Watanzania tutaendelea kusubiri mpaka lini Bunge likitunga Sheria batili na kuuchomekea ubatili huo ndani ya Katiba yetu? Tufanye nini?

Pascal Mayalla

Platinum Member
Sep 22, 2008
50,502
113,610
Wanabodi,
Kama kawaida yangu kila nipatapo fursa huja na makala zangu elimishi za Kwa Maslahi ya Taifa, ambazo zinachapishwa kwenye gazeti la Nipashe kila siku za Jumapili.

Leo naendelea na sehemu nyingine ya Ijue Katiba ya JMT kwa jicho la mtunga katiba. Sehemu ya kwanza nilifundisha katiba ni nini na katiba ni ya nani Ijue Katiba ya JMT Kwa Jicho la Mtunga Katiba: Watanzania Tusishabikie Uhaini!. Hukuna Uhaini wa Kauli na Maneno, Uhaini ni Mipango na Matendo!.
Sehemu ya pili nikazungumzia Mtunga katiba alimaanisha nini aliposema Katiba ni Sheria Mama Ijue Katiba kwa Jicho la Mtunga Katiba: Mtunga Katiba alimaanisha nini aliposema "Katiba ni Sheria Mama"? Ni kweli Katiba ni Sheria Mama? leo nazungumzia jinsi Bunge letu Tukufu, linavyotunga sheria batili zinakwenda kinyume cha katiba na nyingine sio tuu Bunge letu limetunga sheria batili, bali ubatili huo ukachomekewa (kiubatili) mpaka ndani ya katiba yetu ya JMT ya mwaka 1977 ndio maana hitaji la katiba mpya ni hitaji very bonafide genuine kwa Watanzania kuweza kusonga mbele kimaendeleo kwa kuwapata viongozi able people wenye uwezo, ability, capacity and capability ya kututoa hapa tulipo na kutufikisha kule tulipaswa kuwepo kama Singapore, Taiwan, Malaysia, Indonesia, ambazo tulipata nazo uhuru wakati mmoja, sisi tukiwa with everything wao wakiwa with nothing!, lakini angalia leo wenzetu walipo compared na sisi tulipo!, the magic is, the right people and the right strategies, hatua ya kwanza is to get the right people!.

Bandiko hili ni la swali

Watanzania tutaendelea kusubiria mpaka lini wakati Bunge letu Tukufu likitunga Sheria batili na sometimes kuuchomekea ubatili huo hadi ndani ya Katiba yetu na kuifanya katiba yetu kuwa na vipengele batili?. Je Watanzania tufanye nini?, au tunaweza kulifanya nini Bunge la aina hii?.​


Sii wengi wanafahamu Bunge letu Tukufu linaporidhia mkataba wowote wa kimataifa, mfano ile IGA ya ajabu ajabu ya DPW, maana yake hicho kilichoridhiwa kwenye huo mkataba ulioridhiwa na Bunge, kinakuwa ni sehemu ya sheria zetu za ndani, under local laws!. Ina maana Bunge ni linatunga sheria zetu za ndani kupitia miswada ya sheria inayoletwa bungeni na kupitishwa kuwa sheria, na Bunge linaporidhia mikataba ya kimataifa, maana yake ni Tanzania tume imports sheria hizo za nje na kuzi domesticate kuwa ni sheria za ndani, hivyo hivi tunapozungumza ile IGA ya DPW na Bandari zetu ni sheria yetu halali!.

Kwa mujibu wa sheria yetu ya Rasilimali za Taifa, ile IGA ya DPW na Bandari zetu ni batili!, lakini kwa mujibu wa katiba yetu, mamlaka pekee ya kutangaza ubatili wa katiba au sheria yoyote ni Mahakama Kuu ya JMT. Mahakama Kuu imeibariki IGA ile licha ya mapungufu yote ya kisheria ya ile IGA.

Kuna upungufu mmoja mkubwa ambao hakutajwa sana, huu ni upungufu wa illegality. IGA ile ya DPW na Bandari zetu, ina illegalities mbili.
Ya kwanza ni illegality ya the capacity of Dubai to contract an international Treaty, kwasababu Dubai sio nchi, haina sovereignty hivyo haina the capacity to enter into an international Treaty with a nation kama Tanzania, mwenye uwezo huo ni UAE tuu na hakukuwa na POA (power of attorney) kutoka UAE kuiwezesha Dubai kuingia an international Treaty!.

Illegality ya pili, mkataba ule una kipengele kilicho kinyume cha sheria zetu, hivyo it's an illegal contract, lakini Bunge letu Tukufu limeipitisha hivyo hivyo.
Hii sii mara ya kwanza kwa Bunge letu kutufanyia mambo ya ajabu kama haya!.

Leo naomba niwaletee mifano Bunge letu Tukufu kutunga sheria batili inayokwenda kinyume cha katiba ya JMT. Kwa kuonyesha Katiba inasema nini, hiyo sheria batili ikasema nini, na mwisho kuonyesha sheria batili hiyo, imekinzana wapi na katiba ya JMT.

Kama wewe sio mpenzi wa kusoma mambo marefu na huna interest na kujua vifungu vya katiba na sheria, unaweza ku skip sehemu hii, ukaibukia kule kwa Mchungaji Mtikila
  1. Tuanze na Ibara ya 5 ya katiba ya JMT inasema
1694164010500.png

Haki hii ndio haki kuu ya kwanza ya kidemokrasia, haki ya kupiga kura, japo haki hii bado ipo kwenye katiba yetu, haki hii imeingiliwa na kukiukwa na ukosekanaji wa haki ya kuchaguliwa, hivyo Watanzania kuruhusiwa kuwachagua sio viongozi wao wanaowapenda kwa uhuru, bali Watanzania wanalazimika kuwachagua viongozi waliopitishwa na wahuni fulani (kudhaminiwa na chama cha siasa), hivyo ni kukiuka nia njema ya mtunga katiba ya kila Mtanzania anakuwa na haki ya kupiga kura kuchagua kiongozi anamtaka kwa Tanzania ni kumchagua kiongozi chama kilicho wachagulia!.

2. Ibara ya 5 (2) inalipa Bunge mamlaka ya kutunga sheria kuzuia mtu kupiga kura
1694165480986.png

Haki hii ya uhuru wa kupiga kura kuchagua ni moja ya haki zinazoitwa fundamental rights, yaani haki za msingi za binadamu.

3. Ibara ya 3 imelipa Bunge la JMT, mamlaka ya kutunga sheria ya uchaguzi
1694165980211.png

Mamlaka haya ya Bunge kutunga sheria ya uchaguzi pia limewekewa masharti, hivyo Bunge halina mamlaka ya kutunga sheria inayokwenda kinyume cha katiba.

Kisha tuje ibara ya 21 ya katiba ya JMT
1694173404805.png

Tuje ibara ya 39 ya katiba ya JMT.
1694173650041.png

Tumalizie Ibara ya 67 ya Katiba ya JMT
1694174067043.png

Baada ya kukuwekea vifungu, sasa twende taratibu nikuchambulie
Ibara ya 5 ni haki ya kupiga kura kwa kila Mtanzania aliyetimiza umri wa miaka 18. Ili haki hii iwe na maana, Mtanzania huyu anapaswa kuwa huru kumchagua kiongozi yoyote anayemtaka. Lakini kwa Tanzania haki hii inabaguliwa, Watanzania wanalazimishwa kuwachagua wanachama tuu wa vyama vya siasa ambayo ni kinyume cha Ibara ya 11!.
Ibara hii ya 21 cha Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, inatoa haki ya kila Mtanzania mwenye sifa, kuwa huru kushiriki katika siasa na uongozi kuanzia serikali za mtaa hadi serikali kuu, bila ubaguzi wowote.
Uhuru wa kushiriki shughuli za umma
21.-(1) Bila ya kuathiri masharti ya ibara ya 5, ya Katiba hii na ya sheria za nchi kuhusiana na masharti ya kuchagua na kuchaguliwa, au kuteua na kuteuliwa kushiriki katika shughuli za utawala wa nchi, kila raia wa Jamhuri ya Muungano anayo haki ya kushiriki katika shughuli za utawala wa nchi, ama moja kwa moja au kwa kupitia wawakilishi waliochaguliwa na wananchi kwa hiari yao, kwa kuzingatia utaratibu uliowekwa na sheria au kwa mujibu wa sheria.


Lakini kukafanyika uhuni fulani kwa maslahi ya watu fulani na chama fulani kwa vile serikali ni yao, wakaipindua katiba kwa kuinyofoa haki hiyo ya kila mtu kushiriki siasa, iliyotolewa na katiba, na kupachika shurti la kudhaminiwa na chama cha siasa hivyo kujenga ubaguzi katika kushiriki shughuli za uongozi wa umma kwa watu kulazimishwa kwanza kujiunga na vyama vya siasa, ndipo upate haki ya kugombee nafasi yoyote ya uongozi wa umma, huku sio kuwatendea haki Watanzania wengine wote, wasiotaka kujiunga na vyama vyovyote vya siasa, kutokana na kuviona karibu vyama vyote ni vyama vya hovyo hovyo, isipokuwa chama kimoja, lakini kuna watu wazuri na wana uwezo mkubwa wa uongozi, hawawezi kugombea uongozi kwasababu ya ujinga huo!. Shurti hili la kudhaminiwa na chama cha siasa ni kinyume cha Ibara ya 11 ya katiba ya JMT ya mwaka 1977!.

Hii ni haki muhimu iliyotolewa na katiba, kitendo cha kuingiza shurti la kudhaminiwa na chama cha siasa ni kinyume cha katiba. Hivyo sheria hii ibadilishwe ili kukidhi kile ambacho mtunga katiba ilidhamiria ilipoiweka haki hii, ndani ya katiba yetu!, hivyo baada ya mabadiliko hayo ya mlango wa nyuma, kipengele hicho sasa kinasomeka hivi

Uhuru wa kushiriki shughuli za umma Sheria ya 1984 Na.15 ib.6 Sheria ya 1994 Na.34 ya ib.4
21.-(1) Bila ya kuathiri masharti ya ibara ya 5, ya 39 na ya 67 ya Katiba hii na ya sheria za nchi kuhusiana na masharti ya kuchagua na kuchaguliwa, au kuteua na kuteuliwa kushiriki katika shughuli za utawala wa nchi, kila raia wa Jamhuri ya Muungano anayo haki ya kushiriki katika shughuli za utawala wa nchi, ama moja kwa moja au kwa kupitia wawakilishi waliochaguliwa na wananchi kwa hiari yao, kwa kuzingatia utaratibu uliowekwa na sheria au kwa mujibu wa sheria.


Ule uhuru uliotolewa na Katiba wa kila mtu kuwa huru kushiriki shughuli za uongozi, kupitia ibara ya 21, umekuja kunyofolewa na ibara ya 39 na 67 (b)(c) kwa kuweka sherti, ili mtu kuweza kugombea nafasi yoyote ya uongozi wa umma, ni lazima awe ni mwanachama, na mgombea aliyependekezwa na chama cha siasa hivyo lazima adhaminiwe na chama cha siasa!, Haki zinatolewa na ibara moja halafu zinaporwa na ibara nyingine ya katiba hiyo hiyo!.

Mchungaji Mtikila (Mungu amuweke mahala pema peponi), mwaka 1993, alifungua kesi No. 5 ya 1993, alifanya juhudi kubwa kukipinga kifungu hiki na Mahakama Kuu kupitia kwa Jaji Lugakingira, (Mungu amuweke mahala pema peponi), ikatamka wazi na bayana kipengele hicho ni batili na kinakiuka katiba ya JMT ya mwaka 1977, hivyo kifutwe, na kutoa haki kwa kila Mtanzania ana haki ya kushiriki kugombea Uongozi wowote wa nchi.

Baada tuu ya Mtikila kushinda kesi serikali ikafanya mambo mawili makubwa ya ajabu!, kwanza ilikata rufaa!. Hivi kwa uamuzi kama huu, serikali ilikata rufaa kwa maslahi ya nani?. Wiki iliyopita nilisema ile Ibara ya 64(5) iayotamka Katiba ni sheria Mama, sheria nyingine yoyote inayokwenda kinyume cha katiba ni batili, aliyebatilisha sheria batili ni katiba yenyewe na sio Mahakama!. Kazi ya Mahakama ni kutamka tuu huo ubatili na tangu baada ya tamko hilo, sheria hiyo inakuwa tayari ni imebatika!, unawezaje kukata rufaa kwa kitu kilicho batilishwa na katiba?. Kiukweli kabisa hili ni jambo la ajabu sana!.

Jambo la pili la ajabu sana na kubwa ya mwaka ni serikali yetu ilipeleka bungeni kwa hati ya dharura, sheria No. 34 ya mwaka 1994, kufanya marekebisho ya 8 ya Katiba ya JMT na kukichomeka kipengele hicho ndani ya katiba, hivyo kuibatilisha ile hukumu ya Jaji Lugakingira!. Hapa ndipo ujinga unapoanzia katika siasa zetu kwa serikali kufanya kazi kwa maslahi ya kisiasa ya watu fulani na chama fulani, hivyo kupoteza haki ya wengi kwa ajili ya kuwanufaisha wachache!..

Hiki kilichofanyika, mimi nakiita ni kitendo cha kihuni!, Watanzania tulifanyiwa uhuni na serikali yetu, kwa kuinajisi katiba yetu!, kitu kimeelezwa ni kinyume cha katiba, kinatoa haki zilizotolewa na katiba, halafu serikali hiyo inakuja kuihalalisha haramu hiyo kwa kuiingiza rasmi kwenye katiba!, huku sii kuinajisi katiba yetu?. Uhuni huu ulifanywa na awamu zilizopita, lakini kitu cha ajabu ni serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Samia, inataka kuurudia uhuni huu!, nimeshauri kwa vile ni sio kosa la awamu ya Rais Samia, hivyo kosa lililofanyika sio kosa kwasababu watendaji waliofanya hayo hawakujua kuwa ni makosa, kutenda kosa bila kujua ni kosa, sii kosa, kosa ni kurudia kosa Kufanya Kosa, Si Kosa, Kosa Kurudia Kosa!. Sheria ya Uchaguzi ni Kosa!, Kwanini Tunarudia Kosa?!. Haki Sii Hisani ni Stahiki!. Bunge Tutendeeni Haki!
Mchungaji Mtikila, licha ya kuwa ni mwanasiasa, Mwenyekiti wa chama cha siasa cha DP, (Democratic Party), lakini alikuwa ni mtu wa Mungu kiukweli kabisa, kwa sababu hakukubali kabisa katiba yetu inajisiwe!, hivyo akafungua kesi nyingine No. 10 ya mwaka 2009 kupinga marekebisho hayo ya 8 ya katiba na kuyaita ni ubatili!.

Kwa vile mimi ni Mtanzania na nawafahamu vizuri Watanzania walio wengi hawako deep kusoma makitu marefu, hivyo kwa wale wa short and clear mnaweza kuishia hapa and jump kwenye A way forward na conclusions, wale wa deep tuendeleeni

Katika kesi hiyo, Mchungaji Mtikila aliomba mambo mawili makuu
mambo hayo ni

(a) Mahakama itamke ibara 39 na 67 za katiba zilizorekebishwa na marekebisho ya 8 kwa sharia No. 34 ya mwaka 1994, ni batili na kinyume cha katiba.

(b) Kutamka wazi kuwa Kila Mtanzania ana haki ya kugombea kwa mujibu wa ibara ya 21 ya Katiba, bila kulazimishwa kudhaminiwa na chama cha siasa, hivyo mtu anaweza kugombea kama mgombea binafsi.

