Hili Tangazo la Timu Lowassa linatudharau!

Hili Tangazo la Timu Lowassa linatudharau!

Leteni hoja zingine...kama ugonjwa wengi tu humu ni wagonjwa...Wengine nawafahamu ni marehemu bado maziko...
In short ile tu kuzaliwa na kuishi Tanzania ni ugonjwa tosha....
Kama kuna anayebisha aende akapime afya yake hospitali ya maana!!!

Leteni zinazojadilika....
 
!.. Lile Ni Gonjwa Tu, Hata Anavyoongea Anaonekana Tu.
 
Lowasa anaumwa hata ukimwangalia usoni tu anaonyesha dalili ya kutaka tiba ya kimwili na kiroho.

Du, afadhali wewe mkuu umekuja na vipimo vya macho,

lakini huyu Lowasa ni Mbunge, ni Mjumbe wa NEC ya CCM na pia ni mwenyekiti wa moja ya kamati muhimu za bunge. haya magonjwa yanakuja baada ya kugombea uraisi? Kwanini tusiamini hizi ni siasa za maji taka toka kwa wapinzani wake wa kisiasa? Du, ile ya Richmond vp imefail????!!!
 
Lowassa ni Buheri wa afya njema,wabaya wake ndio wanaupanda ugonjwa kisa walikusudia kumlazimisha afe mapema kwa chemical kuleta mauti wakashindwa.

Japo mpaka leo hii wanatafuta mwanya wautumie kumdhuru,mbona aliwahimiza watangaza nia wakapimwe wote kama HAWATAKUTWA WENGINE NI HOI BIN TAABANI.

Ukweli chuki dhidi ya Lowassa imeongezeka zaidi kuliko wakati wowote ule hasa wakati huu wa KUMPATA RAIS MPYA WA AWAMU YA TANO.
 
Tazameni hii video, coordination ya mikono na pia coordinatio ya ulimi na anapojaribu kulifuta povu, pia na hilo povu zito hjeupe linalomtoka mdomoni linaonesha anatumia madawa makali sana.

Nilishauri zamani sana atumie bangi kutwa mara tatu, kuvuta na kunywa supu yake itamsaidia sana.



Ambaee haoni dalili za Lowassa kuwa ni mgonjwa basi nae huyo pia ni mgonjwa.
 
Last edited by a moderator:
Ndugu na Jamaa zangu nawaomba wala msiumize vichwa vyenu na hawa jamaa kwa sababu hivi ndivyo viashirio vyenyewe ya kuwa ADUI MKUBWA wa UMASKINI ni sisi MASKINI wenyewe. Tunaishi kwa mazoea - Kwetu mkono mtupu haulambwi

Hawa jamaa zetu wanajua vizuri kabisa kwamba Lowassa mgonjwa ni swala la muda tu lakini fedha inayomwagwa huko ni kama masinia la pilau siku ya Maulid ama Harusi kwa mwaliko!. Mwisho wa siku, waloshiba watakuwa wameshiba na walokosa nyama watafurahia shibe maana Maulid ama Harusi hii ipo mara moja tu kwa mwaka mitano.

Kitu cha muhimu kwenu ni kujitambua, kuzisoma alama hizi ya kwamba sasa hivi nchi yetu imefika mahala ambapo UFISADI unaweza kununuwa UTU wa watu kama ilivyotokea UTUMWA wakati wa mkoloni watu wakinunuliwa kwa shanga. Tunarudi katika kutawaliwa kifikra na fedha japo mwalimu alipiga kelele sana kuwa fedha sio msingi wa maendeleo lakini leo fedha inaweza kununua anything on the market sii soko huria bana! Fedha sabuni ya roho au sivyo?

Mnashangaa nini ikiwa baina yetu wapo radhi kuua binadamu wengine sii kwa chuki ama ubaguzi bali utajiri wa haraka kwa malipo ya Usd 75, 000 kwa viuongo vya Albino na alonunua anataka uongozi? Mnashangaa nini ikiwa baina yetu wapo wanaoua Tembo mzima na kukata pembe tu zenye kuthamanishwa sijui hadi Usd 10,000 kwa kilo na mwenye uwezo na ruksa ni kiongozi! hao wauza Unga na kadhalika hawa sii ndio wanaoendesha uchumi nchini na wanaosifika! Nini Pedegee Lowassa ya Mbongo awe mutu mubaya bana!

