Kumbuka Division One ni zaidi ya elfu 60, Division Two karibu elfu 40, na Division Three zipo chache zaidi elfu 10.
Hii inaonyesha ushindani mkubwa sana kwenye udahili unaoendelea vyuoni, hasa vile vya serikali (Udsm, Mzumbe, Udom, Must, Dit, Tia, Ifm, Mipango, Mweka, n.k)
si kwamba ukiwa na Division Two au Three huwezi kupata chuo kikubwa lakini ukweli ni kwamba ushindani ni mkubwa, na nafasi ni chache. Wanafunzi wengi wenye Division One nao wanaziwania hizo nafasi, jambo linalopunguza uwezekano kwa wengine.
Kwa hiyo, jiongeze kwa kuomba vyuo vingi, usijikite tu kwenye vya serikali. vya makanisa na binafsi pia vipo na vina nafasi zaidi kwa walio na division hizo za kati.
Kama una hizo division omba vyuo vingi hasa vya makanisa na private
Mifano ya vyuo unavyoweza kuzingatia:
Ruaha Catholic University
Catholic University of Mbeya
Moshi catholic
Tumaini - Arusha na Iringa
Saut Mwanza
Teku Morovian Mbeya
Mihayo - Tabora
Stela Maris - Mtwara
n.k.
Ni jambo la kusikitisha kuona mtu mwenye Division 2 au 3 akiomba vyuo viwili vitatu, tena vyote vya serikali. Hapo kuna hatari ya kukosa chuo kabisa.
Tafadhali jipangie vizuri: Omba vyuo vingi, jipange kutimiza ndoto zako.
Hii inaonyesha ushindani mkubwa sana kwenye udahili unaoendelea vyuoni, hasa vile vya serikali (Udsm, Mzumbe, Udom, Must, Dit, Tia, Ifm, Mipango, Mweka, n.k)
si kwamba ukiwa na Division Two au Three huwezi kupata chuo kikubwa lakini ukweli ni kwamba ushindani ni mkubwa, na nafasi ni chache. Wanafunzi wengi wenye Division One nao wanaziwania hizo nafasi, jambo linalopunguza uwezekano kwa wengine.
Kwa hiyo, jiongeze kwa kuomba vyuo vingi, usijikite tu kwenye vya serikali. vya makanisa na binafsi pia vipo na vina nafasi zaidi kwa walio na division hizo za kati.
Kama una hizo division omba vyuo vingi hasa vya makanisa na private
Mifano ya vyuo unavyoweza kuzingatia:
Ruaha Catholic University
Catholic University of Mbeya
Moshi catholic
Tumaini - Arusha na Iringa
Saut Mwanza
Teku Morovian Mbeya
Mihayo - Tabora
Stela Maris - Mtwara
n.k.
Ni jambo la kusikitisha kuona mtu mwenye Division 2 au 3 akiomba vyuo viwili vitatu, tena vyote vya serikali. Hapo kuna hatari ya kukosa chuo kabisa.
Tafadhali jipangie vizuri: Omba vyuo vingi, jipange kutimiza ndoto zako.