Godbless Lema avuliwa ubunge

Godbless Lema avuliwa ubunge

Status
Not open for further replies.
Nafasi nyingine ya wanasiasa kutumia fedha zetu sisi walipa kodi wavuja jasho ambao tunaamka alfajiri na kurudi nyumbani usiku!
 
  • Thanks
Reactions: FJM
Hiyo ni sawa kutwanga maji kwenye kinu, wasikate rufaa wala nini, acha twende kwenye uchaguzi ili tuizike rasmi CCM na kutangaza habari za ukombozi wa nchi hii kupitia kwenye huo uchaguzi, pole Lema bu am sure ndani ya miezi mitatu jimbo litakuwa mikononi mwetu tena.
 
jaji amekula chake kutoka kwa chama cha matusi ccm .ushindi kwa chadema arusha uko palepale kwa kila chaguzi ni sawa na serikali kupoteza pesa kwa kitu ambacho kiko wazi kabisa kwamba ccm hawawezi kushinda arusha
 
Hili lilikuwa wazi sana kuwa Lema atavuliwa ubunge, kitendo cha Batilda Burian kutokutokea kutoa ushahidi na Jaji kufunga bila shahidi mkuu huyo kutokea mahakamani ilikuwa ishara tosha.
Pamoja na Majaji kula viapo vya kutenda kazi yao vizuri, Jaji Mkuu MH. Chande alinukuliwa akilalamika Serikali kuingilia Mhimili huo muhimu na matokeo yake ni hayo.
Pesa za walipa kodi zitatumika tena kwenye uchaguzi mdogo wakati umaskini umetukalia kooni.
 
Hata sababu zenyewe anazotoa wakili wa serikali ni weak mno! pambafu zao wanataka kufanya compansation ya Arumeru East na watashindwa vibaya na aibu ipo juu yao ngoja tuone sasa
 
hasara kwa taifa maana uchaguzi utarudiwa na mshindi wameshamjua

Mshindi kwa ars, ha ha ha! wamejampia mtoni hao waje tu tunawasubiri na this time tunawahamisha kabisa ili wajue Arusha ni nchi na chama tawala ni CDM.
 
wadau mlioko arusha tupeni nakala ya hukumu hapa jukwaani nasi tupime
 
Pole sana wana Chadema jipangeni na uchaguzi mpya...siasa zina matamu yake na machungu yake.
Thanks, tumekubali matokeo na Lema kasema hatokata rufaa,kwa hiyo kuanzia leo jimbo liko wazi. Tukutane tena ulingoni hakuna ushindi wamezani. Ila CCM inachofanya ni kuitangaza CDM, kwa vile najua jimbo la Arusha mtapata kura chache kuliko mlizopata na CDM inakwenda kuvunja rekodi ya kushinda chaguzi ndogo mfululizo.
 
  • Thanks
Reactions: FJM
Hii nikupotezeana muda na kutiana hasara.
 
Poleni wana-CHADEMA! Poleni wan-Arusha! Poleni watanzania wote wapenda demokrasia maana inatufundisha wazi kuwa demokrasia ina gharama zake.
 
ni vilio mji mzima hapa, siwezi hata kuelezea.....
 
Kama hakuhusishwa na rushwa anaruhusiwa kugombea tena, atachukua tu jimbo lake.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom