Mkuu wala usiwalalamikie hawa ni madalali na Makuhadi kazi yao ni kukushawishi wewe umchague EL sio kwamba wao wanampenda sana bali wameahidiwa pepo kama Boko Haram vile. Kwa hiyo kazi ipo kwetu sisi wapiga kura tumehadaika kiasi gani na nachoogopa ni hii kuishi kwa mazoea - Ombaomba!.Mkuu Mkandara nashangaa, na ndiyo maana nimesema hapo mwanzo, wanatudharau. Maana TeamLowasa wanajua jamaa yao ni mgonjwa, halafu kuna watu tunanunuliwa kuja kumpokea kwa bashasha kama mgombea pendwa wa chama.
respect wa boda sina dhamira ya kuendelea kubishana na wewe, maana hujaelewa, ama hutaki au umezingwa na hisia za mapenzi kwa mgombea wako, kuwa, kupima inawezekana kwa wagombea/watia nia wote, lakini kutangaza ni ngumu kwani "ethics" za kitabibu haziruhusu siri ya daktari na mgonjwa wake kutangazwa na daktari bali mgonjwa mwenye au mwakilishi wa mgonjwa kwa ridhaa ya mgonjwa.
nyinyi mlokubali kununuliwa na kuaminishwa upuuzi endeleeni kuamini Lowasa yuko fit; wenye kuona mbali twasema yu hoi bin taaban. Hata video aliyoweka FaizaFoxy hapo juu inaoneka hujaangalia kwa upofu wa hisia juu ya jamaa yenu.
Hongereni...
Hawa jamaa wanaulamba mkono hadi mabaki na harufu ya pilau hilo iishe, kesho EL hatakuwa naye maana kazi walotakiwa kuifanya wameifanya. All what matters ni kiasi gani wewe, mimi pamoja na wananchi wapiga kura wamehadaika kiasi gani na hii comedy ya mchaka mchaka Chinja! Arinselema Arijaa!