kama suala la matusi basi kila mbunge alitukana mbona nao hawajapigwa chini?
jaji kama yule sikudhani kama hatatumia busara ya kujali chaguo la wananchi,kuangalia garama za kurudia uchaguzi ni kubwa sana...,
Mkuu,hapo nyekundu, Mh. Lema amevuliwa ubunge kwa sababu ya matusi? Mimi sidhani kama hiyo ndiyo sababu kuu. Ninawaomba waliokuweko mahakamani na wanaokijua kisa kizima watuwekee hapa. Lakini ikiwa amevuliwa ubunge kwa matusi, na unasema kila mbunge alitukana, unataka kusema suala la matusi liachwe liendelee kama aibu aliyoitia Lusinde Tanzania kule Arumeru.
Na hapo kijani, hii nchi imeoza, watendaji hawajali Taifa linagharamika vipi, hawajali shida za wananchi. Viongozi wamezowea kula kupitia jasho letu, wanafaidika na mashaka yetu. Umeme ukikosekana, wanaofaidika ni wauza mafuta na majenereta, unadhani hawa wako tayari Tanzania iwe na umeme wa kudumu? Madaktari wakigoma, hispitali binafsi zinafanya biashara nzuri, na nyingi zao zinaendeshwa na vigogo au jamaa zao, kwa hivyo mgomo ni mtaji kwao. Na kila kero inayotokea TZ - ukosefu wa bidhaa muhimu kwa mfano - ujue kuna mtu nyuma yake anafaidika nalo, na pengine husababisha makusudi litokee ili apate manufaa.
Kwa hivyo, hata kurejewa kwa huo uchaguzi, kuna wachache wanalifurahia - viwanda vya uchapishaji, wenye usafiri, mafuta, mahoteli, posho kwa watendaji, yale maji ya washwasha, risasi.... wanataka vitumiwe wakanunue vyengine...kwa hivyo nani atajali mwananchi wa kawaida anateseka vipi?