwa rahisi ungesema moja moja ni hivi na siyo huenda
 
Namshauri waziri afike Tumbi awatume tena watu wake huko wajifanye wagonjwa, hosptali unaambiwa gloves kuanzia atakazotumia Dr utakayemwona, umnunulie Gloves nesi atayekuja kukuchukuwa sampli. Yaaani shida tupu.

Ndugu, hiyo ni kwa sababu Serikali ya Magufuli kwa karibia miaka miwili mfululizo haikupeleka fedha za ununuzi wa dawa, vifaa tiba na vitendanishi huko mahospitalini.

Hivyo, badala ya yeye kwenda kukemea hilo, apeleke kwanza hizo fedha
 
Sasa marahisi vipi huku unaweka huenda??? Hiii sentensi yako umeweka neno huenda, ikimaanisha hauna uhakika, ingekuwa rahisi ungesema moja moja ni hivi na siyo huenda
Nilidhani unaweza ukaelewa kwamba hapa ni jukwaa na hakuna mwenye majibu ya moja kwa moja bali maoni, anayeweza kuwa na majibu ni Dr na mgonjwa wake. Jiulize ailyetibiwa guest ni mfanyakazi wa wizara ya afya, aliyekuwa anamtibu ni Dr ambaye pia ni mwajiliwa wizara afya. Hebu tafakari kidogo alafu rudia kusoma post yangu utaelewa kitu
 
Mhalifu Jina kapuni.
Huyu waziri namuona kafeli kabla hata hajaanza.
Too much noise!!!
Inabidi Mambosasa akalifanyie kazi maana toka lini utangaze uhalifu wa mtu huku jina lake unalificha.Wapi na wapi bana,Hawa akina Gwajima hawa ,mh! Ngoja twende tutajua mbele ya safari.
 
Back
Top Bottom