Mahakama Kuu chini ya majaji watatu, (majaji watatu kisheria inaitwa Half Bench), Manento, Masati na Mihayo, wakayakubali mambo yote ya Mchungaji Mtikila na kumpa ushindi tena kwa kutamka marekebisho hayo ya katiba ni batili!. Lakini serikali yetu ilivyo ya ajabu, ikakata tena rufaa, na safari hii Mahakama Kuu ikakaa Full Bench ya majaji 7, chini ya Jaji Mkuu Mwenyewe, Agustino Ramadhani, akisaidiwa na Jaji Eusebio Munuo, Jaji January Msoffe, Jaji Natalia Kimaro, Jaji Kassim Mbarouk, Jaji Benard Luanda, na Jaji Sauda Mjasir, ambapo tarehe 17 mwezi June, mwaka 2010 ikatoa hukumu ya ajabu kabisa kuwa kutokea Tanzania!.

Tena Mahakama ya rufaa haikuwa peke yake, bali iliwaita mabinga wabobezi na wabobevu wa sheria na katiba kuisaidia, hawa wanaitwa marafiki wa mahakama, kwa kiingereza ni friends of the Court, kisheria wanaitwa Amicus Curiae, hivyo ma Amicus Curiae hawa, Mr. Othman Masoud, Prof. Palamagamba Kabudi, na Prof.Jwan Mwaikusa(Mungu Aiweke Roho yake Mahala Pema Peponi).

Uamuzi wa Mahakama Kuu ya Rufaa uliamua kitu cha ajabu sana na hapa naomba kunukuu
“So as to let the will of the people prevail as to whether or not such [independent] candidates are suitable. We are definite that the Courts are not the custodian of the will of the people. That is the property of elected Members of Parliament”.

Hii kiukweli ni kauli ya ajabu sana kutolewa na mahakama yetu kwenye jambo zito na muhimu kama hili!. Kitendo cha Mahakama kujivua jukumu la kuwa the custodian of the will of the people!, ni kitendo cha ajabu sana na kushangaza sana!. Hakuna will of the people kubwa kuliko katiba!, kama katiba imetoa haki fulani, halafu Bunge likatunga sheria ya ajabu kabisa kuifuta haki hiyo, halafu mahakama ikatamka haiwezi kuliingilia Bunge!, where is the doctrine of separation of powers, checks and balance?!.

Kwa ajili ya kulinda heshima ya Mahakama Kuu, naomba niweke ilichokisema bila kukitafsiri.

“In our case, we say that the issue of independent candidates has to be settled by Parliament which has the jurisdiction to amend the Constitution and not the Courts which, as we have found, do not have that jurisdiction. The decision on whether or not to introduce independent candidates depends on the social needs of each State based on its historical reality. Thus the issue of independent candidates is political and not legal However, we give a word of advice to both the Attorney General and our Parliament: The United Nations Human Rights Committee, in paragraph 21 of its General Comment No. 25, of July 12, 1996, said as follows on Article 25 of the International Covenant on Civil and Political Rights, very similarly worded as Art 23 of the American Convention and our Art 21: The right of persons to stand for election should not be limited unreasonably by requiring candidates to be members of
parties or of specific parties. Tanzania is known for our good record on human rights and particularly our militancy for the right to self determination and hence our involvement in the liberation struggle. We should seriously ponder that comment from a Committee of the United Nations, that is, the whole world.
DATED at DAR ES SALAAM this 17th day of June, 2010”


Mahakama ya Rufaa ikaamua kuwa Mahakama haina mamlaka ya kuliingilia Bunge, katika vipengele vya katiba, kumaanisha kwa vile marekebisho hayo ya 8 yamefanywa na Bunge, hivyo ni Bunge ndio lirekebishe kipengele hicho!, kiukweli kabisa, kwa maoni yangu, uamuzi huu sio utii wa mhimili wa Mahakama kwa mhimili Bunge, bali huu ni ukondoo wa hali ya juu kwa Mhimili wa Mahakama kwa serikali kwa manufaa ya watu wachache!.

Uchaguzi wa Mwaka 2015 ukalithibitisha hili, kumbe baadhi ya majaji wetu ni makada!, Jaji Mkuu Mstaafu aliyeongoza jopo hilo, alichukua fomu kugombea urais!, for what my God?!. Baadhi ya wale ma amicus curiae naamini tunawajua na tunawaona na ukada wao!. Unategemea nini kama sheria za nchi hii zitafinyangwa finyangwa kwa manufaa ya wachache?!. President Samia must stop this nonsense!.

Japo Lengo la Kudhaminiwa na Chama ni zuri, ila Huu Sii Ujinga Tuu?!.
Katiba ilisema kila Mtanzania ana haki ya kushiriki uongozi, hili sherti la kudhaminiwa na chama lilitoka wapi? na kwa kwa nini watu walazimishwe kuwa wanachama wa vyama ili wadhaminiwe, ndipo waweze kugombea?. Mfano mimi, sina chama kwa sababu naziona siasa za vyama ni za hovyo hovyo, ikitokea nina uwezo wa kuwatumikia wananchi wa eneo langu na kuwaletea maendeleo bila kupitia chama chochote, kwa nini nizuiliwe?!. Kiukweli kabisa, kwa maoni yangu, huu ni ujinga uliopitiliza!, tutaliacha Bunge letu Tukufu kutufanyia ujinga huu mpaka lini?, is this not nonsense?.

Watanzania tusikubali ujinga huu uendelee hadi 2025!, tupiganie milango ya wagombea binafsi ifunguliwe kabla ya, 2025, ili watu wenye nia ya kugombea, na wana uwezo wa kuwaletea wananchi maendeleo, bila kupitia hizi nonsense za vyama waingie, washindane kwa hoja na sio kushindana kuhonga, kama hali inavyoendelea sasa!. Hili shurti la vyama lingekuwa limendolewa, mngeweza kushangaa watu wazalendo wa kweli wa nchi hii, kama kina Reginald Mengi, Ali Mfuruki, Yogesh Manek, SS Bakhresa, Pascal Mayalla, and the like, wenye uchungu wa dhati na umasikini wa taifa hili, wangejitokeza kugombea kuwatumikia wananchi!.

Kiongozi Akiishachaguliwa, Anakuwa ni Kiongozi wa Watu, na Sio Kiongozi wa Chama, Kwa Sababu Anachaguliwa na Watu na Sio Chama!.
Kiukweli kwenye hili jambo, kuna ujinga mwingi!, ujinga mwingine mkubwa kabisa ni huu, hata kama mgombea amedhaminiwa na chama cha siasa kugombea, akiishapitishwa na Tume ya Uchaguzi kuwa Mgombea, japo anatambulika kama ni mgombea wa chama fulani, lakini akiishachaguliwa, mwenyekiti wa mtaa, diwani, mbunge au rais, anakuwa sio kiongozi tena wa chama kilichomdhamini, bali sasa anakuwa ni kiongozi wa umma, kiongozi wa wananchi. Mfano baada ya rais Magufuli kuchaguliwa kuwa rais kwa tiketi ya CCM, lakini hakuchaguliwa na wana CCM pekee, amechaguliwa na Watanzania wote, yeye anakuwa sio kiongozi wa CCM bali kiongozi wa Watanzania wote, vivyo hivyo kwa wabunge, madiwani na viongozi wa serikali ya mtaa, kitendo cha mtu ambaye ni kiungozi wa umma, kujitoa chama na kupoteza ubunge, udiwani au uongozi wa umma, ni ujinga ambao haupaswi kuvumiliwa. Nini muhimu kati ya umma na chama?. Kuukosesha umma kiongozi wao waliemchagua kwa sababu za chama, sio tuu sio haki kwa wananchi waliomchagua, bali pia ni dhambi, kuwalipisha masikini hawa gharama za uchaguzi wa marudio kwa sababu za kijinga!.
Nini Kifanyike, A Way Forward.
Kama nilivyowahi kushauri humu, ukosoaji wenye kujenga, huandamana na ushauri wa nini kifanyike kurekebisha kasoro hizi ili kuundoa ujinga huu unaoendelea nchini mwetu kwa sasa kwa viongozi wa umma kuhama vyama na kupoteza uongozi wa umma.
  1. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amirati Jeshi Mkuu, Samia Suluhu Hassan asiruhusu ule ujinga wa kuhama vyama unaosababisha hasara kwa taifa, kwa kuwashukuru kumuunga mkono na kuunga mkono juhudi zake, lakini wabaki huko huko kwenye vyama vyao, hadi 2025, wakiishamaliza muhula wao, ndipo wajitoe na kuhama vyama!.
  2. Ikulu ni mahali patakatifu, Rais wa Nchi, akiwa Ikulu yetu, atenganisha kofia zake mbili za rais wa nchi na Mwenyekiti wa chama cha CCM, rais wetu akiwa Ikulu yetu afanye kazi takatifu, asiendeshee vikao vya CCM, pale patakatifu petu, vikao vya CCM akavifanyie ofisi ya CCM Lumumba au kumbi za CCM Dodoma. Japo hakuna kosa lolote kuendeshea vikao vya CCM Ikulu yetu, lakini halileti picha nzuri kwa rais wetu, ambaye ni mpenda haki, kwa sababu yeye sio rais wa CCM ni rais wa Watanzania wote!.
  3. Tubadili sheria yetu ya uchaguzi, kwa kufuta chaguzi zote ndogo, na tuanzishe utaratibu wa proportional representation kwa mwenye kura nyingi ndiye mshindi, lakini likitokea lolote, akasita kuwa rais, kwa rais tunaye VP, kwa mbunge au diwani, yule aliyemfuatia kwa kura katika uchaguzi uliopita ndio anatangazwa mbunge, kama alipata zaidi ya 10% ya kura zote, kama hayupo aliyefikia asilimia hizo, ndipo uchaguzi mdogo unafanyika.
  4. Kile kipengele cha kudhaminiwa na chama kiishie kwenye uteuzi tuu, kiongozi akiishachaguliwa, anakuwa kiongozi wa watu, anaweza kuhama chama bila kupoteza uongozi wake kama ilivyo nchini Kenya na nchi nyingine zenye kuheshimu demokrasia ya kweli na sio hii demokrasia fake ya vyama!.
  5. Tubadili sheria yetu ya uchaguzi, kwa kuondoa kipengele cha kudhaminiwa na vyama ili kila Mtanzania mwenye sifa za kugombea uongozi wa nafasi yoyote, aruhusiwe, ila kwenye urais, tuweke vigezo vya ziada, ili asijetokea tajiri mmoja mwenye ukwasi wa kuwanunua watanzania wote, tukajikuta tuna rais wa kununuliwa. Ila kwenye ubunge, udiwani na serikali za mtaa, kila mtu awe free kugombea, hivyo tuwe na wagombea huru, na hili likifanyika hata sisi tusio na vyama tutashiriki, mfano mimi, naweza kabisa kugombea jimbo fulani na kulitwaa kama kuokota embe dodo lililojiangukia, ambapo mbunge wa hapo, nitamsukuma kama nimesukuma mlevi!.
  6. Tuibadili Tume yetu ya Uchaguzi iwe Tume Huru zaidi na Shirikishi, tujenge uwanja sawa wa ushindani wa haki kwa vyama vyote, uchaguzi uendeshwe kwa transparency ya hali ya juu kwa kuruhusu mawakala hadi kwenye tallying, na vyama au taasisi zozote ziwe free kuwa na tallying centers zake, kitu ambacho hakitaruhusiwa na talling centers hizo ni kutangaza matokeo, kama matokeo yote ya uchaguzi hadi wa rais yanahesabiwa kituoni na kubandikwa ukutani, kama hakuna jambo lolote la kificho, yaani nothing to hide, kwanini uzuie independent tallying?!. Uchaguzi wa 2020, kila mwenye uwezo wa kufanya tallying aruhusiwe afanye ila sitangaze matokeo, hii itazuia bao la mkono!.
Hitimisho.
Mambo ya ajabu kulihusu Bunge letu ni mengi nineisha wahi kuyaulizia humu na miongoni mwake ni haya,
Japo maswali hayo kuhusu Bunge letu Tukufu hayajapatiwa majibu muafaka, madhali sasa tunaye mtu msikivu, tuendelee kuyauliza labda this time around, hatimaye yatapatiwa majibu muafaka!.

Watanzania tutaendelea kusubiria mpaka lini wakati Bunge letu Tukufu likitunga Sheria batili na sometimes kuuchomekea ubatili huo hadi ndani ya Katiba yetu na kuifanya katiba yetu kuwa na vipengele batili?. Je Watanzania tufanye nini?, au tunaweza kulifanya nini Bunge la aina hii?.​

Mhimili wa serikali unapotukosea tunaweza kuushitaki mahamani, lakini mhimili wa Bunge na mhimili wa Mahakama, niliwahi kuuliza humu, kiukweli in reality kwa mujibu wa katiba yetu, there is nothing anybody can do zaidi ya kumlilia Mama!.

Tanzania tumebarikiwa kumpata rais mpenda haki na mtenda haki, ni tumuombe tuu kutumia mamlaka yake as an executive president kubadili katiba na sheria ya uchaguzi kwa kutumia hati ya dharura, kwa jinsi ile ile ubatili huo ulivyochomekewa ndani ya katiba yetu, na afanye mabadiliko ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi, NEC kuifanya kuwa ni tume huru na Shirikishi na kuiwezesha NEC wasimamie chaguzi zote toka uchaguzi wa serikali za mitaa mpaka Uchaguzi Mkuu kwa kuajiri wasimamizi wa uchaguzi na sio huu mtindo wa sasa wa kuwatumia makada wa chama kimoja waliolamba uteuzi.

Mungu Ibariki Tanzania

Paskall
 
Mzee unatupeleka mbele, unaturudisha nyuma! Kuna wakati unakuja na hoja za Ki great thinker kama hizi! Kuna wakati unaunga mkono hata vile vitu visivyoeleweka!! Dah!! Yaani hata hueleweki eti!

All in all, nadhani ifikie wakati CCM ikubali kuwaachia wengine madaraka, ili tuone pia sura zao halisi. Na hii ni baada ya kukubali kuwepo na Tume huru ya uchaguzi, na pia Katiba yenye maslahi kwa Taifa! Na siyo maslahi kwa chama fulani cha siasa, au watu fulani wenye ushawishi.
 
Leo naendelea na sehemu nyingine ya Ijue Katiba ya JMT kwa jicho la mtunga katiba. Sehemu ya kwanza nilifundisha katiba ni nini na katiba ni ya nani. Sehemu ya pili nikazungumzia Mtunga katiba alimaanisha nini aliposema Katiba ni Sheria Mama.

Sasa leo nawaletea mifano ya sheria batili inayokwenda kinyume cha katiba ya JMT. Kwa kuonyesha Katiba inasema nini, hiyo sheria ikasema nini, na mwisho kuonyesha sheria batili hiyo, imekinzana wapi na katiba ya JMT, hi si mara ya kwanza kwa Bunge letu Tukufu kutunga sheria batili!, Watanzania Tutaendelea Kusubiri Mpaka Lini, Bunge Likitunga Sheria Batili, na Kuuchomekea Ubatili Huo Ndani ya Katiba Yetu?. Tufanye Nini?.
  1. Tuanze na Ibara ya 5 ya katiba ya JMT inasema
View attachment 2743038
Haki hii ndio haki kuu ya kwanza ya kidemokrasia, haki ya kupiga kura, japo haki hii bado ipo kwenye katiba yetu, haki hii imeingiliwa na kukiukwa na ukosekanaji wa haki ya kuchaguliwa, hivyo Watanzania kuruhusiwa kuwachagua sio viongozi wao wanaowapenda kwa uhuru, bali Watanzania wanalazimika kuwachagua viongozi waliopitishwa na wahuni fulani (kudhaminiwa na chama cha siasa), hivyo ni kukiuka nia njema ya mtunga katiba ya kila Mtanzania anakuwa na haki ya kupiga kura kuchagua kiongozi anamtaka kwa Tanzania ni kumchagua kiongozi chama kilicho wachagulia!.

2. Ibara ya 5 (2) inalipa Bunge mamlaka ya kutunga sheria kuzuia mtu kupiga kura

View attachment 2743067
Haki hii ya uhuru wa kupiga kura kuchagua ni moja ya haki zinazoitwa fundamental rights, yaani haki za msingi za binadamu.

