Hili Tangazo la Timu Lowassa linatudharau!

Hili Tangazo la Timu Lowassa linatudharau!

Wewe utakuwa umetumwa na teammembe Lowassa ni mzima wa afya kutetemeka ni jadi ya wamaasai kwasababu ya kunywa kloriti sana na kuchunga ng'ombe wakati wa baridi kali.Isitoshe Ikulu imeandaa chuma cha madaktari watakaokuwa na kazi ya kuangalia afya ya Lowassa 24 hours shida iko wapi.Mwisho kama atashindwa kutekeleza majukumu yake Makamu wa Rais yupo ndio maana tunachagua Rais na mgombea mwenza.

Mkuu, kweli afya ya mtu ni siri yake na daktari wake. Hilo halina ubishi. Rais wa nchi si mtu tu kama watu wengine. Afya yake ni suala la kitaifa. Afya yake ina implications kwenye mambo mengi ya kitaifa. Anatibiwa kwa gharama ya mlipa kodi, ikiwa bahati mbaya ataaga dunia (hatuombei hilo), kikatiba makamu wake atashika nafasi yake lakini si yule wananchi waliomchagua japo watanzania hatulipi sana umuhimu la nani ni mgombea mwenza. Siku likitupa ndiyo tutajua umuhimu wa kufuatilia mgombea mwenza maana anaweza kushika hatamu muda wowote.

Tena ningetamani from the word go, mtu akitangaza nia, aseme nani atakuwa mgombea mwenza tupime package nzima.

Katiba mpya ijayo (siyo hii ya nyoka wa makengeza) suala la afya ya Rais liwekwe wazi. Asiyetaka asigombee. Akafiche afya yake kwa mke/mumewe huko.
 
Wewe utakuwa umetumwa na teammembe Lowassa ni mzima wa afya kutetemeka ni jadi ya wamaasai kwasababu ya kunywa kloriti sana na kuchunga ng'ombe wakati wa baridi kali.Isitoshe Ikulu imeandaa chuma cha madaktari watakaokuwa na kazi ya kuangalia afya ya Lowassa 24 hours shida iko wapi.Mwisho kama atashindwa kutekeleza majukumu yake Makamu wa Rais yupo ndio maana tunachagua Rais na mgombea mwenza.


Huyo mgombea mwenza unamjua? Au yeyote bora liende?
 
Ugonja ni hali, hakuna anayeamua awe mgonjwa au awe mzima bali ni Mola wetu.

Uamuzi wa kuweka bayana uzima au ugonjwa ni uamuzi binafsi wa mtu, daktari wake na familia yake!, maadam amejieleza wazi kuwa yuko fit!, no matter how sick he looks, nasisitiza yuko fit!.

Maadam hali ya afya sio kigezo cha kuupata au kuukosa urais, this is a non issue!.

Hakuna mtu anayeung'ang'ania uras, maadam urais upo, na umetangazwa kwa yoyote anayeutaka, amejipima amajiona anauwezo, why not asiutake!, kwani hao wengine 37 wao hawautaki?!, au wamechukua fomu za kujaribishia tuu?, si ni wote wanautaka?!.

Rais wa Tanzania 2015, ni yule tuu aliyeandikiwa!, ikitokea ni yeye, no one can change a thing!, kama sio yeye, hatu watu humu mdhikir uchi, hawi!.

Pasco

Mkuu Pasco kweli umefikia hapo afya ya Rais ni issue kubwa sana kwa wananchi wote.Kumbukuka Rais ni kiongozi mkuu,amiri jeshi mkuu leo afya yake isiwe issue kweli Pasco ?.
 
Last edited by a moderator:
1. Makamu wa Rais Simba Mtoto.

2. Waziri Mkuu Mzee wa Vijisenti.

3. Waziri wa fedha Rost tamu

4. Waziri wa Mambo ya ndani Bashe

5. Waziri wa miundombinu Karamagi

6. Waziri wa Mambo ya nje Ayatollaaah Zitoo Kabwe

Wewe unataka jina la mgombea mwenza wakati sisi tunalijua baraza la mawaziri lote hapo nimekumegea kiduchu tu.

Huyo mgombea mwenza unamjua? Au yeyote bora liende?
 
1. Makamu wa Rais Simba Mtoto.

2. Waziri Mkuu Mzee wa Vijisenti.

3. Waziri wa fedha Rost tamu

4. Waziri wa Mambo ya ndani Bashe

5. Waziri wa miundombinu Karamagi

6. Waziri wa Mambo ya nje Ayatollaaah Zitoo Kabwe

Wewe unataka jina la mgombea mwenza wakati sisi tunalijua baraza la mawaziri lote hapo nimekumegea kiduchu tu.

Duh, hapo nimekubali. Kwa baraza hilo la mawaziri, wakati nchi jirani zinatembea Tanzania itakuwa inapaa kuelekea kuzimu!

Umesahau wachache ...

Waziri wa Afya - Sophia Simba
Waziri wa Tawala za Mikoa - Msukuma
Waziri wa Ulinzi - Kapuya
Waziri Ofisi ya Rais Shughuli Maalum - Mgana Msindai
Waziri asiye na wizara maalum - Ngombare Mwilu
 
Mh. ENL ni mgonjwa. Haiwekani mtu aliyeandaliwa atoke jukwaa kuu mara tatu kwenda haja mara 3 ndani ya masaa 3 jukwaani au na hiyo imeeditiwa??? ilikuwa LIVE coverage oale Arusha. Mikono kutopanda juu anaposema CCM oyee Live!!!