Ni lini Udalali na Ukuhadi uliharamishwa? sii ndio mupango wa Mujini maana wengine wanaogopa dhambi za kuua ama kukamatwa na unga lakini Udalali na Ukuhadi sii kataka mwenyewe!..Kwa hiyo wanazidi kuweka mirija tu wanamnyonya mzee wa watu subiri jina likatwe tutamsikilizia ICU na hatamuona mmoja! Hawajui Wabongo mzee wa watu! Mkono mtupu haulambwi!.
 
Du, afadhali wewe mkuu umekuja na vipimo vya macho,

lakini huyu Lowasa ni Mbunge, ni Mjumbe wa NEC ya CCM na pia ni mwenyekiti wa moja ya kamati muhimu za bunge. haya magonjwa yanakuja baada ya kugombea uraisi? Kwanini tusiamini hizi ni siasa za maji taka toka kwa wapinzani wake wa kisiasa? Du, ile ya Richmond vp imefail????!!!

Atakapo katwa jina muendelee kumfariji sio mnamkimbia tena
 
Mimi sijaona nyingi ya hizo video zake ila nimeona akihutubia kupitia runinga za Channel ten, Azam, ITV na zile zingine zinazompatia coverage ya kufa mtu...sioni coordination ya anachotaka kusema na anachokisema. Naona slowness ya mazungumzo. Hii inaweza kuwa either simfahamu vizuri mpendwa huyu au kuna shida. Maneno ni ya kutafutiza na najaribu kutafuta neno lenye ushawishi analotumia kwa "prospective voters" wake silioni. Sanasana nimemsikia karibu kila mkutano kuanzia Arusha na mahali penginepo akisema "hii haijapata kutokea" na kwa kweli sijaona akizungumza maneno mengine "material" yanayonishawishi nimfagilie. Labda sijapata hiyo fursa. Pia kutembea kwake kuna changamoto...anakuwa kama anasahau kisha anakumbuka fulani vile! Naona wakati mwingine anatembea kana kwamba ili asianguke! sijui ukweli ila huo ni mtizamo wangu. Ukweli mwingine ukimtazama unaona kama kuna mgogoro kwenye afya. Nimejiuliza maswali mengi sana...moja ya maswali hayo ni je, "Ikulu kuna nini?" "Ni lazima mtu afie Ikulu?" "Nani anawalazimisha watia nia hawa kuwa wasipoingia ikulu mambo yatawaendea kombo?" Bado sina majibu...nasubiri mtoa mada aje atetee na si kutuambia kitu cha kufanya kwa mtu huyu mtukuka
 
Mimi jamani naomba kuuliza maana hili limeshatangazwa sana hapa..!!!

Inasemekana kwamba Lowassa anaumwa Parkinson Disease, hili limesemwa sana hapa ndani, na huu ugonjwa unasemekana athari kubwa ni kumsababishia mtu kutetemeka na baadhi ya viongo vya mwili kukosa nguvu.

Swali je ugonjwa huu unasababisha hitulafu yoyote kwenye Ubongo? Je waweza kisababisha kifo?

Lowassa mwenyewe amepata kusikika akisema Ugonjwa na uzima ni neema kutoka kwa Mungu. Akadai kwamba yeye ni mzima wa afya. Akasema yeyote mwenye mashaka na afya yake akishawishi chama chao watengeneze utaratibu wa kila mgombea/mtiania Urais kupimwa ili ijulikane nani mgonjwa na nani mzima. Sasa mbona hatujasikia mrejesho toka kwa wagombea wengine wakishinikiza kwenda kipima ili kupata vidhibiti vya kumzuia Lowassa "Kihalali" kugombea nafasi hiyo kuliko wanavyomchafua bila uthibitisho?

Nijuavyo mimi kunamagonjwa ambayo matokeo yake yanaonekana hadharani na mengine ni ngumu kujua bila vithibitisho vya Daktari. Sawa twaweza kusema Lowassa mgonjwa hata tu atakapoonekana kujikwaa na kudondoka. lakini hao wagombea wengine ni wagonjwa kiasi gani? Au kwasababu hawajawahi kujikwaa na kuanguka? Mbona Kikwete amekaa na ugonjwa huo alioenda kutibiwa Us kwa. miaka takribani tisa madarakani bila mtu kujua? Je upi ni ugonjwa hata, Saratani ya kibofu au Mtetemo wa viongo vya mwili? (Haijathibitika)

Nimeona kina FaizaFoxy Nyunyu OLESAIDIMU na wengine wakijaribu kumshambulia Pasco kwa utetezi wake Lowassa, Je mnajua afya za wagombea wengine wa ccm? Au kwasababu wao miili yao inaficha magonjwa yao ndani kwa ndani?