3. Ibara ya 3 imelipa Bunge la JMT, mamlaka ya kutunga sheria ya uchaguzi

View attachment 2743072
Mamlaka haya ya Bunge kutunga sheria ya uchaguzi pia limewekewa masharti, hivyo Bunge halina mamlaka ya kutunga sheria inayokwenda kinyume cha katiba.

Kisha tuje ibara ya 21 ya katiba ya JMT
View attachment 2743182
Tuje ibara ya 39 ya katiba ya JMT.
View attachment 2743193
Tumalizie Ibara ya 67 ya Katiba
View attachment 2743204
Baada ya kukuwekea vifungu, sasa twende taratibu nikuchambulie

Ibara hii ya 21 cha Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, inatoa haki ya kila Mtanzania mwenye sifa, kuwa huru kushiriki katika siasa na uongozi kuanzia serikali za mtaa hadi serikali kuu, bila ubaguzi wowote.
Uhuru wa kushiriki shughuli za umma
21.-(1) Bila ya kuathiri masharti ya ibara ya 5, ya Katiba hii na ya sheria za nchi kuhusiana na masharti ya kuchagua na kuchaguliwa, au kuteua na kuteuliwa kushiriki katika shughuli za utawala wa nchi, kila raia wa Jamhuri ya Muungano anayo haki ya kushiriki katika shughuli za utawala wa nchi, ama moja kwa moja au kwa kupitia wawakilishi waliochaguliwa na wananchi kwa hiari yao, kwa kuzingatia utaratibu uliowekwa na sheria au kwa mujibu wa sheria.


Lakini kukafanyika uhuni kwa maslahi yao, na kwa vile serikali ni yao, wakaipindua katiba kwa kuinyofoa haki hiyo ya kila mtu kushiriki siasa, iliyotolewa na katiba, na kupachika shurti la kudhaminiwa na chama, hivyo kujenga ubaguzi katika kushiriki shughuli za uongozi umma kwa watu kulazimishwa kwanza kujiunga na vyama vya siasa, ndipo upate haki ya kugombee nafasi yoyote ya uongozi wa umma, huku sio kuwatendea haki Watanzania wengine wote, wasiotaka kujiunga na vyama vyovyote vya siasa, kutokana na kuviona karibu vyama vyote ni vyama vya hovyo hovyo, lakini wana uwezo wa uongozi. Hii ni haki muhimu iliyotolewa na katiba, kitendo cha kuingiza shurti la kudhaminiwa na chama cha siasa ni kinyume cha katiba. Hivyo sheria hii ibadilishwe ili kukidhi kile ambacho katiba ilidhamiria ilipoitoa haki hii, hivyo baada ya mabadiliko hayo ya mlango wa nyuma, kipengele hicho sasa kinasomeka hivi

Uhuru wa kushiriki shughuli za umma Sheria ya 1984 Na.15 ib.6 Sheria ya 1994 Na.34 ya ib.4
21.-(1) Bila ya kuathiri masharti ya ibara ya 5, ya 39 na ya 67 ya Katiba hii na ya sheria za nchi kuhusiana na masharti ya kuchagua na kuchaguliwa, au kuteua na kuteuliwa kushiriki katika shughuli za utawala wa nchi, kila raia wa Jamhuri ya Muungano anayo haki ya kushiriki katika shughuli za utawala wa nchi, ama moja kwa moja au kwa kupitia wawakilishi waliochaguliwa na wananchi kwa hiari yao, kwa kuzingatia utaratibu uliowekwa na sheria au kwa mujibu wa sheria.


Ule uhuru uliotolewa na Katiba wa kila mtu kuwa huru kushiriki shughuli za uongozi, kupitia ibara ya 21, umekuja kunyofolewa na ibara ya 39 na 67 (b)(c) kwa kuweka sherti, ili mtu kuweza kugombea nafasi yoyote ya uongozi wa umma, ni lazima awe ni mwanachama, na mgombea aliyependekezwa na chama cha siasa hivyo lazima adhaminiwe na chama cha siasa!, Haki zinatolewa na ibara moja halafu zinaporwa na ibara nyingine ya katiba hiyo hiyo!.

Mchungaji Mtikila (Mungu amuweke mahala pema peponi), mwaka 1993, alifungua kesi No. 5 ya 1993, alifanya kuhudi kubwa kukipinga kifungu hiki na Mahakama Kuu kupitia kwa Jaji Lugakingira, (Mungu amuweke mahala pema peponi), ikatamka wazi na bayana kipengele hicho ni batili na kinakiuka katiba ya JMT ya mwaka 1977, hivyo kifutwe, na kutoa haki kwa kila Mtanzania ana haki ya kushiriki kugombea Uongozi

Baada tuu ya Mtikila kushinda kesi serikali ikafanya mambo mawili makubwa ya ajabu!, kwanza ilikata rufaa!. Hivi kwa uamuzi kama huu, serikali ilikata rufaa kwa maslahi ya nani?. Pili serikali ilipeleka bungeni kwa hati ya dharura, sheria No. 34 ya mwaka 1994, kufanya marekebisho ya 8 ya Katiba ya JMT na kukichomeka kipengele hicho ndani ya katiba, hivyo kuibatilisha ile hukumu ya Jaji Lugakingira!. Hapa ndipo ujinga unapoanzia katika siasa zetu kwa serikali kufanya kazi kwa maslahi ya kisiasa ya watu fulani, hivyo kupoteza haki ya wengi kwa ajili ya kuwanufaisha wachache.

Kuhusu haki ya kila Mtanzania kugombea nafasi yoyote, ibara ya 21 ya Katiba ya Tanzania ilisema hivi na hapa nina nukuu
“Kila raia wa Jamhuri ya Muungano anayo haki ya kushiriki katika shughuli za utawala wa nchi, ama moja kwa moja au wa kupitia wawakilishi waliochaguliwa na wananchi kwa hiari yao, kwa kuzingatia utaratibu uliowekwa na sheria au kwa mujibu wa sheria”.

Lakini baada ya kufanywa marekebisho, ibara hiyo ilisomeka hivi, na hapa ninanukuu
“ Bila ya kuathiri masharti ya Ibara ya 39, ya 47 na ya 67 ya Katiba hii na ya sheria za nchi kuhusiana na masharti ya kuchaguwa na kuchaguliwa, au kuteua na kuteuliwa kushiriki katika shughuli za utawala wa nchi”

Hiki kilichofanyika, mimi nakiita ni kitendo cha kihuni!, Watanzania tulifanyiwa uhuni na serikali yetu, kwa kuinajisi katiba yetu!, kitu kimeelezwa ni kinyume cha katiba, kinatoa haki zilizotolewa na katiba, halafu serikali hiyo inakuja kuihalalisha haramu hiyo kwa kuiingiza rasmi kwenye katiba!, huku ni kuinajisi katiba yetu!.

Mchungaji Mtikila, licha ya kuwa ni mwanasiasa, Mwenyekiti wa chama cha siasa cha DP, (Democratic Party), lakini alikuwa ni mtu wa Mungu kiukweli kabisa, kwa sababu hakukubali kabila yetu inajisiwe!, hivyo akafungua kesi nyingine No. 10 ya mwaka 2009 kupinga marekebisho hayo ya 8 ya katiba na kuyaita ni ubatili!.

Katika kesi hiyo, Mchungaji Mtikila aliomba mambo mawili makuu

(a) Mahakama itamke ibara 39 na 67 za katiba zilizorekebishwa na marekebisho ya 8 kwa sharia No. 34 ya mwaka 1994, ni batili na kinyume cha katiba.

(b) Kutamka wazi kuwa Kila Mtanzania ana haki ya kugombea kwa mujibu wa ibara ya 21 ya Katiba, bila kulazimishwa kudhaminiwa na chama cha siasa, hivyo mtu anaweza kugombea kama mgombea binafsi.

Mahakama Kuu chini ya majaji watatu, (majaji watatu kisheria inaitwa Half Bench), Manento, Masati na Mihayo, wakayakubali mambo yote ya Mchungaji Mtikila na kumpa ushindi tena kwa kutamka marekebisho hayo ya katiba ni batili!. Lakini serikali yetu ilivyo ya ajabu, ikakata tena rufaa, na safari hii Mahakama Kuu ikakaa Full Bench ya majaji 7, chini ya Jaji Mkuu Mwenyewe, Agustino Ramadhani, akisaidiwa na Jaji Munuo, Jaji Msoffe, Jaji Kimaro, Jaji Mbarouk, Jaji Luanda, na Jaji Mjasir, ambapo tarehe 17 mwezi June, mwaka 2010 ikatoa hukumu ya ajabu kabisa kuwa kutokea Tanzania!. Tena Mahakama haikuwa peke yake, bali iliwaita mabinga wabobezi wa sheria na katiba kuisaidia, hawa ni wanaitwa marafiki wa mahakama, kwa kiingereza ni friends of the Court, kisheria wanaitwa Amicus Curiae, hivyo ma Amicus Curiae hawa, Mr. Othman Masoud, Prof. Palamagamba Kabudi, na Prof.Jwan Mwaikusa(Mungu Aiweke Roho yake Mahala Pema Peponi)

Uamuzi wa Mahakama Kuu ya Rufaa uliamua kitu cha ajabu sana na hapa naomba ninanukuu
“So as to let the will of the people prevail as to whether or not such [independent] candidates are suitable. We are definite that the Courts are not the custodian of the will of the people. That is the property of elected Members of Parliament”.

Hii kiukweli ni kauli ya ajabu sana kutolewa na mahakama yetu kwenye jambo zito na muhimu kama hili!. Kitendo cha Mahakama kujivua jukumu la kuwa the custodian of the will of the people!, ni kitendo cha ajabu sana na kushangaza sana!. Hakuna will of the people kubwa kuliko katiba!, kama katiba imetoa haki Fulani, halafu Bunge likatunga sheria ya ajabu kabisa kuifuta haki hiyo, halafu mahakama ikatamka haiwezi kuliingilia Bunge!, where is the doctrine of separation of powers, checks and balance?.

Kwa ajili ya kulinda heshima ya Mahakama Kuu, naomba niweke ilichokisema bila kukitafsiri.

“In our case, we say that the issue of independent candidates has to be settled by Parliament which has the jurisdiction to amend the Constitution and not the Courts which, as we have found, do not have that jurisdiction. The decision on whether or not to introduce independent candidates depends on the social needs of each State based on its historical reality. Thus the issue of independent candidates is political and not legal However, we give a word of advice to both the Attorney General and our Parliament: The United Nations Human Rights Committee, in paragraph 21 of its General Comment No. 25, of July 12, 1996, said as follows on Article 25 of the International Covenant on Civil and Political Rights, very similarly worded as Art 23 of the American Convention and our Art 21: The right of persons to stand for election should not be limited unreasonably by requiring candidates to be members of
parties or of specific parties. Tanzania is known for our good record on human rights and particularly our militancy for the right to self determination and hence our involvement in the liberation struggle. We should seriously ponder that comment from a Committee of the United Nations, that is, the whole world.
DATED at DAR ES SALAAM this 17th day of June, 2010”


Mahakama Kuu ya Rufaa ikaamua kuwa Mahakama haina mamlaka ya kuliingilia Bunge, katika vipengele vya katiba, kumaanisha kwa vile marekebisho hayo ya 8 yamefanywa na Bunge, hivyo ni Bunge ndio lirekebishe kipengele hicho!, kiukweli kabisa, kwa maoni yangu, uamuzi huu sio utii wa mhimili wa Mahakama kwa mhimili Bunge, bali huu ni ukondoo wa hali ya juu kwa Mhimili wa Mahakama kwa serikali kwa manufaa ya watu wachache!.

Uchaguzi wa Mwaka 2015 ukalithibitisha hili, kumbe baadhi ya majaji wetu ni makada!, Jaji Mkuu Mstaafu aliyeongoza jopo hilo, alichukua fomu kugombea urais!, for what my God?!. Baadhi ya wale ma amicus curiae naamini tunawajua na tunawaona na ukada wao!. Unategemea nini kama sheria za nchi hii zitafinyangwa finyangwa kwa manufaa ya wachache?!. This must stop!.

Japo Lengo la Kudhaminiwa na Chama ni Nini, Huu Sii Ujinga Tuu?!.
Katiba ilisema kila Mtanzania ana haki ya kushiriki uongozi, hili sherti la kudhaminiwa na chama lilitoka wapi, na kwa kwa nini watu walazimishwe kuwa wanachama wa vyama ili wadhaminiwe, ndipo waweze kugombea?. Mfano mimi, sina chama kwa sababu naziona siasa za vyama ni za hovyo hovyo, ikitokea nina uwezo wa kuwatumikia wananchi wa eneo langu na kuwaletea maendeleo bila kupitia chama chochote, kwa nini nizuiliwe?!. Kiukweli kabisa, kwa maoni yangu, huu ni ujinga!, it is nonsense!.

Watanzania tusikubali ujinga huu uendelee hadi 2020!, tupiganie milango ya wagombea binafsi ifunguliwe, 2020, watu wenye nia ya kugombea, kuwaletea wananchi maendeleo, bila kupitia hizi nonsense za vyama waingie, washindane kwa hoja na sio kushindana kuhonga, kama hali inavyoendelea sasa!. Hili shurti la vyama likiondolewa, mnaweza kushangaa watu wazalendo wa kweli wan chi hii, kama kina Reginald Mengi, Ali Mfuruki, Yogesh Manek, SS Bakhresa, Pascal Mayalla, and the like, wenye uchungu wa dhati na umasikini wa taifa hili, wakajitokeza kuwatumikia wananchi!.

Kiongozi Akiishachaguliwa, Anakuwa ni Kiongozi wa Watu, na Sio Kiongozi wa Chama, Kwa Sababu Anachaguliwa na Watu na Sio Chama!.
Kiukweli kwenye hili jambo, kuna ujinga mwingi!, ujinga mwingine mkubwa kabisa ni huu, hata kama mgombea amedhaminiwa na chama cha siasa kugombea, akiishapitishwa na Tume ya Uchaguzi kuwa Mgombea, japo anatambulika kama ni mgombea wa chama fulani, lakini akiishachaguliwa, mwenyekiti wa mtaa, diwani, mbunge au rais, anakuwa sio kiongozi tena wa chama kilichomdhamini, bali sasa anakuwa ni kiongozi wa umma, kiongozi wa wananchi. Mfano baada ya rais Magufuli kuchaguliwa kuwa rais kwa tiketi ya CCM, lakini hakuchaguliwa na wana CCM pekee, amechaguliwa na Watanzania wote, yeye anakuwa sio kiongozi wa CCM bali kiongozi wa Watanzania wote, vivyo hivyo kwa wabunge, madiwani na viongozi wa serikali ya mtaa, kitendo cha mtu ambaye ni kiungozi wa umma, kujitoa chama na kupoteza ubunge, udiwani au uongozi wa umma, ni ujinga ambao haupaswi kuvumiliwa. Nini muhimu kati ya umma na chama?. Kuukosesha umma kiongozi wao waliemchagua kwa sababu za chama, sio tuu sio haki kwa wananchi waliomchagua, bali pia ni dhambi, kuwalipisha masikini hawa gharama za uchaguzi wa marudio kwa sababu za kijinga!.

Nini Kifanyike, A Way Forward.
Kama nilivyowahi kushauri humu, ukosoaji wenye kujenga, huandamana na ushauri wa nini kifanyike kurekebisha kasoro hizi ili kuundoa ujinga huu unaoendelea nchini mwetu kwa sasa kwa viongozi wa umma kuhama vyama na kupoteza uongozi wa umma.

1. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amri Jeshi Mkuu, Dr. John Pombe Magufuli, akemee huu mtindo wa kuhama vyama unasababisha hasara kwa taifa, kwa kuwashukuru kumuunga mkono na kuunga mkono juhudi zake, lakini wabaki huko huko kwenye vyama vyao, hadi 2020, wakiishamaliza muhula wao, ndipo wajitoe na kuhama vyama.

