Maoni yangu kwenye Mkutano wa Vyama vya Siasa kuhusu Muswada wa Sheria Mpya ya Uchaguzi. Muswada sio batilifu, ni Muswada batili

Pascal Mayalla

Platinum Member
Sep 22, 2008
50,498
113,604
Wanabodi,

Sina uhakika sana humu JF, lakini kati ya JF members wanaozungumzia sana, Katiba, Sheria na Haki, mimi ni mmoja wao.

Nimeandika sana kuhusu katiba, sheria na haki toka enzi za JPM. Rais Samia alipoingia, nimeandika sana kuhusu katiba, sheria na haki.

Rais Samia alipounda Kikosi Kazi tulimpongeza.

Alipopokea Ripoti ya Kikosi Kazi, na kuahidi kufanya mabadiliko ya Sheria ya Uchaguzi, Tume ya Uchaguzi na Sheria ya Vyama vya Siasa tulimpongeza.

Mkutano wa Kutoa Mapendekezo kuhusu sheria hizi, mimi ni miongoni mwa tulioalikwa kutoa mawazo yetu, na mimi ni miongoni mwa tulibahatika kuchangia.

Mchango wangu ni huu
View: https://youtu.be/PBpjDhH2XiA?si=GjujW1--LkjxAKOf

Na kwa faida ya wale ambao bundle ni issue naomba niwa paraphrasie

Utangulizi
Naomba nijitambulishe rasmi, mimi ni mwandishi wa habari mkongwe, nimeripoti toka mwaka 1994, ule uchaguzi wa Jimbo la Kwahani, Zanzibar ambao ndio ulikuwa uchaguzi wa kwanza wa vyama vingi, na uchaguzi mkuu wa mwaka 1995 nimeendesha kipindi cha kwanza cha talk show kwenye TV za Tanzania, kipindi cha Mada Moto ile 1995 na baadae kipindi cha Kiti Moto.

Ni mimi ndiye niliyetangaza yale matokeo halali ya uchaguzi wa Zanzibar mwaka 1995, naomba tusirudie kilichotokea. Kwa sasa licha ya kuwa ni mwandishi wa habari, pia ni mwanasheria na wakili wa kujitegemea.

1. Kwanza, kwa niaba ya Jukwaa la Wahariri, naomba kutoa shukrani za dhati kwa Msajili wa vyama, Jaji Mstaafu, Francis Mutungi, kwa kutushirikisha media na kutu engage the media kupitia Jukwaa la Wahariri na kutufanya ni wadau muhimu kwenye huu mchakato.

Vyombo vya habari ni mhimili, ni mhimili wa nne usio rasmi ambao unaunganisha ile mihimili rasmi mitatu na wananchi.

Ukiwa na jambo, haliwezi kufika kule chini kwa wananchi, bila kupitia kwetu sisi waandishi wa habari na kama kuna jambo huku chini, ni kupitia kwetu sisi waandishi wa habari, linawafikia huko juu.

Ombi: Naomba Media zetu zote za public na private, zime engaged na kuwezeshwa kutoa elimu ya uraia kwa Watanzania kuhusu katiba, sheria, haki na wajibu.

2. Naomba kumpongeza Rais Samia kuunda kikosi kazi na kumpongeza kutaka wananchi wafundishwe kuhusu katiba yao, naomba kuongezea sio wananchi tuu wafundishwe kuhusu katiba, bali vyama vya siasa vifundishwe kuhusu katiba, serikali ifundishwe kuhusu katiba, Bunge lifundishwe kuhusu katiba, Mahakama ifundishwe kuhusu Katiba, katiba ndio kila kitu.