Tusidanganyane. Jipange kisaikologia na mzee wenu.
 
1. Pres. LOWASA 2. Vice. JAJ Ramadhan 3. PM Mwandosya 4. ULINZI Pinda 5. M/ndan Chikawe, 6. Sheria migiro 7. EAC membe
 
1. Pres. LOWASA 2. Vice. JAJ Ramadhan 3. PM Mwandosya 4. ULINZI Pinda 5. M/ndan Chikawe, 6. Sheria migiro 7. EAC membe
unaumwa wewe, hatuongozwi na mahututi siye. ikulu si muhimbili.
 
"Mtu mwenye akili akikuambia jambo la
kipumbavu wakati anajua una akili,
ukikubaliana nae anakudharau"-

Bwana Malihoja unataka tukubaliane nawewe ili utudharau??

Basi tusambazie hizo ambazo hazijafanyiwa "slow motion" ili tukubaliane na wew, vinginevyo tutaendelea kukubaliana na aliezifanyia slow motion izo vidios
 
Wakuu msaada jinsi ya kuzipata hizo videos Nimejaribu youtube bila mafanikio. Pengine nakosea key words,nisaidieni niziangalie na mimi.
 
Labda wengine mmeshaliona hili:



My Take: Sasa kama ni kweli wanafikiria hili au wanaamini hili basi bila ya shaka wanatufikiria sisi sote akili zetu ziko kwenye chupa. Hivi kweli video zote hizi zimewekwa slow motion? Seriously? Inawezekana Lowassa hana matatizo makubwa ya kiafya kama inavyohisiwa na baadhi ya watu lakini kusema kuwa video zimefojiwa ili kumfanya aonekane dhaifu zaidi nadhani si kutendea haki watu wengine. Kuna njia moja ya uhakika pkuondoa wasiwasi huu.






Mwanakijiji hizo zimefanyiwa photoshop. Ni muendelezo wa kuchafuana watia nia. Hata km mtu humkubali lakini simama katika ukweli siku zote utaonekana muungwana !
 
1. Makamu wa Rais Simba Mtoto.

2. Waziri Mkuu Mzee wa Vijisenti.

3. Waziri wa fedha Rost tamu

4. Waziri wa Mambo ya ndani Bashe

5. Waziri wa miundombinu Karamagi

6. Waziri wa Mambo ya nje Ayatollaaah Zitoo Kabwe

Wewe unataka jina la mgombea mwenza wakati sisi tunalijua baraza la mawaziri lote hapo nimekumegea kiduchu tu.
Wamejipanga kwelikweli! Na mtu atakayethubutu kuzuia hii safari yao hata panya ndani mwake hawatasalimika.
 
kuna tetesi kuwa jamaa hawezi kupunga mkono hata kwa dakika tano.

Mpaka october dhaifu wotewatajichuja tu.
 
Mtu mjinga wa kwanza ni wewe.unashupaa kumtetea Lowasa na kulazimisha watu waamini lowasa ni mtu safi.huna lolote zaidi ya njaa zinakusumbuwa.
Mkuu
lancanshire, kiukweli kabisa, mtu kuitwa mjinga wengi wankutafsiri kuwa ni kutukanwa, lakini mimi natafsiri kuwa mjinga ni kutokujua tuu, ukiishajulishwa, ukajua, then ujinga unakutoka!. Kama dhambi kuu ya Lowassa ni ufisadi wa Richmond, then endelea na ujinga wako, utakapoelimishwa kuwa Lowassa ni mbebaji tuu, huo ujinga utakutoka!.


Na hii sasa naomba nisiirudie tena, ila kwa msiojua, Richmond ndio ile ile Dowans, na ndio hii hii Simbioni, Mkataba ni ule ule, mitambo ni ile ile, na ile capacity charge ya shilingi 152 kwa siku bado ni ile ile!. Ile tozo ilikwisha lipwa siku nyingi!.

Sisi Watanzania ni wajinga!, tungekuwa na akili tungejiuliza kama tuliuvunja mkataba wa Richmond/Dowans kwa sababu ya ufisadi wa capacity charge ya shilingi milioni 152, tukashitakiwa, tukashindwa kesi, tukatozwa faini, tukailipa kisirisiri, sasa tumepandishiwa bili za umeme kufidia deni, na tunalipa, kisha ile ile Dowans tulioikataa kwa mbwembwe zote kule bungeni, ndio hii hii Simbion, mkataba ni ule ule, capacity charge ile ile!, tumeshuhudia watu waliojiapiza kwa maneno "over my dead body", siku hiyo walicheza ngoma za kwao na Obama kwenye Simbion, na sasa hakuna tena wa kujiuliza!, huu kama sio ujinga ni nini?!.

Niliwahi kusema hivi mahali, Jee Watanzania ni Ignorants? au Tumelogwa?!, na leo bado nasema, tena na tena, we are either ignorants au tumelogwa!.

Pasco
 
Back
Top Bottom