2. Rais wa Nchi, akili Ikulu yetu, atenganisha kofia zake mbili za rais wa nchi na Mwenyekiti wa chama cha CCM. Ikulu ni mahali patakatifu, akiwa ikulu, rais wetu afanye kazi takatifu, hili la kuwaita watu ikulu yetu na kuwaomba wajiunge CCM, asilifanyie patakatifu pale, hili akalifanyie ofisi ya CCM Lumumba. Halileti picha nzuri kwa rais wetu, kwa sababu yeye sio rais wa CCM ni rais wa Watanzania wote.

3. Iwekwe faini maalum kwa kila kiongozi wa umma, atakayejiuzulu nafasi yake kwa sababu za kuhama chama, ikiwemo kukatwa mafao yake na ikibidi kufilisiwa ili kugharimia gharama za uchaguzi wa marudio kwa kulitia hasara taifa.

4. Viongozi wote wanaojiuzulu, wasiruhusiwe tena kugombea nafasi walizojiuzulu,kitendo cha kujiuzulu, kasha kugombea tena nafasi hiyo hiyo uliojiuzulu, ni kuwafanya wajinga, wale waliokuchagua.

5. Na kama vyama vimewaruhusu watu hawa waliotufanya wajinga kugombea tena, then natoa wito kwa Watanzania wenzangu, tusikubali kufanywa wajinga!. Tutangulize mbele maslahi ya taifa kwa kuwakataa, kama adhabu ya kutukataa na kulitia taifa letu hasara ya uchaguzi wa marudio.

6. Ila kama mapenzi yako kwa mgombea wa chama chako ni kitu cha muhimu zaidi kwako kuliko kutanguliza mbele maskahi ya taifa, hivyo chochote unacholetewa na chama chako hata kama ni ujinga, wewe utakichagua tuu, hivyo hapo, utakuwa umefanya chaguo lako, hivyo ni kuthibitisha Watanzania bado tunaweza kuletewa ujinga wowote na sisi tukauchagua ujinga huo!, na labda ndio maana mpaka sasa Watanzania tuko hapa tulipo!.

7. Tubadili sheria yetu ya uchaguzi, kwa kufuta chaguzi zote ndogo, na tuanzishe proportional representation kwa mwenye kura nyingi ndiye mshindi, lakini likitokea lolote, akasita kuwa rais, mbunge au diwani, yule aliyemfuatia katika uchaguzi uliopita ndio anatangazwa mbunge, kama hayupo anachuliwa mtu wa tatu, hadi wa mwisho, kama wote hawapo, ndipo uchaguzi mdogo unafanyika.

8. Kile kipengele cha kudhaminiwa na chama kiishie kwenye uteuzi tuu, kiongozi akiishachaguliwa, anakuwa kiongozi wa watu, anaweza kuhama chama bila kupoteza uongozi wake kama ilivyo nchini Kenya na nchi nyingine zenye kuheshimu demokrasia ya kweli na sio hii demokrasia fake ya vyama!.

9. Tubadili sheria yetu ya uchaguzi, kwa kuondoa kipengele cha kudhaminiwa na vyama ili kila Mtanzania mwenye sifa za kugombea uongozi wa nafasi yoyote, aruhusiwe, ila kwenye urais, tuweke vigezo vya ziada, ili asijetokea tajiri mmoja mwenye ukwasi wa kuwanunua watanzania wote, tukajikuta tuna rais wa kununuliwa. Ila kwenye ubunge, udiwani na serikali za mtaa, kila mtu awe free kugombea, hivyo tuwe na wagombea huru, na hili likifanyika hata sisi tusio na vyama tutashiriki, mfano mimi, naweza kabisa kugombea jimbo fulani na kulitwaa kama kuokota embe dodo lililojiangukia, ambapo mbunge wa hapo, nitamsukuma kama nimesukuma mlevi!.

10. Tuibadili Tume yetu ya Uchaguzi iwe Tume Huru zaidi na Shirikishi, tujenge uwanja sawa wa ushindani wa haki kwa vyama vyote, uchaguzi uendeshwe kwa transparency ya hali ya juu kwa kuruhusu mawakala hadi kwenye tallying, na vyama au taasisi zozote ziwe free kuwa na tallying centers zake, kitu ambacho hakitaruhusiwa na talling centers hizo ni kutangaza matokeo, kama matokeo yote ya uchaguzi hadi wa rais yanahesabiwa kituoni na kubandikwa ukutani, kama hakuna jambo lolote la kificho, yaani nothing to hide, kwanini uzuie independent tallying?!. Uchaguzi wa 2020, kila mwenye uwezo wa kufanya tallying aruhusiwe afanye ila sitangaze matokeo, hii itazuia bao la mkono!

Hitimisho.
Tanzania is too poor spend billions on by elections for foolish and nonsense reasons, nikimaanisha nchi yetu Tanzania ni masikini wa kutupwa, kuhalalisha matumizi ya mabilioni haya ya fedha kuendesha chaguzi ndogo kwa sababu za kuhama vyama. Ili Taifa letu lipate maendeleo ya kweli, ni lazima sisi Watanzania tukubali kuwa wakweli toka ndani ya nafsi zetu, kwa kutanguliza mbele maslahi ya taifa na kufanya siasa za ukweli, tusiukubali huu ujinga wa kuhama vyama, uendelee kutugharimisha sisi masikini wa kutupwa, tunaishi kwenye lindi la umasikini uliotopea, halafu kuendelea kugharimishwa.

Nawatakia Ijumaa Njema.

Paskall
Laiti ungekubali kukaa na rangi moja ya ngozi yako ungekua na nafas kubwa humu ya kutoa elimu! But umechagua kua na ngozi ya kinyonga na hapo ndipo tatizo linaanzia!! NB: Mkiambiwa suluhisho la haya yote ni katiba mpya na tume huru isiyokua nominated na Rais mnabeza na kusema katiba mpya itamsaidia nn bibi kule kijijin au itampelekea ugali mezani!!!
 
Leo naendelea na sehemu nyingine ya Ijue Katiba ya JMT kwa jicho la mtunga katiba. Sehemu ya kwanza nilifundisha katiba ni nini na katiba ni ya nani. Sehemu ya pili nikazungumzia Mtunga katiba alimaanisha nini aliposema Katiba ni Sheria Mama.

Sasa leo nawaletea mifano ya sheria batili inayokwenda kinyume cha katiba ya JMT. Kwa kuonyesha Katiba inasema nini, hiyo sheria ikasema nini, na mwisho kuonyesha sheria batili hiyo, imekinzana wapi na katiba ya JMT, hi si mara ya kwanza kwa Bunge letu Tukufu kutunga sheria batili!, Watanzania Tutaendelea Kusubiri Mpaka Lini, Bunge Likitunga Sheria Batili, na Kuuchomekea Ubatili Huo Ndani ya Katiba Yetu?. Tufanye Nini?.
  1. Tuanze na Ibara ya 5 ya katiba ya JMT inasema
View attachment 2743038
Haki hii ndio haki kuu ya kwanza ya kidemokrasia, haki ya kupiga kura, japo haki hii bado ipo kwenye katiba yetu, haki hii imeingiliwa na kukiukwa na ukosekanaji wa haki ya kuchaguliwa, hivyo Watanzania kuruhusiwa kuwachagua sio viongozi wao wanaowapenda kwa uhuru, bali Watanzania wanalazimika kuwachagua viongozi waliopitishwa na wahuni fulani (kudhaminiwa na chama cha siasa), hivyo ni kukiuka nia njema ya mtunga katiba ya kila Mtanzania anakuwa na haki ya kupiga kura kuchagua kiongozi anamtaka kwa Tanzania ni kumchagua kiongozi chama kilicho wachagulia!.

2. Ibara ya 5 (2) inalipa Bunge mamlaka ya kutunga sheria kuzuia mtu kupiga kura

View attachment 2743067
Haki hii ya uhuru wa kupiga kura kuchagua ni moja ya haki zinazoitwa fundamental rights, yaani haki za msingi za binadamu.

3. Ibara ya 3 imelipa Bunge la JMT, mamlaka ya kutunga sheria ya uchaguzi

View attachment 2743072
Mamlaka haya ya Bunge kutunga sheria ya uchaguzi pia limewekewa masharti, hivyo Bunge halina mamlaka ya kutunga sheria inayokwenda kinyume cha katiba.

Kisha tuje ibara ya 21 ya katiba ya JMT
View attachment 2743182
Tuje ibara ya 39 ya katiba ya JMT.
View attachment 2743193
Tumalizie Ibara ya 67 ya Katiba
View attachment 2743204
Baada ya kukuwekea vifungu, sasa twende taratibu nikuchambulie

Ibara hii ya 21 cha Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, inatoa haki ya kila Mtanzania mwenye sifa, kuwa huru kushiriki katika siasa na uongozi kuanzia serikali za mtaa hadi serikali kuu, bila ubaguzi wowote.
Uhuru wa kushiriki shughuli za umma
21.-(1) Bila ya kuathiri masharti ya ibara ya 5, ya Katiba hii na ya sheria za nchi kuhusiana na masharti ya kuchagua na kuchaguliwa, au kuteua na kuteuliwa kushiriki katika shughuli za utawala wa nchi, kila raia wa Jamhuri ya Muungano anayo haki ya kushiriki katika shughuli za utawala wa nchi, ama moja kwa moja au kwa kupitia wawakilishi waliochaguliwa na wananchi kwa hiari yao, kwa kuzingatia utaratibu uliowekwa na sheria au kwa mujibu wa sheria.


Lakini kukafanyika uhuni kwa maslahi yao, na kwa vile serikali ni yao, wakaipindua katiba kwa kuinyofoa haki hiyo ya kila mtu kushiriki siasa, iliyotolewa na katiba, na kupachika shurti la kudhaminiwa na chama, hivyo kujenga ubaguzi katika kushiriki shughuli za uongozi umma kwa watu kulazimishwa kwanza kujiunga na vyama vya siasa, ndipo upate haki ya kugombee nafasi yoyote ya uongozi wa umma, huku sio kuwatendea haki Watanzania wengine wote, wasiotaka kujiunga na vyama vyovyote vya siasa, kutokana na kuviona karibu vyama vyote ni vyama vya hovyo hovyo, lakini wana uwezo wa uongozi. Hii ni haki muhimu iliyotolewa na katiba, kitendo cha kuingiza shurti la kudhaminiwa na chama cha siasa ni kinyume cha katiba. Hivyo sheria hii ibadilishwe ili kukidhi kile ambacho katiba ilidhamiria ilipoitoa haki hii, hivyo baada ya mabadiliko hayo ya mlango wa nyuma, kipengele hicho sasa kinasomeka hivi

Uhuru wa kushiriki shughuli za umma Sheria ya 1984 Na.15 ib.6 Sheria ya 1994 Na.34 ya ib.4
21.-(1) Bila ya kuathiri masharti ya ibara ya 5, ya 39 na ya 67 ya Katiba hii na ya sheria za nchi kuhusiana na masharti ya kuchagua na kuchaguliwa, au kuteua na kuteuliwa kushiriki katika shughuli za utawala wa nchi, kila raia wa Jamhuri ya Muungano anayo haki ya kushiriki katika shughuli za utawala wa nchi, ama moja kwa moja au kwa kupitia wawakilishi waliochaguliwa na wananchi kwa hiari yao, kwa kuzingatia utaratibu uliowekwa na sheria au kwa mujibu wa sheria.


Ule uhuru uliotolewa na Katiba wa kila mtu kuwa huru kushiriki shughuli za uongozi, kupitia ibara ya 21, umekuja kunyofolewa na ibara ya 39 na 67 (b)(c) kwa kuweka sherti, ili mtu kuweza kugombea nafasi yoyote ya uongozi wa umma, ni lazima awe ni mwanachama, na mgombea aliyependekezwa na chama cha siasa hivyo lazima adhaminiwe na chama cha siasa!, Haki zinatolewa na ibara moja halafu zinaporwa na ibara nyingine ya katiba hiyo hiyo!.

Mchungaji Mtikila (Mungu amuweke mahala pema peponi), mwaka 1993, alifungua kesi No. 5 ya 1993, alifanya kuhudi kubwa kukipinga kifungu hiki na Mahakama Kuu kupitia kwa Jaji Lugakingira, (Mungu amuweke mahala pema peponi), ikatamka wazi na bayana kipengele hicho ni batili na kinakiuka katiba ya JMT ya mwaka 1977, hivyo kifutwe, na kutoa haki kwa kila Mtanzania ana haki ya kushiriki kugombea Uongozi

Baada tuu ya Mtikila kushinda kesi serikali ikafanya mambo mawili makubwa ya ajabu!, kwanza ilikata rufaa!. Hivi kwa uamuzi kama huu, serikali ilikata rufaa kwa maslahi ya nani?. Pili serikali ilipeleka bungeni kwa hati ya dharura, sheria No. 34 ya mwaka 1994, kufanya marekebisho ya 8 ya Katiba ya JMT na kukichomeka kipengele hicho ndani ya katiba, hivyo kuibatilisha ile hukumu ya Jaji Lugakingira!. Hapa ndipo ujinga unapoanzia katika siasa zetu kwa serikali kufanya kazi kwa maslahi ya kisiasa ya watu fulani, hivyo kupoteza haki ya wengi kwa ajili ya kuwanufaisha wachache.

Kuhusu haki ya kila Mtanzania kugombea nafasi yoyote, ibara ya 21 ya Katiba ya Tanzania ilisema hivi na hapa nina nukuu
“Kila raia wa Jamhuri ya Muungano anayo haki ya kushiriki katika shughuli za utawala wa nchi, ama moja kwa moja au wa kupitia wawakilishi waliochaguliwa na wananchi kwa hiari yao, kwa kuzingatia utaratibu uliowekwa na sheria au kwa mujibu wa sheria”.

Lakini baada ya kufanywa marekebisho, ibara hiyo ilisomeka hivi, na hapa ninanukuu
“ Bila ya kuathiri masharti ya Ibara ya 39, ya 47 na ya 67 ya Katiba hii na ya sheria za nchi kuhusiana na masharti ya kuchaguwa na kuchaguliwa, au kuteua na kuteuliwa kushiriki katika shughuli za utawala wa nchi”

Hiki kilichofanyika, mimi nakiita ni kitendo cha kihuni!, Watanzania tulifanyiwa uhuni na serikali yetu, kwa kuinajisi katiba yetu!, kitu kimeelezwa ni kinyume cha katiba, kinatoa haki zilizotolewa na katiba, halafu serikali hiyo inakuja kuihalalisha haramu hiyo kwa kuiingiza rasmi kwenye katiba!, huku ni kuinajisi katiba yetu!.

Mchungaji Mtikila, licha ya kuwa ni mwanasiasa, Mwenyekiti wa chama cha siasa cha DP, (Democratic Party), lakini alikuwa ni mtu wa Mungu kiukweli kabisa, kwa sababu hakukubali kabila yetu inajisiwe!, hivyo akafungua kesi nyingine No. 10 ya mwaka 2009 kupinga marekebisho hayo ya 8 ya katiba na kuyaita ni ubatili!.

Katika kesi hiyo, Mchungaji Mtikila aliomba mambo mawili makuu

(a) Mahakama itamke ibara 39 na 67 za katiba zilizorekebishwa na marekebisho ya 8 kwa sharia No. 34 ya mwaka 1994, ni batili na kinyume cha katiba.

(b) Kutamka wazi kuwa Kila Mtanzania ana haki ya kugombea kwa mujibu wa ibara ya 21 ya Katiba, bila kulazimishwa kudhaminiwa na chama cha siasa, hivyo mtu anaweza kugombea kama mgombea binafsi.