Tatu, mwisho Ibara ya 5 ya katiba ya JMT, imetoa haki kwa kila Mtanzania aliyetimiza umri wa miaka 18, kupiga kura kuchagua viongozi anaowataka, na ibara ya 21, inatoa haki kwa kila Mtanzania aliyetimiza umri wa miaka 21, kuwa huru kugombea nafasi yoyote ya uongozi toka serikali ya mtaa hadi serikali kuu bila masherti yoyote kandamizi. Hivyo ndivyo katiba ya JMT ya mwaka 1977 inavyosema, na hiyo ndio dhima ya mtunga katiba.

Kukatokea mambo fulani hapa katikati, ikatungwa sheria ya uchaguzi yenye kipengele batili, kikaweka shurti batili, ili Mtanzania aweze kugombea, shurti ajiunge na chama cha siasa, na adhaminiwe na chama cha siasa!. Hili ni shurti batili linalokwenda kinyume cha katiba ya JMT, na shurti hili batili, limechomekewa kiubatili ndani ya katiba yetu, Mahakama Kuu ya Tanzania iliishatangaza, ilikuwa Bunge liuondoe ubatili huu, sijui ni kwa nini huu ubatili uko ndani ya katiba yetu mpaka sasa?

Naomba ndugu Mwenyekiti, pendekezo hili liingizwe, lile shurti la kudhaminiwa na chama cha siasa kumlazimisha Mtanzania ili kugombea, liondolewe, ni shurti batili kinyume cha katiba, ili kila Mtanzania awe huru kugombea.

Kwa hiyo, naomba sasa, Ili Uchaguzi wa 2025 uwe wa haki, na Mama Samia ameisha onyesha kwa dhamira ya dhati, kwa kauli na matendo, anataka Watanzania watendewe haki, ili kila Mtanzania mwenye nia ya kugombea, awe huru kugombea, kuna viongozi wazuri wanataka kuwatumikia Watanzania, lakini wanawekewa kauzibe ndani ya vyama vyao, kwasababu wanaonekana "sio wenzetu".

Paskali
 
Pasco

Huu mkutano hauna maana yoyote ni danganya toto. Mzee Mmoja aliongea kutoka Zanzibar, ikaombwa taarifa kutoka kwa CCM. Meza kuu ikashadidia na hata kupiga makofi badala ya kujadili hoja ya yule Mzee kutoka Zanzibar

Waliokaa pale meza kuu ni watu wanaogopa nafasi zao si masilahi ya nchi. Wapo pale wakijikomba komba tu na ku,pendeza , hawana vision yoyote ya nchi. Kwakweli nchi yetu ina matatizo sana, wale ndio wasomi!

Hoja ya Mzee wa Unguja ilikuwa rahisi , hakuna mabadiliko ya maana bila kubadili Katiba na hili ni ukweli mtupu.

Tume huru ni hoja za Zitto na ACT, watu wasiojifunza kutoka Tume Huru ya Zanzibar chini ya Jecha.

Pili, Rais SSH hana nia njema. Laiti ingekuwepo asingeunda kikosi kazi kuua maoni ya tume ya Mzee Warioba.
Kikosi kazi hakikuhoji Watanzania kama Tume ya Mzee Warioba ilivyofanya chini ya Wazee wa Busara.
Rais SSH anatuaminisha kuwa Mkandara na wenzake wana busara kuliko Warioba, Butiku na Salim Ahmed!!

Sikubaliani na mikutano ya kupoteza muda, hakuna tume huru kwasababu mazingira ya uwepo wake hayapo.
Katiba ya JMT na tume huru haiwezekani. Ni ubabaishaji kam kusema Mahakama ni huru!! hakuna uhuru.

Mapendekezo yanayojadiliwa ni upotezaji wa fedha na muda, hakuna nia njema.

Mapendekezo yatajadiliwa na CCM Bungeni halafu uamini nia njema! CCM hawa wa miaka 60 ya umasikini

Tunahitaji rasimu ya Warioba na Katiba mpya!
 
