Mkuu
Nyunyu,
Yaani mimi hii leo nikawe team Lowassa, Team Ufisadi..!!! We jamaa wewe..
Kwenye bandiko langu lililopita nimesema kwamba ccm waweke
kipengere cha Kutangaza hadharani Ugonjwa wa Watiania wao kwakushawishiwa na wao wenyewe (Wagombea) Sasa Daktari atakuwa na kizuizi gani ikiwa mgonjwa mwenyewe ameamua ugonjwa wake uwe wazi? Wao si watakuwa wanajiamini wako fiti, sasa wataogopaje tena siri za vipimo vyao kuwa wazi? Mgombea pekee aliyetoa
suruhisho hilo ni Lowassa na ndo huyohuyo anayedaiwa kwamba anaumwa (Na hapa mi sipingi) Ninachokisema mimi hapa ni kwamba hao wengine wasiutumie ugonjwa wa Lowassa (kama upo) kujijenga wao na kumuangamiza yeye, Kwani ni yeye binafsi kasema yuko tayari kwenda kwenye vipimo..... Ubishi wangu uko wapi hapo?
Ikiwa unataka kubishana kwa hoja, nipo nimejaa tele. Lakini kama unataka kubishana ilmradi kubishana nipuuze mkuu.
Mchana Mwema.
BACK TANGANYIKA