Mahakama Kuu chini ya majaji watatu, (majaji watatu kisheria inaitwa Half Bench), Manento, Masati na Mihayo, wakayakubali mambo yote ya Mchungaji Mtikila na kumpa ushindi tena kwa kutamka marekebisho hayo ya katiba ni batili!. Lakini serikali yetu ilivyo ya ajabu, ikakata tena rufaa, na safari hii Mahakama Kuu ikakaa Full Bench ya majaji 7, chini ya Jaji Mkuu Mwenyewe, Agustino Ramadhani, akisaidiwa na Jaji Munuo, Jaji Msoffe, Jaji Kimaro, Jaji Mbarouk, Jaji Luanda, na Jaji Mjasir, ambapo tarehe 17 mwezi June, mwaka 2010 ikatoa hukumu ya ajabu kabisa kuwa kutokea Tanzania!. Tena Mahakama haikuwa peke yake, bali iliwaita mabinga wabobezi wa sheria na katiba kuisaidia, hawa ni wanaitwa marafiki wa mahakama, kwa kiingereza ni friends of the Court, kisheria wanaitwa Amicus Curiae, hivyo ma Amicus Curiae hawa, Mr. Othman Masoud, Prof. Palamagamba Kabudi, na Prof.Jwan Mwaikusa(Mungu Aiweke Roho yake Mahala Pema Peponi)

Uamuzi wa Mahakama Kuu ya Rufaa uliamua kitu cha ajabu sana na hapa naomba ninanukuu
“So as to let the will of the people prevail as to whether or not such [independent] candidates are suitable. We are definite that the Courts are not the custodian of the will of the people. That is the property of elected Members of Parliament”.

Hii kiukweli ni kauli ya ajabu sana kutolewa na mahakama yetu kwenye jambo zito na muhimu kama hili!. Kitendo cha Mahakama kujivua jukumu la kuwa the custodian of the will of the people!, ni kitendo cha ajabu sana na kushangaza sana!. Hakuna will of the people kubwa kuliko katiba!, kama katiba imetoa haki Fulani, halafu Bunge likatunga sheria ya ajabu kabisa kuifuta haki hiyo, halafu mahakama ikatamka haiwezi kuliingilia Bunge!, where is the doctrine of separation of powers, checks and balance?.

Kwa ajili ya kulinda heshima ya Mahakama Kuu, naomba niweke ilichokisema bila kukitafsiri.

“In our case, we say that the issue of independent candidates has to be settled by Parliament which has the jurisdiction to amend the Constitution and not the Courts which, as we have found, do not have that jurisdiction. The decision on whether or not to introduce independent candidates depends on the social needs of each State based on its historical reality. Thus the issue of independent candidates is political and not legal However, we give a word of advice to both the Attorney General and our Parliament: The United Nations Human Rights Committee, in paragraph 21 of its General Comment No. 25, of July 12, 1996, said as follows on Article 25 of the International Covenant on Civil and Political Rights, very similarly worded as Art 23 of the American Convention and our Art 21: The right of persons to stand for election should not be limited unreasonably by requiring candidates to be members of
parties or of specific parties. Tanzania is known for our good record on human rights and particularly our militancy for the right to self determination and hence our involvement in the liberation struggle. We should seriously ponder that comment from a Committee of the United Nations, that is, the whole world.
DATED at DAR ES SALAAM this 17th day of June, 2010”


Mahakama Kuu ya Rufaa ikaamua kuwa Mahakama haina mamlaka ya kuliingilia Bunge, katika vipengele vya katiba, kumaanisha kwa vile marekebisho hayo ya 8 yamefanywa na Bunge, hivyo ni Bunge ndio lirekebishe kipengele hicho!, kiukweli kabisa, kwa maoni yangu, uamuzi huu sio utii wa mhimili wa Mahakama kwa mhimili Bunge, bali huu ni ukondoo wa hali ya juu kwa Mhimili wa Mahakama kwa serikali kwa manufaa ya watu wachache!.

Uchaguzi wa Mwaka 2015 ukalithibitisha hili, kumbe baadhi ya majaji wetu ni makada!, Jaji Mkuu Mstaafu aliyeongoza jopo hilo, alichukua fomu kugombea urais!, for what my God?!. Baadhi ya wale ma amicus curiae naamini tunawajua na tunawaona na ukada wao!. Unategemea nini kama sheria za nchi hii zitafinyangwa finyangwa kwa manufaa ya wachache?!. This must stop!.

Japo Lengo la Kudhaminiwa na Chama ni Nini, Huu Sii Ujinga Tuu?!.
Katiba ilisema kila Mtanzania ana haki ya kushiriki uongozi, hili sherti la kudhaminiwa na chama lilitoka wapi, na kwa kwa nini watu walazimishwe kuwa wanachama wa vyama ili wadhaminiwe, ndipo waweze kugombea?. Mfano mimi, sina chama kwa sababu naziona siasa za vyama ni za hovyo hovyo, ikitokea nina uwezo wa kuwatumikia wananchi wa eneo langu na kuwaletea maendeleo bila kupitia chama chochote, kwa nini nizuiliwe?!. Kiukweli kabisa, kwa maoni yangu, huu ni ujinga!, it is nonsense!.

Watanzania tusikubali ujinga huu uendelee hadi 2020!, tupiganie milango ya wagombea binafsi ifunguliwe, 2020, watu wenye nia ya kugombea, kuwaletea wananchi maendeleo, bila kupitia hizi nonsense za vyama waingie, washindane kwa hoja na sio kushindana kuhonga, kama hali inavyoendelea sasa!. Hili shurti la vyama likiondolewa, mnaweza kushangaa watu wazalendo wa kweli wan chi hii, kama kina Reginald Mengi, Ali Mfuruki, Yogesh Manek, SS Bakhresa, Pascal Mayalla, and the like, wenye uchungu wa dhati na umasikini wa taifa hili, wakajitokeza kuwatumikia wananchi!.

Kiongozi Akiishachaguliwa, Anakuwa ni Kiongozi wa Watu, na Sio Kiongozi wa Chama, Kwa Sababu Anachaguliwa na Watu na Sio Chama!.
Kiukweli kwenye hili jambo, kuna ujinga mwingi!, ujinga mwingine mkubwa kabisa ni huu, hata kama mgombea amedhaminiwa na chama cha siasa kugombea, akiishapitishwa na Tume ya Uchaguzi kuwa Mgombea, japo anatambulika kama ni mgombea wa chama fulani, lakini akiishachaguliwa, mwenyekiti wa mtaa, diwani, mbunge au rais, anakuwa sio kiongozi tena wa chama kilichomdhamini, bali sasa anakuwa ni kiongozi wa umma, kiongozi wa wananchi. Mfano baada ya rais Magufuli kuchaguliwa kuwa rais kwa tiketi ya CCM, lakini hakuchaguliwa na wana CCM pekee, amechaguliwa na Watanzania wote, yeye anakuwa sio kiongozi wa CCM bali kiongozi wa Watanzania wote, vivyo hivyo kwa wabunge, madiwani na viongozi wa serikali ya mtaa, kitendo cha mtu ambaye ni kiungozi wa umma, kujitoa chama na kupoteza ubunge, udiwani au uongozi wa umma, ni ujinga ambao haupaswi kuvumiliwa. Nini muhimu kati ya umma na chama?. Kuukosesha umma kiongozi wao waliemchagua kwa sababu za chama, sio tuu sio haki kwa wananchi waliomchagua, bali pia ni dhambi, kuwalipisha masikini hawa gharama za uchaguzi wa marudio kwa sababu za kijinga!.

Nini Kifanyike, A Way Forward.
Kama nilivyowahi kushauri humu, ukosoaji wenye kujenga, huandamana na ushauri wa nini kifanyike kurekebisha kasoro hizi ili kuundoa ujinga huu unaoendelea nchini mwetu kwa sasa kwa viongozi wa umma kuhama vyama na kupoteza uongozi wa umma.

1. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amri Jeshi Mkuu, Dr. John Pombe Magufuli, akemee huu mtindo wa kuhama vyama unasababisha hasara kwa taifa, kwa kuwashukuru kumuunga mkono na kuunga mkono juhudi zake, lakini wabaki huko huko kwenye vyama vyao, hadi 2020, wakiishamaliza muhula wao, ndipo wajitoe na kuhama vyama.

2. Rais wa Nchi, akili Ikulu yetu, atenganisha kofia zake mbili za rais wa nchi na Mwenyekiti wa chama cha CCM. Ikulu ni mahali patakatifu, akiwa ikulu, rais wetu afanye kazi takatifu, hili la kuwaita watu ikulu yetu na kuwaomba wajiunge CCM, asilifanyie patakatifu pale, hili akalifanyie ofisi ya CCM Lumumba. Halileti picha nzuri kwa rais wetu, kwa sababu yeye sio rais wa CCM ni rais wa Watanzania wote.

3. Iwekwe faini maalum kwa kila kiongozi wa umma, atakayejiuzulu nafasi yake kwa sababu za kuhama chama, ikiwemo kukatwa mafao yake na ikibidi kufilisiwa ili kugharimia gharama za uchaguzi wa marudio kwa kulitia hasara taifa.

4. Viongozi wote wanaojiuzulu, wasiruhusiwe tena kugombea nafasi walizojiuzulu,kitendo cha kujiuzulu, kasha kugombea tena nafasi hiyo hiyo uliojiuzulu, ni kuwafanya wajinga, wale waliokuchagua.

5. Na kama vyama vimewaruhusu watu hawa waliotufanya wajinga kugombea tena, then natoa wito kwa Watanzania wenzangu, tusikubali kufanywa wajinga!. Tutangulize mbele maslahi ya taifa kwa kuwakataa, kama adhabu ya kutukataa na kulitia taifa letu hasara ya uchaguzi wa marudio.

6. Ila kama mapenzi yako kwa mgombea wa chama chako ni kitu cha muhimu zaidi kwako kuliko kutanguliza mbele maskahi ya taifa, hivyo chochote unacholetewa na chama chako hata kama ni ujinga, wewe utakichagua tuu, hivyo hapo, utakuwa umefanya chaguo lako, hivyo ni kuthibitisha Watanzania bado tunaweza kuletewa ujinga wowote na sisi tukauchagua ujinga huo!, na labda ndio maana mpaka sasa Watanzania tuko hapa tulipo!.

7. Tubadili sheria yetu ya uchaguzi, kwa kufuta chaguzi zote ndogo, na tuanzishe proportional representation kwa mwenye kura nyingi ndiye mshindi, lakini likitokea lolote, akasita kuwa rais, mbunge au diwani, yule aliyemfuatia katika uchaguzi uliopita ndio anatangazwa mbunge, kama hayupo anachuliwa mtu wa tatu, hadi wa mwisho, kama wote hawapo, ndipo uchaguzi mdogo unafanyika.

8. Kile kipengele cha kudhaminiwa na chama kiishie kwenye uteuzi tuu, kiongozi akiishachaguliwa, anakuwa kiongozi wa watu, anaweza kuhama chama bila kupoteza uongozi wake kama ilivyo nchini Kenya na nchi nyingine zenye kuheshimu demokrasia ya kweli na sio hii demokrasia fake ya vyama!.

9. Tubadili sheria yetu ya uchaguzi, kwa kuondoa kipengele cha kudhaminiwa na vyama ili kila Mtanzania mwenye sifa za kugombea uongozi wa nafasi yoyote, aruhusiwe, ila kwenye urais, tuweke vigezo vya ziada, ili asijetokea tajiri mmoja mwenye ukwasi wa kuwanunua watanzania wote, tukajikuta tuna rais wa kununuliwa. Ila kwenye ubunge, udiwani na serikali za mtaa, kila mtu awe free kugombea, hivyo tuwe na wagombea huru, na hili likifanyika hata sisi tusio na vyama tutashiriki, mfano mimi, naweza kabisa kugombea jimbo fulani na kulitwaa kama kuokota embe dodo lililojiangukia, ambapo mbunge wa hapo, nitamsukuma kama nimesukuma mlevi!.

10. Tuibadili Tume yetu ya Uchaguzi iwe Tume Huru zaidi na Shirikishi, tujenge uwanja sawa wa ushindani wa haki kwa vyama vyote, uchaguzi uendeshwe kwa transparency ya hali ya juu kwa kuruhusu mawakala hadi kwenye tallying, na vyama au taasisi zozote ziwe free kuwa na tallying centers zake, kitu ambacho hakitaruhusiwa na talling centers hizo ni kutangaza matokeo, kama matokeo yote ya uchaguzi hadi wa rais yanahesabiwa kituoni na kubandikwa ukutani, kama hakuna jambo lolote la kificho, yaani nothing to hide, kwanini uzuie independent tallying?!. Uchaguzi wa 2020, kila mwenye uwezo wa kufanya tallying aruhusiwe afanye ila sitangaze matokeo, hii itazuia bao la mkono!

Hitimisho.
Tanzania is too poor spend billions on by elections for foolish and nonsense reasons, nikimaanisha nchi yetu Tanzania ni masikini wa kutupwa, kuhalalisha matumizi ya mabilioni haya ya fedha kuendesha chaguzi ndogo kwa sababu za kuhama vyama. Ili Taifa letu lipate maendeleo ya kweli, ni lazima sisi Watanzania tukubali kuwa wakweli toka ndani ya nafsi zetu, kwa kutanguliza mbele maslahi ya taifa na kufanya siasa za ukweli, tusiukubali huu ujinga wa kuhama vyama, uendelee kutugharimisha sisi masikini wa kutupwa, tunaishi kwenye lindi la umasikini uliotopea, halafu kuendelea kugharimishwa.

Nawatakia Ijumaa Njema.

Paskall
Wamekutoa kwenye pay roll nn mkuu, mbona kama umeanza kuwa na akili
 
Tangu lini watu wenye tabia za Zitto wakaaminika?, tangu uitwe na Magufuli kuwa Mayala maana yake ni njaa uligeuka chawa mkubwa tofauti na kipindi kile unajiita "Pasco".



Kila siku unatetea uuzwaji wa Tanganyika na WaTanganyika hivyo ni ngumu watu kukuamini kwa bandiko lako hili.
 
Ulizungumzia mpambano wa Mtikila mpaka mahakama ya rufaa, lakini marehemu Mtikila hakuishia hapo bali aliendelea kufungua kesi Hadi mahakama ya Africa na kushinda kesi ya mgombea binafsi lakini ilipokuja kusajiliwa mahakama kuu serikali ulikuja na utetezi kuwa Kuna mchakato wa katiba mpya na rasimu ya katiba ilipendekeza mgombea binafsi.
Lakini cha ajabu mahakama ilikubaliana na utetezi huo lakini cha ajabu katiba mpya haijapatikana Hadi leo Wala hakuna taasisi yoyote iliyoenda mahakamani na kuhoji juu ya Hilo swala.
Hata kituo cha Sheria za haki za binadamu kilichoungana na marehemu Mtikila hakikurudi kuhoji juu ya maamuzi ya serikali kuhusu mgombea binafsi.
Inaonekana huu mchakato uliisha na marehemu Mtikila.
 
Mkuu mimi nakuelewa sana. Lakini watanzania tunatatizo ha uoga, inawezekana ni malezi na shule tulizopitia ambazo mwanafunzi anatendewa kama mfungwa na kufundishwa kuiogopa mamlaka.

Katiba imeupa mhimili wa mahakama wajibu na mamlaka yote ya kutoa haki. Lakini kuna wakati mahakama hiyohiyo inapata kigugumizi kutimiza wajibu wake na kuja na visingizio vya kutotaka kuliingilia Bunge.

Hata tukiwa na katiba mpya, kama watu wanaendeshwa na hofu na wanashindwa kutimiza wajibu wao bado tutaendelea kuwa na sheria badili au sheria zinazopuuzwa na serikali.

Lengo kuu la lile sharti batili la kudhaminiwa na chama cha siasa ni hofu ya serikali kushindwa kuwadhibiti wabunge. Kwasasa wabunge wanafanya kile mwenyekiti wa chama chao ambaye pia ni mkuu wa serikali anakitaka.

Wakienda kinyume basi wanaweza kuvuliwa uanachama wao na kupoteza ubunge wao, wengi wao hawawezi kuwa na ujasiri wa kwenda kinyume na vyama vyao.

Laiti sharti hilo badili lisingekuwepo, basi wabunge hata baada ya kuvuliwa uanachama, wangeendelea kuwa wabunge. Hii maana yake ni kwamba serikali ingelazimika kuwaridhisha wabunge kuwa inafamya kazi yake inavyotakiwa na sio kinyume chake.