Pasco

Huu mkutano hauna maana yoyote ni danganya toto. Mzee Mmoja aliongea kutoka Zanzibar, ikaombwa taarifa kutoka kwa CCM. Meza kuu ikashadidia na hata kupiga makofi badala ya kujadili hoja ya yule Mzee kutoka Zanzibar

Waliokaa pale meza kuu ni watu wanaogopa nafasi zao si masilahi ya nchi. Wapo pale wakijikomba komba tu na ku,pendeza , hawana vision yoyote ya nchi. Kwakweli nchi yetu ina matatizo sana, wale ndio wasomi!

Hoja ya Mzee wa Unguja ilikuwa rahisi , hakuna mabadiliko ya maana bila kubadili Katiba na hili ni ukweli mtupu.

Tume huru ni hoja za Zitto na ACT, watu wasiojifunza kutoka Tume Huru ya Zanzibar chini ya Jecha.

Pili, Rais SSH hana nia njema. Laiti ingekuwepo asingeunda kikosi kazi kuua maoni ya tume ya Mzee Warioba.
Kikosi kazi hakikuhoji Watanzania kama Tume ya Mzee Warioba ilivyofanya chini ya Wazee wa Busara.
Rais SSH anatuaminisha kuwa Mkandara na wenzake wana busara kuliko Warioba, Butiku na Salim Ahmed!!

Sikubaliani na mikutano ya kupoteza muda, hakuna tume huru kwasababu mazingira ya uwepo wake hayapo.
Katiba ya JMT na tume huru haiwezekani. Ni ubabaishaji kam kusema Mahakama ni huru!! hakuna uhuru.

Mapendekezo yanayojadiliwa ni upotezaji wa fedha na muda, hakuna nia njema.

Mapendekezo yatajadiliwa na CCM Bungeni halafu uamini nia njema! CCM hawa wa miaka 60 ya umasikini

Tunahitaji rasimu ya Warioba na Katiba mpya!
Rasimu ya Warioba ndio mpango mzima !
Mengine yote ni porojo na Abracadabra za ku-buy time !
Kila atakapokuja mwingine atakuja na ngonjera zake !!
Rasimu ya Warioba ilimaliza kila kitu na ipo valid na itaendelea kuwa valid kwa miaka mingi sana !
Katiba yeyote huko Duniani haijawahi kupitwa na wakati eti baada ya kupita miaka 10, huo ni ulaghai tu !
 
Rasimu ya Warioba ilimaliza kila kitu na ipo valid na itaendelea kuwa valid kwa miaka mingi sana !
Katiba yeyote huko Duniani haijawahi kupitwa na wakati eti baada ya kupita miaka 10, huo ni ulaghai tu !
Ni uongo mtupu, yaani wanataka tuamini endapo Rasimu ya Warioba ingepita 2014 baada ya muda Katiba ingebidi iandikwe upya. Maoni ya Rasimu ya Mzee Warioba yalilenga Katiba ya miaka mingi ndiyo maana ni fupi na mambo machache. Ni uongo tu eti imepitwa na wakati.

Tunachoaminishwa ni kwamba Kikosi kazi cha Mkandara kilichohoji watu wasiozidi 2,000 ni bora zaidi ya Rasimu ilihoji mamilion ya Watanzani.

Eti Mzee Warioba, Butiku na Salim Ahmed Salim hawajui lolote ila kikosi kazi cha Samia ndicho kina maoni.

Hii mikutano ya kupeana allowance waendelee nayo, Wananchi wana lao ; Rasimu ya Warioba! Katiba mpya
 
Hoja murua, sio tu itawapa haki ya kikatiba watanzania wote ya kuchagua na kuchaguliwa kwenye nafasi za uongozi, bali pia itaviondolea vyama vya siasa fimbo wanayoitumia kuwanyasa na kuwanyima uhuru wa kafanya kazi zao viongozi wanatokana na vyama vyao. Mambo ya kutishiwa kufutwa uanachama na kisha kupoteza ubunge n.k itakuwa mwisho.
 