BACK TANGANYIKA

Kuuguwa na kuumwa si kufa. Usivichanganye, hizo ni sababu tu za kufa ikiwa utakufa, unaweza ukaumwa usife haraka na yule mzima akafa ghafla. - Kumbuka hilo.

Huo ugonjwa unasababisha usahaulifu na kuchanganya maneno pia. Ushahidi wa Lowassa kuwa na usahaulifu na kuchanganya maneno ni pale alipokuwa anahutubia mkutano wa kutangaza nia Arusha, naomba isikilize hotuba yake, alisema kuwa Makamu wa Rais wa kwanza Sheikh Amri Abeid, kwa kujiamini kabisa kumbe alikuwa amesahau kuwa Amri Abeid ni jina la kiwanja anachohutubia na pia kachanganya badala ya Abeid Karume kuwa ni Makamu wa Rais wa kwanza yeye kampachika jina la Amri Abeid.

Mnataka nini zaidi ya huo ushahidi wa wazi kabisa?
 
Kwavile video zimefanyiwa slow motion basi wao wazifanyie speed motion tushangilie na kumuimbia rahisi Low hasa
 
Mi nimeaiangalia video ya mzee Lowasa inatia huruma. Hata kama humpendi huyu mzee utamhurumia ukiiangalia hii video. Hivi kwa nini familia yake wanamwacha anajidhalilisha kiivi? Kwa nini wasimshauri apumzike na kutafuta matibabu?
 
Mkuu Nyunyu,

Kama chuki kubwa ya kupakaza ugonjwa wa Lowassa hadharani ili kumkosesha kupata nafasi ya kugombea ndani ya ccm imefikia hapo kwanini basi hicho chama, hao wagombea wasiruhusu kupimwa hadharani kama wao wanajitambua wako fiti kiafya? Tena waweke sharti kwamba matokeo yoyote ya vipimo yatakayopatikana yawekwe hadharani, si tunataka kuliepusha taifa kwa kupata hasara ya kurudia uchaguzi? Na hao wengine wanajijua kwamba wako fiti kinachoogopwa ni kipi? Kwa lugha nyingine tunayoipata hapa ni kwamba wagombea wote ndani ya ccm ni WAGONJWA.! otherwise chama chao kisingeogopa kufanya vipimo kwa wagobea wake hadharani.!! Kama ndivyo wanapate sasa moral Authority kuusema ugonjwa wa Lowassa?

Halafu mkuu kumshambulia mtu kwaweza kuwa kwa kumkaripia kwa kile akisemacho kiwe kweli au uongo!! Pia kwaweza kuwa ni watu kadhaa kuungana kwa pamoja kupinga hoja ya mtu mmoja iwe ni ya kweli au uongo. Hivyo ilo la kushambulia Pasco kwa njia ya mjadara is not a case,imeeleka na ni simple tu just relax..!!

Hii ya kushindwa kunyanyuka kwenye kiti hata kama ni kweli kwa mujibu wa kuungwa mkono na Pasco, Lakini je alishindwa au kupata ukakasi kunyanyuka kwasababu ipi? Waweza kuta labda ilitokea hivyo baada ya kupata ganzi kutokana na kukaa kwa muda mrefu kwenye kiti, hili linamtokea yoyote iwe ni mgonjwa au mzima. Je mlisibitisha kwamba kashindwa kunyanyuka kwasababu ya ugonjwa unaomuandama?

Jambo lililowazi sote hapa tunakiri kwamba tunalabdisha tu kwamba Lowassa ni mgonjwa kutokana na mwonekano wake, lakini hakuna wenye uthibitisho wa ukweli wa ugonjwa wa Lowassa zaidi ya yeye mweyewe... Dalili...? Dalili moja wapo ya Ukimwi ni kuumwama mara kwa mara, kutokwa na majipu na vitu kama hivyo,lakini je huwezi kupata majipu kutokana na mchafuko wa damu? Huwezi kupata homa mara kwa mara kwa kuishi kwenye mazingira machafu? Tutajuaje kwamba wewe ni mgonjwa wa Ukimwi kwa kukutazama?

Nasisitiza tena kama wanaccm wanajiamini kwamba wao ni wazima Wakishawishi chama chao kitengeneze utaratibu wa kupima afya kwa wagombea wote wa nafasi zote. Hapo watamuhukumu Kihalali Lowassa vinginevyo hizo ni siasa za maji taka kama alivyopata kusema Muhadhini wa Wanamtandao Rostam Aziz.