Kwa sasa, nchi yetu iko chini ya mfalme. Anadhibiti serikali, chama tawala pamoja na bunge. Mahakama inauhuru lakini majaji hawana ujasiri wa kuutumia uhuru huo kwenda kinyume na matakwa ya mfalme.
 
hayo ndiyo matokeo ya coup next mkitaka kufanya coup fikirieni consequences kwanza mnaweza kuwa na hali mbaya zaidi ya ile mnayoiondoa, coup zote huwa na reparations …
 
Wanabodi,
Kama kawaida yangu kila nipatapo fursa huja na makala zangu elimishi za Kwa Maslahi ya Taifa, leo naendelea na sehemu nyingine ya Ijue Katiba ya JMT kwa jicho la mtunga katiba. Sehemu ya kwanza nilifundisha katiba ni nini na katiba ni ya nani. Sehemu ya pili nikazungumzia Mtunga katiba alimaanisha nini aliposema Katiba ni Sheria Mama.

Sii wengi wanafahamu Bunge letu Tukufu linaporidhia mkataba wowote wa kimataifa, mfano ile IGA ya ajabu ajabu ya DPW, maana yake hicho kilichoridhiwa kwenye huo kinakuwa ni sehemu ya sheria zetu under local laws!.

Licha ya mapungufu yote ya kisheria ya ile IGA kuna upungufu mmoja mkubwa ambao hakutajwa sana, huu ni upungufu wa illegality. IGA ile ya DPW na Bandari zetu, ina illegality mbili.
Ya kwanza ni illegality ya the capacity of Dubai to contract an international Treaty, kwasababu Dubai sio nchi, haina sovereignty hivyo haina the capacity to enter into an international Treaty with a nation kama Tanzania, mwenye uwezo huo ni UAE tuu na hakukuwa na POA (power of attorney) kutoka UAE kuiwezesha Dubai kuingia an international Treaty!.

Illegality ya pili, mkataba ule una kipengele kilicho kinyume cha sheria zetu, hivyo it's an illegal contract, lakini Bunge letu Tukufu limeipitisha hivyo hivyo.

Bandiko hili ni la swali

Watanzania tutaendelea kusubiria mpaka lini wakati Bunge letu Tukufu likitunga Sheria batili na sometimes kuuchomekea ubatili huo hadi ndani ya Katiba yetu na kuifanya katiba yetu kuwa na vipengele batili?. Je Watanzania tufanye nini?, au tunaweza kulifanya nini Bunge la aina hii?.​


Hii sii mara ya kwanza kwa Bunge letu kutufanyia mambo ya ajabu kama haya!. Leo naomba niwaletee mifano Bunge letu Tukufu kutunga sheria batili inayokwenda kinyume cha katiba ya JMT. Kwa kuonyesha Katiba inasema nini, hiyo sheria batili ikasema nini, na mwisho kuonyesha sheria batili hiyo, imekinzana wapi na katiba ya JMT.
  1. Tuanze na Ibara ya 5 ya katiba ya JMT inasema
View attachment 2743038
Haki hii ndio haki kuu ya kwanza ya kidemokrasia, haki ya kupiga kura, japo haki hii bado ipo kwenye katiba yetu, haki hii imeingiliwa na kukiukwa na ukosekanaji wa haki ya kuchaguliwa, hivyo Watanzania kuruhusiwa kuwachagua sio viongozi wao wanaowapenda kwa uhuru, bali Watanzania wanalazimika kuwachagua viongozi waliopitishwa na wahuni fulani (kudhaminiwa na chama cha siasa), hivyo ni kukiuka nia njema ya mtunga katiba ya kila Mtanzania anakuwa na haki ya kupiga kura kuchagua kiongozi anamtaka kwa Tanzania ni kumchagua kiongozi chama kilicho wachagulia!.

2. Ibara ya 5 (2) inalipa Bunge mamlaka ya kutunga sheria kuzuia mtu kupiga kura
View attachment 2743067
Haki hii ya uhuru wa kupiga kura kuchagua ni moja ya haki zinazoitwa fundamental rights, yaani haki za msingi za binadamu.

3. Ibara ya 3 imelipa Bunge la JMT, mamlaka ya kutunga sheria ya uchaguzi
View attachment 2743072
Mamlaka haya ya Bunge kutunga sheria ya uchaguzi pia limewekewa masharti, hivyo Bunge halina mamlaka ya kutunga sheria inayokwenda kinyume cha katiba.

Kisha tuje ibara ya 21 ya katiba ya JMT
View attachment 2743182
Tuje ibara ya 39 ya katiba ya JMT.
View attachment 2743193
Tumalizie Ibara ya 67 ya Katiba ya JMT
View attachment 2743204
Baada ya kukuwekea vifungu, sasa twende taratibu nikuchambulie

Ibara hii ya 21 cha Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, inatoa haki ya kila Mtanzania mwenye sifa, kuwa huru kushiriki katika siasa na uongozi kuanzia serikali za mtaa hadi serikali kuu, bila ubaguzi wowote.
Uhuru wa kushiriki shughuli za umma
21.-(1) Bila ya kuathiri masharti ya ibara ya 5, ya Katiba hii na ya sheria za nchi kuhusiana na masharti ya kuchagua na kuchaguliwa, au kuteua na kuteuliwa kushiriki katika shughuli za utawala wa nchi, kila raia wa Jamhuri ya Muungano anayo haki ya kushiriki katika shughuli za utawala wa nchi, ama moja kwa moja au kwa kupitia wawakilishi waliochaguliwa na wananchi kwa hiari yao, kwa kuzingatia utaratibu uliowekwa na sheria au kwa mujibu wa sheria.


Lakini kukafanyika uhuni fulani kwa maslahi ya watu fulani na chama fulani kwa vile serikali ni yao, wakaipindua katiba kwa kuinyofoa haki hiyo ya kila mtu kushiriki siasa, iliyotolewa na katiba, na kupachika shurti la kudhaminiwa na chama cha siasa hivyo kujenga ubaguzi katika kushiriki shughuli za uongozi umma kwa watu kulazimishwa kwanza kujiunga na vyama vya siasa, ndipo upate haki ya kugombee nafasi yoyote ya uongozi wa umma, huku sio kuwatendea haki Watanzania wengine wote, wasiotaka kujiunga na vyama vyovyote vya siasa, kutokana na kuviona karibu vyama vyote ni vyama vya hovyo hovyo, ispokuwa chama kimoja, lakini kuna watu wazuri na wana uwezo mkubwa wa uongozi, hawawezi kugombea uongozi kwasababu ya ujinga huo!.

Hii ni haki muhimu iliyotolewa na katiba, kitendo cha kuingiza shurti la kudhaminiwa na chama cha siasa ni kinyume cha katiba. Hivyo sheria hii ibadilishwe ili kukidhi kile ambacho mtunga katiba ilidhamiria ilipoiweka haki hii, ndani ya katiba yetu!, hivyo baada ya mabadiliko hayo ya mlango wa nyuma, kipengele hicho sasa kinasomeka hivi

Uhuru wa kushiriki shughuli za umma Sheria ya 1984 Na.15 ib.6 Sheria ya 1994 Na.34 ya ib.4
21.-(1) Bila ya kuathiri masharti ya ibara ya 5, ya 39 na ya 67 ya Katiba hii na ya sheria za nchi kuhusiana na masharti ya kuchagua na kuchaguliwa, au kuteua na kuteuliwa kushiriki katika shughuli za utawala wa nchi, kila raia wa Jamhuri ya Muungano anayo haki ya kushiriki katika shughuli za utawala wa nchi, ama moja kwa moja au kwa kupitia wawakilishi waliochaguliwa na wananchi kwa hiari yao, kwa kuzingatia utaratibu uliowekwa na sheria au kwa mujibu wa sheria.


Ule uhuru uliotolewa na Katiba wa kila mtu kuwa huru kushiriki shughuli za uongozi, kupitia ibara ya 21, umekuja kunyofolewa na ibara ya 39 na 67 (b)(c) kwa kuweka sherti, ili mtu kuweza kugombea nafasi yoyote ya uongozi wa umma, ni lazima awe ni mwanachama, na mgombea aliyependekezwa na chama cha siasa hivyo lazima adhaminiwe na chama cha siasa!, Haki zinatolewa na ibara moja halafu zinaporwa na ibara nyingine ya katiba hiyo hiyo!.

Mchungaji Mtikila (Mungu amuweke mahala pema peponi), mwaka 1993, alifungua kesi No. 5 ya 1993, alifanya juhudi kubwa kukipinga kifungu hiki na Mahakama Kuu kupitia kwa Jaji Lugakingira, (Mungu amuweke mahala pema peponi), ikatamka wazi na bayana kipengele hicho ni batili na kinakiuka katiba ya JMT ya mwaka 1977, hivyo kifutwe, na kutoa haki kwa kila Mtanzania ana haki ya kushiriki kugombea Uongozi wowote wa nchi.

Baada tuu ya Mtikila kushinda kesi serikali ikafanya mambo mawili makubwa ya ajabu!, kwanza ilikata rufaa!. Hivi kwa uamuzi kama huu, serikali ilikata rufaa kwa maslahi ya nani?. Wiki iliyopita nilisema ile Ibara ya 64(5) iayotamka Katiba ni sheria Mama, sheria nyingine yoyote inayokwenda kinyume cha katiba ni batili, aliyebatilisha sheria batili ni katiba yenyewe na sio Mahakama!. Kazi ya Mahakama ni kutamka tuu huo ubatili na tangu baada ya tamko hilo, sheria hiyo inakuwa tayari ni imebatika!, unawezaje kukata rufaa kwa kitu kilicho batilishwa na katiba?. Kiukweli kabisa hili ni jambo la ajabu sana!.

Jambo la pili la ajabu sana na kubwa ya mwaka ni serikali yetu ilipeleka bungeni kwa hati ya dharura, sheria No. 34 ya mwaka 1994, kufanya marekebisho ya 8 ya Katiba ya JMT na kukichomeka kipengele hicho ndani ya katiba, hivyo kuibatilisha ile hukumu ya Jaji Lugakingira!. Hapa ndipo ujinga unapoanzia katika siasa zetu kwa serikali kufanya kazi kwa maslahi ya kisiasa ya watu fulani na chama fulani, hivyo kupoteza haki ya wengi kwa ajili ya kuwanufaisha wachache!..

Hiki kilichofanyika, mimi nakiita ni kitendo cha kihuni!, Watanzania tulifanyiwa uhuni na serikali yetu, kwa kuinajisi katiba yetu!, kitu kimeelezwa ni kinyume cha katiba, kinatoa haki zilizotolewa na katiba, halafu serikali hiyo inakuja kuihalalisha haramu hiyo kwa kuiingiza rasmi kwenye katiba!, huku sii kuinajisi katiba yetu?.

Mchungaji Mtikila, licha ya kuwa ni mwanasiasa, Mwenyekiti wa chama cha siasa cha DP, (Democratic Party), lakini alikuwa ni mtu wa Mungu kiukweli kabisa, kwa sababu hakukubali kabisa katiba yetu inajisiwe!, hivyo akafungua kesi nyingine No. 10 ya mwaka 2009 kupinga marekebisho hayo ya 8 ya katiba na kuyaita ni ubatili!.

Katika kesi hiyo, Mchungaji Mtikila aliomba mambo mawili makuu

(a) Mahakama itamke ibara 39 na 67 za katiba zilizorekebishwa na marekebisho ya 8 kwa sharia No. 34 ya mwaka 1994, ni batili na kinyume cha katiba.

(b) Kutamka wazi kuwa Kila Mtanzania ana haki ya kugombea kwa mujibu wa ibara ya 21 ya Katiba, bila kulazimishwa kudhaminiwa na chama cha siasa, hivyo mtu anaweza kugombea kama mgombea binafsi.

Mahakama Kuu chini ya majaji watatu, (majaji watatu kisheria inaitwa Half Bench), Manento, Masati na Mihayo, wakayakubali mambo yote ya Mchungaji Mtikila na kumpa ushindi tena kwa kutamka marekebisho hayo ya katiba ni batili!. Lakini serikali yetu ilivyo ya ajabu, ikakata tena rufaa, na safari hii Mahakama Kuu ikakaa Full Bench ya majaji 7, chini ya Jaji Mkuu Mwenyewe, Agustino Ramadhani, akisaidiwa na Jaji Eusebio Munuo, Jaji January Msoffe, Jaji Natalia Kimaro, Jaji Kassim Mbarouk, Jaji Benard Luanda, na Jaji Sauda Mjasir, ambapo tarehe 17 mwezi June, mwaka 2010 ikatoa hukumu ya ajabu kabisa kuwa kutokea Tanzania!.

Tena Mahakama ya rufaa haikuwa peke yake, bali iliwaita mabinga wabobezi na wabobevu wa sheria na katiba kuisaidia, hawa wanaitwa marafiki wa mahakama, kwa kiingereza ni friends of the Court, kisheria wanaitwa Amicus Curiae, hivyo ma Amicus Curiae hawa, Mr. Othman Masoud, Prof. Palamagamba Kabudi, na Prof.Jwan Mwaikusa(Mungu Aiweke Roho yake Mahala Pema Peponi).

Uamuzi wa Mahakama Kuu ya Rufaa uliamua kitu cha ajabu sana na hapa naomba kunukuu
“So as to let the will of the people prevail as to whether or not such [independent] candidates are suitable. We are definite that the Courts are not the custodian of the will of the people. That is the property of elected Members of Parliament”.

Hii kiukweli ni kauli ya ajabu sana kutolewa na mahakama yetu kwenye jambo zito na muhimu kama hili!. Kitendo cha Mahakama kujivua jukumu la kuwa the custodian of the will of the people!, ni kitendo cha ajabu sana na kushangaza sana!. Hakuna will of the people kubwa kuliko katiba!, kama katiba imetoa haki fulani, halafu Bunge likatunga sheria ya ajabu kabisa kuifuta haki hiyo, halafu mahakama ikatamka haiwezi kuliingilia Bunge!, where is the doctrine of separation of powers, checks and balance?!.

Kwa ajili ya kulinda heshima ya Mahakama Kuu, naomba niweke ilichokisema bila kukitafsiri.

“In our case, we say that the issue of independent candidates has to be settled by Parliament which has the jurisdiction to amend the Constitution and not the Courts which, as we have found, do not have that jurisdiction. The decision on whether or not to introduce independent candidates depends on the social needs of each State based on its historical reality. Thus the issue of independent candidates is political and not legal However, we give a word of advice to both the Attorney General and our Parliament: The United Nations Human Rights Committee, in paragraph 21 of its General Comment No. 25, of July 12, 1996, said as follows on Article 25 of the International Covenant on Civil and Political Rights, very similarly worded as Art 23 of the American Convention and our Art 21: The right of persons to stand for election should not be limited unreasonably by requiring candidates to be members of
parties or of specific parties. Tanzania is known for our good record on human rights and particularly our militancy for the right to self determination and hence our involvement in the liberation struggle. We should seriously ponder that comment from a Committee of the United Nations, that is, the whole world.
DATED at DAR ES SALAAM this 17th day of June, 2010”


Mahakama ya Rufaa ikaamua kuwa Mahakama haina mamlaka ya kuliingilia Bunge, katika vipengele vya katiba, kumaanisha kwa vile marekebisho hayo ya 8 yamefanywa na Bunge, hivyo ni Bunge ndio lirekebishe kipengele hicho!, kiukweli kabisa, kwa maoni yangu, uamuzi huu sio utii wa mhimili wa Mahakama kwa mhimili Bunge, bali huu ni ukondoo wa hali ya juu kwa Mhimili wa Mahakama kwa serikali kwa manufaa ya watu wachache!.

