Dr Akili
JF-Expert Member
- Aug 21, 2011
- 4,953
- 4,326
Duniani kote usafiri wa reli ndiyo usafiri wa bei rahisi sana kuliko usafiri mwingine wowote. Malengo makuu ya kuboresha usafiri huu kwa kiwango cha SGR yalikuwa:
~Trip moja ya treni ya mizigo ingaliweza kusafirisha mzigo wa sawa na semi-trailers za malori 500 kwa mara moja, kwa spidi ya 120 kph na kwa bei ya sawa na bure ukilinganisha na malori.
Yaani mzigo wa ukubwa huo wa semi trailer 500 ungeweza kuondolewa kutoka bandari yetu ya Dar es Salaam kila siku na kufikishwa Mwanza au Kigoma ndani ya masaa 10 au 12 tu. Hakungalikuwa tena na mrundikano wa mizigo pale bandari ya Dar es Salaam.
Hata hizo bandari kavu zilizoko mkoa wa Dar es Salaam zingalikosa kazi. Bandari kavu zingalijengwa Mwanza na Kigoma. Uchumi wa nchi ungepaa kwa kasi kubwa na ndani ya muda mfupi tungeifikia Singapore ambayo uchumi wake unategemea bandari tu.
Barabara zetu zingalidumu zaidi kwani usafiri wa malori unalifikia kiama chake. Hata hizo ajali lukuki za barabarani zinazosababishwa na malori haya katika njia hizi kuu zingalifikia tamati. Traffic police wetu wangetafutiwa kazi zingine.
~ Hivyo ndivyo ingalikuwa kwa usafirishaji wa abiria. Trip moja ya passenger train yenye urefu wa si chini ya kilomita 3 ingalikuwa sawa na mabasi yasiyopungua 500 na wangalisafirishwa kwa raha kwa spidi ya 170 kph.
Yaani kutoka Dar es Salaam hadi Mwanza au Kigoma ni mwendo wa saa 7 tu, kwa bei ya chee ukilinganisha na mabasi ambayo nayo yalikuwa yafikie kiama chake kwa njia hizi kuu za uchumi wa nchi na kuokoa uharibifu wa barabara zetu na ajali lukuki za barabarani. Uchumi wa nchi ungalipaa na wananchi wangalipata furaha.
Bahati mbaya kabisa matarajio hayo ya wananchi yameshindikana kufikiwa. TRC imepanga nauli za train hizo za spidi kubwa kuwa mara tatu ya bei za usafiri wa mabasi. Kwa sasa mtu anasafiri kwa basi kutoka Dar es Salaam hadi Mwanza kwa nauli ya Sh 55,000 hadi 65,000.
Hii ni nauli ya kupanda kwa mafuta kwa sababu ya Ukraine. Kabla ya hapo ilikuwa Shs 35,000 hadi 45,000 na tunategemea hiyo Ukraine itakapokwisha bei hizi zitarejea. Sasa TRC wamepanga ziwe Sh 150,000 kwani hadi Dodoma tu ni Sh 75,000. Yaani ni karibu sawa na nauli ya ndege. Hawa Waha na Wasukuma wetu kweli watazipanda hizo treni?
Bado TRC hawajatoa nauli za mabehewa ya mizigo. Kwa mantiki hiyo hiyo bei inayotarajiwa ni mara tatu ya bei ya kukodi lori la semi trailer. Hivyo tutegemee mambo kubaki kama kawa. Matajiri wa malori na mabasi wamekataa kufika kiama.
Wameshinda hiyo vita na inasemekana hata hizo treni za SGR zitaendeshwa na wafanya biashara binafsi kwa mtindo wa PPP (private public partnership)! Ni wajanja, wametupokonya SGR yetu tuliyoijenga na tunaendelea kuijenga kwa kodi zetu. Zingine tumekopa lakini tutazirejesha kwa kodi zetu.
Mapendekezo:
1. Nauli ya abiria kutoka Dar had Mwanza isizidi Sh 25,000 kwa economy class. Yaani isizidi nusu ya nauli ya basi. Hayo madaraja mengine mnaweza kuweka mnavyotaka. Hao wanaoishia njiani hususani Dodoma ziende kwa uhusiano huo wa umbali hadi Mwanza.
2. Behewa la mizigo bei yake isizidi theluthi moja ya bei ya kukodi lori.
3. Hakuna mantiki ya kuwa na tofauti ya nauli kati ya MGR inayotumia dizeli na SGR inayotumia umeme. Kwa vyovyote vile uendeshaji (running cost) ya ile ya umeme ni rahisi kuliko ile ya dizeli.
TRC lazima ijue kuwa jukumu lake ni kutoa huduma na si biashara ya kutaka kurejesha kile serikali imewekeza kwenye huo mradi wa SGR. Wanachotakiwa ni kukusanya tu pesa itakayowawezesha kulipa mishahara ya staff wao na mambo mengine ya uendeshaji.
