Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 117,752
- 218,339
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mwamba Freeman Mbowe, atahutubia Taifa la Tanzania kupitia Mkutano wake na Waandishi wa Habari utakaofanyika kwenye Makao Makuu ya Chama hicho, Kinondoni Dar es Salaam.
Mkutano huo uliobeba Mustakabhali wa nchi na Dira ya Taifa utafanyika 14/07/2023 kuanzia saa 8 mchana, ambapo Mbowe anatarajiwa kuyaanika hadharani maazimio yote ya Kamati Kuu iliyokutana Bahari Beach Hotel tarehe 08/07/2023.
Tunafahamu changamoto mnazozipitia Waandishi wa habari wa Tanzania kwa kuzuiliwa kuandika habari za Chadema, lakini kwa gazeti lolote kukosa taarifa za mkutano wa kesho yaweza kuwa hasara ya milele ya gazeti hilo.
Milango itakuwa wazi kuanzia saa 2 Asubuhi .
Wote Mnakaribishwa.