Uchaguzi wa Mwaka 2015 ukalithibitisha hili, kumbe baadhi ya majaji wetu ni makada!, Jaji Mkuu Mstaafu aliyeongoza jopo hilo, alichukua fomu kugombea urais!, for what my God?!. Baadhi ya wale ma amicus curiae naamini tunawajua na tunawaona na ukada wao!. Unategemea nini kama sheria za nchi hii zitafinyangwa finyangwa kwa manufaa ya wachache?!. President Samia must stop this nonsense!.

Japo Lengo la Kudhaminiwa na Chama ni zuri, ila Huu Sii Ujinga Tuu?!.
Katiba ilisema kila Mtanzania ana haki ya kushiriki uongozi, hili sherti la kudhaminiwa na chama lilitoka wapi? na kwa kwa nini watu walazimishwe kuwa wanachama wa vyama ili wadhaminiwe, ndipo waweze kugombea?. Mfano mimi, sina chama kwa sababu naziona siasa za vyama ni za hovyo hovyo, ikitokea nina uwezo wa kuwatumikia wananchi wa eneo langu na kuwaletea maendeleo bila kupitia chama chochote, kwa nini nizuiliwe?!. Kiukweli kabisa, kwa maoni yangu, huu ni ujinga uliopitiliza!, tutaliacha Bunge letu Tukufu kutufanyia ujinga huu mpaka lini?, is this not nonsense?.

Watanzania tusikubali ujinga huu uendelee hadi 2025!, tupiganie milango ya wagombea binafsi ifunguliwe kabla ya, 2025, ili watu wenye nia ya kugombea, na wana uwezo wa kuwaletea wananchi maendeleo, bila kupitia hizi nonsense za vyama waingie, washindane kwa hoja na sio kushindana kuhonga, kama hali inavyoendelea sasa!. Hili shurti la vyama lingekuwa limendolewa, mngeweza kushangaa watu wazalendo wa kweli wa nchi hii, kama kina Reginald Mengi, Ali Mfuruki, Yogesh Manek, SS Bakhresa, Pascal Mayalla, and the like, wenye uchungu wa dhati na umasikini wa taifa hili, wangejitokeza kugombea kuwatumikia wananchi!.

Kiongozi Akiishachaguliwa, Anakuwa ni Kiongozi wa Watu, na Sio Kiongozi wa Chama, Kwa Sababu Anachaguliwa na Watu na Sio Chama!.
Kiukweli kwenye hili jambo, kuna ujinga mwingi!, ujinga mwingine mkubwa kabisa ni huu, hata kama mgombea amedhaminiwa na chama cha siasa kugombea, akiishapitishwa na Tume ya Uchaguzi kuwa Mgombea, japo anatambulika kama ni mgombea wa chama fulani, lakini akiishachaguliwa, mwenyekiti wa mtaa, diwani, mbunge au rais, anakuwa sio kiongozi tena wa chama kilichomdhamini, bali sasa anakuwa ni kiongozi wa umma, kiongozi wa wananchi. Mfano baada ya rais Magufuli kuchaguliwa kuwa rais kwa tiketi ya CCM, lakini hakuchaguliwa na wana CCM pekee, amechaguliwa na Watanzania wote, yeye anakuwa sio kiongozi wa CCM bali kiongozi wa Watanzania wote, vivyo hivyo kwa wabunge, madiwani na viongozi wa serikali ya mtaa, kitendo cha mtu ambaye ni kiungozi wa umma, kujitoa chama na kupoteza ubunge, udiwani au uongozi wa umma, ni ujinga ambao haupaswi kuvumiliwa. Nini muhimu kati ya umma na chama?. Kuukosesha umma kiongozi wao waliemchagua kwa sababu za chama, sio tuu sio haki kwa wananchi waliomchagua, bali pia ni dhambi, kuwalipisha masikini hawa gharama za uchaguzi wa marudio kwa sababu za kijinga!.

Nini Kifanyike, A Way Forward.
Kama nilivyowahi kushauri humu, ukosoaji wenye kujenga, huandamana na ushauri wa nini kifanyike kurekebisha kasoro hizi ili kuundoa ujinga huu unaoendelea nchini mwetu kwa sasa kwa viongozi wa umma kuhama vyama na kupoteza uongozi wa umma.

1. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amri Jeshi Mkuu, Samia Suluhu Hassan asiruhusu ule ujinga wa kuhama vyama unaosababisha hasara kwa taifa, kwa kuwashukuru kumuunga mkono na kuunga mkono juhudi zake, lakini wabaki huko huko kwenye vyama vyao, hadi 2025, wakiishamaliza muhula wao, ndipo wajitoe na kuhama vyama!.

2. Ikulu ni mahali patakatifu, Rais wa Nchi, akiwa Ikulu yetu, atenganisha kofia zake mbili za rais wa nchi na Mwenyekiti wa chama cha CCM, rais wetu akiwa Ikulu yetu afanye kazi takatifu, asiendeshee vikao vya CCM, pale patakatifu petu, vikao vya CCM akavifanyie ofisi ya CCM Lumumba au kumbi za CCM Dodoma. Japo hakuna kosa lolote kuendeshea vikao vya CCM Ikulu yetu, lakini halileti picha nzuri kwa rais wetu, ambaye ni mpenda haki, kwa sababu yeye sio rais wa CCM ni rais wa Watanzania wote.

3. Tubadili sheria yetu ya uchaguzi, kwa kufuta chaguzi zote ndogo, na tuanzishe utaratibu wa proportional representation kwa mwenye kura nyingi ndiye mshindi, lakini likitokea lolote, akasita kuwa rais, mbunge au diwani, yule aliyemfuatia katika uchaguzi uliopita ndio anatangazwa mbunge, kama hayupo anachuliwa mtu wa tatu, hadi wa mwisho, kama wote hawapo, ndipo uchaguzi mdogo unafanyika.

4. Kile kipengele cha kudhaminiwa na chama kiishie kwenye uteuzi tuu, kiongozi akiishachaguliwa, anakuwa kiongozi wa watu, anaweza kuhama chama bila kupoteza uongozi wake kama ilivyo nchini Kenya na nchi nyingine zenye kuheshimu demokrasia ya kweli na sio hii demokrasia fake ya vyama!.

5. Tubadili sheria yetu ya uchaguzi, kwa kuondoa kipengele cha kudhaminiwa na vyama ili kila Mtanzania mwenye sifa za kugombea uongozi wa nafasi yoyote, aruhusiwe, ila kwenye urais, tuweke vigezo vya ziada, ili asijetokea tajiri mmoja mwenye ukwasi wa kuwanunua watanzania wote, tukajikuta tuna rais wa kununuliwa. Ila kwenye ubunge, udiwani na serikali za mtaa, kila mtu awe free kugombea, hivyo tuwe na wagombea huru, na hili likifanyika hata sisi tusio na vyama tutashiriki, mfano mimi, naweza kabisa kugombea jimbo fulani na kulitwaa kama kuokota embe dodo lililojiangukia, ambapo mbunge wa hapo, nitamsukuma kama nimesukuma mlevi!.

6. Tuibadili Tume yetu ya Uchaguzi iwe Tume Huru zaidi na Shirikishi, tujenge uwanja sawa wa ushindani wa haki kwa vyama vyote, uchaguzi uendeshwe kwa transparency ya hali ya juu kwa kuruhusu mawakala hadi kwenye tallying, na vyama au taasisi zozote ziwe free kuwa na tallying centers zake, kitu ambacho hakitaruhusiwa na talling centers hizo ni kutangaza matokeo, kama matokeo yote ya uchaguzi hadi wa rais yanahesabiwa kituoni na kubandikwa ukutani, kama hakuna jambo lolote la kificho, yaani nothing to hide, kwanini uzuie independent tallying?!. Uchaguzi wa 2020, kila mwenye uwezo wa kufanya tallying aruhusiwe afanye ila sitangaze matokeo, hii itazuia bao la mkono!

Hitimisho.
Tanzania tumebarikiwa kumpata rais mpenda haki na mtenda haki, tumuombe kubadili sheria ya uchaguzi na Tume ya Taifa ya Uchaguzi, NEC wasimamie toka uchaguzi wa serikali za mitaa mpaka Uchaguzi Mkuu

Mungu Ibariki Tanzania

Paskall
Ukiendelea kuwa muungwana kwa kuongea vitu vinavyoiponya Tanganyika kama hili bandiko la kizalendo, hakika tutakurudishia hadhi ya nyota 7 ambayo hapa katikati uliipoteza.
 
Sasa hivi akili zako zimerudi baada ya kukosa teuzi? Shenzi kabisa mnafiki mkubwa.ijiharibia mwenyewe pengine ili uanze upya nenda hukoupinzani ukaanze kupopoma
 
Wanabodi,
Kama kawaida yangu kila nipatapo fursa huja na makala zangu elimishi za Kwa Maslahi ya Taifa, leo naendelea na sehemu nyingine ya Ijue Katiba ya JMT kwa jicho la mtunga katiba. Sehemu ya kwanza nilifundisha katiba ni nini na katiba ni ya nani. Sehemu ya pili nikazungumzia Mtunga katiba alimaanisha nini aliposema Katiba ni Sheria Mama.

Sii wengi wanafahamu Bunge letu Tukufu linaporidhia mkataba wowote wa kimataifa, mfano ile IGA ya ajabu ajabu ya DPW, maana yake hicho kilichoridhiwa kwenye huo kinakuwa ni sehemu ya sheria zetu under local laws!.

Licha ya mapungufu yote ya kisheria ya ile IGA kuna upungufu mmoja mkubwa ambao hakutajwa sana, huu ni upungufu wa illegality. IGA ile ya DPW na Bandari zetu, ina illegality mbili.
Ya kwanza ni illegality ya the capacity of Dubai to contract an international Treaty, kwasababu Dubai sio nchi, haina sovereignty hivyo haina the capacity to enter into an international Treaty with a nation kama Tanzania, mwenye uwezo huo ni UAE tuu na hakukuwa na POA (power of attorney) kutoka UAE kuiwezesha Dubai kuingia an international Treaty!.

Illegality ya pili, mkataba ule una kipengele kilicho kinyume cha sheria zetu, hivyo it's an illegal contract, lakini Bunge letu Tukufu limeipitisha hivyo hivyo.

Bandiko hili ni la swali

Watanzania tutaendelea kusubiria mpaka lini wakati Bunge letu Tukufu likitunga Sheria batili na sometimes kuuchomekea ubatili huo hadi ndani ya Katiba yetu na kuifanya katiba yetu kuwa na vipengele batili?. Je Watanzania tufanye nini?, au tunaweza kulifanya nini Bunge la aina hii?.​


Hii sii mara ya kwanza kwa Bunge letu kutufanyia mambo ya ajabu kama haya!. Leo naomba niwaletee mifano Bunge letu Tukufu kutunga sheria batili inayokwenda kinyume cha katiba ya JMT. Kwa kuonyesha Katiba inasema nini, hiyo sheria batili ikasema nini, na mwisho kuonyesha sheria batili hiyo, imekinzana wapi na katiba ya JMT.
  1. Tuanze na Ibara ya 5 ya katiba ya JMT inasema
View attachment 2743038
Haki hii ndio haki kuu ya kwanza ya kidemokrasia, haki ya kupiga kura, japo haki hii bado ipo kwenye katiba yetu, haki hii imeingiliwa na kukiukwa na ukosekanaji wa haki ya kuchaguliwa, hivyo Watanzania kuruhusiwa kuwachagua sio viongozi wao wanaowapenda kwa uhuru, bali Watanzania wanalazimika kuwachagua viongozi waliopitishwa na wahuni fulani (kudhaminiwa na chama cha siasa), hivyo ni kukiuka nia njema ya mtunga katiba ya kila Mtanzania anakuwa na haki ya kupiga kura kuchagua kiongozi anamtaka kwa Tanzania ni kumchagua kiongozi chama kilicho wachagulia!.

2. Ibara ya 5 (2) inalipa Bunge mamlaka ya kutunga sheria kuzuia mtu kupiga kura
View attachment 2743067
Haki hii ya uhuru wa kupiga kura kuchagua ni moja ya haki zinazoitwa fundamental rights, yaani haki za msingi za binadamu.

3. Ibara ya 3 imelipa Bunge la JMT, mamlaka ya kutunga sheria ya uchaguzi
View attachment 2743072
Mamlaka haya ya Bunge kutunga sheria ya uchaguzi pia limewekewa masharti, hivyo Bunge halina mamlaka ya kutunga sheria inayokwenda kinyume cha katiba.

Kisha tuje ibara ya 21 ya katiba ya JMT
View attachment 2743182
Tuje ibara ya 39 ya katiba ya JMT.
View attachment 2743193
Tumalizie Ibara ya 67 ya Katiba ya JMT
View attachment 2743204
Baada ya kukuwekea vifungu, sasa twende taratibu nikuchambulie

Ibara hii ya 21 cha Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, inatoa haki ya kila Mtanzania mwenye sifa, kuwa huru kushiriki katika siasa na uongozi kuanzia serikali za mtaa hadi serikali kuu, bila ubaguzi wowote.
Uhuru wa kushiriki shughuli za umma
21.-(1) Bila ya kuathiri masharti ya ibara ya 5, ya Katiba hii na ya sheria za nchi kuhusiana na masharti ya kuchagua na kuchaguliwa, au kuteua na kuteuliwa kushiriki katika shughuli za utawala wa nchi, kila raia wa Jamhuri ya Muungano anayo haki ya kushiriki katika shughuli za utawala wa nchi, ama moja kwa moja au kwa kupitia wawakilishi waliochaguliwa na wananchi kwa hiari yao, kwa kuzingatia utaratibu uliowekwa na sheria au kwa mujibu wa sheria.


Lakini kukafanyika uhuni fulani kwa maslahi ya watu fulani na chama fulani kwa vile serikali ni yao, wakaipindua katiba kwa kuinyofoa haki hiyo ya kila mtu kushiriki siasa, iliyotolewa na katiba, na kupachika shurti la kudhaminiwa na chama cha siasa hivyo kujenga ubaguzi katika kushiriki shughuli za uongozi umma kwa watu kulazimishwa kwanza kujiunga na vyama vya siasa, ndipo upate haki ya kugombee nafasi yoyote ya uongozi wa umma, huku sio kuwatendea haki Watanzania wengine wote, wasiotaka kujiunga na vyama vyovyote vya siasa, kutokana na kuviona karibu vyama vyote ni vyama vya hovyo hovyo, ispokuwa chama kimoja, lakini kuna watu wazuri na wana uwezo mkubwa wa uongozi, hawawezi kugombea uongozi kwasababu ya ujinga huo!.

Hii ni haki muhimu iliyotolewa na katiba, kitendo cha kuingiza shurti la kudhaminiwa na chama cha siasa ni kinyume cha katiba. Hivyo sheria hii ibadilishwe ili kukidhi kile ambacho mtunga katiba ilidhamiria ilipoiweka haki hii, ndani ya katiba yetu!, hivyo baada ya mabadiliko hayo ya mlango wa nyuma, kipengele hicho sasa kinasomeka hivi

Uhuru wa kushiriki shughuli za umma Sheria ya 1984 Na.15 ib.6 Sheria ya 1994 Na.34 ya ib.4
21.-(1) Bila ya kuathiri masharti ya ibara ya 5, ya 39 na ya 67 ya Katiba hii na ya sheria za nchi kuhusiana na masharti ya kuchagua na kuchaguliwa, au kuteua na kuteuliwa kushiriki katika shughuli za utawala wa nchi, kila raia wa Jamhuri ya Muungano anayo haki ya kushiriki katika shughuli za utawala wa nchi, ama moja kwa moja au kwa kupitia wawakilishi waliochaguliwa na wananchi kwa hiari yao, kwa kuzingatia utaratibu uliowekwa na sheria au kwa mujibu wa sheria.


Ule uhuru uliotolewa na Katiba wa kila mtu kuwa huru kushiriki shughuli za uongozi, kupitia ibara ya 21, umekuja kunyofolewa na ibara ya 39 na 67 (b)(c) kwa kuweka sherti, ili mtu kuweza kugombea nafasi yoyote ya uongozi wa umma, ni lazima awe ni mwanachama, na mgombea aliyependekezwa na chama cha siasa hivyo lazima adhaminiwe na chama cha siasa!, Haki zinatolewa na ibara moja halafu zinaporwa na ibara nyingine ya katiba hiyo hiyo!.