~Trip moja ya treni ya mizigo ingaliweza kusafirisha mzigo wa sawa na semi-trailers za malori 500 kwa mara moja, kwa spidi ya 120 kph na kwa bei ya sawa na bure ukilinganisha na malori.
Yaani mzigo wa ukubwa huo wa semi trailer 500 ungeweza kuondolewa kutoka bandari yetu ya Dar es Salaam kila siku na kufikishwa Mwanza au Kigoma ndani ya masaa 10 au 12 tu. Hakungalikuwa tena na mrundikano wa mizigo pale bandari ya Dar es Salaam.
Hata hizo bandari kavu zilizoko mkoa wa Dar es Salaam zingalikosa kazi. Bandari kavu zingalijengwa Mwanza na Kigoma. Uchumi wa nchi ungepaa kwa kasi kubwa na ndani ya muda mfupi tungeifikia Singapore ambayo uchumi wake unategemea bandari tu.
Barabara zetu zingalidumu zaidi kwani usafiri wa malori unalifikia kiama chake. Hata hizo ajali lukuki za barabarani zinazosababishwa na malori haya katika njia hizi kuu zingalifikia tamati. Traffic police wetu wangetafutiwa kazi zingine.
~ Hivyo ndivyo ingalikuwa kwa usafirishaji wa abiria. Trip moja ya passenger train yenye urefu wa si chini ya kilomita 3 ingalikuwa sawa na mabasi yasiyopungua 500 na wangalisafirishwa kwa raha kwa spidi ya 170 kph.
Yaani kutoka Dar es Salaam hadi Mwanza au Kigoma ni mwendo wa saa 7 tu, kwa bei ya chee ukilinganisha na mabasi ambayo nayo yalikuwa yafikie kiama chake kwa njia hizi kuu za uchumi wa nchi na kuokoa uharibifu wa barabara zetu na ajali lukuki za barabarani. Uchumi wa nchi ungalipaa na wananchi wangalipata furaha.
Bahati mbaya kabisa matarajio hayo ya wananchi yameshindikana kufikiwa. TRC imepanga nauli za train hizo za spidi kubwa kuwa mara tatu ya bei za usafiri wa mabasi. Kwa sasa mtu anasafiri kwa basi kutoka Dar es Salaam hadi Mwanza kwa nauli ya Sh 55,000 hadi 65,000.
Hii ni nauli ya kupanda kwa mafuta kwa sababu ya Ukraine. Kabla ya hapo ilikuwa Shs 35,000 hadi 45,000 na tunategemea hiyo Ukraine itakapokwisha bei hizi zitarejea. Sasa TRC wamepanga ziwe Sh 150,000 kwani hadi Dodoma tu ni Sh 75,000. Yaani ni karibu sawa na nauli ya ndege. Hawa Waha na Wasukuma wetu kweli watazipanda hizo treni?
Bado TRC hawajatoa nauli za mabehewa ya mizigo. Kwa mantiki hiyo hiyo bei inayotarajiwa ni mara tatu ya bei ya kukodi lori la semi trailer. Hivyo tutegemee mambo kubaki kama kawa. Matajiri wa malori na mabasi wamekataa kufika kiama.
Wameshinda hiyo vita na inasemekana hata hizo treni za SGR zitaendeshwa na wafanya biashara binafsi kwa mtindo wa PPP (private public partnership)! Ni wajanja, wametupokonya SGR yetu tuliyoijenga na tunaendelea kuijenga kwa kodi zetu. Zingine tumekopa lakini tutazirejesha kwa kodi zetu.
Mapendekezo:
1. Nauli ya abiria kutoka Dar had Mwanza isizidi Sh 25,000 kwa economy class. Yaani isizidi nusu ya nauli ya basi. Hayo madaraja mengine mnaweza kuweka mnavyotaka. Hao wanaoishia njiani hususani Dodoma ziende kwa uhusiano huo wa umbali hadi Mwanza.
2. Behewa la mizigo bei yake isizidi theluthi moja ya bei ya kukodi lori.
3. Hakuna mantiki ya kuwa na tofauti ya nauli kati ya MGR inayotumia dizeli na SGR inayotumia umeme. Kwa vyovyote vile uendeshaji (running cost) ya ile ya umeme ni rahisi kuliko ile ya dizeli.
TRC lazima ijue kuwa jukumu lake ni kutoa huduma na si biashara ya kutaka kurejesha kile serikali imewekeza kwenye huo mradi wa SGR. Wanachotakiwa ni kukusanya tu pesa itakayowawezesha kulipa mishahara ya staff wao na mambo mengine ya uendeshaji.
Which of the following is the cheapest mode of transport.(A) Roadways(B) Railways(C) Waterways(D) Airways
Which of the following is the cheapest mode of transport.(A) Roadways(B) Railways(C) Waterways(D) Airways. Ans: Hint:Transportation is the movement from one place to another by means of any source it could be of any mode Roadways, Railways, Waterways...
www.vedantu.com