Nb mimi hata kama ningekuwa nafunga kamwe nisingeweka hadharani kwamba nafunga, Dini yangu hainielezi hivyo! Nitakie tu siku njema kama ambavyonakutakia wewe siku njema mkuu.

BACK TANGANYIKA
 
Last edited by a moderator:
Kuuguwa na kuumwa si kufa. Usivichanganye, hizo ni sababu tu za kufa ikiwa utakufa, unaweza ukaumwa usife haraka na yule mzima akafa ghafla. - Kumbuka hilo.

Huo ugonjwa unasababisha usahaulifu na kuchanganya maneno pia. Ushahidi wa Lowassa kuwa na usahaulifu na kuchanganya maneno ni pale alipokuwa anahutubia mkutano wa kutangaza nia Arusha, naomba isikilize hotuba yake, alisema kuwa Makamu wa Rais wa kwanza Sheikh Amri Abeid, kwa kujiamini kabisa kumbe alikuwa amesahau kuwa Amri Abeid ni jina la kiwanja anachohutubia na pia kachanganya badala ya Abeid Karume kuwa ni Makamu wa Rais wa kwanza yeye kampachika jina la Amri Abeid.

Mnataka nini zaidi ya huo ushahidi wa wazi kabisa?

Huyu haumwi na ndiyo raisi anayefuata. Hata hao walioko huko sidhani kama wote wazima. Na kama angekuwa na tatizo asingepewa fomu
 
Atakapo katwa jina muendelee kumfariji sio mnamkimbia tena

Wagombea karibu 40 ni lazima apatikane mmoja na sio lazima awe yeye. kwani hatuwezi kujadili utendaji kazi wake, na au vp wengine hawajulikani! Sio sahihi kila mtu awe doctor na hakimu wa ufisadi tena wa mgombea mmoja tu.
 
Mi nimeaiangalia video ya mzee Lowasa inatia huruma. Hata kama humpendi huyu mzee utamhurumia ukiiangalia hii video. Hivi kwa nini familia yake wanamwacha anajidhalilisha kiivi? Kwa nini wasimshauri apumzike na kutafuta matibabu?
Ndio utajua binadamu tulivyokuwa wanyama kasoro mkia. Sasa hivi Money and Fame unaweza kumuuza hata baba yako mzazi..Na hakuna watu waongo na walaghai kama Wabongo, nadhani duniani tunaweza kuongoza sema hayajawahi tokea mashindano yake tu!.
 
kwa bahati nzuri na kwa mda maalumu nimekuwa karibu na huyo anayetajwa humu....mengi nimeyashuhudia na ni zadi ya haya yanayosemwa humu...ni ukweli usiopingika kwamba lowassa anauwa tena anaumwa sana...hali yake si nzuri kabisa. siku za mwanzo kabla hajabadili utaratibu wa maisha hasa nyakati za usiku alikuwa anapata shida sana anapolala, kugeuka hawezi. ikitokea daktari amechelewa kumdunga sindano na kumpa vidonge basi atavimba vidole,miguu, kutembea hataweza na akitembea basi atajikokota sana, hataweza hata kupiga mswaki, achilia mbali kushika kikombe cha chai....
kuna siku alikuwa arusha kuonana na baba askofu wa katoriki wakati wa mazungumzo alimba udhuru zaidi ya mara sita kwenda kujisaidia haja ndogo hata baada ya kuonyeshwa mahali pa haja hiyo bado aliomba mtu wake ampeleke (siku natangazia nia arusha alikwenda haja ndogo mara mbili akitkea pale jukwaa kuu)...alitembea kwa shida sana, vidole vilikuwa vikitetemeka sana,na baada ya mazungumzo mzee alishindwa kupanda kwenye gari..kunyanyua mguu ilikuwa ni shida sana mpaka akasaidiwa....
lowasa hapo alipo hawezi kugeuza shingo..anageuka mwili mzima ..ngozi ya mwili wake imebadilika kwa kiasi kikubwa ..weupe alio nao wa sasa si kawaida, hawezi hata kukunja nne...hatua ilipofika kwa sasa analala chumba kimoja na daktari wake na mkewe chumba kingine ili daktari aweze kumwangalia kwa ukaribu...

wakati flani kwenye mazungumzo alisikika akisema anatamani awe rais wa nchi hata kwa wiki mbili tu...hata hivyo tahadhari zote zimezingatiwa katika kumpata rais wa nchi anayefaa ...

Duh..!!! Kama hii maneno ni kweli basi kazi ipo
 
Back
Top Bottom