Mchungaji Mtikila (Mungu amuweke mahala pema peponi), mwaka 1993, alifungua kesi No. 5 ya 1993, alifanya juhudi kubwa kukipinga kifungu hiki na Mahakama Kuu kupitia kwa Jaji Lugakingira, (Mungu amuweke mahala pema peponi), ikatamka wazi na bayana kipengele hicho ni batili na kinakiuka katiba ya JMT ya mwaka 1977, hivyo kifutwe, na kutoa haki kwa kila Mtanzania ana haki ya kushiriki kugombea Uongozi wowote wa nchi.

Baada tuu ya Mtikila kushinda kesi serikali ikafanya mambo mawili makubwa ya ajabu!, kwanza ilikata rufaa!. Hivi kwa uamuzi kama huu, serikali ilikata rufaa kwa maslahi ya nani?. Wiki iliyopita nilisema ile Ibara ya 64(5) iayotamka Katiba ni sheria Mama, sheria nyingine yoyote inayokwenda kinyume cha katiba ni batili, aliyebatilisha sheria batili ni katiba yenyewe na sio Mahakama!. Kazi ya Mahakama ni kutamka tuu huo ubatili na tangu baada ya tamko hilo, sheria hiyo inakuwa tayari ni imebatika!, unawezaje kukata rufaa kwa kitu kilicho batilishwa na katiba?. Kiukweli kabisa hili ni jambo la ajabu sana!.

Jambo la pili la ajabu sana na kubwa ya mwaka ni serikali yetu ilipeleka bungeni kwa hati ya dharura, sheria No. 34 ya mwaka 1994, kufanya marekebisho ya 8 ya Katiba ya JMT na kukichomeka kipengele hicho ndani ya katiba, hivyo kuibatilisha ile hukumu ya Jaji Lugakingira!. Hapa ndipo ujinga unapoanzia katika siasa zetu kwa serikali kufanya kazi kwa maslahi ya kisiasa ya watu fulani na chama fulani, hivyo kupoteza haki ya wengi kwa ajili ya kuwanufaisha wachache!..

Hiki kilichofanyika, mimi nakiita ni kitendo cha kihuni!, Watanzania tulifanyiwa uhuni na serikali yetu, kwa kuinajisi katiba yetu!, kitu kimeelezwa ni kinyume cha katiba, kinatoa haki zilizotolewa na katiba, halafu serikali hiyo inakuja kuihalalisha haramu hiyo kwa kuiingiza rasmi kwenye katiba!, huku sii kuinajisi katiba yetu?.

Mchungaji Mtikila, licha ya kuwa ni mwanasiasa, Mwenyekiti wa chama cha siasa cha DP, (Democratic Party), lakini alikuwa ni mtu wa Mungu kiukweli kabisa, kwa sababu hakukubali kabisa katiba yetu inajisiwe!, hivyo akafungua kesi nyingine No. 10 ya mwaka 2009 kupinga marekebisho hayo ya 8 ya katiba na kuyaita ni ubatili!.

Katika kesi hiyo, Mchungaji Mtikila aliomba mambo mawili makuu

(a) Mahakama itamke ibara 39 na 67 za katiba zilizorekebishwa na marekebisho ya 8 kwa sharia No. 34 ya mwaka 1994, ni batili na kinyume cha katiba.

(b) Kutamka wazi kuwa Kila Mtanzania ana haki ya kugombea kwa mujibu wa ibara ya 21 ya Katiba, bila kulazimishwa kudhaminiwa na chama cha siasa, hivyo mtu anaweza kugombea kama mgombea binafsi.

Mahakama Kuu chini ya majaji watatu, (majaji watatu kisheria inaitwa Half Bench), Manento, Masati na Mihayo, wakayakubali mambo yote ya Mchungaji Mtikila na kumpa ushindi tena kwa kutamka marekebisho hayo ya katiba ni batili!. Lakini serikali yetu ilivyo ya ajabu, ikakata tena rufaa, na safari hii Mahakama Kuu ikakaa Full Bench ya majaji 7, chini ya Jaji Mkuu Mwenyewe, Agustino Ramadhani, akisaidiwa na Jaji Eusebio Munuo, Jaji January Msoffe, Jaji Natalia Kimaro, Jaji Kassim Mbarouk, Jaji Benard Luanda, na Jaji Sauda Mjasir, ambapo tarehe 17 mwezi June, mwaka 2010 ikatoa hukumu ya ajabu kabisa kuwa kutokea Tanzania!.

Tena Mahakama ya rufaa haikuwa peke yake, bali iliwaita mabinga wabobezi na wabobevu wa sheria na katiba kuisaidia, hawa wanaitwa marafiki wa mahakama, kwa kiingereza ni friends of the Court, kisheria wanaitwa Amicus Curiae, hivyo ma Amicus Curiae hawa, Mr. Othman Masoud, Prof. Palamagamba Kabudi, na Prof.Jwan Mwaikusa(Mungu Aiweke Roho yake Mahala Pema Peponi).

Uamuzi wa Mahakama Kuu ya Rufaa uliamua kitu cha ajabu sana na hapa naomba kunukuu
“So as to let the will of the people prevail as to whether or not such [independent] candidates are suitable. We are definite that the Courts are not the custodian of the will of the people. That is the property of elected Members of Parliament”.

Hii kiukweli ni kauli ya ajabu sana kutolewa na mahakama yetu kwenye jambo zito na muhimu kama hili!. Kitendo cha Mahakama kujivua jukumu la kuwa the custodian of the will of the people!, ni kitendo cha ajabu sana na kushangaza sana!. Hakuna will of the people kubwa kuliko katiba!, kama katiba imetoa haki fulani, halafu Bunge likatunga sheria ya ajabu kabisa kuifuta haki hiyo, halafu mahakama ikatamka haiwezi kuliingilia Bunge!, where is the doctrine of separation of powers, checks and balance?!.

Kwa ajili ya kulinda heshima ya Mahakama Kuu, naomba niweke ilichokisema bila kukitafsiri.

“In our case, we say that the issue of independent candidates has to be settled by Parliament which has the jurisdiction to amend the Constitution and not the Courts which, as we have found, do not have that jurisdiction. The decision on whether or not to introduce independent candidates depends on the social needs of each State based on its historical reality. Thus the issue of independent candidates is political and not legal However, we give a word of advice to both the Attorney General and our Parliament: The United Nations Human Rights Committee, in paragraph 21 of its General Comment No. 25, of July 12, 1996, said as follows on Article 25 of the International Covenant on Civil and Political Rights, very similarly worded as Art 23 of the American Convention and our Art 21: The right of persons to stand for election should not be limited unreasonably by requiring candidates to be members of
parties or of specific parties. Tanzania is known for our good record on human rights and particularly our militancy for the right to self determination and hence our involvement in the liberation struggle. We should seriously ponder that comment from a Committee of the United Nations, that is, the whole world.
DATED at DAR ES SALAAM this 17th day of June, 2010”


Mahakama ya Rufaa ikaamua kuwa Mahakama haina mamlaka ya kuliingilia Bunge, katika vipengele vya katiba, kumaanisha kwa vile marekebisho hayo ya 8 yamefanywa na Bunge, hivyo ni Bunge ndio lirekebishe kipengele hicho!, kiukweli kabisa, kwa maoni yangu, uamuzi huu sio utii wa mhimili wa Mahakama kwa mhimili Bunge, bali huu ni ukondoo wa hali ya juu kwa Mhimili wa Mahakama kwa serikali kwa manufaa ya watu wachache!.

Uchaguzi wa Mwaka 2015 ukalithibitisha hili, kumbe baadhi ya majaji wetu ni makada!, Jaji Mkuu Mstaafu aliyeongoza jopo hilo, alichukua fomu kugombea urais!, for what my God?!. Baadhi ya wale ma amicus curiae naamini tunawajua na tunawaona na ukada wao!. Unategemea nini kama sheria za nchi hii zitafinyangwa finyangwa kwa manufaa ya wachache?!. President Samia must stop this nonsense!.

Japo Lengo la Kudhaminiwa na Chama ni zuri, ila Huu Sii Ujinga Tuu?!.
Katiba ilisema kila Mtanzania ana haki ya kushiriki uongozi, hili sherti la kudhaminiwa na chama lilitoka wapi? na kwa kwa nini watu walazimishwe kuwa wanachama wa vyama ili wadhaminiwe, ndipo waweze kugombea?. Mfano mimi, sina chama kwa sababu naziona siasa za vyama ni za hovyo hovyo, ikitokea nina uwezo wa kuwatumikia wananchi wa eneo langu na kuwaletea maendeleo bila kupitia chama chochote, kwa nini nizuiliwe?!. Kiukweli kabisa, kwa maoni yangu, huu ni ujinga uliopitiliza!, tutaliacha Bunge letu Tukufu kutufanyia ujinga huu mpaka lini?, is this not nonsense?.

Watanzania tusikubali ujinga huu uendelee hadi 2025!, tupiganie milango ya wagombea binafsi ifunguliwe kabla ya, 2025, ili watu wenye nia ya kugombea, na wana uwezo wa kuwaletea wananchi maendeleo, bila kupitia hizi nonsense za vyama waingie, washindane kwa hoja na sio kushindana kuhonga, kama hali inavyoendelea sasa!. Hili shurti la vyama lingekuwa limendolewa, mngeweza kushangaa watu wazalendo wa kweli wa nchi hii, kama kina Reginald Mengi, Ali Mfuruki, Yogesh Manek, SS Bakhresa, Pascal Mayalla, and the like, wenye uchungu wa dhati na umasikini wa taifa hili, wangejitokeza kugombea kuwatumikia wananchi!.

Kiongozi Akiishachaguliwa, Anakuwa ni Kiongozi wa Watu, na Sio Kiongozi wa Chama, Kwa Sababu Anachaguliwa na Watu na Sio Chama!.
Kiukweli kwenye hili jambo, kuna ujinga mwingi!, ujinga mwingine mkubwa kabisa ni huu, hata kama mgombea amedhaminiwa na chama cha siasa kugombea, akiishapitishwa na Tume ya Uchaguzi kuwa Mgombea, japo anatambulika kama ni mgombea wa chama fulani, lakini akiishachaguliwa, mwenyekiti wa mtaa, diwani, mbunge au rais, anakuwa sio kiongozi tena wa chama kilichomdhamini, bali sasa anakuwa ni kiongozi wa umma, kiongozi wa wananchi. Mfano baada ya rais Magufuli kuchaguliwa kuwa rais kwa tiketi ya CCM, lakini hakuchaguliwa na wana CCM pekee, amechaguliwa na Watanzania wote, yeye anakuwa sio kiongozi wa CCM bali kiongozi wa Watanzania wote, vivyo hivyo kwa wabunge, madiwani na viongozi wa serikali ya mtaa, kitendo cha mtu ambaye ni kiungozi wa umma, kujitoa chama na kupoteza ubunge, udiwani au uongozi wa umma, ni ujinga ambao haupaswi kuvumiliwa. Nini muhimu kati ya umma na chama?. Kuukosesha umma kiongozi wao waliemchagua kwa sababu za chama, sio tuu sio haki kwa wananchi waliomchagua, bali pia ni dhambi, kuwalipisha masikini hawa gharama za uchaguzi wa marudio kwa sababu za kijinga!.

Nini Kifanyike, A Way Forward.
Kama nilivyowahi kushauri humu, ukosoaji wenye kujenga, huandamana na ushauri wa nini kifanyike kurekebisha kasoro hizi ili kuundoa ujinga huu unaoendelea nchini mwetu kwa sasa kwa viongozi wa umma kuhama vyama na kupoteza uongozi wa umma.

1. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amri Jeshi Mkuu, Samia Suluhu Hassan asiruhusu ule ujinga wa kuhama vyama unaosababisha hasara kwa taifa, kwa kuwashukuru kumuunga mkono na kuunga mkono juhudi zake, lakini wabaki huko huko kwenye vyama vyao, hadi 2025, wakiishamaliza muhula wao, ndipo wajitoe na kuhama vyama!.

2. Ikulu ni mahali patakatifu, Rais wa Nchi, akiwa Ikulu yetu, atenganisha kofia zake mbili za rais wa nchi na Mwenyekiti wa chama cha CCM, rais wetu akiwa Ikulu yetu afanye kazi takatifu, asiendeshee vikao vya CCM, pale patakatifu petu, vikao vya CCM akavifanyie ofisi ya CCM Lumumba au kumbi za CCM Dodoma. Japo hakuna kosa lolote kuendeshea vikao vya CCM Ikulu yetu, lakini halileti picha nzuri kwa rais wetu, ambaye ni mpenda haki, kwa sababu yeye sio rais wa CCM ni rais wa Watanzania wote.

3. Tubadili sheria yetu ya uchaguzi, kwa kufuta chaguzi zote ndogo, na tuanzishe utaratibu wa proportional representation kwa mwenye kura nyingi ndiye mshindi, lakini likitokea lolote, akasita kuwa rais, mbunge au diwani, yule aliyemfuatia katika uchaguzi uliopita ndio anatangazwa mbunge, kama hayupo anachuliwa mtu wa tatu, hadi wa mwisho, kama wote hawapo, ndipo uchaguzi mdogo unafanyika.

4. Kile kipengele cha kudhaminiwa na chama kiishie kwenye uteuzi tuu, kiongozi akiishachaguliwa, anakuwa kiongozi wa watu, anaweza kuhama chama bila kupoteza uongozi wake kama ilivyo nchini Kenya na nchi nyingine zenye kuheshimu demokrasia ya kweli na sio hii demokrasia fake ya vyama!.

5. Tubadili sheria yetu ya uchaguzi, kwa kuondoa kipengele cha kudhaminiwa na vyama ili kila Mtanzania mwenye sifa za kugombea uongozi wa nafasi yoyote, aruhusiwe, ila kwenye urais, tuweke vigezo vya ziada, ili asijetokea tajiri mmoja mwenye ukwasi wa kuwanunua watanzania wote, tukajikuta tuna rais wa kununuliwa. Ila kwenye ubunge, udiwani na serikali za mtaa, kila mtu awe free kugombea, hivyo tuwe na wagombea huru, na hili likifanyika hata sisi tusio na vyama tutashiriki, mfano mimi, naweza kabisa kugombea jimbo fulani na kulitwaa kama kuokota embe dodo lililojiangukia, ambapo mbunge wa hapo, nitamsukuma kama nimesukuma mlevi!.

6. Tuibadili Tume yetu ya Uchaguzi iwe Tume Huru zaidi na Shirikishi, tujenge uwanja sawa wa ushindani wa haki kwa vyama vyote, uchaguzi uendeshwe kwa transparency ya hali ya juu kwa kuruhusu mawakala hadi kwenye tallying, na vyama au taasisi zozote ziwe free kuwa na tallying centers zake, kitu ambacho hakitaruhusiwa na talling centers hizo ni kutangaza matokeo, kama matokeo yote ya uchaguzi hadi wa rais yanahesabiwa kituoni na kubandikwa ukutani, kama hakuna jambo lolote la kificho, yaani nothing to hide, kwanini uzuie independent tallying?!. Uchaguzi wa 2020, kila mwenye uwezo wa kufanya tallying aruhusiwe afanye ila sitangaze matokeo, hii itazuia bao la mkono!

Hitimisho.
Tanzania tumebarikiwa kumpata rais mpenda haki na mtenda haki, tumuombe kubadili sheria ya uchaguzi na Tume ya Taifa ya Uchaguzi, NEC wasimamie toka uchaguzi wa serikali za mitaa mpaka Uchaguzi Mkuu

Mungu Ibariki Tanzania

Paskall
Hii hoja sio yako ni ya Mtikila wewe hauna uwezo huo wa kuchambua mambo haya
 
Back
Top Bottom