Hoja binafsi: Vyama vya siasa viwe makini sana kwenye uteuzi wa wagombea wenza katika chaguzi zijazo ama sivyo Katiba imulikwe

Wasalaam wakuu,

Hili ni wazo langu tu kwaajili ya kuleta afya ya kiuongozi kwa Tanzania yetu ili kupunguza hatari za kiuongozi zinazoweza kutokea na nchi kujikuta ikiangukia kwenye mikono ya watu ambao hawakujiandaa kuwa kwenye nafasi fulani fulani za kiuongozi.

Katiba yetu iko wazi jinsi madaraka yanavyoweza kubadilika ikiwa kitatokea chochote wakati wowote.

Hivyo basi ni muhimu sasa kwa vyama vya siasa viweke umakini mkubwa kwenye uteuzi wa wagombea wenza ili tuhakikishe watu wanao patikana tuwe na uhakika na uwezo wao kwenye nafasi kubwa kama hiyo pindi itakapotokea dharura yoyote ile tusiteteleke kiutawala.

Ni ukweli ulio wazi kuwa vyama vya siasa mara nyingi sana vimekuwa vikifanya mizaha kwenye uteuzi wa wagombea wenza bila ya kuangalia kwa makini takwa la kikatiba kuwa watu hao wanaweza kuja kuwa wakuu wa nchi siku moja.

Wagombea wenza limeonekana Kama suala dogo sana lisilo na uzito wowote na maranyingi limechukiliwa kirafiki na kishikaji sana bila kujali madhara yake.

Rejea uchaguzi wa 2020 angalia wagombea wenza wote kwenye vyama vyote kisha angalia katiba yetu inasemaje ndipo utagundua mzaha tunao ufanya Watanzania.

Mungu tusaidie waja wako, kama ugombea wenza ni ushkaji basi tuimulike Katiba kwenye vipengele fulani.
kwahiyo unataka kusema Mama hafai.

Pro-Magufulism mnateseka sana
 
Ni kweli bro.
Ile seriousness inayotumika kumpata running mate wa mgombea uraisi waTanzania IPO kimdhaa kimdhaa. tofauti na umakini unaotumika kumpata rais wa Zanzibar.

Kuna ule upofu kwamba rais ni MKUU mno na hafagi njiani, na hanaga record hiyo..

kwahivyo mgombea mwenza ni sub tu wa kuridhidhisha kanuni.
Ni sub ambayo Mara nyingi haina matumizi kama ya kipa.

Ni kama leo tunavyoona ugumu ulioje Philip mpango kuwa rais kabla ya 2025.
Hili lipo kwa vyama vyote.
Hoja hapa sio kubeza wagombea mwenza waliopitishwa na vyama vyao.ila ni kuvikumbusha kuweka attention kubwa kwny nafasi hizi.

Kuna mwaka CCM. Baada ya kuona gharib bilal ana nguvu na ushawishi MKUBWA Zanzibar wakati wao tayari walikuwa wana jina lao mfukoni (Shein)
Wakaona ni heri Bilal apozwe kuwa mgombea mwenza na baadae kuwa makamu Wa Rais, kuliko bilal kuwa raisi kule.

Likewise, heri Maalim self (now late) awe makamu wa kwanza na sio wa pili,
wakiamini umakamu wa pili ni ukubwa Wa geresha.
 
Ni kweli; hata mimi nimeshaona tatizo la kikatiba hata. Ile katiba ya zamani ilikuwa inasema rais akifa, basi uchaguzi mwingine mdogo wa rais unafanyika kujaza nafasi yake kama ambavyo anapokufa mbunge nafasi yake inajazwa kwa uchaguzi mdogo wa bunge.

Mabadiliko ya kusema makamu wa rais anakuwa automatic rais na akishachukua madaraka anafanya lolote atakalo ikiwa ni pamoja na kupangua serikali aliyokuta linaweza kuwa na unintended consequences kwa mustkhabali wa nchi. Inabidi katiba ingaliwe upya namna ya kurithisha kiti cha uraisi aliyefariki na kuongeza checks and balances zaidi kwa mrithi wa kiti hicho. Njia rahisi sana ni ile ya kuundwa kwa kamati ya urais itakaokuwa inaongozwa na aliyekuwa Makamu wa rais kabla ya kifo cha rais; kamati hii uhai wake utakwisha baada ya uchaguzi mkuu unaofuata. Halafu rais aliyerithi asiwe na power zote za rais aliyechaguliwa; sehemu ya powers za rais aliyechaguliwa ziwe mikononi mwa kamati hii. Utaratibu huu utapunguiza kidogo tamaa ya madaraka kwa makamu wa rais.

Kusema tu kuwa waliaminiana wakati wa uchaguzi siyo hoja kabisa, binadamu huamini wenzao walio hai tu, baada ya vifo husahauliana kabisa. Kesi hii ya kifo cha Magufuli imeonyesha tafsiri hiyo kwa uwazi sana tena kwa muda mfupi sana. Ndani ya mwezi mmoja tu wa kifo chake, mkataba wa bandari ya Bagamoyo uliopingwa na magufuli unaaza kujadiliwa tena!
Nchi iongozwe na kamati ?
 
Mkuu kwenye hili nimecheka sana. Hivi tulipoungana haikujulikana ukubwa wa eneo la Zanzibar? Au ndiyo ile dhana ya kuitawala ili isifurukute? au ndio mbadala wa kutupwa kwenye bahari ya Hindi? Waswahili husema ukipenda boga, penda na mti wake. Hata hivyo mama yupo, ni Raisi kikatiba na ataendelea kuwepo mpaka muda wa kuondoka utakapofika.
Zanzibar ni koloni la Tanzania bara kwa mustakabali wa usalama wa Tanzania bara.

Hivyo makoloni ya sasa hayakaliwi kwa nguvu bali kwa akili na maarifa mengi.

Ni watanzania wajinga tu ndiyo watakuwa tayari kuachia Zanzibar ijitawale.
 
Ni kweli vyama vyote vilikuwa vinadharau sana juu ya hili kwa kuchagua wagombea wenza incompetent. Ila kwa hili lililotokea naamini litakuwa no funzo tosha.
Mgombea mwenza yupi ambaye alikuwa ni incompetent kwenye chaguzi zote ?

2015 wagombea urais ndiyo walikuwa incompetent kuliko wagombea wenza.
 
Mwacheni Samia afanye kazi. Mwendazake alichaguliwa na watu ila Samia kaletwa na MUNGU.

Na siku zote penye ukweli uongo hujitenga!
Dhalimu alichaguliwa na watu ama vyombo vya dola na tume ya uchaguzi?
 
Nahisi kuna fundisho watakuwa wamelipata hao wanaochagua wagombea wenza, hili la sasa lililotokea itakuwa kama CASE STUDY.

Miaka mingi wagombea wenza walichukuliwa kama watu ambao majukumu yao yanaishia kwenye KERO ZA MUUNGANO na mambo ya MAZINGIRA tu na watu waliopoa(Shein,Gharibu,Ali Jumaa) sana.
 
Mnapochagua Mgombea mwenza mjue ya kwamba Raisi akifariki yeye ndio anashika nafasi ya Uraisi .kwa hio mara ingine mjue mnachagua mtu ambe yupo tayari kushika na kuongoza nchi kuliko kuongozwa.ata sijui kama nimefahamika ,maana watanganyika wagumu kufahamu.
Nadhani sasa tushapata funzo kubwa sana Kama nchi tabia ya kuweka weka watu kisa tu kutimiza kanuni au huruma na kuwapa watu fulani kipaombele nadhani sasa itaishia hapa
 
Back
Top Bottom