Ni uongo mtupu, yaani wanataka tuamini endapo Rasimu ya Warioba ingepita 2014 baada ya muda Katiba ingebidi iandikwe upya. Maoni ya Rasimu ya Mzee Warioba yalilenga Katiba ya miaka mingi ndiyo maana ni fupi na mambo machache. Ni uongo tu eti imepitwa na wakati.

Tunachoaminishwa ni kwamba Kikosi kazi cha Mkandara kilichohoji watu wasiozidi 2,000 ni bora zaidi ya Rasimu ilihoji mamilion ya Watanzani.

Eti Mzee Warioba, Butiku na Salim Ahmed Salim hawajui lolote ila kikosi kazi cha Samia ndicho kina maoni.

Hii mikutano ya kupeana allowance waendelee nayo, Wananchi wana lao ; Rasimu ya Warioba! Katiba mpya
Kabisa !
Huwezi kuwadanganya watu wote kwa wakati wote !
Rasimu ya Warioba iwekwe mezani mengine yote ni porojo tu !
 
Wewe ndio ulitangaza DTV Maalim Serif ameshinda Urais Zanzibar kabla Nyerere hajapinduwa matokeo?
Yes ndio mimi, tulitumia matokeo ya ZEC jimbo kwa jimbo, wakati yamebaki majimbo mawili, ya Darajani na Wawi, tuka asume hata kura zote za majimbo hayo zikienda CCM, bado Maalim aliomgoza kwa margin kubwa!, siunajua mambo ya scup, tukaruka nayo!.

Hayo niliyo tangaza ndio yalikuwa matokeo OG!.

Hata ile 2015, niliwashauri vizuri sana jamaa zangu hawa Kumuepushia aibu ya Kushindwa, CCM isimsimamishe Dr. Shein hawakunisikia!. Matokeo ni Elections 2015 - Imethibitishwa pasi na shaka kuwa ni kweli kabisa, Zanzibar, Maalim Seif na CUF ndio walioshinda


P
 
Pasco

Huu mkutano hauna maana yoyote ni danganya toto. Mzee Mmoja aliongea kutoka Zanzibar, ikaombwa taarifa kutoka kwa CCM. Meza kuu ikashadidia na hata kupiga makofi badala ya kujadili hoja ya yule Mzee kutoka Zanzibar

Waliokaa pale meza kuu ni watu wanaogopa nafasi zao si masilahi ya nchi. Wapo pale wakijikomba komba tu na ku,pendeza , hawana vision yoyote ya nchi. Kwakweli nchi yetu ina matatizo sana, wale ndio wasomi!

Hoja ya Mzee wa Unguja ilikuwa rahisi , hakuna mabadiliko ya maana bila kubadili Katiba na hili ni ukweli mtupu.

Tume huru ni hoja za Zitto na ACT, watu wasiojifunza kutoka Tume Huru ya Zanzibar chini ya Jecha.

Pili, Rais SSH hana nia njema. Laiti ingekuwepo asingeunda kikosi kazi kuua maoni ya tume ya Mzee Warioba.
Kikosi kazi hakikuhoji Watanzania kama Tume ya Mzee Warioba ilivyofanya chini ya Wazee wa Busara.
Rais SSH anatuaminisha kuwa Mkandara na wenzake wana busara kuliko Warioba, Butiku na Salim Ahmed!!

Sikubaliani na mikutano ya kupoteza muda, hakuna tume huru kwasababu mazingira ya uwepo wake hayapo.
Katiba ya JMT na tume huru haiwezekani. Ni ubabaishaji kam kusema Mahakama ni huru!! hakuna uhuru.

Mapendekezo yanayojadiliwa ni upotezaji wa fedha na muda, hakuna nia njema.

Mapendekezo yatajadiliwa na CCM Bungeni halafu uamini nia njema! CCM hawa wa miaka 60 ya umasikini

Tunahitaji rasimu ya Warioba na Katiba mpya!
lets be optimistic!.
P
 
Back
Top Bottom